Injili ya Mathayo ni moja ya vitabu vinne katika Agano Jipya ambavyo vinaelezea kuhusu maisha ya Yesu Kristo. Waandishi wa Injili waliandika juu ya mambo mbalimbali yaliyoonyesha kama Yesu alikuwa nani na ni nini alichofanya. Mathayo aliashiria kwamba Yesu alikuwa Masiya, na kama Mungu angeweza kuokoa Israeli kupitia kwake. Mathayo mara nyingi alielezea kwamba Yesu alitimiza unabii wa Agano la Kale kuhusu Masiya. Hii inaweza kuonyesha kwamba alitarajia kuwa wasomaji wake wengi wa kwanza watakuwa Wayahudi.
Watafsiri wanaweza kuchagua kukiita kitabu hiki kwa kichwa chake asilia, "Injili ya Mathayo," au "Injili kulingana na Mathayo." Au wanaweza kuchagua kichwa ambacho ni wazi, kama vile "Habari Njema ya Yesu ambayo Mathayo aliandika."
Kitabu hakitupi jina la mwandishi. Hata hivyo, tangu nyakati za hapo mwanzo za Kikristo, Wakristo wengi wamefikiri kwamba mwandishi alikuwa Mtume Mathayo.
Mathayo alizungumza juu ya ufalme wa mbinguni kwa njia ile ile ambayo waandishi wengine wa injili walizungumzia juu ya Ufalme wa Mungu. Ufalme wa mbinguni unawakilisha Mungu akitawala juu ya watu wote na viumbe vyote kila mahali. Wale ambao Mungu anakubali katika ufalme wake watabarikiwa. Wataishi pamoja na Mungu milele.
Watu walimwona Yesu kama rabi. Rabi ni mwalimu wa sheria ya Mungu. Yesu alifundisha kwa njia iliyokuwa sawa na njia ya walimu wengine wa kidini huko Israeli. Alikuwa na wanafunzi ambao walimfuata kila mahali alipoenda. Wanafunzi hawa waliitwa wanafunzi. Mara nyingi aliwaambia mifano. Mifano ni hadithi zinazofundisha masomo ya maadili. and na )
Vitabu vya Mathayo, Marko na Luka huitwa injili za sinoptiki kwa sababu vina vifungu vingi vinavyofanana. Neno "sinoptiki" linamaanisha "kuona kwa pamoja."
Maandiko husemekana kuwa "sawa" wakati ambapo injili mbili au tatu zinafanana au zinakaribia kufanana. Wakati wa kutafsiri vifungu sambamba, wafasiri wanapaswa kutumia maneno sawa na kuyafananisha iwezekanavyo.
Katika Injili, Yesu anajiita mwenyewe "Mwana wa Binadamu." Ni kumbukumbu ya Danieli 7:13-14. Katika kifungu hiki kuna mtu anayeelezewa kuwa "Mwana wa binadamu." Hiyo ina maana kwamba mtu huyo alifanana na mwanadamu. Mungu alitoa mamlaka kwa mwana wa binadamu kutawala mataifa milele. Na watu wote watamwabudu milele.
Wayahudi wa wakati wa Yesu hawakutumia "Mwana wa Binadamu" kama jina la mtu yeyote. Kwa hiyo, Yesu aliitumia kwa ajili yake mwenyewe ili kuwasaidia kuelewa kama yeye alikuwa nani.
Kutafsiri jina "Mwana wa Binadamu" kunaweza kuwa vigumu kwa lugha nyingi. Labda wasomaji hawataelewa tafsiri halisi. Watafsiri pia wanaweza kutumia jina mbadala, kama vile "Yule aliye Mtu." Inaweza pia kusaidia wanapoingiza maelezo ya chini ya tanbihi ili kulielezea.
Haya ni masuala muhimu zaidi ya maandishi katika Kitabu cha Mathayo:
Watafsiri wanashauriwa kutoingiza vifungu hivi. Hata hivyo, ikiwa katika eneo la watafsiri, kuna matoleo ya zamani ya Biblia ambayo yanajumuisha moja au zaidi ya vifungu hivi, watafsiri wanaweza kuvijumuisha. Ikiwa vinajumuishwa, wanapaswa kuviweka ndani ya mabano ya mraba
1Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo mwana wa Daudi, mwana wa Ibrahimu.2Ibrahimu alikuwa baba wa Isaka, na Isaka baba wa Yakobo, na Yakobo baba wa Yuda na ndugu zake.3Yuda alikuwa baba wa Peresi na Sera kwa Tamari, Peresi baba wa Hezeroni, na Hezeroni baba wa Ramu.4Ramu alikuwa baba wa Aminadabu, Aminadabu baba wa Nashoni, na Nashoni baba wa Salimoni.5Salimoni alikuwa baba wa Boazi kwa Rahabu, Boazi baba wa Obedi kwa Ruth, Obedi baba wa Yese,6Yese alikuwa baba wa mfalme Daudi. Daudi alikuwa baba wa Sulemani kwa mke wa Uria.7Sulemani alikuwa baba wa Rehoboamu, Rehoboamu baba wa Abiya, Abiya baba wa Asa.8Asa alikuwa baba wa Yehoshafati, Yehoshafati baba wa Yoramu, na Yoramu baba wa Uzia.9Uzia alikuwa baba wa Yothamu, Yothamu baba wa Ahazi, Ahazi baba wa Hezekia.10Hezekia alikuwa baba wa Manase, Manase baba wa Amoni na Amoni baba wa Yosia.11Yosia alikuwa baba wa Yekonia na kaka zake wakati wa kuchukuliwa kwenda Babeli.12Na baada ya kuchukuliwa kwenda Babeli, Yekonia alikuwa baba wa Shatieli, Shatieli alikuwa babu yake na Zerubabeli.13Zerubabeli alikuwa baba wa Abiudi, Abiudi baba wa Eliakimu, na Eliakimu baba wa Azori.14Azori alikuwa baba wa Zadoki, Zadoki baba wa Akimu, na Akimu baba wa Eliudi.15Eliudi alikuwa baba wa Elieza, Elieza baba wa Matani na Matani baba wa Yakobo.16Yakobo alikuwa baba wa Yusufu mume wa Mariamu, ambaye kwa yeye Yesu alizaliwa, aitwaye Kristo.17Vizazi vyote tangu Ibrahimu hadi Daudi vilikuwa vizazi kumi na vinne, kutoka Daudi hadi kuchukuliwa kwenda Babeli vizazi kumi na vinne, na kutoka kuchukuliwa kwenda Babeli hadi Kristo vizazi kumi na vinne.18Kuzaliwa kwa Yesu Kristo kulikuwa kwa namna hii. Mama yake, Mariamu, alichumbiwa na Yusufu, lakini kabla hawajakutana, alionekana kuwa na mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.19Mume wake Yusufu, alikuwa mtu mwenye haki hakutaka kumwaibisha hadharani. Aliamua kusitisha uchumba wake naye kwa siri.20Alipokuwa akifikiri juu ya mambo haya, Malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema,” Yusufu mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Mariamu kama mkeo, kwa sababu mimba aliyonayo ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.21Atajifungua mtoto wa kiume na utamwita jina lake Yesu, kwa maana atawaokoa watu wake na dhambi zao.”22Yote haya yalitokea kutimizwa kile kilichonenwa na Bwana kwa njia ya nabii, akisema,23“Tazama, bikira atachukua mimba na kuzaa mtoto wa kiume, na watamwita jina lake Imanueli”-- maana yake, “Mungu pamoja nasi.”24Yusufu aliamka kutoka usingizini na kufanya kama malaika wa Bwana alivyomwamuru na alimchukua kama mkewe.25Hata hivyo, hakulala naye mpaka alipojifungua mtoto wa kiume na alimwita jina lake Yesu.
Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka kando kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari ya 1:23, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.
Nasaba ni orodha ambayo hurekodi mababu au wazao wa mtu. Orodha hizo zilikuwa muhimu sana katika kuamua nani aliyekuwa na haki ya kuwa mfalme, kwa sababu mamlaka ya mfalme mara nyingi ilipokelewa au kurithiwa kutoka kwa baba yake. Ilikuwa pia ya kawaida kwa mtu yeyote mashuhuri kuwa na kizazi cha kumbukumbu.
Sauti tulivu hutumiwa kwa makusudi katika sura hii ili kuonyesha kwamba Yesu hakuzaliwa kupitia uhusiano wa ngono. Hapa, sauti tulivu inaashiria Roho Mtakatifu kama aliyetanguliza uja uzito wake Maria alipombeba mtoto Yesu. Kwa kuwa lugha nyingi hazina sauti tulivu, watafsiri wanapaswa kutafuta njia nyingine za kuwasilisha ukweli huo.
Mwandishi anaanza na ukoo wa Yesu ili kuonesha kwamba yeye ni mzaliwa wa mfalme Daudi na wa Ibrahimu.
Ungeweza kutafsiri hii kama sentenso kamili.
Kulikuwa na vizazi vingi kati ya Yesu, Daudi, na Ibrahimu. Hapa "mwana" humaanisha "mzaliwa" "mzaliwa wa Daudi, ambaye alikuwa mzaliwa wa Ibrahimu.
wakati mwingine kirai "mwana wa Daudi" hutumika kama cheo, lakini hapa inaonekana kutumika kutambulisha tu ukoo wa Yesu.
Kuna njia mbalimbali ungeweza kutafsiri maelezo haya. Kwa namna yoyote unavyo natafsiri hapa, ingekuwa bora zaidi kuyatafsiri kwa namna ilele kwa orodha yote ya mababu wa Yesu. "Ibrahimu akawa baba wa Isaka" au "I brahimu alikuwa na mwana Isaka" au "Ibrahimu alikuwa na mwana aliitwa Isaka."
Haya ni majina ya wanaume
"Peresi alikuwa baba... Hesroni alikuwa baba.
"Salamoni alikuwa baba wa Boazi, na mama wa Boazi alikuwa Rahabu" au "Salmoni na Rahabu walikuwa wazazi wa Boazi.
"Boazi alikuwa baba wa Obedi, na mama wa Obedi alikuwa Ruth" au "Boazi na Ruth walikuwa wazazi wa Obedi"
"Daudi alikuwa baba wa Sulemani, na mama wa Sulemani alikuwa mke wa Uria" au "Daudi na mke wa Uria walikuwa wazazi wa Sulemani"
Sulemani alizaliwa baada ya Uria kufa. "mjane wa Uria."
Yoramu alikuwa kwa kweli babu ya babu yake na Uzia, hivyo 'baba" linaweza kutafsiriwa kama " babu"
Wakati mwingine jina hili limetafsiriwa "Amosi"
Yosia alikuwa kwa kweli babu yake na Yekonia.
"wakati walipoamriwa kwa nguvu kuondoka kwenda Babeli" au "wakati Wababeli walipo washinda na kuwahamisha kwenda kuishi Babeli." Kama lugha yako inahitaji kuwataja wazi ambao walienda Babeli, unaweza kusema "Waisraeli" au Waisraeli ambao waliishi Yuda.
Hapa humaanisha nchi ya Babeli, sio tu mji wa Babeli.
Tumia maneno yale yale uliyoyatumia katika Mat.1:9
Shealitieli kwa kweli alikuwa babu yake na Zerubabeli.
Mwandhishi anahitimisha ukoo wa Yesu, ambayo yalianza katika Mat.1: 1
Mariamu, ambaye alimzaa Yesu
Hii inaweza kuelezwa kwa namna iliyo hai. "watu ambao humwita Kristo."
"14"
Tumia maneno yale yale uliyotumia katika Mat.1:9.
"Mama yake Mariamu alikuwa mbioni kuolewa na Yusufu" kwa kawaida wazazi walifanya mipango ya ndoa za watoto wao." Wazazi wa Mariamu, mama wa Yesu, walikuwa wamemwahidi kuolewa na Yusufu.
Tafsiri kwa namna ambayo huweka wazi kwamba Yesu alikuwa bado hajazaliwa wakati Mariamu alikuwa amechumbiwa na Yusufu. "Mariamu, ambaye angekuwa mama wa Yesu, alikuwa amechumbiwa,"
"kabla hawajaoana." Hii pengine inamaanisha Mariamu na Yusufu kulala pamoja. kabla hawajalala pamoja."
Hii inaweza kuelezwa kwa namna iliyo tendaji. "wakatambua kwamba alikuwa mbioni kupata mtoto" au 'ilitokea kuwa alikuwa mjamzito.
Uwezo wa Roho Mtakatifu ulikuwa umemwezesha kupata mtoto kabla ya kuwa amelala na mwanamume.
Yusufu alikuwa bado hajamwoa Mariamu, lakini wakati mwanamume na mwanamke waliahidi kuoana, Wayahudi waliwahesabu mume na mke ingawa hawakuishi pamoja. "Yusufu, ambaye aliyepaswa kumwpoa Mariamu" au "Yusufu."
kuvunja mipango ya kuoana
"Kama Daudi alivyofikiri"
"alikuja kwake wakati Yusufu alikuwa akiota ndoto"
Hapa "mwana" humaanisha "mzaliwa"
Hii inaweza kuelezewa kwa namna iliyo tendaji. "Roho Mtakatifu alisababisha Mariamu kuwa mjamzito na kuwa na mtoto huyu."
Kwa sababu Mungu alimtuma malaika, malaika alijua mtoto atakuwa mvulana.
Hii ni amri. "utamwita" au "yakupasa kumpa jina"
Mtafsiri anaweza kuongeza rejeo inayo sema "Jina 'Yesu' maana yake Bwana huokoa."
Hii humaanisha Wayahudi
Mwandishi amnukuu nabii Isaya kuonesha kwamba kuzaliwakwa Yesu kulikuwa kwa mujibu wa andiko
Malaika hazungumzi tena. Mathayo sasa anaeleza umuhimu wa kile malaika alikisema.
Hii inaweza kuelezwa kwa namna iliyo tendaji. "kile ambacho Bwana alimwambia nabii Isaya kuandika zamani."
Hapa Mathayo anamnukuu nabii Isaya.
Neno hili huongeza msisitizo kwa kile kilicho fuata kusemwa. "Tazama" au "Sikia" au "Kuwa makini kwa kile ninachotaka kukuambia"
Hili ni jina la kiume.
Hii haimo katika kitabu cha Isaya. Mathayo anaeleza maana ya jina "Emanueli." Unaweza kulitafsiri kama sentenso iliyo peke yake. "Jina hili maana yake 'Mungu pamoja nasi.'"
Mwandishi anahitimisha maelezo ya matukio kuelekea kuzaliwa kwa Yesu.
Malaika alikuwa amemwambia Yusufu kumchukua Mariamu kama mke wake na kumpa mtoto jina Yesu.
"alimwoa Mariamu"
Hakika ni wazi kuwa Yusufu si baba halisi "kwa mtoto wa kiume" au "kwa mwana wake."
"Yusufu alimwita mtoto Yesu"
Mababu wawili walioorodheshwa wa kwanza ni Daudi na Ibrahimu.
Mariam, mke wa Yusufu ametajwa, kwasababu yeye ndiye alimzaa yesu.
Mariamu alipata mimba kwa Roho Mtakatifu kabla hajawa pamoja na Yusufu.
Yusufu alikuwa mtu wa haki.
Yusufu aliamua kuvunja uchumba na Mariamu kwa siri.
Malaika alimwambia Yusufu katika ndoto kumchukua Mariamu kama mke wake kwa sababu mtoto alichukuliwa mimba kwa Roho Mtakatifu.
Yusufu aliambiwa amwite mtoto Yesu kwa sababau atawaokoa watu wake na dhambi zao.
Unabii wa Agano la Kale ulisema kuwa bikira atazaa mtoto wa kiume, na kwamba watamwita jina lake Emanueli, ambalo maana yake "Mungu pamoja nasi".
Yusufu alikuwa mwangalifu kulala na Mariamu hadi pale alipomzaa Yesu.
1Baada ya Yesu kuzaliwa katika Bethelehem ya Uyahudi katika siku za mfalme Herode, wataalamu wa nyota kutoka mashariki ya mbali walifika Yerusalemu wakisema,2“Yuko wapi yeye ambaye aliyezaliwa Mfalme wa Wayahudi? Tuliiona nyota yake mashariki nasi tumekuja kumwabudu.”3Pindi Mfalme herode aliposikia haya alifadhaika, na Yerusalemu yote pamoja naye.4Herode akawakusanya wakuu wa makuhani wote na waandishi wa watu, naye akawauliza, “Kristo atazaliwa wapi?”5Wakamwabia, “Katika Bethelehemu ya Uyahudi, kwa kuwa hivi ndivyo ilivyoandikwa na nabii,6Nawe Bethelehemu, katika nchi ya Yuda, si mdogo miongoni mwa viongozi wa Yuda, kwa kuwa kutoka kwako atakuja mtawala atakayewachunga watu wangu Israeli.”7Hivyo Herode aliwaita wale watalaamu wa nyota kwa siri na kuwauliza ni wakati gani hasa nyota ilikuwa imeonekana.8Akawatuma Bethelehem, akisema, “Nendeni kwa uangalifu mkamtafute mtoto aliyezaliwa. Wakati mtakapomwona, nileteeni habari ili kwamba mimi pia niweze kuja na kumwabudu.”9Baada ya kuwa wamemsikia mfalme, waliendelea na safari yao, na nyota ile waliyokuwa wameiona mashariki iliwatangulia hadi iliposimama juu ya mahali mtoto aliyezaliwa alipokuwa.10Wakati walipoiona nyota, walifurahi kwa furaha kuu mno.11Waliingia nyumbani na kumuona mtoto aliyezaliwa na Mariamu mama yake. Walimsujudia na kumwabudu. Walifungua hazina zao na kumtolea zawadi za dhahabu, uvumba, na manemane.12Mungu aliwaonya katika ndoto wasirudi kwa Herode, hivyo, waliondoka kurudi katika nchi yao kwa njia nyingine.13Baada ya kuwa wameondoka, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto na kusema, “Inuka, mchukue mtoto na mama yake na mkimbilie Misri. Bakini huko mpaka nitakapowaambia, kwa kuwa Herode atamtafuta mtoto ili amwangamize.14Usiku huo Yusufu aliamka na kumchukua mtoto na mama yake na kukimbilia Misri.15Aliishi huko hadi Herode alipo kufa. Hii ilitimiza kile Bwana alichokuwa amenena kupitia nabii, “Kutoka Misri nimemwita mwanangu.”16Kisha Herode, alipoona kuwa amedhihakiwa na watalaamu wa nyota, alikasirika sana. Aliagiza kuuawa kwa watoto wote wa kiume waliokuwa Bethelehemu na wote katika eneo lile ambao walikuwa na umri wa miaka miwili na chini yake kulingana na wakati aliokuwa amekwisha thibitisha kabisa kutoka kwa wale watalaamu wa nyota.17Ndipo lilipotimizwa lile neno lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yeremia,
Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka kando kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mstari yote ya mistari ya 6 na18, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.
Huenda labda inaelezea nyota ambayo wasomi waliamini kuwa ishara ya mfalme mpya wa Israeli.
Tafsiri za Kiingereza hutumia maneno mengi tofauti ili kutafsiri maneno haya. Maneno haya ni pamoja na "wanajimu" na "watu wenye hekima." Watu hawa wangeweza kuwa wanasayansi au majusi. Ni bora kutafsiri hii kwa neno la kawaida "waakili," inapowezekana.
Sehsmu mpya ya habari huanza hapa na kuendelea hadi mwisho wa sura. Mwandishi anasimulia kuhusu jaribio la Herode kumwua mfalme mpya wa Wayahudi.
"mji wa Bethlehemu katika jimbo la Uyahudi"
"wakati Herode alipokuwa mfalme huko"
Hii humaanisha Herode Mkuu.
"watu wenye elimu ya nyota"
"kutoka nchi ya mbali mashariki ya Uyahudi.
Watu wale walijua kutokana na elimu ya nyota kwamba yule ambaye atakuja kuwa mfalme alikuwa amekwisha zaliwa. Walikuwa wanajaribu kuchunguza mahali alipokuwa. Mtoto mdogo ambaye atakuja kuwa mfalme wa Wayahudi amezaliwa. Yuko wapi?"
Walikuwa hawasemi kwamba mtoto mdogo alikuwa mmiliki halali wa nyota. "nyota ambayo hutuambia kuhusu yeye" au "nyota ambayo imehusishwa na kuzaliwa kwake.'
"ilikuja tokea mashariki" au wakati tulopkuwa katika nchi yetu"
uwezekano wa maana ni 1) walikusudia kumwabudu mtoto mdogo kama Mungu, au 2) walitka kumpa heshima kama mfalme wa kibinadamu. Kama lugha yako ina neno ambalo huhusisha maana zote mbili, unapaswa kuzingatia kulitumia hapa.
"alitaabishwa." Herode alitaabishwa kwamba mtoto mdogo huyu atachukua nafasi yake kama mfalme.
Hapa "Yerusalemu" ina maanisha watu. Pia "yote" humaanisha "wengi." Mathayo anaongeza chumvi kusisitiza watu wangapi walitaabishwa. "watu wengi wa Yerusalemu."
Ktoka mstari wa 6, makuhani wakuu na waandishi wa watu wanamnukuu nabii Mika kuonesha kwamba Kristo angezaliwa Bethlehemu.
"Katika mji wa Behlehemu katika jimbo la Yuda"
Hili linaweza kuelezwa kwa namna iliyo tendaji. hiki ndicho likchoandikwa na nabii zamani.
Wanamnukuu nabii Mika.
MIka alikuwa akizungumza na watu wa Bethlehemu kana kwamba walikuwa pamoja naye, lakini hawakuwa naye. Pia "hu mdogo" linaweza kutafsiriwa na kirai chanya. "ninyi watu wa Bethlehemu,...mji wenu ni miongoni mwa miji iliyo muhimu zaidi kuliko yote katika Yuda.
Mika anamzungumza mtawala huyu mchungaji. Hii inamaanisha ata waongoza na kuwahudumia watu. "ambaye atawaongoza watu wangu Israeli kama mchungaji aongozavyo kondoo wake."
Hii inamaanisha kwamba Herode alizungumza na mamajusi bila ya watu wengine kujua.
Hii inaweza kutafsiriwa kama nukuu ya moja kwa moja. "na akawauliza, lini hasa nyota hii ilionekana?"
Hii inadokeza kwamba mamajusi walimwambia nyota ilionekana lini. "wakati gani nyota ilikuwa umeonekana. Mamajusi walimwambia Herode lini wakati nyota ilipoonekana mara ya kwanza."
Inamaanisha Yesu.
"nijulishe" au "niambie"
Tafsiri hii kama ulivyofanya katika Mat 2:1
"baada ya mamajusi"
"walikuwa wamekwisha iona ikija kutoka mashariki" au "walikuwa wamekwisha iona katika nchi yao."
"iliwaonesha njia" au "iliwaongoza"
"ilisimama juu"
"mahali ambapo mtoto mchanga alikuwapo"
Hapa mandhari yanahamia kwenye nyumba mahari Mariamu, Yusufu, na mtoto mchanga Yesu walikuwa wakiishi.
"Mamajusi walienda"
Trafsiri neno hili kama ulivyofanya katika Mat.1:1
"hazina" humaanisha kasha au mifuko waliotumia kubebea hazina. "vyombo ambavyo vilishikilia hazina zao."
"Baadaye, Mungu aliwaonya mamajusi." Mungu alijua kwamba Herode alitaka kumdhuru mtoto.
Hii inaweza kutafsiriwa kama nukuu ya moja kwa moja. "kusema, 'Msirudi kwa mfalme Herode."
Katika mstari wa 15, mwandishi amnukuu nabii Hosea kuonesha kwamba Kristo angekaa Misri.
:mamajusi walikuwa wameondoka"
"alikuja kwa Yusufu wakati alipokuwa anaota.
Mungu anazungumza na Yusufu, haya yanapaswa kuwa katika umoja.
Maana kamili ya maelezo haya yanaweza kufanywa kuwa wazi. "mpaka nitakapo kuambia ni salama kurudi."
Hapa "nitakapo kuambia" inamaanisha Mungu. Malaika anazungumza kwa ajili ya Mungu.
Inamaanisha kwamba Yusufu, Mariamu, na Yesu walibaki Misri. "Walibaki"
Herode hafi mpaka Maelezo haya yanaelezea urefu wa muda wa kukaa Mirsi, na hayasemi kwamba Herode alikufa kwa wakati huu.
"Nimemwita mwanangu kutoka Misri"
Hapa mandhari yahamia kurudi kwa Herode na hueleza alifanya nini baada ya kugundua kuwa mamajusi walikuwa wamemdanganya.
Matukio haya yalitokea kabla kifo cha Herode, ambayo mwandishi ameyataja katika2:13
Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "mamajusi walikuwa wamemwaibisha kwa kumdanganya."
Herode hakuua watoto yeye mwenyewe. "Alitoa amri ili maaskali wake watoto wote wa kiume" au "Aliwatuma maaskari pale kuwa watoto wote wa kiume.
"Umri wa miaka 2 na wadogo chini ya umri huo.
"kutegemeana na wakati"
Mwandishi amnukuu nabii Yeremia kuonesha kwamba kifo cha watoto wote wa kiume katika mkoa wa Bethlehemu kilikuwa kwa mujibu wa Maandiko.
Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Hii ilitimizwa" au "matendo ya Herode yalitimiza."
Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "kile Bwana alikinena hapo zamani kwa njia ya nabii Yeremia"
Mathayo anamnukuu nabii Yeremia.
Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Watu walisikia sauti" au "kulikuwa na sauti kubwa."
Raheli aliishi miaka mingi kabla ya wakati huu. Unabii huu huonesha Raheli, ambaye amekufa, akiwalilia wazaliwa wake.
Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "hakuna yeyote angeweza kumfariji"
kwa sababu watoto walikuwa wametoweka na kamwe hawatarudi." Hapa "hawapo tena" ni njia laini ya kusema wamekufa. "kwa sababu walikuwa wamekufa"
Hapa mandhari ya hamia kwenda Misri, mahali Ysufu, Mariamu, na mtoto Yesu wanaishi.
Hii inaweka alama ya mwanzo wa tukio jingine katika habari ndefu. inaweza kuhusisha watu wengi kuliko matukio yaliyotangulia. Lugha yako inaweza kuwa namna ya kufanya hivi.
"wale ambao walikuwa wanamtafuta mtoto ili wamwue"
Hii ina maanisha mfalme Herode na washauri wake.
Huu ni mwisho wa sehemu ya simulizi ambayo ilianza katika Mat. 2:1. kuhusu jaribio la Herode kumwua mfalme mpya wa Wayahudi.
"Lakini Yusufu aliposikia"
Hili ni jina la mwana wa Herode.
"Yusufu aliogopa"
Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "lile Bwana alilolinena hapo zamani kwa njia ya manabii"
Hapa "ataitwa" anamaanisha Yesu. Manabii kabla ya wakati wa Yesu wangelimtaja kama Masihi au Kristo. "watu wangesema kuwa Kristo ni Mnazarayo."
Yesu alizaliwa Bethlehemu ya Uyahudi.
Wenye hekima(mamajusi) kutoka mashariki walimpa Yesu cheo cha " Mfalme wa Wayahudi"
Wenye hekima(mamajusi) walikuwa wameona nyota ya Mfalme wa Wayahudi huko mashariki.
Mfalme Herode aliposikia habari kutoka kwa Wenye hekima(mamajusi), alifadhaika.
Walifahamu juu ya unabii uliosema Kristo angezaliwa katika Bethelehemu.
Walifahamu juu ya unabii uliosema Kristo angezaliwa katika Bethelehemu.
Nyota kutoka mashariki iliwatangulia hadi ilisimama juu mahali alipozaliwa Yesu.
Yesu alikuwa mtoto mdogo wakati mamajusi walipo kuja kumwona.
Mamajusi walitoa zawadi ya dhahabu, manemane na uvumba kwa Yesu.
Mamajusi walirudi nyumbani kwa njia nyingine kwa sababu Mungu aliwaonya katika ndoto kwamba wasirudi kwa Herode.
Yusufu alielekezwa katika ndoto kumchukua Yesu na Mariamu na kukimbilia Misri, kwa sababu Herode alikuwa anaelekea kujaribu kumuua Yesu.
Unabii wa " kutoka Misri nimemwita mwangu" ulitimizwa wakati Yesu aliporudi kutoka Misri?
Herode aliwaua watoto wote wa kiume katika mkoa wa Bethlehemu waliokuwa wa umri wa miaka miwili au chini yake.
Yusufu alielekezwa katika ndoto kurudi katika nchi ya Israeli.
Yusufu alielekezwa katika ndoto kurudi katika nchi ya Israeli.
Yusufu alifanya makazi ya kuishi pamoja na Mariamu na Yesu Nazareti ya Galilaya.
Yusufu alifanya makazi ya kuishi pamoja na Mariamu na Yesu Nazareti ya Galilaya.
Unabii kuwa Kristo ataitwa Mnazorayo ulitimizwa.
1Katika siku zile Yohana Mbatizaji alikuja akihubiri katika nyika ya Yuda akisema,2“Tubuni kwa maana ufalme wa mbinguni u karibu.”3Kwa maana huyu ndiye aliyenenwa na nabii Isaya akisema, “Sauti ya mtu aitaye kutoka jangwani; ‘wekeni tayari njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.”’4Sasa Yohana alivaa manyoya ya ngamia na mkanda wa ngozi kiunoni mwake. Chakula chake kilikuwa nzige na asali ya mwituni.5Kisha Yerusalemu, Yuda yote, na eneo lote linalozunguka mto Yorodani wakaenda kwake.6Walikuwa wakibatizwa naye katika mto Yorodani huku wakitubu dhambi zao.7Lakini alipowaona wengi wa Mafarisayo na Masadukayo wakija kwake kubatizwa, akawaambia, “Enyi uzao wa nyoka wenye sumu nani aliye waonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?8Zaeni matunda yaipasayo toba.9Na msifikiri na kusemezana miongoni mwenu, ‘Tunaye Ibrahimu kama baba yetu.’ Kwa kuwa nawaambieni Mungu anaweza kumwinulia Ibrahimu watoto hata kutoka katika mawe haya.10Tayari shoka limekwisha kuwekwa kwenye mzizi wa miti. Kwahiyo kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa kwenye moto.11Ninawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba. Lakini yeye ajaye baada yangu ni mkuu kuliko mimi nami sistahili hata kubeba viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.12Na pepeto lake li mkononi mwake kusafisha kabisa uwanda wake na kuikusanya ngano yake ghalani. Lakini atayachoma makapi kwa moto ambao hauwezi kuzimika.13Kisha Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka mto Yorodani kubatizwa na Yohana.14Lakini Yohana alitaka kumzuia akisema, “Mimi nahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu?”15Yesu akajibu akasema, “Ruhusu iwe hivi sasa, kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote.” Kisha Yohana akamruhusu.16Baada ya kuwa amebatizwa, mara Yesu alitoka kwenye maji, na tazama, Mbingu zikafunguka kwake. Na alimuona Roho wa Mungu akishuka kwa mfano wa njiwa na kutulia juu yake.17Tazama, sauti ilitoka mbinguni ikisema, “Huyu ni mwanangu mpendwa, ninaye pendezwa sana naye.”
Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka kando kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari yote ya mstari wa 3, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.
Matunda ni taswira ya kawaida katika maandiko. Inatumika kuelezea matokeo ya tabia nzuri au mbaya. Katika sura hii, matunda mazuri ni matokeo ya kuishi kama Mungu anavyoamuru.
Wataalam wanajadili ikiwa "ufalme wa mbinguni" ulikuwepo wakati huu au bado unakuja. Tafsiri za Kiingereza mara nyingi hutumia maneno "karibu," lakini hii inaweza kusababisha changamoto katika kutafsiri. Matoleo mengine hutumia maneno "inakaribia" na "yamekaribia."
Huu ni mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi mahali ambapo mwandishi anaisimulia huduma ya Yohana Mbatizaji. Katika mst. 3. mwandishi anamnukuu nabii Isaya kuonesha kwamba Yohana Mbatizaji alikuwa mjumbe aliyechaguliwa na Mungu kuandaa huduma ya Yesu.
Hii ni miaka mingi baada ya Yusufuna familia kuondoka Misri na kwenda Nazareti.Hii pengine karibu na wakati ambao Yesu alianza huduma yake. "Baadaye" au "Miaka kadhaa baadaye."
Hii iko katika wingi. Yohana anazungumza na umati.
Kirai "ufalme wa mbinguni" humaanisha Mungu kutawala kama mfalme. Kirai hiki kiko katika kitabu cha Mathayo tu. Kama inawezekana, tumia neno "mbinguni" katika tafsiri yako. "Mungu wetu uliye mbinguni baada ya muda mfupi atajionesha mwenyewe kuwa mfalme."
Hii inaweza kuelezwa katika nmna iliyo tendaji. "Kwa kuwa Isaya nabii alikuwa anamnena Yohana Mbatizaji wakati aliposema."
Hapa "sauti" humaanisha nafsi yote. "Kuna mtu."
"Andaeni njia ya Bwana, nyosheni njia yake." Hii ni sitiari ya ujumbe wa Yohana ambao unawita watu kujiandaa na ujio wa Yesu kwa kufanya toba ya dhambi zao. "Badilika katika maisha yako hivyo utakuwa tayari wakati Bwana ajapo."
Neno "sasa" limetumika hapa kuweka alama kutenganisha mtiririko mkuu wa simulizi. Hapa Mathayo ana simulia habari za historia ya nyuma kuhusu Yohana Mbatizaji.
Vazi hili huashiria kwamba Yohana ni nabii kama manabii wa tangu zamani, hususan nabii Eliya.
Hii humaanisha watu kutoka maeneo yale. "Hapa neno "yote" humaanisha "wengi." Mathayo anasisitiza jinsi watu wengi walivyoenda kwa Yohana Mbatizaji.
Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Yohana aliwabatiza."
Hii inamaanisha watu waliokuja kutoka Yerusalemu, Uyahudi, na mkoa kuzunguka Mto Yordani.
Yohana Mbatizaji aanza kuwakemea Mafarisayo na Masadukayo.
Hii ni sitiari. Nyoka wa sumu ni hatari na wanwaklisha uovu. "Enyi nyoka wa sumu waovu!" au "Mu waovu kama nyoka wa sumu."
Yohana anatumia swali kuwaonya Mafarisayo na Masadukayo kwa sababu walikuwa wakimwomba kuwabatiza ili kwamba Mungu asiwahukumu, lakini hawakutaka kuacha kufanys dhambi. "hamwezi kuikimbia ghadhabu ya Mungu namna hii" au "msifikiri kwamba mnaweza kuikimbia ghadhabu ya Mungu kwa sababu ya kuwabatiza tu.
Neno "ghadhabu" linatumika kumaanisha adhabu ya Mungu kwa sababu ghadhabu yake hutangulia. "kimbieni kutoka kwenye hukumu ambayo inakuja" au "iepukeni kwa sababu Mungu anaenda kuwaadhibu ninyi."
Kirai "zaeni matunda" ni sitiari inayomaanisha matendo ya mtu. "Acha matendo yenu yaoneshe kwamba mmetubu kweli."
"Ibrahimu ni babu yetu" au "ni wazaliwa wa Ibrahimu." Viongozi wa Kiyahudi walifikiri kwamba Mungu hangewahukumu kwa kuwa ni wazaliwa wa Ibrahimu.
Hii inaongeza msisitizo kwa kile Yohana anchokwenda kukisema
"Mungu angeweza kufanya wazaliwa wa mwili kutokana hata na mawe haya na kumpa Ibrahimu"
Yohana Mbatizaji anaendelea kuwakemea Mafarisyo na Masadukayo.
Sitiari hii inamaanisha Mungu yuko tayari kuawaadhibu wenye dhambi. Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Mungu ana shoka lake na yuko tayari kukata na kuchoma mti wowote unaozaa matunda mabaya" au "Kama vile mtu atayarishavyo shoka kukata na kuchoma mti ambao huzaa matunda mabaya, Mungu yuko tayari kuwaadhibu ninyi kwa ajili ya dhambi zenu."
"kuonesha kwmba umekwisha tubu"
Yesu ni mtu yule ambaye anakuja nyuma ya Yohana
'ni wa muhimu zaidi kuliko mimi"
Sitiari hii hulinganisha ubatizo wa Yohana wa maji kwa ubatizo ujao wa moto. Hii humaanisha ubatizo wa Yohana kiishara huwatakasa watu dhambi zao. Ubatizo kwa Roho Mtakatifu na moto utatakasa dhambi za watu kwa kweli. Kama inawezekana, tumia neno "batiza" katika tafsiri yenu kutunza ulinganishaji wa ubatizo wa Yohana.
Sitiari hii hulinganisha namna Kristo atakavyo watenganisha watu wenye haki na watu wasio haki kwa namna mtu atenganishavyo nafaka ya ngano na makapi. "Kristo ni kama mtu ambaye pepeto lake liko mkononi mwake."
Hapa "mkononi mwake" humaanisha mtu yuko tayari kutenda. "Kristo ameshikilia pepeto kwa sababu yuko tayari."
Hiki ni kifaa kwa ajili ya kurusha juu hewani kutenganisha nafaka za ngano na makapi. Nafaka zenye uzito hurudi na kuanguka chini na makapi yasiyotakiwa hupeperushwa na upepo. Kina fanana na umbo la uma ya nyasi lakini kina meno mapana kimetengenzwa kutokana na mbao.
"kiwanja chake" au " kiwanja mahali ambapo hutenganisha nafaka na makapi"
Hii ni sitiari inayoonesha jinsi Mungu atakavyowatenganisha watu wenye haki na watu waovu. Wenye haki wataenda mbinguni kama ngano katika ghala ya mkulima, na Mungu atawachoma watu ambao ni kama makapi kwa moto ambao hautazimika.
Hii inweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "kamwe hautazimika."
Hapa mandhari yahamia kwenda wakati wa baadaye wakati Yohana Mbatizaji ambatiza Yesu.
Hii inaweza kueleza katika namna iliyo tendaji. "hivyo Yohana aliweza kumbatiza."
Yohana anatumia swali kuonesha kushangazwa kwake na ombi la Yesu. "Wewe ni wa maana zaidi kuliko mimi. Sipaswi kukubatiza wewe. Wewe unapaswa kunibatiza mimi."
Hapa "sisi" humaanisha Yesu na Yohana.
Huu ni mwisho wa sehemu ya simulizi kuhusu Yohana Mbatizaji na hueleza kilichotokea baada ya kumbatiza Yesu.
Hii inaweza kueleza katika namna iliyo tendaji. "Baadaya Yohana kumbatiza Yesu"
Neneo "tazama" hapa hututahadharisha sisi kuwa makini kwa habari ya kushtukiza ambayo inafuata.
Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Yesu aliona mbingu zimefunguka" au "Mungu alizifungua mbingu kwa Yesu."
Maana zinaweza kuwa 1) haya ni maelezo dhahiri kwamba Roho alikuwa katika umbo la njiwa au 2) huu ni mfanano ambao hulinganisha Roho kushuka chini kuja juu ya Yesu kwa upole, ndivyo njiwa angefanya.
"Yesu alisikia sauti kutoka mbinguni." Hapa "sauti" humaanisha Mungu anazungumza. "Mungu alizungumza kutoka mbinguni."
Hiki ni cheo cha maana cha Yesu, Mwana wa Mungu
Yohana alihubiri "Tubuni kwa maana ufalme wa mbinguni u karibu".
Unabii ulisema kuwa Yohana Mbatizaji angetayarisha njia ya Bwana.
Walipokwisha kubatizwa, watu walitubu dhambi zao.
Yohana mbatizaji aliwaambia Masadukayo na Mafarisayo wazae matunda kulingana na toba.
Yohana mbatizaji aliwaonya Masadukayo na Mafarisayo wasifikiri miongoni mwao kuwa wanaye Ibrahimu kama baba yao.
Yohana anasema kwamba kila mti usiozaa matunda mazuri hukutwa na kuanguka chini na kutupwa motoni.
Aliyekuwa anakuja baada ya Yohana angebatiza kwa Roho Mtakatifu na moto.
Yesu alimwambia kwamba ilikuwa haki kwa Yohana kumbatiza Yesu ili kutimiza haki yote.
Alipotoka majini, Yesu alimwona Roho wa Mungu akishuka kama njiwa na kuwa juu yake.
Sauti kutoka mbinguni ilisema, "huyu ni Mwanangu mpendwa, ninayependezwa naye".
1Kisha Yesu aliongozwa na Roho mpaka jangwani ili ajaribiwe na Ibilisi.2Alipokuwa amefunga kwa siku arobaini mchana na usiku alipata njaa.3Mjaribu akaja na akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe mkate.”4Lakini Yesu alimjibu na kumwambia, “Imeandikwa, ‘Mtu hataishi kwa mkate peke yake, bali kwa kila neno litokalo kinywani mwa Mungu.’”5Kisha Ibilisi akampeleka katika mji mtakatifu na kumweka mahali pa juu sana pa jengo la hekalu,6na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jirushe chini, kwa maana imeandikwa, ‘Ataamuru malaika wake waje wakudake,’ na, ‘watakuinua kwa mikono yao, ili usijikwae mguu wako katika jiwe.’”7Yesu akamwambia, “Tena imeandikwa, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’”8Kisha, Ibilisi akamchukua na kumpeleka sehemu ya juu zaidi akamwonyesha falme zote za ulimwengu na fahari ya hizo zote.9Akamwambia, “Nitakupa vitu vyote hivi ukunisujudia na kuniabudu.”10Kisha Yesu akamwambia, “Nenda zako Shetani! Kwa maana imeandikwa, ‘Yakupasa kumwabudu Bwana Mungu wako, na umtumikie yeye peke yake.’”11Kisha Ibilisi akamwacha, na tazama, malaika wakaja wakamtumikia.12Basi Yesu aliposikia kuwa Yohana amekamatwa, aliondoka mpaka Galilaya.13Aliondoka Nazareti alienda na kuishi Kaperanaumu, iliyoko kandokando na Bahari ya Galilaya, mipakani mwa majimbo ya Zabuloni na Naftali.14Hii ilitokea kutimiza kile kilichonenwa na nabii Isaya,
Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka kando kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari yote ya mistari ya 6, 10, 15 na 16, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.
Wataalam wanajadili ikiwa "ufalme wa mbinguni" ulikuwepo wakati huu au bado unakuja. Tafsiri za Kiingereza mara nyingi hutumia maneno "karibu," lakini hii inaweza kusababisha changamoto katika kutafsiri. Matoleo mengine hutumia maneno "inakaribia" na "yamekaribia."
Kwa Kiingereza, msomaji anaweza kuelewa kauli hii katika 4:6 kama inayoonyesha kwamba Shetani hajui kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu. Kwa sababu Shetani anajua kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, haipaswi kutafsiriwa kwa njia hii. Inaweza kutafsiriwa kama "kwa sababu wewe ni Mwana wa Mungu." na )
Hapa mwandishi anaanza sehemu mpya ya simulizi ambayo Yesu anatumia siku 40 nyikani, mahali ambapo Shetani anamjaribu. Katika mst. 4, Yesu anamkemea Shetani kwa nukuu kutoka Kumbukumbu la Torati.
Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Roho alimwongoza Yesu."
Hiiinaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "hivyo Ibilisi aliweza kumjaribu Yesu."
Haya yana maanisha kiumbe yuleyule. unaweza kutumia neno lilelile kutafsiri yote mawili.
Haya yanamaanisha Yesu.
"Siku 40 mchana na usiku" Hii ina maanisha vipndi vya saa 24. "siku 40."
Ina wezekana kuwa na maana 1) hili ni jaribu la kufanya miujiza kwa ajili ya manufaa ya Yesu mwenyewe. "Wewe ni mwana wa Mungu, hivyo amuru." Au 2) "Thibitisha kwamba wewe ni Mwana wa Mungu kwa kuamuru." Ni vizuri kuamini kuwa Shetani alijua kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.
Hiki ni cheo muhimu kinacho eleza uhusiano kati ya Yesu na Mungu.
Hikini cheo cha maana cha Yesu.
Ungeweza kutafsiri hii na nukuu ya moja kwa moja. "sema kwa mawe haya, Kuwa mkate."'
"chakula"
Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Musa aliandika hivi katika maandiko hapo zamani."
Hii inamaanisha kuwa kuna kitu ambacho ni cha muhimu zaidi katika maisha kuliko chakula
Hapa "neno" na "kinywa" humaanisha kwa kile Mungu anasema.
Katika mstari 6, Shetani ananukuu kutoka Zaburi ili kumjaribu Yesu.
Inaweza kuwa na maana 1) hili ni jaribu kufanya muujiza kwa ajili ya manufaa ya Yesu mwenyewe. "Kwa kuwa Mwana wa Mungu kwa kweli, unaweza kujitupa chini." Au, 2) hii ni changamoto au shtaka. "Thibitisha kuwa wewe kwakweli ni Mwana wa Mungu kwa kujitupa chini" Ni vizuri kuamini kuwa Shetani alijua kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.
Hiki ni cheo cha maana ambacho kinaeleza uhusiano kati ya Mungu na Yesu.
"jiachie mwenyewe hadi chini" au ruka kwenda chini"
Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "kwa maana mwimba zaburi aliandika katika maandiko" au " kwa maana inasema katika maandiko."
"Mungu atawaagiza malaika wake wakutunze." Hii inaweza kutafsiriwa na nukuuu ya moja kwa moja. "Mungu atasema kwa malaika wake, Mlindeni."'
"Malaika watakushika
Katika mstari wa 7, Yesu amemkemea Shetani na nukuu nyingine kutoka Kumbu kumbu
Imefahamika kuwa Yesu anamaanisha ana nukuu maandiko tena. Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Tena, nitawaambia Musa alichoandika katika maandiko."
Hapa "usi" inamaanisha yeyote. "Mtu hapaswi kumjaribu" au "Hapana mtu anapaswa kumjaribu."
"Baada ya hapo, Ibilisi"
"Ibilisi alimwambia Yesu"
"Nitakupa vitu vyote hivi." Mjaribu anasisitiza kuwa atampa "vitu vyote," si tu baadhi yake.
Huu ni mwisho wa sehemu ya simulizi kuhusu jinsi Shetani alivyo mjaribu Yesu
Katika mstari su10, Yesu anamkemea ShetanTi na nukuu nyingine kutoka Kumbukumbu la Torati.
Hii inaweza kuelezwa katika namna yamuundo tendaji. "Musa pia aliandika katika maandiko."
Hapa "yakupasa" inamaanisha yeyote.
Neno "tazama" hapa lina tutahadharisha kuwa makini kwenye habari mpya muhimu ambazo zinafuata.
Huu ni mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi ambayo katika hiyo mwandishi anaeleza mwanzo wa huduma ya Yesu Galilya. Mistari hii inaeleza jinsi Yesu alivyokuja Galilaya
Neno hili lintumika hapa kuweka alama ya kuanzisha mtiririko wa habari kuu wa simulizi. Hapa Mathayo anaanza kutuambia sehemu mpya ya simulizi.
Hii inaweza kuelezwa katika namna ya muundo tendaji. "mfalme alikuwa amemkamata Yohana."
Haya ni majina ya makabila ambayo yaliishi katika maeneo haya kabla ya wageni kudhibiti nchi ya Israeli miaka mingi kabla.
Katika mstari wa 15 na 16, mwandishi anamnukuu nabii Isaya kuonesha kwamba huduma ya Yesu Galilaya ilikuwa ni kutimizwa kwa unabii.
Hii inamaanisha Yesu kwenda kuishi Kaperenaumu.
Hii inaweza kuelezwa katika namna ya muundo tendaji. "kile Mungu alichonena"
Majimbo haya yote yanaeleza eneo lilelile. Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi timilifu. "Katika jimbo la Zabuloni na Naftali...katika jimbo hilo huishi Wamataifa wengi."
Hii ni bahari ya Galilaya.
Hapa "giza" humaanisha maisha ya gizani au dhambi ambayo huwatenga watu na Mungu. Na "mwanga" humaanisha ujumbe wa kweli wa Mungu ambao huwaokoa watu kutoka katika dhambi yao. Hii ni taswira ya watu ambao hawa kuwa na tumaini sasa wana tumaini kutoka kwa Mungu.
Kimsingi hii ina maana ileile kama sehemu ya kwanza ya sentensi. Hapa "eneo" na kivuli cha kifo" humaanisha kifo cha kiroho au kutengana na Mungu.
Sentensi "ufalme wa mbinguni" humaanisha utawala ambao Mungu ndiye mfalme. Sentensi hii imetumika katika injili ya Mathayo tu. Kama inawezekana tumia neno "Mbinguni" katika tafsiri yako. "Si muda mrefu Baba yetu aliye mbinguni atajidhirisha kuwa ni mfalme" Angalia jinsi ilivyotafsiriwa katika Mat. 3:1
Hii huanza mandhari mpya katika sehemu ya simulizi kuhusu huduma ya Yesu kule Galilaya. Hapa huanza kwa kuwakusanya watu kuwa wanafunzi wake.
"Kutupa nyavu majini ili kuvua samaki"
"Yesu anawakaribisha Simoni na Andrea kumfuata, kuishi naye, na kuwa wanafunzi wake. ""Iweni wanafunzi wangu."
Hii sitiari humaanisha Simoni na Andrea watawafundisha watu ujumbe wa kweli wa Mungu hivyo wengine pia waanze kumfuata Yesu. "Nitawafundisha kuwaleta watu kwangu kama mlivyo kuwa mnavua samaki"
Yesu anawaita watu zaidi kuwa wanafunzi wake.
"Yesu aliwaita Yohana na Yakobo." Kirai hiki pia humaanisha kwamba aliwakaribisha kumfuata, kuishi naye, na kuwa wanafunzi wake.
"wakati huo huo"
Inapaswa kuwa wazi kwamba haya ni mabadiliko ya maisha. Watu hawa hawaendi tena kuwa wavuvi na wanaacha shughuli za familia zao kumfuata Yesu kwa maisha yao waliyo nayo.
Huu ni mwisho wa sehemu ya simulizi kuhusu mwanzo wa huduma ya Yesu Galilaya. Mistari hii ni muhtasari wa kile alichofanya na jinsi watu walivyoitikia.
"kufundisha katika masinagogi ya Wagalilaya" au kufundisha katika masinagogi ya watu wale"
Hapa "ufalme" humaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. "kuhubiri habari njema kuhusu jinsi Mungu atakavyojifunua mwenyewe kama mfalme."
"kila maradhi na kila ugonjwa." Maneno "maradhi" na :magonjwa" yanakaribia sana lakini yanapaswa kutafsiriwa kama maneno mawili tofauti kama inawezekana. "Maradhi ni kile kinacho sababisha mtu kuwa mgonjwa. "Ugonjwa ni udhifu wa mwili au maumivu ambayo ni matokeo ya kuwa na maradhi.
Hii inaweza kuelezwa katika namna ya mfumo tendaji. "walio na pepo" au "wale ambao wanatawaliwa na pepo."
"wale waliokuwa na kifafa" au wale walio na maradhi ambayo yalisababisha kuzirai."
"wale ambao hawakuweza kutembea"
Jina hili humaanisha "Miji Kumi."
Roho Mtakatifu alimwongoza Yesu kwenda nyikani kujaribiwa na mwovu.
Yesu alifunga siku arobaini mchana na usiku huko nyikani.
Mwovu alimjaribu Yesu kugeuza jiwe liwe mkate.
Yesu alisema kwamba mtu hataishi kwa mkate peke yake, bali kwa kila neno litokalo kinywani mwa Mungu.
Mwovu alimjaribu Yesu kujitupa mwenyewe chini kutoka kwenye hekalu.
Mwovu alimjaribu Yesu kujitupa mwenyewe chini kutoka kwenye hekalu.
Yesu alisema kwamba usimjaribu Bwana Mungu wako.
Mwovu alimjaribu Yesu kumwabudu ili ampe falme zote za ulimwengu.
Yesu alisema kwamba yakupasa kumwabudu Bwana Mungu wako na kumtumikia yeye peke yake.
Unabii wa Isaya ulitimizwa ambao uliosema kwmba watu wa Galilaya wangeona mwanga mkuu.
Yesu alihubiri, "tubuni, kwa kuwa ufalme wa mbinguni umekaribia."
Petro na Andrea walikuwa wavuvi.
Yesu aliwaambia Petro na Andrea atawafanya kuwa wavuvi wa watu.
Yakobo na Yohana walikuwa wavuvi.
Yesu alifundisha katika masinagogi ya Galilaya.
Wote waliokuwa wagonjwa na kupagawa na mapepo waliletwa kwa Yesu na Yesu aliwaponya.
Umati makubwa ulikuwa ulikuwa ukimfuata Yesu kwa wakati huu.
1Yesu alipo uona umati, akaondoka na kuelekea mlimani. Alipokuwa ameketi chini, wanafunzi wake wakaja kwake.2Akafunua kinywa chake na akawafundisha, akisema,
Mathayo 5-7, ambayo huitwa "Mahubiri ya Mlimani," ni funzo moja ndefu ya Yesu. Mgawanyiko wa sura husababisha kuchanganyikiwa hapa. Kichwa kinaweza kumsaidia msomaji kuelewa kwamba sura hizi zinaunda sehemu moja au kitengo. Mtafsiri anapaswa kufahamu kuwa kuna swali fulani kuhusu ikiwa mafundisho yanahusu Israeli, kanisa, au ufalme wa Mungu wa baadaye.
5:3-10, inayojulikana kama Heri au Baraka, imewekwa kwa kutumia uingizaji, na kila mstari unaanza na neno "heri." Uingizaji huu unaashiria fomu ya ushairi wa mafundisho haya.
Inawezekana kutaja mtu yeyote aliyemfuata Yesu kama mfuasi au mwanafunzi. Yesu aliwachagua wafuasi wake kumi na wawili kuwa watu wake wa ndani, wale wanafunzi kumi na wawili. Baadaye walijulikana kama mitume. Inaweza kuwa na maana kwamba mafundisho haya yalikuwa kwa mitume hao kumi na wawili.
Huu ni mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi ambayo Yesu alianza kuwafundisha wanafunzi wake. Sehemu hii huendelea hadi mwisho wa sura ya 7 na mara kwa mara huitwa mahubiri ya Mlimani.
Katika msyari wa 3, Yesu anaanza kueleza tabia za watu ambao wamebarikiwa.
"Yesu alianza kunena."
Neno "aliwa" humaanisha wanafunzi wake.
Hii inamaanisha mtu ambaye ni mnyenyekevu. "wale ambao wanajua wanamhitaji Mungu."
Hapa "ufalme wa mbinguni" humaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. Kirai hiki kiko katika kitabu cha Mathayo tu. Kama inawezekana weka "mbinguni" katika tafsiri yako. "kwa kuwa Mungu wa mbinguni atakuwa mfalme wao."
Sababu zinazopelekea kuwa wenye huzuni ni 1) hali ya dhambi ya ulimwengu au 2) dhambi zao au 3) kifo cha mtu. Usieleze bayana sababu ya kuhuzunika isipkuwa lugha yako inataka hivyo.
Hii inaweza kuelezwa katika namna ya mfumo tendaji. "Mungu atawafariji."
"wapole" au "wale ambao hawategemei uwezo wao wenyewe"
"Mungu atawapa nchi yote."
Sitiari hii humaanisha mtu anapaswa kwa uhodari kufanya kilicho sahihi. "kutamani kuishi kwa unyofu kama ilivyo kutamani chakula na kinywaji.
Hii inaweza kuelezwa katika namna ya mfumo tendaji. "Mungu atawashibisha" au "Mungu atawatosheleza."
"watu ambao mioyo yao ni safi." Hapa "safi" hurejelea kwa kutamani kwa mtu. wale ambao tu wanataka kumtumikia Mungu."
Hapa "kuona" inamaanistha wataweza kuishi katika uwepo wa Mungu." "Mungu atawaruhusu kuishi naye."
Hawa ni watu ambao husaidia wengine kuwa na amani na wengine miongoni mwao.
Hii inaweza kuelezwa katika namna ya muundo tendaji. "kwa kuwa Mungu atawaita watoto wake" au "watakuwa watoto wa Mungu.
Ni vizuri kutafsiri "wana" kwa neno lile lile lugha yako kwa kawaida ungelitumia kurujelea kwa mwana au mtoto wa binadamu
Hii inaweza kuelezwa katika namna muundo tendaji. "watu wale ambao wengine huwatendea kwa isivyo haki"
"kwa sababu wanafanya kile ambacho Mungu hutaka wafanye"
angalia jinsi ulivyotafsiri katika Mat. 5:1
Yesu anamaliza kueleza tabia za watu ambao wamebarikiwa.
Neno "ninyi" ni wingi.
"watasema kila aina ubaya dhidi yenu" au "watasema mambo mabaya juu yenu ambayo si ya kweli"
"kwa sababu mwanifuata mimi" au "kwa sababu mwaniamini"
"Furahini" na "kushangilia" humaanisha karibu kitu kile kile. Yesu alitaka wasikilizaji wake sio tu kufurahi bali hata kufanya zaidi kuliko kufurahi kama inawezekana.
Yesu anaanza kufundisha juu ya jinsi wanafunzi wake walivyo kama chumvi na nuru.
Inawezekana kumaanisha 1) kama vile chumvi inavyokifanya chakula kuwa kizuri, mwanafunzi wa Yesu yampasa kuwaathiri watu wa ulimwengu ili kwamba wawe wazuri au 2) kama vile chumvi iwezavyo kutumika kwa kutunza chakula, kadhalika wanafunzi wa Yesu wawalinde watu wasiharibike
"Watu hawawashi taa"
"kuiweka taa chini ya kikapu." Hii ni kusema kuwa ni ujinga kutengeneza nwanga kwa lengo la kuufunika ili watu wasiuone mwanga wa taa.
Hii inamaanisha kuwa wanafunzi wa Yesu wanapaswa kuishi maisha ambayo yatawafnya wengine wajifunze kuhusu ukweli wa Mungu. "Maisha yenu yawe kama nuru iangazayo mbele ya watu.
Ni vizuri zaidi ikitafsiriwa "Baba" kwa maana ya maneno sawa na yale yanayotumika kumaanisha baba wa katika mwili huu.
Yesu anaanza kwa kufundisha jinsi alivyokuja kuitimiliza sheria ya agano la kale
Hii inamaanisha kile walichoandika manabii katika maandiko.
"Nawaambia ukweli" Kirai hiki kinaongeza nguvu juu ya kile Yesu atakachosema baadaye.
Hapa "mbingu" na "dunia" humaanisha ulimwengu wote. "Kama vile mbingu zidumuvyo"
"hapana hata ile herufi ndogo iliyoandikwa au sehemu ndogo ya herufi. Hii ni sitiari inayomaanisha kitu fulani katika maandiko kinachoweza kuonekana kuwa si cha muhimu. "wala sheria zinazoonekana kuwa si za muhimu
Hiki kinaweza kuelezwa kwa kutumia mfumo tendaji. "Mambo yote yametokea" au "Mungu huyafanya mambo yote yatimie".
Kirai cha "kila kitu" kinamaanisha kila kitu kilicho kwenye sheria. "kila kitu kilicho kwenye sheria" au " kila kilichoandikwa kwenye sheria".
"yeyote asiyetii" au "yeyote apuuziaye"
"yeyote kati ya amri hizi, hata zile ndogo kabisa"
Hii inaweza kuelezeka kwa muunda tendaji. "Mungu atamwita mtu huyo" au "Mungu atawaita watu hao".
Kirai hiki kimetumika katika injili ya Mathayo tu. Kama inawezekana tumia "mbingu" katika tafsiri yako. "asiye na umuhimu kabisa kwenye ufalme wa Mungu" au "asiye na umuhimu katika utawala wa Mungu wetu wa mbingunij".
"anayetii amri zote hizi na kuwafundisha wengine kufanya hivyo hivyo"
"wa muhimu zaidi"
Hiki kinaongeza msisitizo kwa kile ambacho Yesu atasema baadaye.
hivi ni viwakilishi vya wingi
Hii inaweza kuelezeka kwa muundo hai. "kwamba haki yenu lazima izidi... ili kuingia"
Yesu anaendelea kufundisha jinsi alivyokuja kutimiliza sheria za agano la kale. Hapa anaanza kufundisha juu ya kuua na hasira
Yesu anawaambia kikundi cha watu juu ya kile ambacho kinaweza kutokea kwao kama watu binafsi. Neno "mme" katika sentensi "mmesikia" na "nawaambia" ni maneno ya wingi. Ile amri ya "usiue"ni ya umoja, lakini unahitaji kuitafsiri katika wingi.
Hii inaweza kuelezeka kwa mfumo tendaji. "Mungu alisema na mababu zetu zamani za kale".
Hapa "hukumu" inamaanisha kuwa hakimu ndiye atakayemhukumu mtu kufa. "Hakimu atamhukumu yeyote amuuaye mtu mwingine"
Neno hili linamaanisha kitendo cha mauji ya kudhamiria, na wala siyo kila aina ya mauji
Kiwakilishi "na" kinatia msisitizo. Hii inamaanisha kuwa kile anachosema Yesu kina umuhimu sawa na amri itokayo kwa Mungu. Jaribu kutafsiri hili kataka mazingira yanayonesha msisitizo.
Neno hili linamaanisha muumini mwenzetu
Inaovyoonekana hapa Yesu hamaanishi hakimu wa kibinadamu bali Mungu anamhukumu mtu mwenye hasira kwa ndugu yake.
Hii ni mizaha kwa watu wasioweza kufifkiri kwa usahihi. "Mtu asiyefaa" ni sawa na "mtu asiye na akili," ambapo "mjinga" inaongezea wazo la kutokuwa mwaminifu kwa Mungu.
Yawezekana hili ni baraza dogo, siyo lile kuu.
Yesu anawaambia kundi la watu juu ya kile kinachoweza kutokea kwao kibinafsi. matukio yote yanayohusiana na viwakilishi "una" na "yako" yametumika katika hali ya umoja, lakini lugha yako inaweza kukutaka utafsiri katika wingi
"kutoa sadaka yako" au "kuleta sadaka yako"
Hii inamaanisha kuwa ni madhabahu ya Mungu iliyo hekaluni kule Yerusalemu, " madhabahuni pa Mungu hekaluni".
"na ukumbuke ukiwa umesimama madhabahuni"
"mtu mwingine ana hasira na wewe kwa sababu ya kile ulichomfanyia"
Hili linaweza kuelezeka katika muundo tendaji. "jambo la kwanza ni kutafuta suluhu"
Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea katika hali ya mtu mmoja. Matukioyote ya viwakilishi vya "uki" na "wako" viko katika umoja, lakini lugha yako inaweza kukutaka uvitafsiri katika wingi.
Huyu ni mtu anayemtuhumu mtu kwa kufanya jambo fulani ambalo ni ovu. Anampeleka mtuhumiwa mahakamani ili kumshitaki kwa hakimu.
Hapa neno "kukuacha mikononi mwa" inamaanisha kukukabidhi katika udhibiti wa mtu mwingine. "kumwachia hakimu ashughulike na wewe".
Hapa neno "kukuacha mikononi mwa" inamaanisha kukukabidhi katika udhibiti wa mtu mwingine. "hakimu atamkabidhi kwa askari"
ni mtu mwenye mamlaka ya kufanya maamuzi ya hakimu.
Hili linaelezeka katika hali ya muundo tendaji. "na askari anaweza kukutupa gerezani"
"Nawaambieni ukweli." Hiki kirai kinaongeza msisitizo kwa kile ambacho Yesu alisema baadaye.
"kutoka gerezani"
Yesu anaendelea kufundisha juu ya jinsi alivyokuja kuitimiliza sheria ya Agano la Kale. Na hapa anaongelea uzinzi na kutamani mwanamke.
Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea katika maisha ya mtu binafsi. Neno "mme..." kutokana na "mmesikia" na "nawaambieni" yametumika katika wingi. Amri ya "Usizini" imetumika katika umoja "usi," lakini unaweza kuitafsiri katika wingi "msi".
Hii inaweza kuelezeka katika muundo tendaji. "kuwa Mungu alisema".
Hili neno ni kitenzi kikuu cha kufanya jambo fulani
Neno "nawa" ni msisitizo. Hii inamaanisha kuwa kile ambacho Yesu anasema kina umhimu sawa na kile kilicho kwenye amri kuu kotoka kwa Mungu. Tafsiri kirai hiki katika namna ambayo inaonesha msisitizo huo. Tazama ilivyotafsiriwa katika 5:21
Sitiari hii inamaanisha kuwa mwanamume amtamaniye mwanamke anahatia sawa na mwanamume aliyefanya uzinzi halisi.
"na kumtamani mwanamke" au "na kutamani kulala naye"
Hapa "moyo" inamaanisha fikra za mtu. "akilini mwake" au "Katika fikra zake"
Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye kwa mtu binafsi Matukio yote ya viwakilishi vya "ku" na "lako" viko katika umoja, lakini unaweza kuvitafsiri katika wingi.
Hapa "jicho" linamaanisha kile ambacho mtu hukiona. Na "kujikwaa". Ni sitiari ya "dhambi." "Kama kile ukionacho hukusababisha kujikwaa" au "kama unataka kufanya dhambi kwa sababu ya kile ukionacho"
Hii inamaanisha jicho au mkono ule wa muhimu zaidi, dhidi ya mkono au jicho la kushoto. Hapa unaweza kutafsri "kulia" kuwa "ndiyo nzuri zaidi" au "kulia pekee."
"litoe kwa nguvu" au "liharibu" kama jicho lako la kulia halijatajwa rasmi, unaweza kuitafsiri hii kama " kuharibu macho yako." kama macho yametajwa, unaweza kuyatafsiri kama "yaharibu"
Yesu analikuza zaidi jambo hili juu ya jinsi ambavyo mtu anapaswa kuiona jinsi dhambi ilivyo mbaya kulichukulia kwa umakini swala hili.
"achana nao"
"upoteze sehemu ya mwili wako"
Hili linaweza kuelezeka katika muundo tendaji. "kuliko Mungu kuutupa mwili wako wote jehanamu"
katika hii lugha ya umbo, mkono unasimama badala ya matendo la mwili wote
Yesu anaendelea kufundisha juu ya jinsi alivyokuja kutimiliza sheria za Agano la kale. Hapa anaanza kwa kufundisha juu ya talaka
Mungu ndiye "alisema." anatumia mfumo tendewa ili kuifanya kuwa laini kuwa si Mungu au neno la Mungu ambalo hakubaliani nalo. Badala yake anasema kuwa talaka inawezekana pale tu sababu ni ya kweli. talaka inaweza isikubalike hata kama mwanamume atatii kuandika hati ya talaka,
hii ni tafisida ya talaka
"lazima ampatie"
Kiwakilishi "mimi" ni cha msisitizo. Hiki kinamaanisha kuwa anachosema Yesu kina umuhimu sawa na amri kuu kutoka kwa Mungu. Jaribu kutafsiri kirai hiki katika namna inayoonesha msisitizo. Tazama ilivyotafsiriwa katika 5:21.
Ni mwanamume anayemtaliki mwanamke bila utaratibu humsababisha kufanya uzinzi" Katika tamadunii nyingi ni kawaida kwake kuolewa tena, lakini kama talaka hiyo haiko sahihi, basi hiyo ndoa ya pili ni batili.
Hii inaweza kuelezeka katika muundo tendaji. "yeye mwanamke baada ya kutalikiwa na mumewe" au "mwanamke aliyetalikiwa"
Yesu anaendelea kufundisha juu ya jinsi alivyokuja kuitimiliza sheria ya Agano la kale. Na hapa anaanza kuongelea juu ya kuapa viapo
Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha ya mtu binafsi. Kiwakilishi "mme" kutokana na "mmesikia" na "nawaambia" viko kataka wingi. na kiwakilishi cha "msi" katika " msiape" na " ni" katika " pelekeni" navyo pia viko katika wingi
"Pia, mme" au "huu ni mfano mwingine. wa kiwakilishi "mme."
Yesu anaweka bayana kuwa anakubaliana na Mungu na neno lake. Lakini, anawaambia wasikilizaji wake wasitimie vile amabvyo si vyao il ikuwashawishi watu kuamini maneno yao. "viongozi wenu wa dini wamewaambieni kuwa Mungu alisema ... viapo vya uongo.
Hi inaweza kumaanisha mambo yafuatayo 1)usiape kwa Mungu kuwa utafanya jambo fulani na usilifanye au 2) Usiape kwa jina la Bwana kuwa unajua kitu fulani kuwa ni kwe ili hali unajua kuwa si kweli.
Kiwaakilishi "na" ni cha msisitizo. Hii inamaanisha kuwa anachosema Yesu kina umuhimu sawa na kile kilicho kwenye amri kuu kutoka kwa Mungu. Kirai hiki kitafsriwe katika namna inayoonesha msisitizo. Tazama ilivyotafsiriwa katika 5:21
Hapa Yesu anamaanisha kuwa mtu asiape katika jambo lolote. inaonekana kuwa kuna mtu aliyekuwa akifundisha kwamba kuapa haina madhara kama mtu ataapa kwa kitu kingine na asikijali kiapo chake kama hakuapa kwa Mungu. ,kama vile kuapa kwa mbingu, dunia, au Yerusalemu. Yesu anasema hata kiapo cha hivyo ni kibaya kwa sababu vyote ni mali ya Mungu.
Kama lugha yako ina muundo wa wingi katika agizo inaweza kutumika hapa. "hamtaapa kwa kwa kiapo cha uongo" waruhusu watu watoe viapo lakini wazuieni viapo vya uongo. "msiape hata kidogo" hii inazuia viapo vya uongo.
Hapa neno "enzi" linamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. "linatokana chanzo hiki kwamba Mungu ni mtawala.
Kirai hiki kinamaanisha kuwa dunia ni mali ya Mungu. "ni kama mahali pa kuweka kiti cha kukanyagia miguu yake"
"kwa maana ni mji unaomilikiwa na Mungu
Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao binafsi. Matukio yote ya viwakilishi hivi viko katika umoja, lakini inakupass kuvitafsiri kama wingi.
Hii inamaanisha kuapa. Tazama ilivyotafsiriwa katika 5:23
kama unamaanisha 'ndiyo.' sema 'ndiyo,' na kama unamaanisha ;hapana,' sema 'hapana,'
Yesu anaendelea kufundisha jinsi alivyokuja kuitimiliza sheria ya Agano la kale. Anaanza kwa kuongelea juu ya kisasi kwa maadui
Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha ya mtu kibinafsi. Kiwakilishi cha "mme" katika "mmesikia" na "mimi nawaambia" viko katika wingi. Kirai hiki "mtu akikupiga" kimesemwa katika umoja "akiku...," lakini unaweza kukitafsiri katika wingi "akiwa..."
Yesu anakubaliana na Mungu na neno lake. Lakini hakubaliani na jinsi viongozi wa dini walivyolitumia neno la Mungu. "Viongozi wenu wa dini wamewambieni kuwa Mungu alisema." Tazama ilivyotafsiriwa katika 5:33
Sheria ya Musa ilimruhusu mtu kumwumiza kwa njia ileile kama alivyomwumiza, lakini hakumwumiza zaidiya kiasi kile
Kiwakilishi cha "mimi" kinaongeza msisitizo. Hii inamaanisha kuwa alichosema Yesu kina umuhimu sawa na ule ulio kwenye amri kuu kuto kwa Mungu. Jaribu kutafsiri kirai hiki katika namna ambayo italeta msisitizo. Tazama ilivyotafsiriwa 5:21.
"ni mtu mwovu" au "mtu yeyote aliyewahi kukuumiza"
Kumpiga mtu upande mmoja wa uso kilikuwa kitendo cha fedheha katika utamaduni wa Yesu. Kama ilivyo katika jicho na mkono, shavu la kulia ni la muhimu, kwa hiyo kukupiga shavu la kulia ilikuwa fedhaha kubwa mno.
"kuzabua," hii inammanisha kupiga kumpiga mtu kofi kwa ubapa wa mkono,
"mwache akupige na shavu jingine pia"
Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha ya watu binafsi. Viwakilishi vyote vya "wewe" na "yako" viko katika umoja kama vile amari za "mwachie," "nenda," "mpatie," na "usimwepuke," lakini waweza kuzitafsiri katika wingi.
Hii "kanzu" ilivaliwa karibu na mwili, kama shati zito au sweta. "kanzu," hili lilikuwa la thamani zaidi kati ya haya mavazi mawili, ilivaliwa juu ya kanzu kwa ajili ya koongeza joto na pia lilitumika usiku kama blanketi.
"mpatie pia huyo mtu"
"na kama mtu," hii inamaanisha kuwa huyu ni askari wa Kirumi.
Hizi na sawa na hatua elfu moja ambao ndiyo umbali ambao askari wa kirumi angeweza kumlazimisha kisheria mtu kubeba kitu kwa ajili yake. Kama maili moja haieleweki, basi inaweza kutafsiriwa kama "kilometa moja" au "umbali mrefu."
Hii inamhusu yule akulazimishaye kwenda.
"uende ile maili anayokulazimisha kwenda, halafu nenda maili nyingine. kama "maili" haieleweki tumia kilometa mbili" au "mara mbili ya mwendo."
"usikatae kumpatia."hii inaweza kuelezeka kwa kutumia muundo halisi. "na umpatie"
Yesu anaendelea kufundisha jinsi alivyokuja kuitimiliza sheria ya Agano la Kale. Hapa anaanza kufundisha juu ya kuwapenda maadui.
Yesu anaongea na makutano juu ya kile kianachoweza kutokea kwao katika maisha yao kibinafsi. "Utampenda ... na kumchukia adui yako" maneno haya yametumika katika hali ya umoja, lakini unaweza kuyatafsiri katika wingi. Matukio mengine ya viwakilishi vya "u" na vile vya amri ya "umpende" na "omba viko katika wingi.
Yesu anakubaliana na Mungu na neno lake. Lakini hakubaliani na jinsi viongozi wa dini wanvyolitumia neno la Mungu. Hili linaweza kuelezeka katika muundo tendaji. "viongozi wenu wa dini wamewaambia kwamba Mungu alisema" Tazama ilivyotafsiriwa 5:33
Neno "jirani" hapa linamaanisha mtu ndani ya jamii ile ile au watu wa kundi moja ambao mtu hutamani na anapaswa kumtendea kwa upole. Haimaanishi mtu anayeishi karibu. Unaweza kutafsiri katika wingi.
Kiwakilishi "na.." kinatia msisitizo. Hii inaonesha kuwa kile anachokisema Yesu kina Uzito sawa na kile kilicho kwenye amri kuu ya Mungu.Jaribu kutafsiri kirai hiki kwa kutia msisitizo. Tazama ilivyotafsirwa katika 5:21
Ni vizuri kutafsiri "wana" katika lugha ambayo kwa asili hutumika kumaanisha baba wa watoto wa kimwili.
Hiki ni cheo cha muhimu cha Mungu
Yesu anamaliza kufundisha juu ya jinsi alivyokuja kuitimiliza sheria ya Agano la kale. Kipengere hiki kinaanzia 5:17
Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao kibinafsi. Matukio yote ya viwakilishi vya "mki.." na "zenu" viko katika wingi. Maswali katika mistari hii ni yale usemaji ambao pengine si lazima kujibiwa
Hili ni neno la jumla kwa ajili ya kuwatamanisha wasikilizaji.
Hiki ni cheo cha muhimu cha Mungu
Walio masikini wa roho wamebarikiwa kwa kuwa ufalme wa mbinguni ni wao.
Wale ambao wanahuzunika wamebarikiwa kwa sababu watafarijiwa.
Wanyenyekevu wamebarikiwa kwa sababu watarithi nchi.
Wenye kiu na njaa ya haki wamebarikiwa kwa sababu watashibishwa.
Wale ambao wanatukanwa na kuteswa kwa ajili ya Yesu wamebarikiwa kwa sababu thawabu yao mbinguni ni kubwa.
Nuru ya waumini huangaza mbele ya watu kwa kufanya matendo mema.
Yesu alikuja kutimiza sheria na manabii wa Agano la Kale.
Wale ambao wazishikao amri na kuzifundisha kwa wengine wataitwa wakubwa katika ufalme wa mbinguni.
Yesu alifundisha kwamba si tu wale ambao wanaua, bali pia wale wanaowachukia ndugu zao wako katika hatari ya hukumu.
Yesu alifundisha kwamba tunapaswa kumwendea na kupatanishwa na ndugu yetu kama ana jambo lolote dhidi yetu.
Yesu alifundisha kwamba tunapaswa kukubaliana na mshtaki wetu kabla ya kufika mahakamani.
Yesu alifundisha kuwa haikuwa tu sahhi kuzini, bali pia kumtamani mwanamke.
Yesu alisema kwamba yatulazimu kukiondoa kitu chochote kile kinacho tusababisha kutenda dhambi.
Kwa swala la zinaa aliruhusu talaka.
Mume anamsababisha mke wake kuwa mzinzi kama atamwacha isivyo sitahili na kuolewa tena.
Yesu anasema kwamba badala ya kuapa viapo kwa vitu hivi vyote tunapaswa kusema ndio kuwa ni ndio au hapana kuwa ni hapana.
Yesu anasema badala ya kuapa kwa vitu tunapaswa maneno yetu yawe "Ndiyo, ndiyo" au "Hapana, hapana"
Yesu alifundisha kwamba hatupaswi kumpinga yule ambaye ni mbaya kwetu.
Yesu alifundisha kwamba tunapaswa kuwapenda na kuwaombea maadui wetu na wale wanao tutesa.
Yesu lisema kwamba kama tunawapenda tu wale ambao wanatupenda sisi, hatupokei thawabu kwa sababu tunafanya tu kile Wamataifa tayari wanafanya.
1Zingatia kutotenda matendo ya haki mbele ya watu ili kujionyesha, vinginevyo hutapata thawabu kutoka kwa Baba aliye mbinguni.2Hivyo basi unapotoa usipige tarumbeta na kujisifu mwenyewe kama wanafiki wanavyofanya katika masinagogi na katika mitaa, ili kwamba watu wawasifu. Kweli nawaambia, wamekwisha kupokea thawabu yao.3Lakini wewe unapotoa, mkono wako wa kushoto usijue kinachofanywa na mkono wa kulia,4ili kwamba zawadi yako itolewe kwa siri. Ndipo Baba yako aonaye sirini atakupatia thawabu yako.5Na unapokuwa ukiomba, usiwe kama wanafiki, kwa kuwa wanapenda kusimama na kuomba kwenye masinagogi na kwenye kona za mitaani, ili kwamba watu wawatazame. Kweli nawaambia, wamekwishapokea thawabu yao.6Lakini wewe, unapo omba, ingia chumbani. Funga mlango, na uombe kwa Baba yako aliye sirini. Ndipo Baba yako aonaye sirini atakupatia thawabu yako.7Na unapokuwa ukiomba, usirudie rudie maneno yasiyo na maana kama mataifa wanavyofanya, kwa kuwa wanafikiri kwamba watasikiwa kwa sababu ya maneno mengi wanayosema.8Kwa hiyo, usiwe kama wao, kwa kuwa Baba yako anatambua mahitaji yako hata kabla hujaomba kwake.9Hivyo basi omba hivi: ‘Baba yetu uliye mbinguni, ulitukuze jina lako.
Mathayo 6 inaendelea na mafundisho ya Yesu yaliyojulikana kama "Mahubiri ya Mlimani."
Labda mtafsiri atapenda kulitenga sala katika 6:9-11 kwa kutumia uingizaji. Kwa kuwa sura hii hubadilika haraka kutoka kwa mada moja hadi nyingine, inawezekana kutumia mstari wa nafasi kati ya mada tofauti ili kuwasaidia wasomaji kutambua mabadiliko katika mada kwa urahisi zaidi.
Yesua anaendelea kufundisha wanafunzi wake katika mafundisho ya mlimani yanayoanzia 5:1.Katika sehemu hii, Yesu anahutubia juu ya "matendo ya haki" ya utoaji sadaka, maombi, na kufunga.
Yesu anaongea na makutano juu kile kinachoweza kutokea kwao baadaye katika maisha yao binafsi. viwakilishi vyote vya "ni" na " yao" viko katika wingi.
Hii ilimaanisha kuwa wale wanaomuona mtu huyo watamheshimu. Hili linaweza kuelezeka katika mfumo tendaji. "mbele ya watu kwa kusudi la kutazamwa na watu ili wakupe heshima kwa kile ulichofanya."
"Ninakuambia ukweli." Huu msemo unaongeza na kusisitiza kile ambacho Yesu atakisema baadaye.
Hii ni sifa muhimu ya Mungu
Kirai hiki kina maanisha kitendo cha kukusudia kupata usikivu wa watu. "Usijipatie usikivu wa watu kwa lengo binafsi kama mtu anayepiga panda katikati ya watu.
"Nawaambia ukweli." Kirai hiki kinaongeza msisitizo wa kile Yesu atakachokisema baadaye.
Yesu anaendelea kuwafundisha wanafunzi wake juu ya sadaka
Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea kwao baadaye katika maisha binafsi. Viwakilishi vya "wewe" na " ""wako" viko katika wingi.
Huu ni msemo unaonyesha usiri. Kama vile mikono inavyofanya kazi pamoja na inasemekana "kujua" kila kitu kinachofanywa kwa wakati wote, hivyo hata watu wako wa karibu wasijue unapotoa msaada kwa maskini
Hii inaweza kuelezeka kwa mfumo tendaji "utawapa maskini pasipo watu wengine kujua."
Yesu anaanza kufundisha juu ya maombi
Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha binafsi.. Viwakilisha vya "una" na "yao" katika mstari wa 5 na 6 viko katika wingi: katika mstari wa 6 viko katika umoja lakini waweza kuvitafsiri katika wingi.
Inamaanisha kwamba wale wanaowatazama watawapa heshima. Hii inaweza kuelezeka kwa mfumo tendaji"ili kwamba watu wawatazame wao na kuwapa heshima."
ukweli ninakuambia." Huu msemo jnaongeza na kusisitiza kile ambacho Yesu atakisema baadaye'
"nenda sehemu ya usiri" au "nenda sehemu ambayo utakuwa peke yako"
Tafsiri inayowezekana ni 1) hakuna anayeweza kumwona Mungu au 2) Mungu yuko sehemu ya siri pamoja na mtu anayeomba.
Hii ni sifa muhimu ya Mungu
Baba yako ataona kile ufanyacho sirini"
"kurudia maneno yasiyo na maana"
Hii inaweza kuelezeka kwa mfumo tendaji. "miungu yao ya uongo itawasikiliza"
sara ndefu" au "maneno mengi"
Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha binfsi. anawaambia kama kundi kwa kutumia wingi kama vile "ombeni hivi." viwakilishi vyote vya "lako" baada ya "baba yetu uliye mbinguni" viko katika umoja.
Hii ni sifa muhimu ya Mungu
Hapa "jina" linamaanisha Mungu mwenyewe. "linamfanya kila mmoja kujua yeye ni mtakatifu."
Hapa "ufalme" inamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. AT: "Waweza kutawala juu ya yote na kila kitu kikamilifu"
Hii inaweza kuelezeka kwa mfumo hai. AT: "Kila mmoja duniani atii mapenzi yako kama wanavyofanya kila mmoja huko mbinguni."
Mionekano ya viwakilishi vya "nasi," "utu," "wetu" unaonesha makutano ambao Yesu alikuwa akiwahutubia.
Hapa "mkate" inamaanisha chakula kwa ujumla,
Deni ni kile ambacho mtu anamdai mwingine. Huu ni msemo wa dhambi.
Mdai ni mtu ambaye anadai deni kwa mwingine. Huu ni msemo kwa wenye dhambi.
Neno "majaribu" jina la kitenzi, inaweza kuelezwa kama kitenzi. "usituletee kitu chochote cha kutujaribu" au "usituletee kitu cha kutufanya tushawishike na dhambi"
viwakilishi vyote vya "mta" na "yako" ni vya wingi. hata hivyo, Yesu anawaambia kile kitakachotokea baadaye katika maisha binafsi kama kila mmoja hatasamehe wengine
"makosa" au "dhambi"
Hii ni sifa muhimu ya Mungu
Yesu anaanza kufundisha juu ya kufunga
Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea katika maisha yao binafsi. Viwakilishi vyote vya "una" na "zao" katika mstari wa 17 na 18 viko katika umoja, lakini vinaweza kutafsiriwa katika wingi ili vioane na kile cha "wa" katika mstari wa 16.
"Zaidi ya"
Wanafiki hawakuosha nyuso zao au kuchana nywele zao. Walifanya hivyo makusudi kuvuta hisia zao ili kwamba watu wawatazame wao na kuwapa heshima kwa sababu ya kufunga.
"Ukweli ninakuambia." Huu msemo unaongeza na kusisitiza kile ambacho Yesu atakiongea baadaye.
"paka mafuta kwenye nywele zako" au "tengeneza nywele zako" Kutunza kichwa hapa ni hali ya kawaida ya kutunza nywele. Halina uhusiano na "Kristo" ikimaanisha "mpakwa mafuta" Yesu alikuwa anamaanisha kwamba watu wanapaswa kuonekana kawaida haijalishi wamefunga au hawakufunga.
Tazama unavyotafsiri hii kwenye 6:5
Hii ni sifa muhimu ya Mungu
"Aonaye kile unachokifanya unapokuwa pekee yako" Tazama ilivyotafsriwa katka 6:5
Yesu anaanza kufundisha juu ya fedha na mali
Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao binafsi. viwakilishi vya "usi" na "yako" viko katika wingi isipokuwa vile vya mstari wa 21, amabvyo viko katika umoja.
"utajiri"
"ambapo nondo na kutu wanashambulia akiba"
mdudu mdogo, anayeruka na kuharibu nguo
ni vitu vya rangi ya kahawia vinavyopatikana kwenye chuma
Huu ni msemo ambao unamaanisha kwamba fanya mambo mazuri hapa duniani ili Mungu akubariki mbinguni.
Hapa "moyo" maana yake ni mawazo ya mtu na mapenzi yake.
Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao binafasi. viwakilishi vya "yako" vimo katika umoja lakini waweza kuvitafsiri katika wingi.
Hii inalinganisha macho mazima ambayo yanamwezesha mtu kuona macho mabovu ambayo yanasababisha mtu kuwa kipofu. Huu ni msemo unaomaanisha uzima wa kiroho. Mara nyingi, wayahudi walitumia msemo "macho mabaya" wakimaanisha uovu. Maana yake ni hii ikiwa mtu amejitoa kwa Mungu na kuona vitu vinafanyika kwa njia hiyo wanafanya vizuri. Endapo mtu ana tamaa ya utajiri wa vitu vingine hivyo anafanya uovu.
Unaweza kutafsiri kwa wingi, "macho"
Hii aimanishi maajabu. Wayahudi mara zote walitumia msemo huu kwa mtu ambaye ni mwovu.
Yote kwa pamoja kimsingi yana maana moja. Yanasisitiza kwamba mtu hawezi kupenda na kujitoa kwa Mungu na fedha kwa wakati mmoja.
"Huwezi kumpenda Mungu na fedha kwa wakati mmoja"
Hapa viwakilishi vya "ku" na "yako" vyote viko katika wingi
Hii inaongeza msisitizo kwa kile atakachosema Yesu baadaye
Yesu anaongea kwa kikundi cha watu kuhusu kitakachotokea kwao kwa mtu binafsi. Anapotumia "kwako" na "wako" yote ni wingi.
Yesu anatumia swali kufundisha watu. "uhakika maisha ni zaidi ya kile unachokula, na mwili wako ni zaidi ya kile unachovaa."
sehemu ya kutunza mazao
Hii ni sifa muhimu ya Mungu
Yesu anatumia swali kufundisha watu. "uhakika ninyi mna thamani zaidi ya ndege."
Yesu ansema na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea kwao katika maisha binafsi.viwakilishi vya "mwenu" na "yake" vimo katika wingi.
Yesu anatumia swali kufundisha watu. Anamaanisha hakuna atakayeishi maisha marefu kwa kuwa na hofu.
"inchi" ni pungufu ya mita. Hapa ni msemo wa kuongeza kiasi cha miaka mingapi ya kuishi mtu.
Yesu anatumia swali kufundisha watu. AT:"Usiwe na hofu kuhusu nini utavaa."
'Zingatia"
aina ya maua ya porini
Hii inaongeza msisitizo wa kile ambacho Yesu ataongea baadae
Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai. AT:"hakuvaa nguo nzuri kama haya maua."
Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao kibinafsi. viwakilishi vya "ninyi" na "wenye" vimo katika wingi.
Huu ni msemo ukiwa na maana Mungu anayapendezesha maua
Ikiwa lugha yako ina neno linalohisi "majani" na neno ulilotumia kwa "maua" kwa mstari uliopita, unaweza kutumia hapa.
Wayahudi tena walitumia majani kwa moto na kupikia vyakula vyao. Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai. "mtu mmoja alitupa katika moto" au "mtu mmoja alichoma"
Yesu anatumia swali kufundisha watu.AT: yeye hakika atawavisha ninyi...imani."
"ninyi ambao mna imani ndogo." Yesu anawatuhumu watu kwa sababu walikuwa na imani ndogo na Mungu.
"Kwa sababu ya hayo yote"
"kwa mataifa wanajali san juu ya kile watachokula, kunywa na kuvaa"
Yesu anamaanisha kwamba Mungu atahakikisha mahitaji ya muhimu mnapata
Hii ni sifa muhimu ya Mungu
Hapa "ufalme" inamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. "umaanishe mwenyewe katika kumtumikia Mungu, ambaye ni mfalme wako, na ufanye yaliyo haki."
Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai.AT: "Mungu atakupatia hayo yote wewe."
"Kwa sababu ya hayo yote"
Yesu anafafanua "kesho" kama mtu ambaye anaweza kuhofu. Yesu anamaanisha kwamba mtu anaweza kuhofu endapo siku inayofuata imefika.
"kila siku huwa ina mabaya yake yakujitosheleza" au "Kila siku ina matatizo yake ya kutosha"
Wale wanaofanya matendo ya haki ili watazamwe na watu wanapokea sifa kutoka kwa watu kama thawabu yao.
Tuapaswa kufanya matendo yetu ya haki katika faragha.
Wale wanaoomba kinafiki ili watu wawaone wanapokea thawabu yao kutoka kwa watu.
Wale waombao katika faragha wanapokea thawabu kutoka kwa Baba.
Yesu anasema tusiombe kwa kurudia maneno yasiyo na maana kwa sababu Baba anajua kitu gani tunahitaji hata kabla hatujamwomba yeye.
Tumwombe Baba ili mapenzi yake yafanyike hapa duniani kama yanavyofanyika mbinguni.
Kama hatutawasemehe wengine makosa yao, Baba yetu hatusamehe makosa yetu.
Tunapaswa kufunga bila kuonyesha watu kama tumefunga na ndipo Baba atatupatia thawabu.
tunapaswa kutunza hazina zetu mbinguni kwa sababu haziwezi kuharibiwa au kuibiwa.
Mioyo yetu itakuwepo mahali zilipo hazina zetu.
Lazima tuchague kati ya Mungu na utajiri kama mabwana zetu.
Hatupaswi kuwa na hofu kuhusu chakula,vinywaji na mavazi kwa vile Baba anawalinda na kuwatunza ndege, na nasi tuna thamani zaidi kuliko wao.
Yesu anatukumbusha sisi kwamba hatuwezi kuongeza kipimo kimoja cha maisha ya kuishi kwa kuwa na wasiwasi
Ni lazima tutafute kwanza ufalme na haki ya Baba na baada ya hapo mahitajiyetu yote ya mwilini tutapatiwa.
1Usihukumu, nawe usije ukahukumiwa.2Kwa hukumu unayohukumu, nawe utahukumiwa. Na kwa kipimo unachopima na wewe pia utapimiwa hicho hicho.3Na kwa nini unatazama kipande cha mti kilichoko kwenye jicho la ndugu yako, lakini hutambuwi kipande cha gogo ambalo limo katika jicho lako?4Unawezaje kusema kwa ndugu yako, ngoja nikutolee kipande kilichomo kwenye jicho lako, wakati kipande cha gogo kimo ndani ya jicho lako?5Mnafiki wewe; kwanza toa gogo lililomo kwenye jicho lako, na ndipo utakapoweza kuona vizuri na kukitoa kipande cha mti kilichomo kwenye jicho la ndugu yako.6Usiwape mbwa kilicho kitakatifu, na usiwarushie nguruwe lulu mbele yao. Vinginevyo wataviharibu na kuvikanyaga kwa miguu, na tena watakugeukia wewe na kukurarua vipande vipande.7Omba, nawe utapewa. Tafuta, nawe utapata. Bisha hodi, na wewe utafunguliwa.8Kwa yeyote anayeomba, hupokea. Na kwa yeyote anayetafuta, hupata. Na kwa mtu ambaye anayebisha hodi, atafunguliwa.9Au kuna mtu miongoni mwenu ambaye, ikiwa mtoto wake akimwomba kipande cha mkate atampa jiwe?10Au ikiwa atamwomba samaki, na yeye atampa nyoka?11Kwa hiyo, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu zawadi nzuri, Je! Ni kiasi gani zaidi Baba aliye mbinguni atawapa vitu vizuri wale wanao muomba yeye?12Kwa sababu hiyo, unapotaka kufanyiwa kitu chochote na watu wengine, nawe pia itakupasa kuwafanyia hivyo hivyo wao. Kwa kuwa hiyo ni sheria na manabii.13Ingieni kwa kupitia geti jembamba. Kwa kuwa geti ni pana na njia ni pana inayoongoza kwenye uharibifu, na kuna watu wengi wanaopitia njia hiyo.14Njia ni jembamba, njia inayongooza katika uzima na ni wachache wanaoweza kuiona.15Jihadhari na manabii wa uongo, wanaokuja wamevaa ngozi ya kondoo, lakini kweli ni mbwa mwitu wakali.16Kwa matunda yao mtawatambua. Je watu wanaweza kuvuna matunda kwenye miba, au mtini kwenye mbengu ya mbaruti?17Kwa jinsi hiyo, kila mti mzuri huzaa matunda mazuri, lakini mti mbaya huzaa matunda mabaya.18Mti mzuri hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri.19Kila mti ambao hauzai matunda mazuri utakatwa na kutupwa katika moto.20Hivyo basi, utawatambua kutokana na matunda yao.21Si kila mtu aniambiaye mimi, ‘Bwana, Bwana,’ ataingia katika ufalme wa mbinguni, bali ni yule pekee atendaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.22Watu wengi wataniambia siku hiyo, ‘Bwana, Bwana, hatukutoa unabii kwa jina lako, hatukutoa mapepo kwa jina lako, na kwa jina lako tulifanya matendo mengi makuu?’23Ndipo nitawaambia wazi, ‘Sikuwatambua ninyi! Ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu!’24Kwa hiyo, kila mmoja asikiaye maneno yangu na kutii atafanana na mtu mwenye hekima aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba.25Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, na upepo ukaja na ukaipiga nyumba hiyo, lakini haikuweza kuanguka chini, kwa kuwa ilikuwa imejengwa juu ya mwamba.26Lakini kila mtu anayesikia neno langu na asilitii, atafananishwa na mtu mpumbavu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga.27Mvua ikaja, mafuriko yakaja, na upepo ukaja na kuipiga nyumba hiyo. Na ikaanguka, na uharibifu wake ukakamilika.”28Ulifika wakati ambao Yesu alipomaliza kuongea maneno haya, makutano walishangazwa na mafundisho yake,29kwa kuwa alifundisha kama mtu mwenye mamlaka, na si kama waandishi wao.
Kwa kuwa sura hii hubadilika haraka kutoka kwa mada moja hadi nyingine, inawezekana kutumia mstari wa nafasi kati ya mada ili kutofautisha kati yao kwa urahisi zaidi.
Mathayo 5-7 kwa pamoja huunda mahubiri au mafundisho ya Yesu. Mgawanyiko wa sura husababisha kuchanganyikiwa hapa.
Matunda ni taswira ya kawaida katika maandiko. Inatumika kuelezea matokeo ya tabia nzuri au mbaya. Katika sura hii, matunda mazuri ni matokeo ya kuishi kama Mungu anavyoamuru.
Yesu anaendelea kuwafundisha wanafunzi wake katika mahubiri ya mlimani, yanayoanzia 5:1
Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea kwao baadaye katika maisha binafsi. viwakilishi vya "nawe" na amri viko katika wingi.
Inamaanisha hapa kwamba "hukumu" ina maana ya msingi kuwa "kushutumu vibaya" au "kutangaza kosa"AT:"Usishutumu watu vibaya."
Hii inaweza kutafsiriwa kwa mfumo hai.AT:"Mungu hawezi kukushutumu wewe vibaya."
Uwe na uhakika msomaji anaelewa maelezo ya mstari wa 7:2 uwe na msingi alichokisema Yesu katika wa 7:1
Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai.AT: "Mungu atakushutumu wewe hivyo hivyo kama
Tafsiri inayowezekana ni 1) hii ni kipimo cha hukumu unayopewa au 2) hiki ni kiwango kinachotumika kwa kuhukumu.
Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai. "Mungu atatumia kipimo hicho kwako."
Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao binafasi. viwakilishi vya "u" na "yako" vimo katika umoja lakini vinaweza kutafsirika katika wingi.
Yesu anatumia maswali yote kufundisha na kutoa changamoto kwa watu. Yeye anataka wao wajiangalie dhambi zao kabla ya kuangalia dhambi za mtu mwingine.
ni msemo
Hii inamaanisha mkristo mwenzako, siyo kaka halisi au jirani
Sehemu ya kipande kikubwa cha mti ambacho mtu amekikata chini. Ni kipande cha ubao kwa mbali kikubwa kiualisia kimeingia kwenye jicho la mtu. Huu ni msemo muhimu kwa mtu mwenye makosa
Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao binafsi. viwakilishi vya "u" na "yao" viko katika wingi.
Wayahudi waliwachukulia wanyama hawa kuwa wachafu, na Mungu aliwaambia wayahudi wasiwale. Huu ni msemo kwa watu waovu ambao hawathamini vitu vitakatifu. Itakuwa vizuri kutafsiri maneno haya kiualisia.
Hiki ni sawa na mviringo,jiwe la thamani au glasi. Ni misemo ya elimu ya Mungu au vitu vyenye ubora kiujumla.
"nguruwe wataviharibu"
"na mbwa watageuka na kurarua"
Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao binafsi. viwakilishi vya "wewe" na "wake" wake katika wingi.
Hii ni misemo ya maombi kwa Mungu. Mfumo wa kitenzi inaonyesha kwamba tuendelee kuomba mpaka yeye ajibu. Ikiwa lugha yako ina mfumo wa kufanya kitu na kurudia rudia tena, unaweza kutumia hapa.
Hii ina maana ya kuhitaji kitu kutoka kwa Mungu
Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai.AT:"Mungu atakupa kile unachotaka."
"Tafuta kutoka kwa Mungu kile unachotaka"
Kugonga mlango ilikuwa njjia ya upole ya kumwomba mtu aliye ndani ya nyumba au chumba afungue mlango.Ikiwa kugonga mlango si kwa upole kwenye utamaduni wenu, tumia neno ambalo linaelezea kwa upole mtu anapotaka kufunguliwa mlango.
Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo tendaji. Mungu atakufungulia kwa ajili yako"
Yesu anatumia swali kufundisha watu. "Hakuna mtu miongoni mwenu ... jiwe,"
Hii inamaanisha chakula kwa ujumla. "chakula"
Haya majina yatafsiriwe kiualisia.
Yesu anauliza swali jingine kufundisha watu. Inaeleweka kwamba yesu alikuwa anarejea mtu na kijana wake. "Na hakuna mtu miongoni mwenu, ikiwa kijana amemwomba samaki, atampatia nyoka."
Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao binafsi. Viwakilishi vya "ninyi" na :wenu" ni vya wingi.
Yesu anatumia swali kujibu watu. "ndipo Baba yenu aliye mbinguni hakika atampa....yeye."
Hii ni sifa muhimu ya Mungu.
kwa njia yeyote lolote unalotaka ufanyiwe na wengine"
Hapa "sheria" na "unabii" kinarejea kile ambacho Musa na manabii walikiandika. kwa kuwa hiki ndicho kile Musa na manabii walifundisha kwenye maandiko."
unapotafsri, tumia neno sahihi la "pana" na la "pana sana" kama yanavyotofautiana na "embamba" kama inavyowezekana ili kukazia tofauti ya hizo jozi za malango na njia.
Hiki ni kivuli cha mtu anayetembea njiani na kuingia kwenye ufalme kwa kupita lango. Ufalme mmoja ni rahisi kuingia na mwingine si rahisi kuingia. Huu ni msemo unaomaanisha kwamba mtu anapaswa kukubali njia ngumu ya maisha ya kumtii Mungu na kupata uzima wa milele. Ikiwa watachagua njia nyepesi ya maisha ya kutomtii Mungu, wataingia kuzimu.
Unatakiwa kuendelea hadi mwisho wa mstari wa 14: "Hivyo basi, ingia kwa kupitia njia nyembamba."
Tafsiri inayowezekana ni 1) hii inarejea langoi la kuingia katika ufalme na njia inayoongoza kwenye lango. Ikiwa hivyo, unaweza kubadilisha mpangalio kinyume kama walivyofanya UDB au 2) "lango" na "njia" vyote vinarejea lango la ufalme. ikiwa hivyo, una haja ya kubadili mpangilio.
Haya majina ya sifa yanaweza kutafsiriwa kwa vitendo. "katika eneo ambalo utakufa.... katika eneo ambalo utaishi."
"jilindeni na"
Huu msemo una maana manabii wa uongo watajifanya wazuri na kutaka kuwasaidia, lakini kwa ualisia ni waovu na watawadhuru.
Huu msemo unarejea matendo ya mtu. "Kama vile unavyofahamu mti kwa tunda linalotokea, utamtabua nabii wa uongo kwa matendo yao."
Yesu anatumia swali kujibu watu. Watu wangetambua kwamba jibu siyo. "watu hawezi kuvuna...miba."
Yesu anaendelea kutumia msemo wa tunda akimaanisha nabii mzuri ambaye anafanya kazi nzuri au maneno mazuri.
Yesu anaendelea kutumia mfano wa matunda kwa kurejea kwa nabii mbaya ambaye anafanya kazi ya uovu.
Yesu anaendelea kutumia mti wa matunda kama msemo akimaanisha manbii wa uongo. Hapa, yeye anaongelea kile kitakachotokea kwa mti mbaya. Ikimaanisha kwamba kitu hicho kitafanyika kwa manabii wa uongo.
Hii inaweza kuelezeka kwa mfumo hai. "mtu ataukata chini na kuuchoma."
Neno "yao" inaweza kurejea labda manabii au miti. Huu msemo unamaanisha kwamba matunda ya mti na matendo ya manabii yote yanafunua kuwa yaweza kuwa mabaya au mazuri. Kama ikiwezekana, unaweza kutafsiri ikimaanisha maana moja kati ya hayo'
Hapa "ufalme" inamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. Msemo "ufalme wa mbinguni" umetumika pekee katika kitabu cha mathayo. Ikiwa inawezekana, andika "mbingu" katika tafsiri yako. "wataishi pamoja na Mungu mbinguni pindi atakapojifunua kuwa mfalme."
"wale wanaotenda kile ambcho Baba yangu anataka"
Hii ni sifa muhimu ya Mungu
Yesu alisema "siku hiyo" akijua wasikilizaji walielewa alichomaanisha siku ya hukumu. Unaweza kuhusisha "siku ya hukumu" endapo tu wasikulizaji wako hawatakuelewa vinginevyo.
Watu walitumia maswali kusisitiza kwamba walifanya mambo hayo. "tulitabiri..tulitoa pepo...tulifanya miujiza mingi."
Hii "sisi" haimuhusishi Yesu.
Hapa "jina" maana yake katika nguvu na mamlaka ya Yesu
"miujiza"
Hii ina maana mtu huyu si wa Yesu."Wewe si mfuasi wangu" au "Sina kitu cha kufanya pamoja nawe"
"Kwa sababu hiyo"
Hapa "maneno" yanarejea kile ambacho Yesu alisema
Yesu analinganisha wale wanaotii neno lake na mtu aliyejenga nyumba ambayo haitazulika na kitu.
Huu ni mwamba mbaya chini ya mchanga ulio juu na udongo, sio jiwe kubwa au mpaka juu ya ardhi.
Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo tendaji. "yeye alijenga"
Huu ndio mwisho wa mahubiri ya Yesu ya mlimani yanayoanzaia 5:1
Yesu aliendelea kutumia mlinganyo kutoka mstari uliopita. Yeye analinganisha wale ambao hawatii neno lake na mpumbavu aliyejenga nyumba. Mpumbavu pekee aweza kujenga nyumba juu ya mchanga ambapo mvua,mafuriko na upepo vinaweza kuhamisha mchanga.
Tumia neno la ujumla kwa lugha yako ambalo linaelezea kilichotokea wakati nyumba inaanguka chini.
Mvua,mafuriko na upepo hakika yaliangamiza nyumba.
Mistari hii inafafanua jinsi watu katika makutano walivyoyapokea mafundisho ya Yesu ya mlimani.
Huu usemi unaonyesha hitimisho la hotuba ya mlimani.
iko wazi katika 7:29 kwamba walishangazwa si kwa sababu ya alichofundisha Yesu bali pia jinsi alivyofundisha . "walishangazwa kwa jinsi alivyoweza kufundisha."
Ni lazima kwanza kujihukumu wenyewe na kutoa gogo kwenye macho yako kabla ya kusaidia ndugu zetu.
Tunapaswa kwanza kujihukumu wenyewe na kuondoa gogo kutoka kwenye macho yetu ndipo tuweze kumsaidia ndugu yetu.
Endapo utawapa kitu kitakatifu mbwa, watakivuruga hicho na tena kukugeukia na kukularua vipande.
Lazima tuombe, tutafute na kubisha ili kupokea kutoka kwa Baba.
Mungu anawapa vitu wale wanaomwomba.
Sheria na manabii inatufundisha kuwatendea wengine matendo ambayo nasisi tunapenda watu tutendewe
Njia pana inaongoza kwenye uharibifu
Tunaweza kuwatambua manabii wa uongo kwa matunda ya maisha yao.
Wale wanaofanya mapenzi ya Baba wataingia katika ufalme wa mbinguni.
Yesu atawaambia " sikuwatambua ninyi! Ondokeni kwangu , ninyi watenda mabaya"!
Yule anayesikia maneno ya Yesu na kuyatii ni kama mtu mwenye hekima.
Yule anayesikia maneno ya Yesu na asiyatii ni kama mtu mpumbavu.
Yesu aliwafundihsa watu kama mtu mwenye mamlaka , si kama waandishi.
1Wakati Yesu aliposhuka chini kutoka mlimani, umati mkubwa ulimfuata.2Tazama, mkoma alikuja na kusujudu mbele yake, akasema, “Bwana, ikiwa uko tayari, unaweza kunifanya niwe safi.”3Yesu akanyoosha mkono wake na kumgusa, akasema, “Niko tayari. Uwe msafi.” Hapo hapo alitakaswa ukoma wake.4Yesu akamwambia, “Angalia kwamba usiseme kwa mtu yeyote. Shika njia yako, na jioneshe mwenyewe kwa kuhani na utoe zawadi ambayo Musa aliagiza, kwa ajili ya ushuhuda kwao.”5Wakati Yesu alipofika Kapernaumu, jemedari akaja kwake akamuuliza6akisema, “Bwana, mtumishi wangu amelala nyumbani amepooza na ana maumivu ya kutisha.”7Yesu akamwambia, “Nitakuja na kumponya.”8Jemedari akajibu na kumwambia, “Bwana, mimi si wathamani hata uje na kuingia ndani ya dari yangu, sema neno tu na mtumishi wangu ataponywa.9Kwa kuwa mimi pia ni mtu niliye na mamlaka, na ninao askari walio chini yangu. Nikisema kwa huyu ‘Nenda,’ na huenda, na kwa mwingine ‘Njoo,’ na yeye huja, na kwa mtumishi wangu, ‘Fanya hivi,’ na yeye anafanya hivyo.”10Wakati Yesu aliposikia haya, alishangazwa na kuwaambia wale waliokuwa wakimfuata, “Kweli ninawaambia, sijapata kuona mtu mwenye imani kama huyu katika Israel.11Ninawaambieni, wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, wataketi katika meza pamoja na Abrahamu, Isaka, na Yakobo, katika ufalme wa mbinguni.12Lakini watoto wa ufalme watatupwa katika giza la nje, ambapo kutakuwa na kilio na kusaga meno.”13Yesu akamwambia jemedari, “Nenda! Kama ulivyokwisha amini, na itendeke hivyo kwako.” Na mtumishi aliponywa katika saa hiyo.14Wakati Yesu alipofika kwenye nyumba ya Petro, alimwona mama mkwe wake na Petro amelala akiwa mgonjwa wa homa.15Yesu akamgusa mkono wake, na homa yake ikamwacha. Kisha akaamka akaanza kumhudumia.16Na ilipofika jioni, watu wakamletea Yesu wengi waliotawaliwa na pepo. Akawafukuza pepo na wale walio wagonjwa akawaponya.17Kwa jinsi hii yalitimia yale yaliyo kwisha kunenwa na Isaya nabii, “Yeye mwenyewe alichukua magonjwa yetu na alibeba maradhi yetu.”18Kisha Yesu alipoliona kusanyiko limemzunguka, alitoa maelekezo ya kwenda upande mwingine wa bahari ya Galilaya.19Kisha mwandishi akaja kwake na kumwambia, “Mwalimu, nitakufuata popote utakapoenda.”20Yesu akamwambia, “Mbweha wana mashimo, na ndege wa angani wana viota, lakini mwana wa Adamu hana sehemu ya kulaza kichwa chake.”21Mwanafunzi mwingine akamwambia, “Bwana, niruhusu kwanza niende kumzika baba yangu.”22Lakini Yesu akamwambia, “Nifuate, na uwaache wafu wazike wafu wao.”23Yesu alipoingia kwenye mtumbwi, wanafunzi wake wakamfuata mtumbwini.24Tazama, ikainuka dhoruba kuu juu ya bahari, kiasi kwamba mtumbwi ulifunikwa na mawimbi. Lakini Yesu alikuwa amelala.25Wanafunzi wakaja kwake na kumwamsha wakisema, “Bwana, tuokoe sisi, tunaelekea kufa!”26Yesu akawaambia, “Kwa nini mnaogopa, ninyi wenye imani ndogo?” Ndipo akaamka na kuukemea upepo na bahari. Kisha kukawa na utulivu mkuu,27wanaume wakashikwa na mshangao wakasema, “Huyu mtu niwa namna gani, kwamba hata pepo na bahari vinamtii yeye?”28Wakati Yesu alipokuwa amekuja upande mwingine wa nchi ya Magadala, wanaume wawili waliotawaliwa na pepo walikutana naye. Walikuwa wakitokea makaburini na walikuwa wakifanya vurugu sana, kiasi kwamba hakuna msafiri angeweza kupita njia ile.29Tazama, walipaza sauti na kusema, “Tuna nini cha kufanya kwako, mwana wa Mungu? Umekuja hapa kututesa kabla ya wakati kufika?”30Sasa kundi kubwa la nguruwe lilikuwa likichunga, hapakuwa mbali sana walipokuwa,31pepo waliendelea kulalamika kwa Yesu na kusema. “Ikiwa utatuamuru kutoka, tupeleke kwenye kundi la nguruwe.”32Yesu akawaambia, “Nendeni!” Pepo wakawatoka na kwenda kwa nguruwe. Na tazama, kundi lote likashuka kutoka mlimani kuteremkia baharini na lote likafia majini.33Wanaume waliokuwa wakichunga nguruwe walikimbia. Na walipoenda mjini wakaelezea kila kitu, kilichotokea kwa wanaume waliotawaliwa na mapepo.34Tazama, mji mzima ukaja kukutana na Yesu. Walipomwona, walimsihi aondoke kwenye mkoa wao.
Sura hii inaanza sehemu mpya.
Miujiza ya Yesu katika sura hii inaonyesha kwamba ana mamlaka juu ya mambo yanayopita udhibiti wa binadamu. Inaonyesha pia kwamba kumwabudu Yesu ni jibu sahihi kwa matendo yake.
Huu ni mwanzo wa sehemu mpaya ya simulizi ambalo limebeba simulizi nyingi za uponya wa watu. Wazo hili linaendelea hadi hadi 9:35.
"Baada ya Yesu kuja kushuka chini kutoka mlimani, umati mkubwa ulimfuata," Umati yawezekana ulijumuisha watu waliokuwa nae juu mlimani na watu ambao hawakuwahi kuwa nae.
Neno "tazama" inatupa dokezo sisi la mtu mwingine katika hadithi. Lugha inaweza kuwa namna ya kufanya hivyo.
"mtu ambaye ana ukoma" au "mtu ambaye ana ugonjwa wa ngozi"
Hii ni ishara ya unyenyekevu heshima mbele ya Yesu.
"ikiwa unataka kufanya" au "ikiwa unahitaji" mwenye ukoma alijua yesu ana nguvu za kumponya, lakini hakujua endapo Yesu alitaka kumgusa yeye.
Hapa "kusafisha" maana yake kuponywa na ili kuweza kuishi kwenye jamii tena."
"sasa hivi"
Matokeo ya Yesu kusema"Uwe mzima" ilikuwa kwamba mtu huyo akaponywa.Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai.AT:"yeye alikuwa mzima" au "ukoma ulimwacha" au "ukoma ulikoma"
Hii alikuwa anarejea mtu ambaye alimponya
"usiseme kitu chochote kwa mtu yeyote" au "usimwambie mtu yeyote nimekuponya wewe"
Sheria ya wayahudi ililazimu kwamba mtu akaonyeshe ngozi aliyoponywa kwa kuhani, ambaye tena angemruhusu yeye au yule kuwa pamoja na watu wengine.
Sheria ya Musa ililazimu kwamba yeyote aliyeponywa ukoma atoe sadaka ya shukrani kwa kuhani. Endapo kuhani atakubali zawadi, watu watajua kwamba mtu huyo ameponywa.
Hii kwa uhakika inaweza kurejea kwa 1) makuhani au 2) wapingaji wa Yesu. Ikiwezekana, tumia kiwakilishi ambacho kitaonyesha kati ya makundi hayo.
Hapa simulizi hili linabadili mandhari ya muda na eneo na simulizi inakuwa ni ya habari za Yesu akimponya mtu mwingine
Hapa "yeye" anarejea kwa Yesu.
"Asiyeweza kutembea kwa sababu ya ugonjwa"
"Yesu akamwambia jemedari"
"nitakuja nyumbani kwako na kumfanya mtumishi wako apone"
Msemo "kuingia ndani ya dari" maana yake "nyumba yangu"
Hapa "neno" maana yake sema amri.AT: "toa amri"
Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai.AT: "atakuja kuwa mzima"
Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai.AT:"ambaye yuko chini ya mamlaka ya mwingine"
Kuwa "chini" mtu inamaanisha kutokuwa na umuhimu sana na kutii agizo la mtu mwenye umuhimu zaidi.
"mtalaamu wa kupigana"
"Ninawaambia ukweli." Huu usemi unaongeza na kusisitiza kile ambacho yesu atazungumza baadae.
Wasikilizaji wa Yesu wangefikiri kwamba wayahudi katika Israeli, ambao wanadai kuwa ni watoto wa Mungu, watakuwa na imani kuliko yeyote. Yesu anasema hawako sahihi na kwamba imani ya jemedari ilikuwa kubwa.
Hapa "wewe" ni wingi na ina maanisha "wale ambao walikuwa wakimfuata yeye"
Unapotumia kinyume "mashariki" na "magharibi" ni njia ya kusema "kila mahali," "kutoka kila mahali" au "kutoka mbali kila upande"
watu katika utamaduni walikaa chini pembeni ya meza wakiwa wanakula. Huu msemo unaonyesha kwamba wale walio mezani ni familia na marafiki wa karibu. "ishi kama familia na rafiki."
Hapa "ufalme" ina maanisha utawala wa Mungu kama mfalme. Msemo "ufalme wa mbinguni" umetumika katika kitabu cha Mathayo. Ikiwezekana, andika "mbinguni" katika tafsiri yako. "wakati Mungu wetu mbinguni anaonyesha kwamba yeye ni mfalme."
Hii inaweza kuelezwa katika mfumo hai. "Mungu atawatupa watoto katika ufalme."
Usemi "watoto wa"ina maanisha wale ambao wanamikiwa na kitu fulani, kwa namna hiyo ufame wa Mungu. Kuna kejeli pia hapa kwa sababu "watoto" watatupwa nje wakati wageni watakaribishwa. "wale ambao waliruhusu Mungu awatawale wao."
Haya maelezo yanamaanisha hatua ya mwisho ya milele kwa wale waliomkataa Mungu. "sehemu ya giza mbali kwa Mungu" au "kuzimu"
Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai. "hivyo nitafanya kwa ajili yako wewe"
Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai. "Yesu alimponya mtumishi"
kwa muda ule Yesu alisema yeye atamponya mtumishi."
Hapa simulizi inabadili mandhari ya muda na eneo. simulizi inakuwa ni ya Yesu akimponya mtu mwingine
Hawa wanafunzi yawezekana walikuwa na Yesu, lakini mtazamo wa hadithi Yesu alisema nini na kufanya nini, hivyo watambulishe wanafunzi pekee ikiwa inalazimika kuepusha maana ya uongo.
Mkwe - "mama wa mke wa Petro"
Ikiwa lugha yako itaelewa msemo kuwa homa inaweza kufikiri na kutenda yenyewe, hii inaweza kutafsiriwa kama "yeye akawa mzima" au "Yesu akamponya yeye:
"akaamka toka kitandani"
Mandhari yanahamia katika muda wa jioni ambapo Simulizi inakuwa ya Yesu kuponya watu zaidi na kufukuza mapepo..
Katika mstari wa 17, mwadishi anamnukuu nabii Isaya il ikuonesha kuwa huduma ya Yesu ilikuwa kutimiza unabii.
Hii inajulisha kwamba hii ni baada ya Sabato, kwa sababu wayahudi walikuwa hawafanyi kazi au kusafiri siku ya Sabato. Walisubiri muda wa jioni kuleta watu kwa Yesu. Hauhitaji kutaja Sabato isipokuwa unataka kuepuka tafsiri ya uongo
Hii inaweza kutafsiriwa kwa mfumo hai.AT:"wengi ambao mapepo yaliwatawala" (UDB) au "wengi ambao walipagawa na mapepo"
Hapa "neno" inamaanisha amri. Yeye aliwaamuru pepo kuondoka."
Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai. "Yesu alitimiza unabii kwamba nabii Isaya aliongea na watu wa Israeli."
Mathayo anamnukuru nabii Isaya. Hii misemo miwili kiualisi inamaana moja na kusisitiza kwamba yeye aliponya magonjwa yetu yote. "aliponya wale walio wagonjwa na kuwafanya wazima."
Hapa simulizi linabadilika na kusimulia jinsi Yesu alivyosema juu ya watu waliotaka kumfuata
Hili neno limetumika hapa kuonyesha alama ya kikomo cha hadithi. Hapa Mathayo anaanza kueleza sehemu mpya ya hadithi.
"aliwaambia wanafunzi wake"
Hapa inamaanisha baada ya Yesu "kutoa maelekezo" lakini kabla yake kuingia ndani ya boti.
"sehemu yeyote"
Hii ina maana hata wanyama wakali wana sehemu ya kupumzika.
Mbwea ni wanyama kama mbwa. Wanakula ndege wadogo na wanyama wengine wadogo. Ikiwa mbwea hawajulikani kwenye eneo lako, tumia kwa ujumla mbwa - kama viumbe au mnyama mwingine mkali.
Mbwea wanatengeneza mashimo ardhini kwa kuishi humo. Tumia neno sahihi kwa eneo ambalo mnyama "mbwea" anaishi.
Yesu anaongelea kuhusu yeye mwenyewe
Hii ina maanisha sehemu ya kulala. "hana sehemu yake ya kulala."
Aieleweki kwamba baba wa mtu alikufa na angemzika mapema, au ikiwa mtu anaataka akae muda mrefu baba yake afe na amzike. Pointi ya muhimu mtu anataka kufanya kitu kingine kwanza kabla ya kumfuata Yesu.
Yesu hana maana halisi kwamba watu wafu watazika wafu wengine. Tafsiri inayowezekanaya "wafu" ni 1) ni msemo kwa wale ambao watakufa punde, au 2) ni msemo kwa wale ambao hawamfuati Yesu na kiroho wamekufa. Pinti ya muhimu ni kwamba wanafunzi wasiruhusu kitu chochote kumchelewesha kumfuata yesu.
Hapa mandhari yanahamia kwenye simulizi la Yesu akituliza dhoruba wakati yeye na wanafunzi walipokuwa wakivuka bahari ya Galilaya.
"kuingia ndani ya boti"
Jaribu kutumia neno lilelile kwa "wanafunzi" na "kufuata" ambalo umelitumia
Hii inaonyesha kuanza kwa kutukio jingine kubwa la hadithi. Lugha yako inaweza ikawa na njia nyingine ya kuonyesha hili.
"wimbi la nguvu likatokea baharini"
Hii inaweza kutafsiriwa kwa mfumo tendaji. "ndipo sasa mawimbi yakafunika boti"
Maana inayowezekana ni 1) kwanza walimwamsha Yesu na ndipo wakasema, "tuokoe" au 2) walipokuwa wakimwamsha walimwambia "tuokoe"
ikiwa unataka kutafsiri neno hili kama pamoja au kipekee, ndipo kipekee ni bora. Wanafunzi yawezekana walimaanisha walitaka Yesu awaokoe wanafunzi na yeye mwenyewe kwenye kuzama.
"sisi tunakwenda kufa"
"kwa wanafunzi"
Yesu alikuwa anakemea wanafunzi kwa swali la kejeli. "hampaswi kuogopa...imani" au "hamna sababu ya ninyi kuogopa ....imani."
Angalia jinsi unavyotafsiri hii
"Hata upepo na bahari vinamtii yeye! Huyu mtu ni wa namna gani?" Hili swali la kejeli linaonyesha kwamba wanafunzi walishangazwa. "huyu mtu niwa tofauti na hatujawahi kumwona! hata upepo na mawimbi vinamtii yeye!"
Kwa watu au wanyama kutii au kutotii haishangazi, lakini kwa upepo na maji inashangaza.Hii kibinadamu inaeleza vitu asili kama viumbe vinaweza kusikia na kuitikia kama watu.
Hapa mwandishi anaturudisha kwenye wazo kuu la Yesu akiwaponyawatu. Hii inanzisha simulizi la Yesu akiwaponya wanaume wawili waliokuwa na pepo.
"upande mwingine wa bahari ya galilaya"
Gadalene ulitajwa kwa jina la Gadara.
Mapepo yaliyowatawala watu hawa wawili yalikuwa hatari kwamba hakuna hata mmoja angeenda kupitia eneo hilo.
Hii inaonyesha kuanza kwa kutukio jingine kubwa la hadithi. Inaweza kuhusisha watu tofauti na tukio lililopita, Lugha inaweza kuwa na njia ya kuonyesha hili.
Hili swali la kwanza la kejeli ni hostile
hili swali la pili la kejeli nalo pia ni uhasama na linamaanisha "Haupaswi kutomtii Mungu kwa kutuadhibu sisi kabla ya muda wenyewe ambao Mungu ameupanga ambao atuhukumu sisi"
hili neno linaonyesha kwamba mwandishi atawaambia wasomaji habari anazotaka kufahamu kabla ya hadithi kuendelea. Nguruwe walikuwa kule kabla ya Yesu kufika.
"kwa sababuunakwenda kututoa sisi nje"
Hii ni pamoja ,ina maanisha nguruwe pekee"
mapepo ndani ya mtu
"Mapepo wakamwacha mtu na kuwaingia nguruwe"
Neno "ndipo" hapa linatoa angalizo kwetu kuwa tayari kwa taarifa za kushangaza zinazokuja.
"kimbia haraka chini kwenye mteremko"
"waliingia kwenye maji na kuzama"
Hii inahitimisha habari ya Yesu ya kuwaponya wanaume wawili waliokuwa na pepo
"kulinda nguruwe"
"Yesu alifanya nini kwa mwanaume ambaye alitawaliwa na mapepo"
Hii inaonyesha mwanzo wa tukio jingine kubwa la hadithi. Inaweza kuhusisha watu tofauti na tukio la zamani.Lugha yako inaweza kuwa na njia kwa kuonyesha hili
Hii ina maanisha wengi au idadi ya watu wengi, sio lazima kila mtu.
"jiji na ardhi inayoizunguka"
Yesu alimwambia mkoma aliyeponywa kwenda kwa kuhani kwa ushuhuda wao.
Yesu alisema angeenda kwenye nyumba ya jemedari na kumponya mtumishi wake.
Jemedari alisema kwamba yeye hanakuwa na thamani kwa Yesu kuingia katika nyumba yake na kwamba Yesu angeweza kusema neno tu na kumponya mtumishi.
Yesu alisema kwamba hata katika Israeli hajawahi kuona mtu mwenye imani kuu kama jemedari.
Yesu alisema kwamba wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi na kuketi katika meza katika ufalme wa Mungu.
Yesu alisema kuwa wana wa ufalme wangetupwa katika giza la nje.
Yesu alimponya mama mkwe wa Petro alipoingia kwenye nyumba ya Petro.
Unabii wa Isaya,"Yeye mwenyewe alichukua magonjwa yetu na alibeba maradhi yetu" ulitimia.
Yesu alisema hakuwa na nyumba ya kudumu.
Yesu alimwambia mwanafunzi kumfuata yeye na kuacha wafu kuzika wafu wenzao
Yesu alikuwa amelala wakati dhiruba kuu inatokea juu ya bahari.
Yesu aliwaambia wanafunzi, "Kwa nini mnaogopa, ninyi wenye imani ndogo"?
Wanafunzi walimshangaa Yesu kwa sababu upepo na bahari vilimtii.
Yesu alikutana na watu wawili waliopagawa na pepo ambao walikuwa wasumbufu
Pepo waliongea kuhusu kuja kwa Yesu kuwatesa kabla ya wakati kufika.
Wakati Yesu alipowafukuza pepo, waliingia katika kundi la nguruwe na wale nguruwe wakakimbilia majini na kuangamia.
Watu walimsihi Yesu aondoke katika mkoa wao.
1Yesu akaingia kwenye boti, akavuka na akafika kwenye mji alipokuwa anaishi.2Tazama, wakamletea mtu aliyepooza amelazwa kwenye godoro. Alipoiona imani yao, Yesu akamwambia mtu aliyepooza, “Mwanangu, uwe na furaha, dhambi zako zimesamehewa.”3Tazama, baadhi ya walimu wa sheria wakasemezana wao kwa wao, “Huyu mtu anakufuru.”4Yesu akatambua mawazo yao na kusema, “Kwa nini mnawaza maovu moyoni mwenu?5Kipi kilicho rahisi kusema, ‘Dhambi zako zimesamehewa’ au kusema, ‘Simama na utembee?’6Lakini mtambue ya kwamba Mwana wa Adamu anao uwezo wa kusamehe dhambi.” Aliyasema haya kwa yule aliyepooza, “Simama, chukua godoro lako, na uende nyumbani kwako.”7Ndipo yule mtu akasimama na kuondoka kwenda nyumbani kwake.8Makutano walipoona hayo, walishangaa na kumsifu Mungu, ambaye amewapa uwezo huo watu.9Na Yesu alipokuwa akipita kutoka hapo, alimwona mtu ambaye aliitwa kwa jina la Mathayo, ambaye alikuwa amekaa sehemu ya watoza ushuru. Naye akamwambia, “Nifuate mimi.” Naye akasimama na kumfuata.10Na Yesu alipoketi ili ale chakula ndani ya nyumba, wakaja watoza ushuru wengi na watu waovu wakashiriki chakula pamoja na Yesu na wanafunzi wake.11Ndipo Mafarisayo walipoona hayo, wakawaambia wanafunzi, “Kwa nini mwalimu wenu anakula chakula pamoja na watoza ushuru na watu waovu?”12Yesu aliposikia hayo, naye alisema, “Watu walio na afya nzuri hawahitaji mganga, isipokuwa wale walio wagonjwa.13Inawapasa muende mkajifunze maana yake, ‘Ninapenda rehema na siyo dhabihu,’ kwa kuwa nilikuja, si kwa wenye haki kutubu, lakini kwa wenye dhambi.”14Ndipo wanafunzi wa Yohana wakaja kwake na kusema, “Kwa nini sisi na mafarisayo tunafunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?”15Yesu akawaambia, “Je, wasindikizaji wa arusi wanaweza kuwa na huzuni pindi Bwana arusi anapokuwa pamoja nao? Lakini siku zinakuja ambapo Bwana arusi atachukuliwa kutoka kwao, na ndipo watakapofunga.16Hakuna mtu anayeweka kipande cha nguo mpya kwenye nguo ya zamani, kiraka kitaipasua nguo na mpasuko mkubwa utatokea.17Hakuna watu wanaoweka mvinyo mpya katika chombo cha mvinyo wa zamani, ikiwa watafanya, ngozi itachanika, mvinyo utatoweka na ngozi itaharibika. Badala yake, huweka mvinyo mpya katika ngozi mpya na vyote vitakuwa salama.”18Wakati Yesu alipokuwa akiwaambia mambo hayo, tazama, afisa akaja akasujudu mbele yake, naye akasema, “Binti yangu amefariki punde, lakini njoo na uweke mkono wako juu yake na yeye ataishi tena.”19Ndipo Yesu akasimama na kumfuata na wanafunzi wake pia.20Tazama, mwanamke ambaye alikuwa anatokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, akaja karibu na Yesu na akagusa sehemu ya pindo la vazi lake.21Kwa kuwa alisema, “Endapo nitagusa vazi lake, nami nitapata uponyaji.”22Yesu akageuka na kumtazama na kumwambia. “Binti, jipe moyo, imani yako imekufanya upone.” Na muda huo huo mwanamke akapata uponyaji.23Na Yesu alipofika kwenye nyumba ya afisa, naye aliwaona wapiga tarumbeta na umati wa watu ulikuwa ukipiga kelele.24Naye akasema, “Tokeni hapa, kwa kuwa binti hajafa, bali amelala.” Lakini wao walicheka na kumkebehi.25Na wale watu walipotolewa nje, naye akaingia chumbani na kumshika mkono na msichana akaamka.26Na habari hizi zikaenea katika mji mzima.27Ndipo Yesu alipokuwa akipita kutoka pale, wanaume wawili vipofu wakamfuata. Waliendelea kupaza sauti wakisema, “Tunaomba uturehemu, Mwana wa Daudi.”28Pindi Yesu apokuwa amefika kwenye nyumba, wale vipofu wakaja kwake. Yesu akawaambia, “Mnaamini kwamba ninaweza kutenda?” Nao wakamwambia “Ndiyo, Bwana.”29Ndipo Yesu akagusa macho yao na kusema, “Na ifanyike hivyo kwenu kama imani yenu ilivyo.”30Na macho yao yakafumbuka. Ndipo Yesu akasisitiza akawaamuru na kusema, “Angalieni mtu yeyote asifahamu kuhusu jambo hili.”31Lakini watu hawa wawili wakaondoka na kutangaza habari hizi sehemu zote za mji.32Ndipo wale wanaume wawili walipokuwa wakienda zao, tazama, mtu mmoja bubu aliyepagawa na pepo akaletwa kwa Yesu.33Na pepo walipomtoka, yule mtu bubu akaanza kuongea. Umati ukashangazwa na kusema, “Hii haijawahi kutokea katika Israel.”34Lakini Mafarisayo walikuwa wakisema, “Kwa wakuu wa pepo, anawafukuza mapepo.”35Yesu akaenda kwenye miji yote na vijiji. Naye akaendelea kufundisha katika masinagogi, akihubiri injili ya ufalme, na kuponya magonjwa ya kila aina na udhaifu wa aina zote.36Wakati alipotazama umati, naye aliwaonea huruma, kwa sababu walisumbuka na kuvunjika moyo. Walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji.37Naye akawaambia wanafunzi wake. “Mavuno ni mengi, lakini wafanya kazi ni wachache.38Hivyo basi upesi mwombeni Bwana wa mavuno, ili kwamba atume wafanya kazi katika mavuno yake.”
Kuna takwimu nyingi za matamshi katika sura hii. Ilikuwa ni kawaida pia kwa Yesu kutumia mifano ya analojia na sitiari katika mafundisho yake. Jinsi yake ya kufundisha ilikuwa na nia ya kukuza imani ndani yake.
Baadhi ya tafsiri za Kiingereza huanzisha sentensi nyingi katika sura hii na neno "na" au "lakini" ili kuonyesha mfululizo wa matukio katika maelezo. ULB kawaida huondoa maneno haya kwa sababu muktadha wa hadithi yenyewe unaonyesha kuwa matukio hutokea kwa mfululizo. Inakubalika kutumia maneno haya ikiwa yana umuhimu katika tafsiri yako.
Mwandishi anarejea kwenye wazo kuu, ambalo linaanzia 8:1, la Yesu akiwaponya watu. Hii inaanzisha habari ya Yesu akimponya mwanamume aliyekuwa amepooza
Wanafunzi yamkini walienda na Yesu'
Yamkini ni boti ile ile
"mji ambao yeye aliishi"
Hii inaonyesha mwanzo wa tukio jingine kubwa la hadithi. Linaweza kuhusisha watu wengine tofauti na tukio lililopita. Lugha yako inaweza kuwa na njia nyingine ya kuonyesha hili.
Hii inaonyesha wale ambao walimleta mgonjwa wa kupooza kwa Yesu. Hii inahusisha mgonjwa aliyepooza mwenyewe.
Huyu mtu hakuwa mtoto halisi wa Yesu. Yesu alikuwa akiongea naye kwa upole. Ikiwa hii inachanganya, inaweza pia kutafsiriwa"Rafiki yangu" au "Kijana" au hata kuondolewa.
"Mungu amesamehe dhambi zako" au "Nimekusamehe dhambi zako"
Hii inaonyesha mwanzo wa tukio jingine kubwa la hadithi. Inaweza kutumia watu wengine tofauti na tukio lililopita. Lugha yako inaweza kuwa njia nyingine kufanya hili.
Hii inaweza kumaanisha "wao kwa wao,"kwenye mawazo yao, au "kwa kila mmoja," kutumia midomo yao.
Yesu alidai kuweza kufanya vitu ambavyo waandishi wa sheria walifikiri Mungu peke yake angevifanya.
Yesu alitambua walichokuwa wakifikiria kwa uwezo wake au kwa sababu aliwaona wakisemezana wao kwa wao.
Yesu alitumia swali kuwakemea wanasheria.
Hizi ni wingi
Huu ni uovu wa kimaadili au ukosefu, sio tu ni kosa kwa uhakika.
Yesu aliuliza swali kukumbusha wanasheria kwamba waliamini mtu amepooza kwa sababu ya dhambi zake na kwamba dhambi zake zimesamehewa, naye angeweza kutembea, ili kwamba alipomponya aliyepooza, wanasheria wajue kwamba yeye anaweza kusamehe dhambi.
"kipi ni rahisi kusema,"Dhambi zako zimesamehewa"? au ni rahisi kusema "Simamama na utembee"?
Hii inaweza kumaanisha 1)"ninakusamehe dhambi" au 2)"Mungu amesamehe dhambi zako."yako" ni umoja.
"Nitawahakikishia ninyi." "ninyi" ni wingi.
Hizi ni umoja
Yesu hamkatazi mtu kwenda sehemu nyingine. Yeye anampa fursa ya kwenda nyumbani.
Hii inahitimisha habari ya Yesu ya kumponya mtu aliyepooza. Kisha Yesu akamwita mtoza ushuru kuawa mmoja wa wanafunzi wake.
"kwa sababu amewapa"
mamlaka ya kuthibitisha kusamehe dhambi
Kirai hiki kinaonyesha mwanzo wa simulizi mpya. Kamalugha yako ina namna ya kufanya hili, unaweza kulitumia mahali hapa.
"alikuwa akiondoka" au "alikuwa akienda"
Utamaduni wa kanisa unasema Mathayo ni mwandishi wa hii Injili, lakini andiko halitoi sababu ya kubadilisha kiwakilishi kutoka "naye" na "yeye" kwa "kwangu" na "mimi"
"Yesu alisema na Mathayo"
"Yesu alimwambia Mathayo"
"Mathayo alisimama na kumfuata yeye" kama mwanafunzi, siyo tu kujumuika na Yesu kwa kinachofuata kukamilisha.
Matukio haya yalitokea kwenye nyumba ya Mathayo mtoza ushuru
Hii yawezekana ni nyumba ya Mathayo, lakini yawezekana kuwa nyumba ya Yesu(walitumia kula Yesu na wanafunzi wake")Kilitengwa maalum ikiwa kitahitajika kuepusha kuchanganywa.
Hii inaonyesha mwanzo wa tukio jingine katika habari kuu. Inaweza kuhusisha watu tofauti kuliko matukio yale ya kwanza. Lugha yako inaweza kuwa na namna ya kulielezea hili.
"Na mafarisayo walipoona kwamba Yesu alikuwa anakula na watoza ushuru na watu wenye dhambi"
Mafarisayo walitumia swali hili kumkosoa Yesu kile alichokuwa akifanya.
Matukio haya yanatokea kwenye nyumba ya Mathayo mtoza ushuru.
Hapa "hayo" inarejea swali ambalo mafarisayo waliuliza kuhusu Yesu kula na watoza ushuru na wenye dhambi.
Yesu anajibu kwa kutumia mithali. Anamaanisha kuwa anakula na watu wa aina hii kwa sababu amekuja kuwaokoa wenye dhambi.
"watu wenye afya"
Kirai "wanahitaji mganga" kinaeleweka. "Wagonjwa ndio wanaohitaji mganga"
Yesu anaelekea kunukuu maandiko. "Inakupasa ujifunze maana ya kile ambacho Mungu alisema katika maandiko"
Kiwakilishi "wa" ni cha wingi kinachomaanisha mafarisayo
Yesu ananukuu kile ambacho nabii Hosea aliandika katika maandiko.. Hapa "Ni" inamaanisha Mungu.
Hapa "Ni" inamaanisha Yesu.
Yesu anatumia kejeli. Hadhani kuwa kuna watu wenye haki ambao hawahitaji kutubu. "wale wanaodhani kuwa ni wenye haki"
Wanafunzi wa Yohana mbatizaji walihoji swala la wanafunzi wa Yesu kutokufunga.
"endeleeni kula kama kawaida"
Yesu anatumia swali kuwajibu wanafunzi wa Yohana. Walijua kuwa watu hawaombolezi na kufunga kwenye sherehe ya harusi. Yesu anatumia mithali hii kuonyesha kuwa wanafunzi wake hawaombolezi kwa sababu yeye bado yuko nao.
"lakini muda utafika"
Hii inaweza kuelezeka katka mfumo tendaji. "Bwana harusi hatakuwa pamoja nao si muda mrefu ujao" au "kuna mmoja atakayemchukua bwana harusi kutoka kwao."
Yamkini Yesu anamaanisha kifo chake, lakini hii isiwekwe wazi kuwa ndichio alichomaanisha. Ili kulinda picha ya harusi, ni vizuri kueleza kuwa bwana harusi ataondoka kitambo.
Yesu anaendelea kujibu swali ambalo wanafunzi wa Yohana walikuwa wameuliza
Huu msemo una maana kwamba watu wanaojua utamaduni wa zamani pekee hawako tayari kukubali mpya.
nguo
"kipande cha nguo mpya" kinatumika kuziba nguo iliyochanika
Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji
Yesu anaendelea kujibu swali ambalo wanafaunzi wa Yohana walikuwa wameuliza
Yesu anatumia mithali Nyingine kuwajibu wanafunzi wa Yohana. Hii inamaanisha ni kitu kilekile sawa na mithali ya 9:16
"Hakuna hata mmoja anayemwaga" au "Watu hawaweki kamwe"
Huu ni mvinyo ambao haujachacha. Kama mizabibu haijulikani kwenye sehemu yenu, tumia neno la ujumla la tunda."mvinyo wa matunda"
Hii inamaanisha mifuko ya mvinyo ambayo imekuwa ikitumika mara nyingi.
"mkoba wa mvinyo" au "mkoba wa ngozi". Hii ni mifuko iliyokuwa imetengenezwa kwa ngozi za wanyama.
Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. "Na hii itaharibu mfuko wa mvinyo na mvinyo kumwagika.
mvinyo mpya unapochacha na kuumuka, ile ngozi huchanika kwa sababu haiwezi tena kutanuka.
"mifuko mipya ya mvinyo" au "begi jipya la mvinyo" Hii inamaanisha ngozi ya mvinyo ambayo haijawahi kutumika.
Hili linaweza kuelezwa kwa mfumo tendaji
Hii inaanzisha simulizi ya Yesu kumfufua binti wa afisa wa Kiyahudi baada ya kufa.
Hii inarejea jibu la Yesu alilowapa wanafunzi wa yohana kuhusu kufunga.
Neno "tazama" linatupa dokezo la mtu mwingine mpya katika hadithi. Lugha yako inawezekana ikawa na njia nyingine ya kufanya hivi.
Hii ni njia mtu yeyote kuonyesha heshima katika utamaduni wa kiyahudi.
Hii inaonyesha kwamba ofisa wa kiyahudi aliamini Yesu ana nguvu ya kurudisha uhai wa binti yake.
wanafunzi wa Yesu
Hii inafafanua jinsi Yesu alivyomponya mwanamke mwingine wakati akiwa njiani kwenda kwa afisa wa Kiyahudi
Neno "tazama" linadokeza juu ya mtu mwingine katika hadithi. Lugha yenu inaweza kuwa na njia nyingine ya kufanya hivi
"kutokwa damu mfululizo"Yawezekana alikuwa akitokwa damu kwenye tumbo lake ingawa haikuwa kipindi cha kawaida yake. Baadhi ya tamaduni yawezekana wana namna nzuri ya kueleza tatizo hili.
"miaka 12"
"kanzu"
Alifikiria hivi kabla hajamgusa Yesu. Unaweza kuiweka sentensi hii mwanzoni.
Kwa mjibu wa sheria za Kiyahudi, kwa sababu ya kutokwa na damu hakutakiwa kumgusa yeyote mtu yeyote. Anagusa vazi la Yesu ili nguvu za Yesu zimponye alidhani kuwa Yesu hatagundua kuwa ameguswa
"Badala" Kile mwanamke alichotumaini kutokea hakikutokea.
Mwanamke hakuwa mtoto halisi wa Yesu. Yesu alikuwa akiongea naye kwa upole. Ikiwa hii inachanganya, inaweza kutafsiriwa "kijana wa kike" au hata kutolewa.
"Kwa sababu uliniamini, Nitakuponya"
Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo tendaji. "Yesu alimponya hapohapo"
Hii inarudisha habari ya Yesu kumfufua binti wa afisa wa Kiyahudi
Hii ilikuwa nyumba ya kiongozi wa kiyahudi
Huu ni utamaduni wa kawaida wa kumboleza pale mtu anapokuwa amekufa.
"watu ambao wanapiga zumari/filimbi"
Yesu alikuwa akiongea kwa watu wengi, hivyo tumia mfumo wa wingi wa kutoa amri kama lugha yenu inao huo.
Yesu anatumia igizo la maneno. Ilikuwa ni kawaida kipindi cha Yesu kusema mtu aliyekufa kuwa "amelala" Lakini hapa binti aliyekufa ataamka, ingawa yeye alikuwa amelala.
Hii inahitimisha simulizi la Yesu la kumfufua binti wa afisa wa Kiyahudi
Mstari wa 26 unatoa muhtasari unaofafanua matokeo ya Yesu kumfufua huyu msichana.
"Baada ya yesu kuwatoa watu nje" au "Baada ya familia kuwatoa watu nje"
"akaamka kutoka kitandani" Hii ni maana ile ile kama iliyo kwenye 8:14
Watu wote wa mji ule walisikia kuhusu hilo" au "Watu walioona binti akiwa hai walianza kuwaambia watu wa eneo hilo habari hizi."
Hii inaanzisha habari ya Yesu akiwaponya wanaume wawili waliokuwa vipofu
Yesu alikuwa akiondoka kwenye mji
"Alikuwa akiondoka" au "alikuwa akienda"
Hii inamaainisha kuwa walikuwa wakitembea nyuma ya Yesu, siyo lazima kuwa walikuwa wameshakuwa wanafunzi wake.
Inamaanisha kuwa walitaka Yesu awaponye
Yesu hakuwa mwana halisi wa Daudi, hivyo inaweza kutafsiriwa kama "Ukoo wa Daudi". Ingawa, "Mwana wa Daudi" pia ni cheo alichopewa Masihi, na wale wanaume yawezekana walikuwa wakimwita Yesu kwa Sifa hii.
Hii inaweza kuwa nyumba ya Yesu au nyumba iliyosemwa kwenye 9:10
Jibulote halijatolewa lakini linaeleweka "Ndiyo, Bwana, tunaamini kuwa unaweza kutuponya."
Haiko wazi kuwa aligusa macho yao wote wakati mmoja au alitumia mkono wake wa kulia kumgusa mmoja na mwingine tena. Mkono wa kushoto kawaida ulitumika kwa makusudi yakutokuwa safi, ni hakika alitumia mkono wa kulia pekee. Pia haiko wazi kwamba aliongea wakati anawagusa au kwanza aliwagusa na ndipo akaongea kwao.
Hii inaweza kutafsriwa katika mfumo tendaji. "Naitafanya kama ulivyomini" au "kwa sababu unaamini, nitakupaonya"
Hii inamaanisha waliweza kuona. Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo tendaji. "Mungu aliponya macho yao" au "wale wanaume wawili vipofu waliweza kuona"
Hapa neno "angalieni" linamaanisha "hakikisha." au "Uwe na Muwe na uhakika hakuna mtu atakaye tafuta juu ya jambo hili" au "Msimwambie mtu yeyeote kuwa nimewaponya"
"Badala yake"Wanaume hawakufanya kile ambacho Yesu aliwaambia kufanya.
"waliwaambia watu wengi kilichotokea kwao"
Hii ni habari ya Yesu akiwaponya watu waliokuwa wamepagawa na pepo
Neno "tazama" linadokeza sisi juu ya mtu mwingine katika simulizi. Lugha yako inaweza ikawa njia nyingine ya kufanya hizi.
Hii inaweza kuelezeka kwa muundo tendaji. "mtu mmoja alimleta bubu kwa Yesu... kwa Yesu"
asiyeweza kuongea
Hii inaweza kueleza katika mfumo tendaji. "ambaye pepo lilikuwa limemumliki" au "amabye pepo lilikuwa linamtawala"
Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. "Baada ya Yesu kuwa amelitoa pepo" au " Baada ya Yesu kuwa ameliamuru pepo kutoka"
"Yule bubu akanza kuongea" au "yule aliyekuwa bubu aliongea" au "mtu ambaye alikuwa bubu akaongea" au yule mtu hakuwa bubu tena"
"Watu walishangazwa"
Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji "Hii haikuwahi kutokea kabla" au "Hakuna hata mmoja aliyewahi kufanya jambo kama hili hapo awali."
"huwalazimisha pepo kutoka"
Kiwakilishi "ana" kinamaanisha Yesu
Mstariwa 35 ni mwisho wa sehemu ya simulizi ambayo imeamnzia katika 8:1 kuhusu huduma ya Yesu ya uponyaji kule Galilaya.
Mstari wa3 6 unaanzisha sehemu nyingine ya simulizi ambapo Yesu anawafundisha wanafunzi wake na kuwatuma kwenda kuhubiri na kuponya kama alivyokuwa akifanya.
Yesu alienda kwa wengi au kwa miji mingi lakini si kwa kila mji. "Katika miji mingi"
"vijiji vikubwa...vijiji vidogo" au "miji mikubwa...miji midogo"
Hapa neno "Ufalme" linamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. tazama ilivyotafsiriwa karika 4:23
"kila magonjwa na kila udhaifu" Neno "magonjwa" na "udhaifu" yanakaribiana kufanana lakini yanapaswa kutafsiliwa tofauti kama inawezekana. "Ugonjwa" unamfanya mtu kuwa dhaifu. "Udhaifu" kukosa nguvu mwili au tokeo linalosababishwa na kuwa na ugonjwa.
Mfanano huu unamaanisha kuwa hawakuwa na kiongozi wa kuwaangalia. "Watu hawakuwa na kiongozi"
Yesu anatumia mithali kuwaambia wanafunzi wake juu ya mavuno ili kuona jinsi watavyopokea mahitaji ya makutano yaliyotajwa katika sehemu ambazo tayari zimepita.
Yesu anatumia mithali kuonyesha jinsi anavyopokea kile anachokiona. Yesu anamaanisha kuwa kuna watu wengi walio tayari kumwani Mungu lakini kuna watu wachache tu wa kuwafundisha ukweli wa Mungu.
"Kuna mazao mengi yaliyoiva na yako tayari kuvunwa."
"watendaji"
"Mwombeni Bwana, kwa sababu yeye mkuu wa mavuno"
Baadhi ya walimu wa sheria walifikiri kwamba Yesu alimkufuru Mungu kwa sababu Yesu alimwambia mtu aliyepooza kwamba dhambi zako zimesamehewa.
Yesu alimwambia aliyepooza dhambi zako zimesamehewa ili kuonyesha kuwa anayo mamlaka duniani kusamehe dhambi.
Walishangaa na kumsifu Mungu aliyewapa mamlaka kama hayo kwa watu.
Mathayo alikuwa mtoza ushuru kabla ya kumfuata Yesu.
Yesu na wanafunzi wake walikula pamoja na watoza ushuru na watu wenye dhambi.
Yesu alisema alikuja kuwaita mwenye dhambi ili watubu
Yesu alisema wanafunzi wake walikuwa hawafungi kwa sababu awakuwa bado yupo pamoja nao.
Yesu alisema wangeweza kufunga wakati atakapokuwa amechukuliwa kutoka kwao.
Mwanamke aliyetokwa na damu kwa wingi aligusa sehemu la nguo ya Yesu akifikiri kwamba endapo atagusa nguo yake tu, atapata uponya na kuwa mzima.
Yesu alisema mwanamke mwenye kutokwa damu nyingi alinywa kwa imani yake.
Watu walimcheka Yesu kwa sababu alisema binti alikuwa hajafa bali amelala.
Habari kuhusu Yesu kumfufua binti zilienea katika mji wote.
Vipofu wawili waliendelea kupiga kelele, "utuhurumie sisi, mwana wa Daudi
Yesu aliwaponya vipofu wawili kutokana na imani yao.
Mafarisayo walimshutumu Yesu kuwa alitoa mapepo kwa nguvu ya mkuu wa mapepo?
Yesu aliwaonea huruma umati kwa sababu kwa sababu walisumbuka na kuvunjika moyo, na walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji.
Yesu aliwaambia wanafunzi wake ni muhimu waombe kwamba Bwana wa mavuno atume wafanyakazi katika mavuno.
1Yesu akawaita wanafunzi wake kumi na wawili pamoja na kuwapa mamlaka juu ya pepo wachafu, kuwakemea na kuwafukuza na kuponya aina zote za maradhi na aina zote za magonjwa.2Majina ya mitume kumi na wawili ni haya. La kwanza, Simeoni (ambaye pia anaitwa Petro), na Andrea kaka yake, Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana kaka yake:3Filipo, na Bartelemayo, Thomaso, na Mathayo mtoza ushuru, Yakobo mwana wa Alfayo, na Tadeo,4Simoni mkananayo, na Yuda Iskariote, ambaye alimsaliti.5Hawa kumi na wawili Yesu aliwatuma. Naye aliwaelekeza akisema, “Msiende sehemu wanakoishi wamataifa na msiingie kwenye miji ya Wasamaria.6Badala yake, mwende kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israel.7Na mnapokwenda, hubirini na kusema, ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia.’8Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma na fukuzeni pepo. Mmepokea bure, toeni bure.9Msichukue dhahabu, almasi au shaba kwenye pochi zenu.10Usichukue mkoba katika safari yenu, au nguo za ziada, viatu au fimbo, kwa kuwa mfanyakazi anastahili chakula chake.11Mji wowote au kijiji mtakachoingia, tafuteni ambaye anastahili na mkae pale mpaka mtakapoondoka.12Mtakapoingia katika nyumba salimieni.13Endapo nyumba inastahili, amani yenu ibaki pale, lakini kama nyumba haistahili, amani yenu iondoke pamoja nanyi.14Na kwa wale wasiowapokea ninyi au kusikiliza maneno yenu, wakati mnaondoka kwenye nyumba au mji huo, kung'uta mavumbi ya nyayo zenu mahali hapo.15Kweli ninawaambia, itakuwa ya kustahimili zaidi miji ya Sodoma na Gomorah siku ya hukumu kuliko mji huo.16Angalia, ninawatuma kama kondoo katikati ya mbwa mwitu, kwa hiyo iweni na werevu kama nyoka na wapole kama njiwa.17Muwe waangalifu na watu, watawapeleka kwenye mabaraza, na watawapiga kwenye masinagogi.18Na mtaletwa mbele ya wakuu na wafalme kwa ajili yangu, kama ushuhuda kwao na kwa mataifa.19Pindi watakapowashutumu, msiwe na wasiwasi jinsi gani au nini cha kuongea, kwa kuwa kitu cha kusema mtapewa kwa wakati huo.20Kwa kuwa sio ninyi mtakaoongea, lakini Roho wa Baba yenu ataongea ndani yenu.21Ndugu atamwinukia ndugu yake kumwua, na baba kwa mtoto wake. Watoto watainuka dhidi ya wazazi, na kuwasababishia kifo.22Nanyi mtachukiwa na kila mtu kwa sababu ya jina langu. Lakini yeyote atakayevumilia mpaka mwisho mtu huyo ataokolewa.23Pindi wanapowatesa katika mji huu, kimbilieni mji unaofuata, kwa kweli ninawaambia, hamtakuwa mmekwenda kwenye miji yote ya Israeli kabla ya Mwana wa Adam hajarudi.24Mwanafunzi si mkuu kuliko mwalimu wake, wala mtumwa aliye juu ya Bwana wake.25Inatosha kwa mwanafunzi kwamba awe kama mwalimu wake, na mtumishi kama Bwana wake. Ikiwa wamemwita Bwana wa nyumba Belzabuli, ni kwa kiasi gani zaidi watawakashifu wa nyumba yake!26Hivyo basi msiwahofu wao, kwa kuwa hakuna jambo ambalo halitafunuliwa, na hakuna lililofichika ambalo halitajulikana.27Kile ninachowaambia gizani, mkiseme nuruni, na mnachokisikia kwa ulaini masikioni mwenu, mkitangaze mkiwa juu ya nyumba.28Msiwaogope wale ambao wanaua mwili lakini hawana uwezo wa kuua roho. Badala yake, mwogopeni yule ambaye awezaye kuangamiza mwili na roho kule kuzimu.29Je kasuku wawili hawauzwi kwa senti ndogo? Hata hivyo hakuna anayeweza kuanguka chini bila Baba yenu kufahamu.30Lakini hata idadi ya nywele zenu zimehesabiwa.31Msiwe na hofu, kwa kuwa mnathamani zaidi kuliko kasuku wengi.32Hivyo basi kila mmoja atakaye nikiri mbele za watu, nami pia nitamkiri mbele ya Baba yangu aliye mbinguni.33Lakini yeye atakaye nikana mbele za watu, nami pia nitamkana mbele ya Baba yangu aliye mbinguni.34Msifikiri kwamba nimekuja kuleta amani duniani. Sikuja kuleta amani, lakini upanga.35Kwa kuwa nilikuja kumweka mtu apingane na baba yake, na binti dhidi ya mama yake, na mkwe dhidi ya mama mkwe wake.36Adui wa mtu watakuwa wale wa nyumbani mwake.37Yeye ambaye anampenda baba au mama zaidi kuliko mimi huyo hanistahili. Na yeye anayempenda kijana au binti zaidi kuliko mimi huyo hanistahili.38Yeye ambaye hatabeba msalaba na kunifuata mimi hanistahili.39Yeye atakayetafuta maisha atayapoteza. Lakini yeye atakayepoteza maisha kwa ajili yangu atayapata.40Yeye atakayewakaribisha amenikaribisha mimi, na yeye atakayenikaribisha mimi amemkaribisha yeye aliyenituma mimi.41Na yeye atakayemkaribisha nabii kwa sababu ni nabii atapokea thawabu ya nabii. Na yeye atakayemkaribisha mwenye haki kwa sababu ni mtu wa haki atapokea thawabu ya mtu wa haki.42Yeyote atakayempatia mmoja wa wadogo hawa, hata kikombe cha maji ya kunywa ya baridi, kwa sababu yeye ni mwanafunzi, kweli ninawaambia, yeye hawezi kukosa kwa njia yeyote thawabu yake.”
Sehemu kubwa ya sura hii inazungumza juu ya Yesu kuwatuma wanafunzi kumi na wawili kutoa ujumbe wake kuhusu ufalme wa mbinguni. Walipaswa kufanya huduma yao kwa inchi ya Israeli pekee na wasije wakashiriki habari hii kwa wasio Wayahudi. Maagizo ya Yesu humpa msomaji hisia kwamba hawakupaswa kupoteza wakati wowote. Sauti yake iliashiria kuwa alitaka waharakishe.
Yafuatayo ni orodha ya wanafunzi kumi na wawili: Katika Mathayo: Simoni (Petro), Andrea, Yakobo mwana wa Zebedayo, Yohana mwana wa Zebedayo, Filipo, Bartholomayo, Tomasi, Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mzeloti na Yuda Iskarioti.
Katika Marko: Simoni (Petro), Andrea, Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana mwana wa Zebedayo (ambaye aliwaita Boanerge, yaani, wana wa ngurumo), Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomasi, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mzeloti, na Yuda Iskarioti.
Katika Luka: Simoni (Petro), Andrea, Yakobo, Yohana, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomasi, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni (aitwaye Mzeloti, Yuda mwana wa Yakobo, na Yuda "Iskarioti.
Inawezekana kuwa Thadayo na Yuda, mwana wa Yakobo, ni majina mawili ya mtu mmoja.
Maneno haya yana umuhimu mkubwa wa kitheolojia. Wataalam wanajadili ikiwa "ufalme wa mbinguni" ulikuwepo wakati huu au bado unakuja. Tafsiri za Kiingereza mara nyingi hutumia maneno "karibu," lakini hii inaweza kusababisha changamoto katika kutafsiri. Matoleo mengine hutumia maneno "inakaribia" na "yamekaribia."
Hii inafungua habari ya Yesu akiwatuma wanafunzi wake wakafanye kazi yake.
"Akawaelezea wanafunzi wake 12"
Uwe na uhakika kwamba ujumbe unakuwa wazi kuwasilisha kwamba haya mamlaka yalikuwa 1) ni kufukuza roho chafu na 2) kuponya magonjwa na udhaifu
"kuwafanya roho wachafu waondoke"
"kila ugonjwa na kila udhaifu." Maneno "ugojwa" na "udhaifu" ni kama yanakaribia kufanana lakini yanapaswa kutafsiliwa tofauti kama inawezekana. "Ugonjwa" ni kisababishi cha mtu kuwa dhaifu. "Udhaifu" ni ukosefu wa nguvu mwilini au kisababishi ambacho matokeo yake ni kuwa na ugonjwa.
Hapa mwanadishi anatoa majina kumi na mbili ya mitume kama taarifa ya itoayo picha ya nyuma.
Neno hili limetumika hapa kuonesha mwanzo wa simulizi jipya. Hapa Mathayo anaonesha historia ya maisha ya mitume kumi na wawili.
Hili kundi ni sawa na kusema "wanafunzi kumi na wawili" katka 10:1
Hi ya kwanza kwa mpangilio si kwa safu
Hii inaweza kumaanisha yafuatayo 1) "Mkananayo" hii ni sifa iliyoonesha kuwa alikuwa ni mshirika wa kundi lililotaka kuwaweke huru wayahudi kutoka kwenye utawala wa Warumi. "Mzalendo" au "mmajumui" au 2) Mkereketwa ni neno linalonesha mtu mwenye kutamani kumjengea heshima Muungu. "mwenye uchu"
"Mathayo ambaye alikuwa mtoza ushuru"
"ambaye atamsaliti Yesu"
Hapa Yesu anaanza kutoa maelekezo kwa wanafunzi wake juu ya jinsi wanavyopaswa kufanya na wategemee nini wakienda kuhubiri.
Ijapokuwa mstari wa tano unaanza kwa kusema kuwa alaiwatuma thenashara, Yesualiwapa maelekezo haya kabla ya kuwatuma.
"Yesu aliwatuma hawa wanaume kumi na wawili" au "Walikuwa ni hawa wanaume kumi na wawili ambao Yesu aliwatuma"
Yesu aliwatuma kwa kusudi maalumu.
"Naye aliwaambia kitu gani walipaswa kutenda" au "aliwaamuru wao"
Hiki ni kirai kinacholinganisha taifa zima la israel na kondoo ambao wamejitenga kutoka kwa mchungaji
Haya maelezo yana maanisha taifa la Israel. "watu wa Israel" au "kizazi cha Israel"
Kiwakilishi "mna" ni cha wingi na kinamaanisha mitume kumi na wawili.
Hiki kirai cha "ufalme wa mbinguni", kinapatikana katika injili ya Mathayo tu. Kinamaanisha Mungu ni mfalalme. kama inawezekana tumia neno "mbinguni" katikatafsiri zako. "Mungu wetu wa mbinguni atajidhihirisha mapema kuw a yeyeni mfalme. Tazama ilivyotafsiriwa katika 3:1
Yesu anaendele kuwaelekeza wanafunzi wake mambo ya kufanya watakapoenda kuhubiri.
Hivi ni viwakilishi vya wingi vinavyomaanisha mitume kumi na wawili
kuna taarifa hapa ambazo hazikuelezwa, lakini inaeleweka . " Nilwasaidia na kuwafundisheni neno la Mungu bure. Kwa hiyo msiwafanye watu wengine wawalipe kwa lengo la kuwasaidia au kuwafundisha ukweli wa Munugu.
Hizi ni metali ambazo zilitumika kutengeneza sarafu. Hii orodha ni ya hela, ikiwa metali hazijulikani katika eneo lako, tafasiri orodha kama"hela."
Hii ina maana "mkanda" au "mkanda wa fedha," lakini kinamaanisha chochote kinachotumika kubebea hela. Mkanda ni kitu kirefu cha kujifunga cha nguo au ngozi kinachopita begani. Kilikuwa ni kipana ambacho kiliweza kukunjwa na kutumiwa kubeba hela
Hii inaweza kuwa begi lolote linalotumika kubeba kitu safarini au begi linalotumiwa na mtu mmoja kukusanya chakula au hela.
Tumia neno hilo hilo ulilotumia kwa "nguo"
"mfanyakazi"
Hapa "chakula" Kitu chochote ambacho ni hitaji kwa mtu.
Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu nini wanachopaswa kufanya watakapoenda kuhubiri.
Hivi viwakilishi vinaonyesha mitume kumi na wawili
"Kwa "Kila mji au kijiji" mtakachokwenda" au
"kijiji kikubwa...kijiji kidogo" au "mji mkubwa...mji mdogo." Tazama ilivyotafsriwa katika 9:35.
Katika 10:11-13 "anayestahili" inamaanisha mtu aliyetayari kuwakaribisha wanafunzi wa Yesu. Yesu anamlinganisha mtu asiyekuwa tayari kuwakaribisha wanafunzi wake saw namtu asiyestahili
Maana halisi ya sentensi hii inaweza kuwa sahihi kama itasemwa "mkae katika nyumba ya huyo mtu mpaka mtakapoondoka kwenye huo mji au kijiji"
Kirai cha "salimieni" inamaanisha isalimuni hiyo nyumba. Salamu ya kawaida kwa nyakati zile ilikuwa "amani iwe katika nyumba hii. "Kaya" inamaanisha watu wanao ishi kwenye hiyo nyumba. mkiwa mnaingia kwenye nyumba, muwasalimu watu wanaoishi ndani yake.
"Nyumba" inamaanisha wale wanaoishi kwenye hiyo nyumba. "watu wanaoishi kwenye nyumba hiyo wakiwakaribisha vizuri" au kaya ile iwakiwakarimu vizuri"
Neno "pale" linamaanisha kaya. Nyumba hapa inamaanisha watu wanaoishi kwenye hiyo nyunba. Amani yenu ibaki pale" au "watu wanaoishi katika nyumba ile wataishi katika amani"
Hii ni amani ambayo mitume wanapaswa kumwomba Mungu awape wanaoishi katika nyumba.
Neno "pale" linamaanisha nyumba . "Nyumba" inamaanisha kaya. "ikiwa hawatawakaribisha vizuri" au ikiwa hawatawakarimu"
Yamkini ina maana zifuatazo: 1) Ikiwa nyumba haistahili, ndipo Mungu atazuia amani au baraka katika nyumba hiyo au 2) Ikiwa kaya haistahili, ndipo mitume walipaswa kufanya kitu, kama vile kumwomba Mungu asikubali heshima ya salaam za amani. Ikiwa lugha yako ina maana kama hii ya kurudisha salaam au matokeo, hivyo itumike hapa.
Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake cha kufanya watakapoenda kuhubiri
"Ikiwa hakuna watu watakaowakaribisha au kuwasikia katika mji huo"
Hivi ni viwakilishi vya wingi ambavyo vinamaanisha mitume kumi na mbili
Hapa "maneno" inamaanisjha kile ambacho wanafunzi wa Yesu watasema. "kusikiliza ujumbe wenu" au "kusikiliza kile mnachotaka kusema"
Unaweza kutafsiri kama ulivyofanya kwa njia hiyo hiyo
"jipanguseni mavumbi y a miguu yenu mnapoondoka." Hii ni ishara inayoonesha kuwa Mungu amaewakataa watu wa mji au nyumba hiyo.
"Nawaambia ukweli." Kirai hiki kinaongeza msisitizo kwa kile ambacho Yesu atasema baadaye.
"mateso yatakuwa machache"
Hii inamaanisha watu walioishi Sodoma na Gomora."watu ambao waliishi katika miji ya Sodoma na Gomora"
Hii inamaanisha watu katika mji ambao hawakutaka kuwapokea mitume au kusikiliza ujumbe wao. "Watu wa mji huo ambao hawakuwapokea"
Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake. Hapa anaanza kuwaambia wao kuhusu dhiki ambayo wanatakiwa kuvumilia pindi watapoenda kuhubiri.
Neno "Angalia" hapa linaongeza na kusisitiza ambacho kitafuatia. "Tazama"au "Sikiliza" au "Zingatia kile ninachotaka kukuambia"
Yesu anawatuma kwa kusudi maalum.
Kondoo ni wanyama wasioweza kuijhami ambao mara kwa mara hushambuliwa na mbwa mwitu. Yesu anasema kuwa watu wanaweza kuwaumiza wanafunzi wake. "Kama kondoo katikati ya mbwa mwitu hatari" au "kama kondoo katikati ya watu wenye tabia kama hizo.
Yesu awaambia wanafunzi wake ili wawe na tahadhari na wasiowamiza watu. Kama kuwafananisha wanafunzi na nyoka au na njiwa kunachanganya, basi ni vizuri kutokuutumia huu mlinganyo. "fanya kwa kuelewa na tahadhari, vile vile kwa makini na wema."
Unaweza kutafsiri kwa kutumia "kwa sababu" ili kuonnesha jinsi hizi sentensi zinavyohusiana. "Muwe waangalifu na watu kwa sababu watawapeleka
"watawasaliti kwa" au "watawakabidhi Kwa" au watawakamata na kuawajaribu"
"mahakama" Hawa ni viongozi wa kidini au wazee ambao kwa pamoja wanalinda amani katika jamii.
"kupiga kwa mijeledi"
AT:"katikati ya watu ambao ni kama mbwa mwitu wa hatari" au "katikati ya watu ambao watenda kama wanyama wa kutisha" au "katikati ya watu ambao watakuvamia wew"
Hii inaweza kuelezeka katika muundo tendaji "watawaleta" au "watawaburuza"
"kwasababu ninyi ni wangu" au "kwa sababu mnanifuata mimi"
Kiwakilishi "kwao" inamaanisha huenda wakawa "magavana au wafalme" au kwa washitaki wa kiyahudi
Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu dhiki wanayotakiwa kuvumilia pindi watapoenda kuhubiri
kiwakilishi "msi" na "yenu" vinamaanisha mitume kumi na wawili
"msiwe na hofu"
"jinsi gani ya kuongea au nini cha kusema." Haya mawazo mawili yanaweza kujumuishwa:"Ni nini cha kusema"
Hii inaweza kutafsirika katika mfumo tendaji. "Kwa kuwa Roho mtakatifu atawapa cha kusema"
Hapa wakati" unamaanisha "muda huohuo" au "kwa muda huo"
Kipindi watu watakapowashitaki kwenye mabaraza.""watu" hapa ni wale wale "watu"
Ikiwa muhimu, inaweza kutafsiliwa kama "Roho ya Mungu baba yako aliye mbinguni" au nyongeza inaweza kuongezwa ili kufafanua kwamba inamaanisha Roho ya Mungu baba na sio roho ya baba wa ulimwengu.
Hii ni sifa muhimu ya Mungu.
"kupitia ninyi"
Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu dhiki wanayotikiwa kuvumilia pindi watakapoenda kuhubiri
Kirai hiki cha "baba na mtoto wake" kinawza kutafsiriwa kama sentensi timilifumilifu. Ndugu atamwinukia ndugu na kumwua, na baba atamwinukia mtoto wake na kumwua"
"saliti" au "kumtoa" Tazama ilivyotafsiriwa kwenye 10:6
Nomino dhania "kifo" inaweza kutafsiriwa uthabiti, kwa uwazi zaidi. "mahakamani il mamlaka iweze kuwahumu
"kupigana dhidi" au "kwenda kinyume dhidi ya"
Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo tendaji. "na kuwaweka katika kifo" au "na wenye mamlaka kuwaweka katika kifo"
Hii inaweza kutafsirika katika muundo tendaji. "Kila mtu atawachukia" au "Watu wote watawachukia ninyi"
Hiki ni kiwakilishi cha wingi kichonamaanisha mitume kumi na mbili.
Hapa "jina" inamaanisha ukamilfu wa nafsi "kwa sababu yangu" au "kwa sababu mlinitumaini mimi"
" atakayebaki kuwa mwaminif."u
"yeyote atakayekuwa mwaminifu"
Neno "hapa" halina maana ya mji maalumu. "mji mmoja"
"mwende mji unaofuata"
"Nawaambia ukweli." Kirai hiki kinaongeza msisitizo wa kile ambacho Yesu atasema baadaye.
Yesu anaongea juu yake mwenyewe
"amewasili"
Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu dhiki wanayotakiwa kuvumilia wakati watakapoenda kuhubiri.
Yesu anatumia mithali kuwafundisha wanafunzi wake ukweli wa jumla. Yesu anasisitiza kwamba wanafunzi wake wasitegeme watu kuwatendea vizuri kuliko walivyomtendea Yesu.
"Mwanafunzi daima si wa mhimu kuliko mwalimu wake". Mwalimu daima ni wa mhimu kuliko mwanafunzi wake.
"na mtumwa daima si wa mhimu kuliko bwana wake" au "na bwana daima ni wa muhimu kuliko mtumwa wake"
"Mwanafunzi atalizika pale atakapokuwa kama mwalimu wake"
Kama inawezekana, unaweza kueleza dhahIri jinsi mwanafunzi anavyofanyika kuwa kama mwalimu, "Ajue kma mwalimu anavyojua"
Kama inawezekana uieleze dhahiri jinsi mtumwa anvyoweza kuwa kama bwana ." "na mtumishi atarizika pale tu atakapokuwa na umuhimu kama Bwana wake"
Kwa mara nyingine Yesu anasisitiza kuwa kama watu walimtenda vibaya, hivyo wanafunzi wategemee kufanyiwa hivyo au zaidi.'
" majina yale wanayotumia kuwaita watu wa nyumba yake hakika yatakuwa mabaya zaidi" au "kwa hakika wataita watu wa nyumba yake majina mabaya zaidi"
"kwa watu wamemwita"
Yesu anatumia hiii kama msemo kwa ajili yake
Hili jina linaweza 1) likaelezwa moja kwa moja kama "Belzabuli" au "2) Kutafsiri kama asili yake, kumaanisha "shetani"
Hii ni sitiari kwa maana ya wanafunzi wa Yesu
Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu dhiki wanayopaswa kuivumilia wakati watakapoenda kuhubiri.
Hapa "wao" inamaanisha watu wanaowatenda vibaya wafuasi wa Yesu
Hizi sentensi zote mbili zinamaanisha kitu kilekile. Yesu anasisitiza kuwa Mungu atayafichua mabo yote. Hii inaweza kutafasiriwa katika mafumo tendaji. "Mungu atafunua mambo ambayo watu wanayaficha."
Sentensi zote hizi mbili zinamanisha kitu kilekile. Yesu anasisitiza kuwa wanafunzi wanapaswa kumwambia kila mmoja kile anachowaambia wanafunzi sirini. "Waambie watu mchana kile ninachokuambia gizani, na tangazeni mkiwa juu ya nyumba kile mnchosikia kwenye masikio yenu"
Hapa "giza" linamaanisha "sirini" Ninachowaambia kisirisiri" au "mambo ninayowaambia peke yenu"
Hapa neno :nuruni" linamaanisha "kwa uwazi. "Semeni kwa uwazi" au "semeni katika umma"
Hii ni namna ya kusema kunakomaanisha kunong'ona. "Kile ninachowanong'onezea"
mapaa ya nyumba wakati wa Yesu yalikuwa ya bapa, hata watu wali mbali wangeweza kumsikia mtu anapokuwa anaongea kwa sauti ya juu. Hapa mapaa ya nyumba yanamaanisha mahali popote ambapo watu wanaweza kusikia. "Ongea kwa sauti katika eneo la umma ili watu wote wasikie"
Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake juu ya dhiki amabyo wanapaswa kuivumilia wakati watakapoenda kuhubiri
Hapa Yesu pia anaanza kutoa sababa kwa nini wanafunzi wake hawapaswi kuiogopa dhiki ambayo itawapata.
Hii haina maana ya kutenganisha kati ya watu wanaoweza kuua mwili na wale wanaoweza kuua roho. Hakuna mtu anayeweza kuua roho. "Msiwaogope watu. Wanaweza kuua mwili, lakini hawawezi kuua roho"
Hii inamaanisha kusababisha mauti ya mwili. Ikiwa maneno haya ni magumu, yanaweza kutafsiriwa kama "kukua wewe" au "Kuua watu wengine."
Sehemu ya mtu inayoweza kuguswa, tofauti na roho au nafsi isiyoweza kuguswa.
kudhuru watu baada ya kufa
sehemu ya mwanadamu ambayo haiwezi kuguswa na ambayo inaishi baada ya kifo cha mwili
unaweza kuongeza "kwa sababu" ili kufafanua kwa nini watu wamwogope Mungu. "Mwogopeni Mungu kwa sababu yeye anaweza"
Yesu anaieleza mithali hii kwa njia ya swali kuwafundisha wanafunzi wake. "Fikiria kuhusu mashomoro . Wana thamani ndogo sana kiasi kwamba unaweza kuwanunua wawili kwa salafu kidogo.
Hawa ni ndege wadogo, wanaokula mbegu. "ndege wadogowadogo"
Hii mara nyingi inatafsiriwa kama sarafu yenye thamani ndogo kabisa katika nchi. inamaanisha sarafu ya shaba thamani yake ni sawa na sehemu ya kumi na sita ya malaipo ya kibarua. "kiasi kidogo cha fedha"
Haya maelezo yanaweza kutafsiriwa kataika mfumo tendaji. "Baba yenu anafahamu hata shomoro mmoja akifa na kuanguka chini"
Hii ni sifa muhimu ya Mungu
Hii inaweza kuelezeka katika mfumo tendaji. "Mungu anajua hata kiasi cha nywele kichwani pako"
"zimehesabiwa"
"Mungu anawathamini kuliko mashomoro wengi"
Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu sababu kuhofia dhiki ambayo itawapata
"yeyote atakayewaambia wengine huyo ni mwanafunzi wangu" au "Yeyote anayekubali mbele za wengine kwamba yeye ni mwamanifu wangu"
Unaweza kuifafanua hiyo ili ieleweke wazi. "nami nitamkiri mbele za Mungu wangu aliye mbinguni kwamba hawa watu ni wangu"
"Baba wa mbinguni"
Hii ni sifa muhimu ya Mungu"
"yeyote atakayenikana mbele za watu" au "yeye atakayenikataa mbele za watu" au "yeyote atakayekataa kunitambua mimi kwa wengine kuwa yeye ni mwanafunzi wangu"
Unaweza kulifafanua kwa uwazi unaoweza kueleweka. "Nitamkana mbele ya Baba aliye mbinguni kuwa huyu ni wangu"
Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu sababu kutohofia dhiki ambayo itawapata.
"Msidhani" au "msilazimike kufikiri"
Hii inamaanisha watu wanaoishi duniani. "kwa watu wa duniani" au "kwa watu"
Hii inamaanisha mgawanyiko, mapigano, na mauji kati ya watu
"kugeuka" au "kugawanya" au "kutenganisha"
"mwana dhidi ya baba yake"
"Adui wa mtu" au "Adui mbaya wa mtu"
"watu wa familia yake"
Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu sababu kutohofia dhiki itakayowapata.
Hapa "ana" anamaanisha mtu yeyote kwa ujumla. "Wale ambao ... hawastahili" au "Kama uta... haustahili"
Neno la "upendo" hapa linamaanisha upendo wa ndugu" au "upendo kutoka kwa rafiki." "KuMjali" au "aliyejitoa kwa" mwenye kupenda"
"anafaa kuwa wangu" au "anastahili kuwa mwanafunzi wangu"
"bebea msalaba wake na kunifuata" Huu ni mfano wa kuwa tayari kufa. Kubeba msalalba inamaanisha utayari wa kuteseka na kufa. "lazima anitii kiasi cha kukubali kuteseka na kufa"
"chukua" au "beba na kunyanyua"
Yesu anatumia mithali kuwafundisha wanafunzi wake. Haya yatafsiriwa kwa maneno machache kwa kadri iwezekanavyo. "Wale wanaotafuta... watayapoteza ... wale wanaoyapoteza ... watayapata" au "wakaoyapata ... uta watakaopoteza ... watapata" au "ikiwa utayapata ... utakosa ... ikiwa utayakosa...utayapata."
Hii ni sitiari ya "kutunza" au "kuhifadhi"" jaribu kuhifadhi" au "jaribu kutunza"
Hii haina maana kwamba mtu atakufa. Ni sitiari " inayomaanisha kuwa mtu hatakuwa na maisha mazuri ya kiroho na Mungu. "Hatakuwa na maisha ya kweli"
Hii haimanishi kufa. Ni sitiari Inayomaanisha mtu kumtii Yesu ni muhimu zaidi kuliko maisha yake. "ambaye anayejikana"
"kwa sababu ananitumaini mimi" au "kwa ajili yangu" au "kwa sababu yangu" Hili ni wazo lile lile kama "kwa ajili yangu" katika 10:6
Tafsiri nyingine:"Wale ambao hawatabeba....sio" au "ikiwa hautabeba...wewe sio" au "endapo utakapobeba ... wewe sio
Huu msemo maana yake "atapata maisha ya kweli"
Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu kutohofia dhiki itakayowakabili.
Neno "yeye" linamaanisha mtu yeyote. "yeyote" au "yeyote ambaye" au " ambaye"
Inamaanisha kumkaribisha mtu kama mgeni
Kiwakilishi "wa" kinamaanisha mitume kumi na wawili ambao Yesu anawaaambia.
Yesu anamaanisha ni sawa na kumkaribisha yeye. "ni kama ananikaribisha mimi" au "ni kama vile alikuwa ananikaribisha mimi"
Hii inamaanisha wakati mtu anamkaribisha Yesu ni sawa na kumkaribisha Mungu. "ni kama vile kumkaribisha Mungu aliyenituma"
Hapa kiwakilishi cha "ni" kinamaanisha mtu anayekaribishwa.
Hii inamaanisha zawadi ambayo Mungu anampa nabii. wala siyo zawadi ambayo nabii anampatia mtu mwingine.
Hapa "wa" haimaanishi mtu anayekaribisha. Inamaaanisha mtu anayekaribishwa.
Hii inamaanisha zawadi ambayo Mungu humpa mtu wa haki, siyo zawadi ambayo mtu wa haki humpatia mtu mwingine.
Yesu anamalizia kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu kitu cha kufanya na nini watarajie watakapoenda kuhubiri.
"yeyote ambaye atampatia."
"mmoja wa hawa wanyenyekevu" au "hawa wasio wa muhimu," Kirai "mmoja wa" mmoja kati ya wanafunzi waYesu.
"Ninawambia ukweli." Kirai hiki kinongeza msisitizo wa kile Yesu atakachokisema baadaye.
Kiwakiloishi "ha" na "yake" kinamaanisha mtu yule anayetoa.
"kwamba mtu hakika atapokea thawabu yake"
"Mungu hatamkana." "kukanwa" Hii haimanishi kutoweka kwa mali. Hii inaweza kuelezeka kwa mfumo tendaji. "Kwa hakika Mungu atampatia"
Yesu aliwapa wanafunzi wake kumi na wawili mamlaka ya kutoa pepo wachafu, na kuponya magonjwa ya kila namna.
Jina la mwanafunzi ambaye angemsaliti Yesu alikuwa Yuda Iskariote.
Yesu aliwatuma wanafunzi wake kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli tu.
Hapana, wanafunzi hawakupaswa kubeba pesa yoyote au mavazi ya ziada.
Wanafunzi walipasa kutafuta mtu ambaye ni anayestahili katika kijiji na kukaa mpaka walipoondoka.
Hukumu katika miji ambayo haikuwapokea wanafunzi au kusikiliza maneno yao itakuwa mbaya zaidi kuliko hukumu ya Sodoma na Gomora.
Yesu alisema watu wangewapeleka wanafunzi kwenye mabaraza, watawapiga na kuwapeleka mbele ya wakuu na wafalme.
Roho wa Baba ataongea ndani ya wanafunzi watakapokuwa wamekamatwa
Yesu alisema wataokolewa wale watakaovumilia hadi mwisho.
Wale waliomchukia Yesu pia wangewachukia wanafunzi wake.
Tusiwaogope wale wauao mwili lakini hawawezi kuua roho.
Tunapaswa kumwogopa yeye awezaye kuangamiza mwili na roho katika jehanamu
Yesu atamkiri yeye mbele za Baba yake wa mbinguni
Yesu pia atamkana mtu huyo mbele Baba wa mbinguni
Yesu alisema kwamba alikuja kuleta mgawanyiko hata ndani ya familia.
Mtu anayepoteza maisha yake kwa ajili ya Yesu atayapata maisha yake.
Mtu ambaye humpatia hata kikombe cha maji baridi kwa mwanafunzi asiye na umuhimu atapokea zawadi yake.
1Ikawa baada ya Yesu kumaliza kuwaelekeza wanafunzi wake kumi na wawili aliondoka pale kwenda kufundisha na kuhubiri katika miji yao.2Na Yohana akiwa gerezani aliposikia habari juu ya matendo ya Kristo, alituma ujumbe kupitia wanafunzi wake,3na wakamuuliza, “Wewe ni yule ajaye, au kuna mwingine tunapaswa kumtazamia?”4Yesu akajibu na kusema kwao “Nendeni mkamwambie Yohana yale mnayoyaona na yale mnayoyasikia.5Vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wakoma wanatakaswa, viziwi wanasikia tena, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa habari njema.6Na amebarikiwa yule asiyeona shaka juu yangu.7Wakati watu hawa walipoondoka, Yesu alianza kusema na umati juu ya Yohana, “Ni nini mlikwenda kuona katika jangwa, matete likitikiswa na upepo?8Lakini nini mlikwenda kuona huko, mtu aliyevaa mavazi mororo? Hakika, wale wavaao mavazi mororo hukaa katika nyumba za wafalme.9Lakini mliondoka kuona nini - Nabii? Ndiyo, nawaambia, na zaidi ya Nabii.10Huyu ndiye aliyeandikiwa, ‘Tazama, namtuma mjumbe wangu mbele ya uso wako, ambaye ataandaa njia yako mbele yako.’11Mimi nawaambia kweli, kati ya waliozaliwa na wanawake hakuna aliye mkuu kuliko Yohana Mbatizaji. Lakini aliye mdogo katika ufalme wa mbinguni ni mkubwa kuliko yeye.12Toka siku za Yohana Mbatizaji mpaka sasa, ufalme wa Mbinguni ni wa nguvu, na watu wenye nguvu, huuchukua kwa nguvu.13Kwa kuwa manabii na sheria, walikuwa wakitabiri mpaka kwa Yohana.14Na kama mko tayari kukubali, huyu ni Eliya, yule ajaye.15Aliye na masikio ya kusikia na asikie.16Nikifananishe na nini kizazi hiki? Ni mfano wa watoto wanaocheza maeneo ya sokoni, wanaokaa na kuitana17na kusema, ‘Tuliwapigia filimbi na hamkucheza. Tuliomboleza, na hamukulia.’18Kwa kuwa Yohana alikuja bila kula mkate au kunywa mvinyo, na wakawa wanasema, ‘Ana pepo.’19Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa na wakasema, ‘Angalia, ni mtu mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na wenye dhambi!’ Lakini hekima inadhihirishwa kwa matendo yake.”20Yesu alianza kuikemea miji ambamo baadhi ya matendo yake ya ajabu yalitendeka, kwa sababu walikuwa hawajatubu,21Ole wako, Kolazini, Ole wako Bethsaida! Kama matendo makuu yaliyofanyika kwenu yangefanyika Tiro na Sidoni, wangekuwa wametubu zamani kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu.22Lakini nawaambia itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni kustahimili siku ya hukumu kuliko ninyi.23Wewe, Kapernaumu, unadhani utainuliwa hadi mbinguni? Hapana, utashushwa hadi chini kuzimu. Kama kwa Sodoma kungefanyika matendo makuu, kama yalifanyika kwako, ingekuwepo hadi leo.24Bali nasema kwako kwamba itakuwa rahisi kwa nchi ya Sodoma kusimama siku ya hukumu kuliko wewe.25Katika muda huo Yesu alisema, “Nakusifu wewe, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa sababu uliwaficha mambo haya wenye hekima na ufahamu, na kuyaweka wazi kwa wasio na elimu, kama watoto wadogo.26Baba, kwa kuwa ilikupendeza hivyo machoni pako.27Mambo yote yamekabidhiwa kwangu kutoka kwa Baba. Na hakuna amjuaye Mwana isipokuwa Baba, na hakuna amjuaye Baba isipokuwa Mwana, na yeyote ambaye Mwana ana hamu ya kumfunulia.28Njooni kwangu, ninyi nyote mnaosumbuka na mnaolemewa na mzigo mzito, nami nitawapumzisha.29Jitieni nira yangu na mjifunze kutoka kwangu, kwa kuwa mimi ni mnyenyekevu na mpole wa moyo na mtapata pumziko la nafsi zenu.30Kwa kuwa nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.”
Baadhi ya tafsiri huingiza kidogo mistari ya nukuu kutoka kwa Agano la Kale. ULB inafanya hivyo kwa mistari ya nukuu zilizotajwa katika 11:10.
Wasomi wengine wanaamini kwamba Mathayo 11:20 huanzisha hatua mpya katika huduma ya Kristo kwa sababu ya kukataliwa kwake na Israeli.
Baada ya Mathayo 11:20, Yesu anaanza kufunua habari kumhusu yeye mwenyewe na kuhusu mipango ya Mungu Baba, huku akificha habari hii kwa wale wanaomkataa. (Angalia: Mathayo 11:25)
Maneno haya yana umuhimu mkubwa wa kitheolojia. Wataalam wanajadili ikiwa "ufalme wa mbinguni" ulikuwepo wakati huu au bado unakuja. Tafsiri za Kiingereza mara nyingi hutumia maneno "karibu," lakini hii inaweza kusababisha changamoto katika kutafsiri. Matoleo mengine hutumia maneno "inakaribia" na "yamekaribia."
Huu ni mwanzo wa sehemu mpya wa simulizi amabapo mwandishi anaonesha jinsi ambavyo Yesu aliwaijibu wanafunzi wa Yohana Mbatizaji.
Hiki kirai kinaibadilisha kutoka habari ya mafundisho ya Yesu kwenda kile kilichotokea baadaye. "Kisha" au "baadaye"
"kufundisha" au "kuamurisha".
Hii inawahusu wale mitume kumi na wawili waliochaguliwa na Yesu.
Kimilikishi "yao" kinamaanisha Wayahudi wote kwa ujumla
Neno hili limetumika hapa kuonesha mwanzo katika habari kuu. Mathayo anaanza kusimulia habari mpaya
"Wakati Yohana, akiwa gerezani aliposikia juu ya" au "Yohana alipoambiwa na mtu, wakati akiwa gerezani kuhusu, "Ingawa Mathayo hajawaambia wasomaji kwamba mfalme Herode alikuwa amemfunga gerezani Yohana mbatizaji, wasomaji wa kwanza wangekuwa wanaielewa habari na maana yake. Mathayo atatoa habari za Yohana mbatizaji baadaye, kwa hiyo yawezekana si vizuri kufafanua zaidi hapa.
Yohana Mbatizaji aliwatuma wanafunzi wake ujumbe kumpelekea Yesu.
kiwakilishi "mu'' kinamrejea Yesu.
"Wewe ndiye yule amabye tunamtarajia kuja." Hii ni namna nyingine ya kumaanisha Masihi au Kristo.
''Tunapaswa kumtazamia mwingine." kiwakilishi "tu" kinarejerea ,wayahudi wote, siyo wanafunzi wa Yohana pekee.
"mwambieni Yohana''
Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo tendaji. "Ninawaponya wenye ukoma"
Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. " Ninawafanya wale waliokufa kuwa hai tena
Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji "Ninawaambia wahitaji"
Hapa neno "shaka" ni nahau inayomaanisha kupoteza imani. "mtu asiyeachca kuamini kwa sababu ya kile ninachofanya" au "mtu asiyeona mashaka kwa sababu yangu"
Yesu anaanza kusema na makutano kuhusu Yohana mbatizaji.
Yesu alitumia swali ili kuwafanya watu wafikiri kuhusu Yohana kuwa ni mtu wa aina gani." Kwa hakika hamkuenda jangwani kuona tete ... upepo.
Hii inaweza kumaanisha 1) majani halisi ya mto Yorodani au 2) Yesu anatumia sitiari kumaanisha aina ya mtu. "mtu anayebadili fikra zake ni kama tete linalopeperushwa na upepo.
Hii inaweza kutafsirwa katika mfumo tendaji. "yumbishwa na upepo" au "peperushwa na upepo"
Yesu anatumia swali ili kuwafanya watu wafikiri juu ya Yohana kuwa ni mtu wa aina gani. Kwa kweli hamkwenda jangwani ili kuona mtu ... aliyevaa?
"kuvaa mavazi yenye gharama kubwa." Watu majiri walivaa mavazi ya aina hii.
Hili neno, linaongezea msisitizo kwa kile kinachofuata. "kwa kweli"
"ikulu za wafalme"
Yesu aliendelea kuongea na umati kuhusu Yohana Mbatizaji.
Katika mstari wa 10, Yesu anamnukuru nabii Malaki kuonyesha kuwa maisha na huduma ya Yohana imetimiza unabii.
Yesu anatumia swali ili kuwafikirisha watu juu ya Yohana mbatizaji kuwa ni mtu wa aina gani. "Lakinini kweli kwamba mlienda jajngwani kumuona nabii"
Kiwakilishi cha wingi ''nyinyi'' inarejelea kwa katika hali zote.
Hii inaweza kutafsirika kama sentensi timilifu. "Siyo nabii wa kawaida" au ''siyo mtu wa kawaida'' au ''ni wa muhimu kuliko nabii wa kawaida''
Hii inaweza kutafsirika katik mfumo tendaji. "Hiki ndicho nabii Malaki aliandika zamamni za kale kuhusu Yohana mbatizaji"
Kiwakilishi ''na'' na ''wangu'' kinamrejea Mungu. Malaki ananukuu ambacho Mungu alisema.
Kiwakilishi "wako" ni cha umoja kwa sababu Mungu alikuwa anasema juu ya Masihi katika nukuu.vPia "uso" inamaanisha nafsi timilifu, "mbele yako" au "kutangulia"
Hii ni sitiari inayomaanisha kuwa mjumbe atawaandaa watu kupokea ujumbe wa Masihi.
Yesu aliendelea kuwaambia makutano juu ya Yohana Mbatizaji
"Nawaambia ukweli." Kirai hiki kinaongeza msisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye.
Hii ni namna ya inayomaanisha watu wote. "kati ya watu wote waliopata kuishi"
Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. ''Yohana Mbatizaji ni mkuu zaidi" au " Yohana mbatizaji ni wa muhimu zaidi".
Ha " ufalme wa mbinguni" unamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. Kirai "ufalme wa mbinguni" kimetumika katika injili ya Mathayo tu. Kama inawezekana jaribu kutumia "mbinguni" unapotafsiri. "aliye mdogo kabisa katika utawala wa Mungu wetu mbinguni"
'' wa muhimu kuliko Yohana''
''Tokea muda ambao Yohana alianza kuhubiri ujumbe''
Kuna maana nyingi zinzazoweza kumaanisha katika mstari huu. 1) Watu wengine huutumia ufalme wa Mungu kwa malengo yao binafsi. na kwamba wako tayari kutumia nguvu dhidi ya watu wengine ili kutimiza hitaji hili. 2)Tafsiri zingine zingine zinatumia maana sahihi kwamba wito wa kuingia katika ufalme wa mbinguni kimekuwa ni kitu cha muhimu, kwamba watu lazima wapokee kwa kuzingatia kabisa. ili kuupokea wito na kuzuia majaribu ya kufanya uovu. 3 )Watu wenye nguvu wanawadhuru watu wa Mungu na kujaribu kumzuia Mungu asitawale.
Yesu aliendelea kuongea na umati juu ya Yohana Mbatizaji.
Hapa neno " manabii na sheria"linamaanisha kile ambacho manabii na Musa waliandika katika maandiko. "Kwa kuwa haya ndiyo mambo ambayo manabii na Musa walitabiri katika maandiko mpaka wakati wa Yohana mbatizaji
Kiwakilishi ''mko''kinarejelea watu katika umati.
''Hii inarejelea kwa Yohana Mbatizaji. Hii haimaanishi Yohana Mbatizaji ni sawa na Eliya. Yesu anamaanisha Yohana mbatizaji anatimiza unabii juu ya "Eliya ajaye" au "Eliya anayefuata". "Wakati nabii Malaki aliposema kuwa Eliya atarudi, alikuwa akiongea juu ya Yohana mbatizaji"
Hii ni namna ya kumwambia kila anayesikilza. ''Kila anayenisikiliza''
Hapa ''asikie" inamaanisha kuwa msikivu. " lazima awe mwangalifu kwa kile nisemacho''
Yesu anaendelea kuongea na makutano juu ya Yohana Mbatizaji.
Yesu anaitumia swali kutoa mlinganisho kati ya watu wa nyakati zile na kile amabacho watoto wanaweza kusema katika eneo la soko. "Hivi ndivyo kizazi hiki kilivyo"
''watu wanaoishi sasa'' au ''watu hawa'' au ''ninyi watu wa kizazi hiki''
Yesu anatumia mfano kuwaelezea watu waliokuwa hai kipindi hicho. Anawalinganisha na kikundi cha watoto wanaojaribu kuwavuta watoto wengine ili wacheze nao. Lakini haijarishi aina ya mbinu yeyote wanayotumia, wale watoto wengine hawataungana nao. Yesu anamaanisha kuwa haijalishi kama Mungu alimtuma mtu kama Yohana mbatizaji, anaishi nyikani na kufunga, au mtu kama Yesu, ambaye anasherehekea na wenye dhambi bila kufunga. Watu, hususani Mafarisayo na viongozi wa dini, bado wanabaki wasumbufu na wanakataa kuupokea ukweli wa Mungu
eneo kubwa, la wazi ambapo watu walikuja kuuza na kununu bidhaa zao.
''tu'' inarejelea watoto waliokuwa wamekaa katika maeneo ya soko. ''wa'' ni wingi na inarejelea lile kundi lingine la watoto
''lakini hamukucheza ule muziki mzuri''
Hii inamaanisha waliimba nyimbo za huzuni kama vile wanawake wafanyavyo kwenye mazishi.
''lakini hamukulia pamoja nasi''
Yesu anahitimisha kuongea na makutano kuhusu Yohana Mbatizaji.
Hapa "mkate" unamaanisha chakula. Haimanishi kuwa Yohana alikuwa hali chakula. Inamaanisha kuwa alikuwa anafunga mara kwa mara na alipofungua hakula vizuri, chakula cha gharama. "Mfungo endelevu na kutokunywa pombe" au "kutokula chakula kizuri na kutokunywa divai"
Hii inaweza kutafsiriwa kama nukuu ya mojakwa moja. ''wanasema kwamba ana pepo'' au ''walimtuhumu kuwa na pepo.''
Matukio yote ya "wali" yanamaanisha watu wa kizazi kile, na zaidi sana mafarisayo na viongozi wa dini.
Yesu anamaanisha yeye mwenyewe. " Mimi mwana wa Adamu"
Hiki ni kinyume cha tabia ya Yohana. Hii ni zaidi ya kula kiasi cha kawaida cha chakula na kinywaji. Inamaanisha Yesu alisherehekea na kufurahia chakula na kinywaji kizuri kama vile watu wengine walivyofanya.
Hii inaweza kutafsiriwa kama nukuu ya moja kwa moja. "wanasema kuwa ni mlaji" "wanamtuhumu kuwa anakula sana" Kama ulitafasiri "Mwana wa mtu" kama "Mimi, Mwana wa mtu," Ile nukuu ya moja kwa moja inaweza kutafsiriwa kama "wanasema kwamba mimi ni mlaji"
"mlevi" au "hunywa pombe nyingi daima."
Hii ni mithali ambayo Yesu anaitumia katika mazingira haya, kwa sababu watu waliomkataa yeye na Yohana walikuwa hawapati hekima. Yesu na Yohana mbatizaji ni watu wa hekima, na ,matokeo ya matendo yao yanathibitisha.
Hapa "hekima" imefafanuliwa kama mwanamke aliyethibitishwa kuwa ni mwema kwa matendo yake. Yesu anamaanisha kuwa matokeo ya matendo ya mtu huthibitisha kuwa ni mwenye hekima. "Hii inawza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Matokeo ya matendo ya mtu humthibitisha kuwa ni mwenye hekima"
Haya maelezo, Yesu anafafanua hekima kama vile ilikuwa ni mwanamke, haitumiki hapa kwa namna kwamba hekima inatoa haki mbele ya Mungu ila kwamba hekima inaonekana haki.
Yesu alianza kuwakemea watu wa miji ambayo alianza kufanya miujiza.
Hapa "miji" inamaanisha watu walioishi kwenye hiyo miji. "alikemea watu wa miji hiyo"
''miji''
Hii inaweza kutafsiriwa kwa mfumo tendaji ''ambamo baadhi ya matendo yake makuu yalitendekea''
" matendo makubwa" au " kazi za nguvu ya Mungu" au "miujiza"
Yesu anaongea kiasi kwamba watu wa miji ya Kolazini na Bethsaida walikuwa pale wakimsikiliza, lakini hawakuwa wao.
Kiwakilishi ''hawa'' inarejelea kwa watu wa miji ile ambayo haikutubu.
Yesu anafafanua kwa kubuni kuwa kama yangekuwa yametokea huko nyuma, lakini haikotokea
Hii inaweza kutafsiriwa kwa mfumo tendaji. "Kama ningefanya matendo makubwa katika watu wa Tiro na Sidoni ambayo nimeyafanya kwenu"
Kiwakilishi cha "kwako" ni cha wingi na kinamaanisha Korazini na Bethisaida. Kama tafsiri hii si kawaida ya lugha yako, utumie neno lenye maana mbili likimaanisha miji miwili au kiwakilishi cha wingi cha "ninyi" kwa kumaanisha watu wa miji ile.
Kiwakilishi "wa"kinarejelea watu wa Tiro na Sidoni.
"inaonesha walihuzunishwa na dhambi zao"
Hapa " Tiro na Sidoni'' zinamaanisha watu wanoishi kwenye hiyo miji. "Mungu ataonyesha huruma zaidi kwa watu wa Tiro na Sidoni katika siku ya hukumu kuliko ninyi" au "Mungu atawapa adhabu kalizadi katika siku ya hukumu kuliko watu wa Tiro na Sidoni"
maelezo kusudiwa yangewekwa wazi. "kuliko kwako, kwas sabasbu haukutubu na kuniamini, ingawa ulioniona nikifanya miujiza"
Yesu anaendelea kukemea miji ambayo miujiza yake ilitendeka karibuni.
Yesu sasa anaongea na watu wa mji wa Kapernaum kama vile walikuwa wanamsikiliza, lakini walikuwa hawasikilizi. Kiwakilishi ''wewe'' ni cha umoja kinarejelea Kapernaum kwa mistari yote miwili.
Matukio yote ya kiwakilishi cha "wewe" yakao katika umoja. Kama kinatumika kila mahali kuonyesha watu wa mji, basi kiwakilishi cha wewe kitafsiriwe katika wingi wake
Majina ya miji hii yametumika kumaanisha watu waliokuwa wanaishi Kapernaum na Sodoma.
"unadhani utainuliwa hadi mbinguni ?" Yesu anatumia balagha kuwakemea watu wa Kapernaum kwa majivuno yao. "inaweza pia kutumika kwa mfumo tendaji. "huwezi kujiinua mwenyewe hadi mbinguni" au "sifa za watu wengine haziwezi kukuinua hadi mbinguni kama unavyodhani atafanya"
Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji ''Mungu atakupeleka hadi kuzimu.''
Yesu anatumia mazingira ya kubuni ambayo yangetokea katika siku zilizopita, lakini haikutokea.
''''matendo makuu'' au ''kazi ya nguvu za Mungu'' au "miujiza"
Kiwakilishi ''inge'' kinarejelea kwa mji wa Sodoma
Kirai hiki kinaongeza msisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye
Hapa "nchi ya Sodoma" inamaansha watu walioishi kule. ''Mungu ataonyesha rehema kwa watu wa Sodoma katika siku ya hukumu kuliko kwako'' au Mungu atawapa adhabu kali zaidi katika siku ya hukumu kuliko watu wa Sodoma.''
Taarifa zilizofumbwa ziwekwe wazi. "kwa sababu haukutubu na kuniamini, ingawa uliniona nikifanya miujiza"
katika mstari wa 25 na 26, Yesu anomba kwa baba yake aliye mbinguni wakati akiwa bado katika uwepo wa makutano. Katika mstari wa 27, anaanza kusema na watu tena.
Hi ni sifa muhimu ya Mungu
"Bwana anayetawala mbingu na nchi" Kirai cha mbingu na nchi ni cha mlinganyo wa jumla amabcho kinaonesha watu wote na vitu vyote duniani. ''Bwana atawalaye ulimwenguni kote"
Haiko wazi ina maanisha nini kwa ''mambo haya.'' Kama lugha yako inahitaji kuweka maana halisi, tafsiri nzuri ni hii ''umeuficha ukweli huu na kuwafunulia"
''umewaficha mambo haya '' au ''haujafanya mambo haya kueleweka kwao.'' Hili tendo ni kinyume cha ''kufunuliwa.''
Hizi nomino sifa zinzweza kutafasiriwa kama visifa ''kutokawatu wenye hekima na ufahamu.''
"kuyafanya yafahamike." kiwakilisha "ya" kinamaanisha "mambo haya" viko mwanzoni katika mstari huu.
"kwa wajinga"
Yesu anamlinganisha mtu asiye na elimu na mtoto mdogo. Yesu anasisitiza kwamba wengi wa wale wanaomwamini ni watu wasio na elimu au wanaojidhania kuwa si wenye elimu
kupendeza machoni pako - Hi kirai "machoni pako" ni sentensi mbadala ionyeshayo jinsi mtu apendavyo kitu kuwa ni cha muhimu. "kwa vile ilikupendeza kuwa ni vizuri kufanya hivi"
Hii inaweza kutafasiriwa kwa muundo tendaji: ''Baba yangu amekabidhi mambo yote kwangu'' au ''Baba yangu ameweka kila kitu kwangu."
Maana kusudiwa ni 1)Mungu Baba amefunua kila kitu kuhusu yeye na ufalme wake kwa Yesu. aua 2) Mungu ametoa mamlaka yote kwa Yesu
Hii ni sifa muhimu ya Mungu amabyo inaonyesha uhusiano kati ya Yesu na Mongu
''Ni Baba pekee amjuaye Mwana.''
Nyakati zote Yesu hutumia kirai hiki, neno "ajuaye" linamaanisha zaidi ya kumjua mtu. Linamaanisha kumjua mtu kwa undani kwa sababu wanauhusiano maalumu
Yesu alikuwa anajirejelea yeye mwenyewe binafsi katika nafsi ya tatu.
Hii ni sifa ya muhimu ya Yesu mwana wa Mungu
''Ni Mwana pekee amjuye Baba''
"ni mwana pekeeamjuaye Baba
"na watu wale ambao mwana anapenda kuwafunulia jinsi Mungu alivyo"
Yesu anamalizia kuongea na makutano.
Viwakilishi vyote vya "niniyi" ni vya wingi
Yesu anaongea kwa watu kama na wanyama, amabao bwana zao wamewabebesha mizigo migongoni mwao. Hii ni sitiari kwa ajili ya Sheria na kanuni ambaazo viongozi wa Kiyahudi waliwabebesha watu ili kuzitii. "msumbukao na sheria ambazo mmebeshwa na viongozi wa dini"
''Nitawaruhusu nyinyi kupumzika kazi na mizigo''
Hapa neno"mpole" na "mnyenyekevu wa moyo" ki msingi yanamaanisha kitu kilekile. Yesu anayaunganisha kuongeza msisitizo kuwa atawajali kwa upole zaidi kuliko vioingozi wa . dini. "mimi ni mpole na mnyenyekevu" au "mimi ni mpole sana"
Yesu anaendelea kutumia sitiari. Yesu anawakaribisha watu kuwa wanafunziwake na kumfuata"
Hapa "nafsi" inamaanisha mtu kamili. "mtapumzikia ninyi wenyewe" au "mtaweza kupumzika"
Virai vyote hivi vinamaanisha kitu kilekile. Yesu anasisitiza kuwa ni rahisi kumtii yeye kuliko sheria za Wayahudi. "kile nitakacho wabebesha kitakuwa ni chepesi"
Neno "mwepesi" hapa ni kinyume cha kizito, siyo kinyume cha giza.
Kabla ya kuondoka Yesu akamilisha kuwapa maelekezo wanafunzi wake kumi na wawili.
Yohana Mbatizaji alituma ujumbe, "Wewe ni yule ajaye, au kuna mwingine tunapaswa kumtazamia?"
Yesu alisema wagonjwa walikuwa wanaponywa, wafu wanafufufliwa, na wahitaji kuhubiriwa habari njema.
Yesu aliahidi baraka kwa wale wasiojikwaa dhidi yake.
Yesu alisema Yohana Mbatizaji alikuwa ni mjumbe aliyetabiliwa ambaye angeandaa njia kabla ya kuja yule ajaye.
Yesu alisema kuwa Yohana Mbatizaji alikuwa Eliya.
Watu wa kizazi kile walisema Yohana alikuwa na pepo
KWatu wa kizazi kile walisema mrafi na mlevi, na rafiki wa watoza ushuru na wenye dhambi.
Yesu aliikemea miji ile ambayo alifanya matendo makuu lakini walikuwa bado hawajatubu.
Yesu alimtukuza Baba kwa kuwaficha wenye hekima na akili habari za ufalme wa mbinguni.
Yesu alimtukuza Baba kwa kuwafunua habari za ufalme wa mbinguni wasio na elimu, na ambao wapo kama watoto wadogo
Yesu alisema yeye ndiye anayemjua Baba na yeyote ambaye anapenda kumfunulia.
Yesua aliahidi pumziko kwa wote wanaosumbuka na wenye mizigo mizito.
1Wakati huo Yesu alienda siku ya sabato kupitia mashambani. Wanafunzi wake walikuwa na njaa na wakaanza kuyavunja masuke na kuyala.2Lakini Mafarisayo walipoona hayo, wakamwambia Yesu, “Angalia wanafunzi wako wanavunja sheria wanatenda yasiyo ruhusiwa siku ya Sabato.”3Lakini Yesu akawaambia, “Hamjasoma jinsi Daudi aliyoyafanya, wakati alipokuwa na njaa, pamoja na watu aliokuwa nao?4Namna alivyoingia ndani ya nyumba ya Mungu na kula mikate iliyowekwa wakfu, ambayo ilikuwa siyo halali kwake kuila na wale aliokuwa nao, ila halali kwa makuhani?5Bado hamjasoma katika sheria, kwamba katika siku ya Sabato makuhani ndani ya hekalu huiharibu Sabato, lakini hawana hatia?6Lakini nasema kwenu kuwa aliye mkuu kuliko hekalu yuko hapa.7Kama mngelifahamu hii ina maanisha nini, ‘Nataka rehema na siyo dhabihu,’ msingaliwahukumu wasio na hatia.8Kwa kuwa Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa Sabato.”9Kisha Yesu akatoka pale akaenda katika sinagogi lao.10Tazama kulikuwa na mtu aliyepooza mkono. Mafarisayo wakamuuliza Yesu, wakisema. “Je, ni halali kuponya siku ya Sabato?” ili kwamba waweze kumshitaki kwa kutenda dhambi.11Yesu akawaambia, “Nani kati yenu, ambaye ikiwa ana kondoo mmoja, na huyu kondoo akaanguka ndani ya shimo siku ya sabato, hatamshika na kumtoa kwa nguvu ndani ya shimo?12Je, ni kipi chenye thamani zaidi, kwani mtu si zaidi ya kondoo? Kwa hivyo ni halali kutenda mema siku ya Sabato.”13Kisha Yesu akamwambia yule mtu,” Nyosha mkono wako.” Akaunyosha, na ukapata afya, kama ule mwingine.14Lakini Mafarisayo wakatoka nje na wakapanga jinsi ya kumwangamiza, walienda nje kupanga kinyume chake. Walikuwa wakitafuta jinsi ya kumuua.15Yesu alipojua hili aliondoka hapo. Watu wengi walimfuata, na akawaponya wote.16Aliwaagiza wasije wakamfanya ajulikane kwa wengine.17Kwamba itimie ile kweli, iliyokuwa imesemwa na nabii Isaya, akisema,
Baadhi ya tafsiri hupendelea huingiza kidogo mistari ya nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari yote ya 12: 18-21, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.
Kutii Sabato ni sehemu muhimu katika sura hii. Hata hivyo, Yesu anafafanua kati ya kufuata Sabato jinsi Mungu alivyoamuru na kufuata sheria ambazo Mafarisayo waliziunda kuhusu Sabato.
Kuna utata mkubwa juu ya kutambua vizuri dhambi hii maalum. Hata hivyo, inaonekana kuwa inahusisha kumtukana Roho Mtakatifu na kazi yake. Kwa kuwa sehemu ya kazi yake ni kuwashawishi watu kuwa wao ni wenye dhambi na kwamba wanahitaji msamaha wa Mungu, yeyote ambaye alikejeli ukweli huu hangetaka kuja kwake Mungu kwa toba. Kwa sababu hii, hangeweza kusamehewa.
Sura hii inaanzisha dhana ya kaka na dada "wa kiroho". Maandiko hutumia maneno haya kwa kutaja uhusiano kati ya Waisraeli. Hapa, wale wanaomfuata Yesu sasa wanajulikana kama kaka na dada. na )
Huu ni mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi ambapo mwandishi anazungumza juu ya kukua kwa upinzani kwa huduma ya Yesu. Hapa, Mafarisaya wanawakosoa wanafunzi wa Yesu kwa kuvuna nafaka ya ngano siku ya sabato.
Hii inaonyesha mwanzo mpya wa simulizi. "Baadaye kidogo"
sehemu ya kupanda nafaka. Kama ngano haifahamiki na "nafaka" ni neno la jumla sana, basi waweza kutumia "shamba" la mazao ambayo wanatengeneza mikate."
Kuvuna nafaka kwenye mashamba ya wengine na kula haikuchukuliwa kuwa ni kuiba. Swali lilikuwa kama mwingine angeweza kufanya shughuli hii kisheria katika siku ya sabato.
"kuchukua baadhi ya ngano na kula" au "kuchukua baadhiya mbegu za ngano na kula"
Hii ni shsemu ya juu ya mmea wa ngano ambayo ni aina ya jani kubwa. Hushikilia nafaka iliyokomaa au mbegu za mmea.
Hiihaimanisha mafarisayo wote. "baadhi tu ya mafarisayo"
"angalia." Mafarisayo hutumia neno hili kupata usikifu wa kile wanafunzi wa Yesu walichokuwa wakifanya.
Yesu anajibu ukosoaji wa mafarisayo
Mafarisayo
Yesu anatumia swali kujibu ukosoaji wa mafarisayo. Yesu anawapa changamoto ili kufikiri juu ya maana ya andiko ambalo walisoma. "Najua mmesoma juu yaa...nao"
Wakati wa Daudi bado hapakuwa na hekalu. "hema" au " mahali pa kumwabudia Mungu"
Huu ni mkate uliotakaswa ambao makuhani walipeleka mbele za Mungu hemani. "Mikate ambayo makuhani walipeleka mbele za Mungu
"watu waliokuwa pamoja na Daudi"
"ni makuhani tu walioruhusiwa kuula."
Yesu anaendelea kuwaitikia Mafarisayo.
Yesu antumia swali kijbu hoja za mafarisayo. Yesu anawataka wafikirie maana yakile walichosoma katika maandiko. "And, na mmesoma katika sheria za Musa... lakini hawana hatia.
"kufanya katika sabato ambayo wangefanya katika siku nyingine."
" Mungu hatawaadhibu" au "Mungu hatawaonea hatia"
Hiki kinaongeza msisitizo kwa kile alichosema baadaye.
" aliye wa muhimu zaidi kuliko hekalu." Yesu alikuwa anarejelea kwake yeye mwenyewe kama mmoja aliye mkuu.
Yesu anaendelea kuwajibu Mafarisayo
Katika mstari 7, Yesu anamnukuu nabii Hosea kuwakemea Mafarisayo.
Hapa Yesu ananukuu andiko. "Nabii Hosea aliandika juu ya haya tangu zamani. "Natakarehema na siyo dhabihu. 'Kama mngalielewa hii ilimaanisha nini, msingaliwalaumu wasio na hatia'
Katika sheria za Musa, Mungu aliwaagiza Waisraeli kutoa sadaka. Hii inamaanisha kuwa Mungu huichukulia rehema kuwa muhimu kuliko sadaka.
"nini Mungu amesema katika maandiko"
Kiwakilishi "Na" kinamrejelea Mungu.
Hii inaweza kutafsiriwa katika muundo tendaji. "Wale wasiokuwa na hatia"
Yesu anamaanisha yeye mwenyewe
"anaitawala Sabato" au "anatengeneza sheria juu ya nini watu wanaweza kufanya siku ya Sabato"
Hapa mandhari yanahamia kwenye kitu kingine mahali ambapo mafarisayo wanamkosoa Yesu kwa kumponya mtu siku ya Sabato.
"Yesu akaondoka kwenye lile shamba la ngano" au "Kisha Yesu akaondoka"
"singogi" Hapa "lao" inamaanisha Wayahudi kwa ujumla na wala si Mafarisayo tu, kutokana na kipengere kilichopita.
Neno " tazama" linatuelekeza kwa mtu mwingine katka simulizi. Lugha yako inaweza kuwa na njia ya kulifanya hili.
"mtu alikuwa namkono uliopooza" au "mtu mwenye ulemavu wa mkono"
"Mafarisayo walitaka kumshitaki Yesu kwa kutenda dhambi, kwa hiyo walimuuliza, 'Je, ni halali kuponya siku ya Sabato?"
Kwa mjibu wa sharia za Musa, Yawezekana mtu kumponya mtu mwingine siku ya Sabato?"
Si tu walitaka kumshitaki Yesu mbele za watu, Mafarisayo walitaka Yesu atoa jibu linalopingana na sheria ili waweze kumpeleka kwa hakimu iwamshitaki kwa kuvunja sheria.
Yesu anjibu hoja za Mafarisayo
Yesu antumia swali kuwajibu Mafarisayo. Anawapa changamoto ya kufikiri juu ya aina gani ya kazi wanayoweza kuifanya siku ya sabato. "Kila mmoja wenu, kama una kondoo mmoja ... angemshika na kumtoa kwa nguvu
Kirai "kipi chenye thamani zaidi" kinaongeza msisitizo kwenye sentensi. " ni wazi mtu ni wa thamani zaidi ya kondoo!" au "Jaribu kufiri vile mtu alivyo wa muhimu kuliko kondoo"
"Wale wanofanya mema siku ya Sabato wantii sheria"
Hii inaweza kutafsiriwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja, "Kisha Yesu akamwamuru yule mtu kunyosha mkono wake"
"yule mtu mwenye mkono uliopoza au " yule mtu mwenye ulemavu wa mkono"
"Utoe mkono wako" au "utanue mkon wako"
"Yule mtu akaunyosha"
Hii inaweza kutafsiriwa katika muundo tendaji. "ule mkono ukawa na afya tena" au "ukawa salama tena"
"wakapanga kinyume chake"
Simulizi hii inaeleza jinsi matendo ya Yesu yalivyotimiza moja kati ya unabii wa Isaya
"Yesu alikuwa anatambua kile Mafarisayo walichokuwa wakipanga
"alitoka" au "aliondoka"
wasimwambie mtu yeyote kuhusu yeye"
Hii inaweza kutafsriwa kama sentensi mpya. "Hii ilitimiza kile"
Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "Kile Mungu alichokuwa amesema zamani kupitia Isaya akaisema..
Hapa Mthayo anamnukuu nabii Isaya kuonesha kuwa huduma ya Yesu ilitimiza unabii
"Angalia." Mungu alitumia neno hili kumleta mtu mwingine
Viwakilishi vyote vinamrejelea Mungu. Isaya ananukuu kile ambacho Mungu alimwambia
Hapa "nafsi" inamanisha nafasi kamil. "na nimependezwa naye"
"na mtumishi wangu atatangaza"
Hapa "hukumu" haimaanishi "adhabu" inamaanisha mtumishi atawambia mtaifa Mungu ni mwenye haki, na atawaokoa
Mathayo anaendelea kumnukuu Isaya
hapa "sauti" inamaanisha nafsi kamili "na hataongea kwa sauti"
Viwakilishivyote hivi vinamaanisha mtumishi wa Mungualiyechaguliwa
Hii ni nahau inayomaanisha "umma."katika miji"
Senttensi hizi zote zinamaanisha kitu kilekile. Ni sitiari zinazosisitiza kuwa mtumishi wa Mungu atakuwa mnyenyekevu na mpole. Vyote "tete lililochubuliwa na utambi utoa moshi" vinawakilisha watu dhaifu na wenye kudhuru.
"hataliweka nje"
Hii inamaanisha utambi ambao moto umezima lakini bado unatoa moshi
Hii inaweza kutafsiriwa kwa sentensi mpya; "moshi Hiki ndicho atachofanya"
"mpaka atakapofaulu kuleta haki na wokovu kwa watu. Maana ya nomino dhania "hukumu" inaweza kutafsiriwa kama "haki" au "okoa". "watuwajue kuwa mimi ni wa haki na nitawaokoa"
Hapa "jina" linamaanisha nafsi kamili
Hapa mandhari yanabadilika na kuongelea wakati mwingine wakati Mafarisyao walipomshitaki Yesu kwa kumponyamtu kwa nguvu za shetani.
Hiiinaweza kutafsiriwa katikamfumo tendaji. "Mtu mmoja alimleta kwa Yesu mtu aliyekuwa kipofu na bubu kwa sababu pepo lilikuwa likimtawala"
"mtu asiyeweza kuona na hawezi kuongea"
"Watu wote waliomwona Yesu akimponya yule mtu walishangaa"
Hi ni sifa ya Masihi au Kristo
Hapa hii inamaanisha "kizazi cha"
Katika mastari wa 25, Yesu anaanza kuwajibu mashataka ya Mafarisayo kwamba amemponya mtu kwa nguvu za shatani
Hii inamaanisha muujiza wa kumponya yule kipofu, bubu na alaiyepagawa na pepo.
Hii inaweza kuelezwa katika muundo chanya. "Huyu mtu anaweza kufukuza pepo kwa sababu ni mtumishi wa Belzabul"
Mafarisayo waliepuka kumwita Yesu kwa jina ili kuonesha kuwa hawamkubali.
"mfalme wa pepo"
Yesu anatumia mithali kuwajibu Mafarisayo. Sentenzi hizi mbili zinmaanishakitu kilekile. Zinasisitiza kuwa haimanishi chochote kwa Belzabul kutumia nguvu zake kuwapinga pepo wengine.
Hpa "ufalme" unamaanisha wale wanaoishi kwenye huo ufalme. Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo tendaji. "Ufalme hautadumu wakati wake wanapigana wao kwa wao"
Hapa"mji" unamaanisha watu wanaoishi humo na. "nyumba" inamaanisha familia. "inaharibu mji au familia watu wanapopigana wao kwa wao
Yesu anaendelea kujibu hoja za mafarisayo za kwamba alimponya mtu kwa nguvu za shetani
Matumizi ya pili ya shetani yanamaanisha pepo wanaomtumikia shetani. "Kama shetani atafanya kazi kinyume na pepo zake"
Majina yote yanamaanisha nafsi moja
Yesu anatumia swali kwapa changamoto Mafarisayo. "Ufalme wa shetani hauwezi kusimama" au "ufalme wa shatani hautadumu"
Yesu anatumia swali lingine kuwapa changamoto Mfarisayo. "kisha lazima useme wafuasi wenu pia huwatoa pepo kwa nguvu za beelzabul. Lakini mnajua kuwa hii siyo kweli"
"Kwa sababu wafuasi wenu huwatoa pepo kwa nguvu za Mungu, wanahakikisha kuwa mmekosea."
Yesu anaendelea kuwajibu Mafarisayo
Hapa "kama" haimaanishi kuwa Yesuanahoji jinsi anavyowatoa pepo. Hapa Yesu anatumia neno kuleta sentensi ya kweli. "Lakimi kwa sababu nina"
"Basi ufalme wa mbinguni umefika kwenu." Hapa "ufalme" utawala wa Mungu kama mfalme. "Hii inamaanisha Mungu anaanzisha ufame kwenu"
Hapa "kwenu" ni wingi na inamaanisha watu wa Israel,
Yesu anatumia mfanokuendelea na majibu yake kwa Mafarisayo. Yesu anamaanisha anaweza kuwatoa pepo kwa sababu ana nguvu kuliko shetani.
Yesu anatuumia swali kuwafundisha Mafarisauo na makutano. "Hakuna awezaye kuingia ..bila kumfunga mwenye nguvu kwanza"
"Ndipo atakapoiba" au "Ndipo atakapoweza kuiba"
"ambaye hashirikiani nami" au "amabye hafanyi kazi p amoja nami"
"ananipinga mimi" au "hufanya kazi kinyume na mimi"
Yesu anatumia kirai amabcho kinamunesha mtu amabye aidha anakusanya kundi la wanyama kwa mchungaji au anayewatapanya totka kwa mchungaji.
Yesu anaendelea kuwajibu Mafarisayo
Hii inaongeza msisitizo wakile Yesu alichosema baadaye
Hapa "kwenj" ni wingi. Yesu anaongea moja kwa moja na Mafarisayo, lakini pia anwafundisha makutano
Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "Mungu atasamahe kila dhambi ambayo watu wanafanya na kila jambo ovu wanlosema
Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. "Mungu hatamsamehe mtu yule amabye anasema mabo maovu dhidi ya Roho Mtakatifu.
Hapa "neno" linamaanisha kile amabcho mtu husema, "N kama mtu atasema chchote kibaya kuhusu Mwana wa Adamu"
Yesu anaongea juu yake mwenyewe
Hili linaweza kuelezwa katikamfumo tendaji. "Mungu atamsamehe mtu kwa ajiloi yahilo"
Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. "Mungu hatamsamehe mtu huyo"
Hapa " ulimwengu huu" na " ule ujao" inamaanisha maisha haya ya leo na maisha yajayo. " katika maisha haya au yajayo" au "sasa au baadaye"
Yesu anaendelea kuwajibu Mafarisayo
maana yake ni 1) kama utafanya mti kuwa mziri na mtunda yake yatakuwa mazuri na kama ukiuharibu mti na matunda yake yatakuwa mabaya" au 2) "Kama ukiufanya mti kuwa mzuri na mataunda yake yatakuwa mazuri kwa sababu matunda yake ni mazuri na kama ukiyafanya matunda kuwa mabaya yatakuwa kwa sababu matunda yake ni mabaya." Hii ni mithali watu walipaswa kuutumia ukweli kwa jinsi wawezavyo kujua kama mtu ni mbaya au mzuri.
"eneye afya ... iliyougua"
Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "Watu hujua kama mti n mbaya aua mzuri kwa kutazama matunda yake"
Hapa "kizazi" inamaanisha "kuwa na tabia za." Kipiribao ni aina ya nyoka wenye sumu ambao ni hatarina wanawakilisha uovu"
Hivi ni viwakilishi vya wingi na vinamaanisha Mafarisayo
Yesu anatumia swali kuwakemea Mafarisayo. "huwezi kusema mambo mazuri "Unaweza kusema mambo maovu tu"
Hapa "akiba ya moyoni" inamaanisha mawazo ya mtu katika akil iyake. "Kinywa" kinawakilishsa mtu. "Kile ambacho mtu husema katikakinywa chake kinafunua jinsi alivyo katika akili yake"
Yesu anaongea juu ya "moyo" kama vile kontena lilivyo amablo mtu anaweza kulijaza kwa mambo mazuri au maovu. Hii ni sitiari inayoonesha kile mtu anachosema kinafunua jinsi mtu alivyo.
Yesu anahitimisha majibu yake hoja za Mafarisayo za kwamba alimponya mtu kwa nguvu za shetani.
Msisitizo wa kileYesu alichosema baadaye
"Mungu atawauliza watu kuhusu" au "atu watajieleza mbele za Mungu"
Hapa "neno" inamaanisha kitu ambacho mtu husema. "kila jambo lenye kudhuru watakolokuwa wamesema"
Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo tendaji. "Mungu atakuhesabia haki ... Mungu atakuhukumu"
Maongezi katika mistari hii yananza mara baada tu ya Yesu kujibu hoja za Mafarisayo kwamba alimponya mtu kwa nguvu za shetani
Katikamstari wa 39, Yesu anaanza kuwakemea waandishi na Mafarisayo
"taka"
Unaweza kuiweka wazi kwa nini wanataka kuona ishara "kuona ishara toka kwako ili kuhakikisha kuwa kile unachosema ni kweli.
Yesu anasema na kizazi kilichokuwepo. "ninyi ni waovu na kizazi cha zinaa wanaotafuta ishara toka kwangu ... itakayotolewa kwao
Hapa "zinaa" ni sitiari ya watu wasio waaminifu kwa Mungu.
Ombi hili linamkasirisha Yesu kwa sababu ya mashaka na tabia ya viongozi wa dini juu ya Yesu. Alikuwa amefanya miujiza mingi, lakini bado walikuwa hawamwamini
Hii inaweza kuelezwa katika mmundo tendaji. "Mungu hatawapa ishara"
"isipokuwa ishara ileile amabyo Mungu alimpa nabii Yona"
Hapa "usiku" na "mchana" inamaanisha kipindi cha saa 24 kamili. "siku tatu kamili"
Yesu anaongea juu ya yeye mwenyewe
Hii inammanisha ndani ya kaburi halisi
Yesu anaendelea kuwakemea waandishi na Mafarisayo
"Raia wa Ninawi"
"watasimama siku ya hukumu na kuwahukumu kizazi hiki"
Yesu anamaanisha watu walioishikipindi hiki
Atakuwa Mungu atayekihukumu kizazi cha watu wa Yesu
"na angalia" Hii inatia msisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye
"mtu wa muhimu sana"
Unaweza kifanya maana ya sentensi ya Yesu iliyofumbwa kuwa wazi. "kuliko Yona yuko hapa, Lakini bado hamjatubu, hii ndiyo sababu Mungu atawahukumu.
Yesu anaendelea kuwakemea waandishi na Mafarisayo
Hii inamaanisha Malkia wa sheba. Sheba ni nchi iliyo kusini mwa Israeli
"atasimama siku ya hukumu na kuwahukumu watu wa kizazi hiki, Tazama ilivyotafsiriwa katika 12:41
Hii inamaanisha watu walioishi wakati Yesu alipokuwa akihubiri
Ni Mungu atakayekihukumu kizazi chxa Yesu. "Na Mungu atawasiliza raiawa Ninawi na kukihukumu kizazi hiki "
Hapa "miishio ya dunia" ni nahau inayomaanisha "mbali." Alikuja tokea mbali"
Sentensi hii inaeleza kwa nini Malkia wa kusini atakihukumu kizazi cha Yesu, "allikuja kwa hilo"
"na anagalia" Hii inaongeza msisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye
"mtu wa muhimu sana"
Yesu anaongea juu yake
Unaweza kuiweka maana ya sentensi ya Yesu iliyofumbwa kuwa wazi. "Kuliko Selemani yuko hapa, lakini hausikilizi. Hiyo ndiyo sababu ya Mungu kuwahukumu"
Yesu anaendelea kuwakemea waandishi na Mafarisyao.
Yesu anatumia mfano kuwaonya watu hatari ya kutokuamini
"eneo kavu"au "mahali ambapo watu hawaishi"
Hapa "ni" inamaanisha kupumzika
Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi na wala si nukuu "kwa hiyo yule roho mchafu huamua kurudi kwenye nyumba yake ambayo alitoka"
Hii ni sitiari ya ya mtu ambaye pepo lilitoka. "pale nilikotoka
Hii inaweza kutafsiriwa katika muunda tendaji. "yule roho mchafu akikuta ile nyumba iko safi na imewekwa kila kitu katika mahali pake",
Hii inamaanisha kama watu wa kizazi cha Yesu hawatamwamini na kuwa wanfunzi wake, watakuwa katika hali mbaya kuliko walivyokuwa mwanzoni
Kufika kwa Mama wa Yesu na ndugu zake inakuwa fursa Kwa Yesu kueleza juu ya familia yake ya kiroho
neno "tazama" lintatuandaakwa ajili ya watu wapya katika simulizi. Lugha yako yaweza kuwa na namna mpya ya kueleza hili
Huyu ni Mariamu, Mam wa Yesu wa mwili.
"wakitaka kuongea"
Hii inaweza kutafsiriwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja. "mtu mmoja alaimwambia Yesu kuwa mama yake na ndugu zake walikuwa nje na walitaka kuongea naye"
Huu ni mwisho wa sehemu ya simulizi lililoanzia 12:1 amabapomwadishi ameeleza juu ya kukua kwa upinzani katika huduma ya Yesu
ukweli wa ujumbe ambao yule mtu aliomwambia Yesu unaeleweka na haukurudiwa. "aliyemwambia Yesu kuwa mama yake na ndugu zake walitka kuongea naye"
Yesu antumia swali hili kuwafundisha watu. "nitwaambia kweli mamayangu na ndugu zangu ni nani"
"anagalia" Hii inatia msisitizo wa kile ambacho Yesu alisema baadaye"
Hii ni sitiari inayoonesha kuwa wanafunzi wa Yesu ni wake katika familia ya kiroho. Hii ni ya muhimu kuliko kuwa kwenye familia ya kimwili.
"mtu yeyote"
Hii ni sifa muhimu ya Yesu
Hii ni sitiari inayomaanisha kuwa wale amabo wanamtii Mungu wanakuwa kwenye familia ya Yesu kiroho. Hii ni muhmu zaidi ya kuwa kwenye familia ya kimwili
Mafarisayo walilalamika kuwa wanafunzi wa Yesu walikuwa wakivunja na suke ya ngano na kula, jambo ambalo Mafarisayo waliamini halikuwa halali kufanyika siku ya sabato.
Yesu alisema alikuwa mkuu kuliko hekalu.
Yesu, mwana wa Adamu ni Bwana wa sabato
Mafarisayo walimuuliza Yesu "Je, ni halali kuponya siku ya Sabato?"
Yesu alisema likuwa ni halali kutenda mema siku ya Sabato.
Mafarisayo walitoka nje na na kupanga njama dhidi yake na kutafuta jinsi ya kumwangamiza.
Watu wa mataifa wangesikia hukumu ya Mungu na kumtumaini Yesu.
Yesu hatalia kwa nguvu, hatavunja tete lilichubuka, au kuuzima utambi unaotoa moshi.
Yesu alisema kuwa kama shetani anampinga Shetani, basi je ufalme wa Shatani utasimama?
Yesu alisema kwamba ufalme wa Mungu umekuja juu yao kama alikuwa anatoa mapepo kwa Roho wa Mungu.
Yesu alisema kufuru dhidi ya Roho haitasamehewa.
Mtu hujulikana kwa matunda yake.
Yesu alisema kuwa Mafarisayo wangepata hukumu na haki kwa maneno yao.
Yesu alisema katika kizazi chake angetoa ishara ya Yona, kuwa ndani ya moyo wa nchi kwa siku tatu mchana na usiku.
Yesu alisema Yeye alikuwa mkuu kuliko Yona.
Watu wa Ninawi watakihukumu kizazi cha Yesu kwa sababu walisikia ujumbe wa Mungu kwa Yona lakini kizazi cha Yesu hakikusikiliza ujumbe wa Mwana wa Adamu ambaye ni mkuu kuliko Yona.
Yesu alisema kuwa Yeye alikuwa mkuu kuliko Sulemani.
Kizazi cha Yesu kitamwacha na kufanana na mtu mwenye roho mchafu kwa sababu roho mchafu hurudi na roho wachafu wengine saba na hali mwisho ya mtu huwa mbaya zaidi kuliko ya kwanza.
Yesu alisema wale wanaofanya mapenzi ya Baba ni ndugu zake na ni mama yake.
1Katika siku hiyo Yesu aliondoka nyumbani na kukaa kando ya bahari.2Umati mkubwa ulikusanyika kwa kumzunguka, aliingia ndani ya mtumbwi na kukaa ndani yake. Umati wote walisimama pembeni ya bahari.3Kisha Yesu alisema maneno mengi kwa mifano. Alisema, “Tazama, mpanzi alienda kupanda.4Alipokuwa akipanda baadhi ya mbegu zilianguka kando ya njia na ndege walikuja wakazidonoa.5Mbegu zingine zilianguka juu ya mwamba, ambapo hazikupata udongo wa kutosha. Ghafla zilichipuka kwa sababu udongo haukuwa na kina.6Lakini jua lilipo chomoza zilichomwa kwa sababu hazikuwa na mizizi, na zilikauka.7Mbengu zingine zilianguka kati ya miti yenye miiba. Miti yenye miiba ilirefuka juu ikaisonga.8Mbegu zingine zilianguka kwenye udongo mzuri na kuzaa mbegu, zingine mara mia moja zaidi, zingine sitini na zingine thelathini.9Aliye na masikio na asikie.10Wanafunzi walikuja na kumwambia Yesu, “Kwa nini unazungumza na umati kwa mifano?”11Yesu alijibu kusema, “Mmepewa upendeleo wa kujua siri za ufalme wa mbinguni, bali kwao hawajapewa.12Lakini yeyote aliyenacho, kwake yeye ataongezewa zaidi, na atapata faida kubwa. Ila asiye nacho hata kile alichonacho atanyang'anywa.13Hivyo naongea nao kwa mifano kwa sababu ingawa wanaona, wasione kweli. Na ingawa wanasikia wasisikie wala kujua.14Unabii wa Isaya umetimia kwao, ule usemao, ‘Msikiapo msikie, lakini kwa namna yoyote hamtaelewa; wakati mwonapo mwaweza kuona, lakini kwa namna yeyote ile msijue.15Na mioyo ya watu hawa imekuwa giza, ni vigumu kusikia, na wamefumba macho yao, ili wasiweze kuona kwa macho yao, au kusikia kwa masikio yao, au kufahamu kwa mioyo yao, hivyo wangenigeukia tena, na ningewaponya.’16Bali macho yenu yamebarikiwa, kwa kuwa yanaona, na masikio yenu kwa kuwa yanasikia.17Hakika nawaambia manabii wengi na watu wenye haki walikuwa na hamu ya kuyaona mambo yale myaonayo, na hawakuweza kuyaona. Walitamani kusikia mambo yale mnayosikia, hawakuyasikia.18Sasa sikilizeni mfano wa mpanzi.19Wakati wowote asikiapo neno la ufalme na asilielewe, ndipo mwovu huja na kukinyakua kilichokwisha kuwekwa ndani ya moyo wake. Hii ni mbegu ile iliyopandwa kando ya njia.20Yeye aliyepandwa katika miamba ni yule asikiaye neno na kulipokea haraka kwa furaha.21Bado hana mizizi ndani yake, ila huvumilia kwa kitambo kifupi. Wakati matatizo au mateso yanapotokea kwa sababu ya neno hujikwaa ghafla.22Aliyepandwa kati ya miti ya miiba, huyu ni yule alisikiaye neno lakini masumbuko ya ulimwengu na udaganyifu wa utajiri hulisonga lile neno lisije likazaa matunda.23Aliyepandwa kwenye udongo mzuri, huyu ni yule asikiaye neno na kulifahamu. Huyu ni yule azaaye matunda na kuendelea kuzaa moja zaidi ya mara mia, nyingine sitini, nyingine thelathini.”24Yesu aliwapa mfano mwingine. Akisema, “Ufalme wa mbinguni unafananishwa na mtu aliye panda mbengu nzuri katika shamba lake.25Lakini watu walipolala, adui wake akaja pia akapanda magugu katikati ya ngano kisha akaenda zake.26Baadaye ngano ilipoota na kutoa mazao yake, ndipo magugu yalitokea pia.27Na watumishi wa mwenye shamba walikuja wakamwambia, ‘Bwana, hukupanda mbengu nzuri katika shamba lako? Imekuwaje sasa lina magugu?’28Akawaambia, ‘Adui ametenda hili.’ Watumishi walimwambia, ‘Kwa hiyo unataka twende tukayang'oe?’29Mwenye shamba akasema, ‘Hapana, wakati mnayang'oa magugu mtang'oa pamoja na ngano.30Yaacheni yakue pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati wa mavuno nitasema kwa wavunaji, ‘Kwanza yang'oeni magugu na yafungeni matita matita na kuyachoma, lakini kusanyeni ngano katika ghala langu.’”31Kisha Yesu aliwatolea mfano mwingine. Akasema, “Ufalme wa mbinguni unafanana na mbegu ya haradali ambayo mtu aliichukua na kuipanda katika shamba lake.32Mbegu hii kwa hakika ni ndogo kuliko mbegu zingine zote. Lakini imeapo huwa kubwa kuliko mimea yote ya bustani, huwa mti, kiasi kwamba ndege wa angani huja na kujenga viota katika matawi yake.”33Akawaambia mfano mwingine tena. “Ufalme wa mbinguni ni kama chachu ile iliyo twaliwa na mwanamke na kuichanganya kwa vipimo vitatu kwa unga mpaka viumuke.”34Hayo yote Yesu aliyasema kwenye umati kwa mifano. Na pasipo mifano hakusema chochote kwao.35Hii ilikuwa kwamba kile kilichokwisha semwa kupitia kwa nabii kiweze kutimia, pale aliposema, “Nitafumbua kinywa changu katika mifano. Nitasema mambo yale yaliyokuwa yamefichwa tangu misingi ya ulimwengu.”36Kisha Yesu aliwaacha umati na kwenda nyumbani. Wanafunzi wake walimwendea na kusema, “Tufafanulie mfano wa magugu ya shambani.”37Yesu alijibu na kusema, “Apandae mbegu nzuri ni Mwana wa Adamu.38Shamba ni ulimwengu; na mbegu nzuri, hawa ni wana wa ufalme. Magugu ni wana wa yule mwovu, na adui aliye zipanda ni Ibilisi.39Na mavuno ni mwisho wa ulimwengu, na wavunaji ni malaika.40Kama vile magugu yanavyo kusanywa na kuchomwa moto, hivyo ndivyo itakavyo kuwa mwisho wa ulimwengu.41Mwana wa Adamu atatuma malaika wake, na kukusanya kutoka katika ufalme wake mambo yote yaliyosababisha dhambi na wale watendao maasi.42Watawatupa wote katika tanuru la moto, ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.43Ndipo watu wenye haki watakapong'aa kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio na asikie.44Ufalme wa mbinguni ni kama hazina iliyofichwa shambani. Mtu akaiona na kuificha. Katika furaha yake akaenda kuuza vyote alivyokuwa navyo, na kulinunua shamba.45Tena, ufalme wa mbinguni ni kama mtu anayefanya biashara atafutaye lulu yenye thamani.46Wakati alipoiona ile yenye thamani, alienda akauza kila kitu alichokuwa nacho na akainunua.47Ufalme wa mbinguni ni kama nyavu iliyo ndani ya bahari, na kwamba hukusanya viumbe vya kila aina.48Ulipojaa wavuvi waliuvuta ufukweni. Kisha wakakaa chini wakakusanya vitu vyema ndani ya vyombo, lakini visivyo na thamani vilitupwa mbali.49Itakuwa namna hii katika mwisho wa dunia. Malaika watakuja na kuwatenga watu waovu kutoka miongoni mwa wenye haki.50Na kuwatupa ndani ya tanuru ya moto, ambako kutakuwa na maombolezo na kusaga meno.51Mmefahamu mambo yote haya?” Wanafunzi walimjibu, “Ndiyo.”52Kisha Yesu akawaambia, “Kila mwandishi ambaye amekuwa mwanafunzi wa ufalme anafanana na mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale.”53IkawaYesu alipomaliza mifano yote hiyo, akaondoka katika sehemu hiyo.54Kisha Yesu akafika katika mkoa wake na akawafundisha watu katika sinagogi. Matokeo yake ni kuwa walishangaa na kusema, “Ni wapi mtu huyu alipopata hekima hii na miujiza hii?55Mtu huyu siyo mwana wa seremala? Mariamu siyo mamaye? Na ndugu zake siyo Yakobo, Yusuph, Simoni na Yuda?56Na dada zake tunao hapa kwetu? Basi mtu huyu ameyapata wapi haya yote?”57Aliwachukiza. Lakini Yesu aliwambia, “Nabii hakosi kuwa na heshima isipokuwa kwao na katika nchi yao.”58Na hakuweza kufanya miujiza mingi kwa sababu hawakuwa na imani naye.
Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka mbele kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari ya 13:14-15, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.
Sura hii inaanza sehemu mpya. Ina baadhi ya mifano ya Yesu kuhusu ufalme wa mbinguni.
Mfano ni hadithi fupi inayotumika kuonyesha mfano wa maadili au wa kidini. Katika sura hii, mifano, yanatangaza ukweli kuhusu ufalme wa mbinguni kwa wale ambao wana imani katika Yesu. Pia yanaficha ukweli huo huo kutoka kwa wale wanaomkataa Yesu (Mathayo 13:11-13). Kawaida mifano hii huchukua fomu ya hadithi.
Katika sura hii, Yesu anazungumzia macho kuona na masikio kusikia. Anatumia takwimu hizi za matamshi ili kuwahimiza wasikilizaji wake kuelewa masomo ya mifano hiyo.
Huu nimwanzo wa simulizi jipaya amabapo Yesu anaanza kufundisha makutano, kwa kutumia mifano juu ya ufalme wa mbinguni
Tukio hili liltokea siku hiyohiyo sawa na yale yaliyo kwenye sura iliyopita.
ilimaanisha kuwa alikaa chini kuwafundishsa watu.
Haijatajwa kuwa ilikuwa nyumba ya nani ambayo Yesu alikuwa akiishi
Inamaanisha kuwa Yesu aliingia kwenye mtumbwi kwa sababu ingemfanya iwe rahisi kuwafundisha watu.
Huu yawezekana mtumbwi wa wazi, uliotengenezwa kwa miti wa kuvulia samaki wenye tanga.
Yesu anafafanua juu ya ufalme wa mbinguni kwa kutumia mfano wa mpanzi
"Yesu aliwaambia maneno mengi kwa mifano"
"kwa wale watu kwenye mkutano"
"angalia" au "sikiliza." neno hili linavuta usukivu wa kile Yesu anachotaka kusema baadaye. "uwe tayari kusikiliza jambo amablo nataka kuwaambia"
"mpanzi alienda kumwaga mbegu shambani"
"mpanzi alipokuwa akiendelea kumwaga mbegu"
Hii inamanisha "njiani wanapopita" peembeni mwa shamba. araidhi ya pale ni ngumu kwa sababu ya watu kuikanyaga.
"wakazila mbegu zote"
Hii ni eneo lililojaa miamba na sehemu nyembamba ya udongo ulio juu ya miamba
"zile mbegu zilimea na kukua"
Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "jua lilichoma ile mimea na ikaungua"
Yesu anamaliza mfano wa mpanzi
"zilianguka mahali ambapo miiba na mimea hukua"
"ikaisinga ile mimea mipya" tumia neno lako magugu kuzuia mimea mingine kukua vizuri.
"kuzaa mazao" au "kuzalisha mbegu zaidi" au kutoa matunda"
unaweza kuiweka vizuri zaidi katika maana inayoeleweka
"100 ... 60 ... 30"
Hii ni njia inayomaaisha kwa kila anayesikiliza. "Kila anayenisikilza." Tazamaulivyotafsiri katika 11:13
Hapa "kusikia" inamaanisha kuwa msikivu. "lazima awe makini na kile ninachokisema"
Yesu anawaeleza wanafunzi wake kwa nini anafundisha kwa kutumia mifano
Hapa"kwao" inamaanisha wanafunzi wa Yesu
Hii inaweza kutafasiriwa kwa kutumia muundo tendaji na kutumia taarifa zinazotolewa. " Mungu amewapa fursa ya kuelewa siri za ufalme wa mbinguni" lakini Mungu hajawapa siri hizi watu hawa" au " Mungu amewafnya ninyi kuzielwa siri za ufalme wa mbinguni lakini hajawafanya hawa tayri kuzielewa"
ni kiwakilishi cha wingi kinacho maanisha wanafunzi wa Yesu
Hapa"ufalme" inamaanisha utawala wa Mungu. Kirai"udalme wa mbinguni" kinaonekena kwenye kitabucha mathayo tu. Kama inawezekana jaribu kuiweka katika tafsiri y ako. "siri kuhusu Mungu wetu na utawala wake"
"yeyote aliye na ufahamu" au "yeyote anayepokea kile nanachofundisha"
Hiiinaweza kutafsiriwa katika muundo tendaji. "Mungu atampatia ufahamu zaidi"
"asiye na ufahamu" au " asiyepokea hiki ninachofudisha"
Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "Mungu atakichukua hata kile alicho nacho"
Yesu anaendelea kuwafundisha wanafunzi wake kwa nini anafundisha kwa kutumia mifano
Katika mstari wa 14 Yesu anamnukuu nabii Isaya ku onyesha kuwa kushindwa kwa watu kuelewa mafundisho ya Yesu ni kutimilika kwa unabii
Viwakilishi vyote vya "kwao" na "hamta" vinamaanisha watu katika kumati.
Huu ni mwanzo wa nukuu kutoka kwa nabii Isaya kuhusu watu wasioamini wakatiwa Isaya. Yesu anatumia nukuu hii kuwa kuwaeleza watu waliokuwa wanamsikiliza. Hii ni semi misambamba inayosisitiza kwamba watu walikataakumwani Yesu.
Matumizi ya pili ya "kuona" hapa yanamaanisha kuelewa.
Inaweza kuwekwa wazi kwa kile watu wanachosikia. "Ingawa wanasikia kile ninachosema, hawaelewi kile ninachomaanisha.
Hii inaweza kuelzwa katika mfumo tendaji. "wanatimiza kile Mungu alisema zamani kuptia nabii Isaya"
Huu ni mwanzo wa nukuu kutoka kwa nabii Isaya kwa watu wasioamini wakati wa Isaya. Yesu anatumia nukuu hii kuwaeleza watu waliokuwa wanamsikiliza. Hii ni misemo sambamba inayosisitiza kuwa watu walikataa kuuelewa ukweli wa Mungu.
"mtaskia vitu lakini hamtavielewa" unaweza kuviweka wazi kile amabcho watu watasikia. "Mtasikia kile Mungu asemacho kupitia nabii lakini hamtaelewa maana halisi"
Unaweza kuweka wazi kile ambacho watu wataona. "mtaona kile amabcho Mungu anafanya kupitia nabii, lakini hamtaelewa"
Yesu anamaliza kumnukuu Isaya
Ktika 13:15 Mungu anawaeleza watu wa Israwli kana kwamba ni wenya ugonjwa wa mwili ambao unawafanya wasiweze kuelewa, kuona na kusikia Mungu anawataka waje kwake ili awaponye.
Mioyo inamaanisha akili. "mioyo yao imekuwa migumu kujifunza"
wao si viziwa wa masikioya mwili 'vigumu kusikia"wanakataa kusika na kujifunza ukweli wa Mungu
hawajafumba macho yao ya mwaili. hii inamaanisha hawataki kuelewa.
"ili kwamba wasiweze kuona kwa macho yao, kusikia kwa masiko yao, au kuelewa kwa mioyo yao amabyo matokeo yake ni kumrudia Mungu.
"kugeukia kwangu tena" au "kutubu"
"mimi ningewaponya" Hii inamaanisha Mungu angewaponya kiroho kwa kuwasamehe makosa yao na kuwapokea tena kama awatu wake.
Yesu anamaliza kuongea na wanafyunzi wake kwa nini anaongea nao kwa mifano
Sentensi zote zina maanisha kitu kilekile. Yesu anasisitiza kuwa wamempendeza kwa sababu wameamini kile ambacho Yesu amesema na wamefanya.
macho yanamaanisha nafsi kamili. mmebarikiwa kwa sababu machoyenu yanaweza kuona
viwakilishi hivi ni vya wingi
masikio yanmaanisha nafsi kamili
"nawambia ukweli" hii inaongeza msisitizo kwa kile anlichosema Yesu baadaye.
Unaweza kuyaweka wazi yale waliyoyaona "Yle mambo uliyoyaona mimi nikfanya
mambo uliyosikia mimi nikisema
Yesu anaanza kufafanua kwa wanafunzi wake ule mfano wa mpanzi unaoanzi 13:3
neno linamaanisha ujumbe "ufalme" unamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme
Yesu anaongea juu ya shaetani anayewafanya kusahau kile walichosikia kama ndege anavyozidonoa mbegu zilizoanguka chini.
shetani
kukichukua kitu kwa mtu aliyesahihi
ujume ule Mungu aliopanda nadani ya moyo wake.
moyo unamanisha akili ya msikilizaji
tafsiri kama ilivyo 13:3
Yesu anaendelea kwaeleza wanafunzi wake mfano wa mpanzi
"kilichopandwa" kinamaanisha mbegu iliyoanguka kwenye miamba.
miamba ambapo mbegu zilianguka inmaanisha udongo uliokuwa juu ya miamba ambapo mbegu zilianguka
katika mfano, mbegu zinamaanisha neno
ujumbe wa Muungu
kulipokea neno kwa furaha
mizizi inamaanisha kile kinachomfanya mtu aendelee kuamini ujumbe wa Mungu
kujikwaa humaanisha kuacha kuamini ujumbe wa Mungu
Yesu anaendelea kuwawleza wanafunziwake kuhusu mfano wa mpanzi
hii ni mbegu iliyopandwa au iliyoanguka
ardhi ilyo na miiba amabapo mbegu ilipandwa
inamaanisha mtu
inaanisha ujumbe wa Mungu
Yesu anaongelea masumbufu ya ulimwengu na udanganyifu wa utajiri hugeuza nia ya mtu na kushindwa kutii neno la Mungu kama vile magugu yanavyoweza kuuelemea mmea na kushindwa kukua.
"mamabo ya dunia ambayo huwafanyawatu wawe na mashaka
Yesu anautumia utajiri kama mtu adanganyaye watu. Hii inamaanisha kuwa watu hudhani kuwa na pesa nyingi huwafanya kuwa na furaha, lakini si kweli.
kutokuzaa matunda
kwenye udongo mzuri ambapo mbegu zilipandwa
Hapa mtu amefananishwa na mti uzaao. "Kama mti wenye afya uzaoa matunda, ambaye ni mzalishaji.
watu wengine huzalisha 100 mara, wengine 60 na wengine 30.
Hapa Yesu anaelezea juu ya uafalme wa mbinguni kwa kutumia mfanao wa shamba lilikuwa na ngano na magugu vikikuwa pamoja
tafasiri islinganishe ufame wa mbinguni na mtu, bali ufalme wa mbinguni kama ulivyoelezwa kwenye mfano.
"Wakti Mungu wa mbinguni atakapojionesha kama mfalme"
wakati Mungu wetu wa mbinguni atakapojidhirisha kama mfalme, itkuwa kama
"mbegu nzuru ya chakula" au "nafaka nzuri"
"adaui wake akaja shambani"
magugu huonekena kama mimea ya chakula yanapokuwa hayajakomaa. laini mbegu zake huwa nasumu" au "mbegu mbaya" au mbegu za magugu"
"badaye mbegu za ngano zilipoota" au "wakati mimea ilipochipua"
"ilipotoa nafaka" au "ilipotoa mbegu za ngano"
"watu waliweza kuyaona magugu shambani pia"
Yesu anaendelea kueleza mfano wa magaugu na ngano kukua kwa pamoja katika shamba
huyu ndiye aliyepanda mbegu nzuri shambani
ulipanda mbegu nzuri katika shamba
tulipanda
"mwenye shamba akawaambia watumishi"
kiwakilishi "tu" kinamaanisha watumishi
Yesu anahitimishas mfano wa magugu yalyokua pamaoja na ngano shambani
"Mwenye shamba akasema kwa watumishi"
"Nitawaambia wavunaji kwanza kuyakusanya magugu na kuyafunga matita matita na kuyachoma, kisha kusanyeni ngano katika ghala langu"
Jengo la shambani ambalo lilitumika kwa kukusanyia nafaka.
Yesu anaufafanua ufalme wa mbinguni kwa kutumia mfano wa mbegu ambayo hukua na kuwa mti mkubwa
"Wakati Mungu wetu wa mbinguni atakapojidhihirisha kama mfalme kuwa mfalme, itakuwa kama", Tazama 13:24.
ni mbegu ndogo sana ambayo huweza kukua na kuwa mti mkubwa
Mbegu za haradari zilikuwa mbegu ndogo zadi ambazo zilifahamika kwa wasikilizaji wa kwanza
"Lakini mmea unapokuwa"
ni mkubwa kuliko
Mmea wa haradli hukua kiasi cha mita 2 had 4 za urefu
"ndege"
Yesu anaelezea ufalme wa mbinguni kwa kutumia mfano wa chahu na jinsi inavyoweza kuufanya udongo
Ufalme si kama chachu, lakini kusambaa kwa ufalme ni kama kusambaa kwa chachu
ufalme wa mbinguni una, maanisha utawala wa Mungu kama mfalme..Kirai "ufalme wa mbinguni" kimetumika katika Mthayo tu. Mungu wetuwa mbinguni atakapojidhihirisha kama mfalme itakuwa kama"
"kipimo kikubwa cha unga" au tumia kipimo kinachotumika katika utamaduni wako cha kuonesha kipimo kikubwa cha unga.
Maana kusudiwa hpa ni kwamba, chachu na vile vipimo vitatu vya unga vilitengenezwa kwa ajiliya kuumulia.
Mwandishi anannukuu toka Zaburi kuonesha kuwa mafundisho ya Yesu kwa mfano ni kwa ajili kutimiza unabii
Sentensi zote zina maana moja. Zimeunganishwa kusisitiza kwamba Yesu alifundisha makutano kwa kutumia mifano.
Hii inamaanisha kuwa kile alichofundisha Yesu kinaanzia 13"1
""hakufundisha chochote isipokuwa kwa mifano"
alaikifanya kiwe kweli kile alichokuwa amemwambia mmoja wa manabii kukiandika hapo zamani
nabii aliposema
Hii ni nahau inayomaanisha kuwa nitasema "nitasema"
mambo ambayo Mungu ameyaficha
"tangu kuanza kwa ulimwengu" au tangu Mungu aumbe ulimwengu"
Mandhari yanahamia kwenye nyumba amabyo Yesu na wanafunzi wake walikuwa wanaishi. Yesu anaanza kuwafundiasha mfano wa shamba ambalo lilikuwa na magugu na ngano alilokuwa amewaambia mwanzoni katika 13:24.
"aliingia ndani" au "aliingia kwenye nyumba ile aliyokuwa anaishi"
"mpamzi"
Yesu anamaanisha yeye mwenyewe
Hapa "wana wa" inamaanisha kuwa mali ya au kuwa na tabia zilezile alizo nazo.
Mungu ni mfalme
watu ambao ni mali ya yule mwovu
"adui aliyepanda magugu"
"mwisho wa nyakati
Yesu anamaliza kuwaeleza wanafunzi wake mfano wa shamba lenye magugu na ngano
Kwa hiyo, kama watu wayakusanyavyo magugu na kuyachoma moto"
mwisho wa nyakati
Yesu anamaanisha yeye mwenyewe
"wale wasio na sheria" au "watu waovu"
moto wa kuzimu
Hii inamaanisha huzuni kubwa na mateso
watakuwa rahisi kuwaona kama jua
hiki ni cheo muhimu cha Mungu
kila anayenisikiliza
Yesu anaelezea juu y a ufalme wa Mungu kwa kutumia mifano miwili ya watu waliouza mali zao kwa kununua kitu cha thamani zaidi
Katika mifano hii Yesu anatumia milinganyo miwili kuwafundisha wanfanzi wake kuhusu mfano wa ufalme wa mbinguni
Tazama ilivyotafsiriwa katika 13:24
hazina ambayo mtu alificha shambani
kkitu cha thamani sana au vitu vilivyokusanywa
alifunika kwa juu
Maana yake nin kwamba yule mtu ananunua lile shamba ili ili achukue ile hazina iliyofichwa
maana yake ni kwamba yule mtu alikuwa anatafuta ile luu ya thamani ili aweze kuinunua
mchuuzaji au mtu anayeshughulika kuuza vitu vya jumla ambaye mara kwa mara hupata wateaja tokea mbali
"lulu" ni kitu lain, kigumu, kinachong'aa, cheupe au shanga yenye mng'ao inayopatikana kwenye viumbe wenye asili ya konokono baharini. Lulu ina bei y a juu sana na hutengenezwa vitu vya thamani kama pete.
Yesu anaelezea ufalme wa mbinguni kwa kutumia mfano wa mvuvi anayetumia nyavu kubwa kukamata samaki
ufalme sikama nyavu, lakini ufalme hukokota watu wa kila aina kamavile nyavu zikokotavyo aina zote za samaki
tazama katika 13:24
kama nyavu ambayo wavuvi hutupa ndani ya bahari
"iliyotupwa baharini"
"ilikamata viumbe wa kila aina
"walivuta ule wavu mpaka ufukweni"
"vile vizuri"
"samaki wabaya" au "samaki wasiofaa"
"havikutunzwa"
Yesu anaeleza mfano wa mvuvi aliyetumia wavu mkubwa kukamata samaki
"mwisho wa nyakati"
"kuja" au "kwenda" au "kuja toka mbinguni"
watu waovu kutoka miongoni mwa wenye haki"
"malaika watawatupa watu waovu"
tazama 13:40
Tazama 8:11
Yesu anaeleza ufalme wa mbinguni kwa kueleza mfano wa mtu anayewatawala watumishi wa nyumbani.Huu ni mwisho wa habari ya Yesu kuwafundisha watu kuhusu ufalme wa mbinguni kwa kutumia mifano
Yesu aliwaulizakamawalikuwa wameelewa yote haya, na walisema kwamba walielwa
amaejifunza ukweli kuhusu Mungu wetu wa mbinguni ambaye ni mfalme.
Yesu anafundisha mfano mwingine. Anawafananisha waandishi, ambao wanalyafahamu maandiko vizuri ambayo Musa na manabii waliandika, na ambao pia sasa wanayapokea mafundisho ya Yesu na kuyalinganisha namwenye nyumba anayetumia vitu hazina ya zamani na mpaya.
Hazina ni kitu cha thamani. Hapa panafananishwa na mahali ambapo vitu huhifadhiwa. "chumba cha kutunzia".
Kirai hiki kinatuhamishaia simulizi yetu ya mafundisho ya Yesu kwenda kile kilichotokea baadaye.
Huu ni mwanzo wa habari mpya inyotupeleka hadi 17:26, ambapo mwandishi anaeleza juu ya mwendelezo wa upinzani katika huduma ya Yesu kuhusu ufalme wa mbinguni. Hapa watu wa nyumbani kwao Yesu wanamkataa..
" Huu ni mji wa Nazarethi ambapo Yesu alikulia
kiwakilishi "yao" kinamaanisha watu wa eneo hilo
"walishangaa
"Yawezekananje mtu wa kawaida kama huyu kuwa na mwenye hekima na kufanya miujiza mikubwa.
Makutano wanatumia maswali haya, kuonyesha mshangao wao kuwa mtu wa kawaida kutoka mji wao anafanya mambo haya yote. Mtu wa kawaida hawezi kuyafanaya haya yote.
watu walimkataa Yesu
nabii hupokea heshima kila mahli
"mji wa kwao"
"nyumbani kwao"
"Yesu hakuweza kufanya miujiza nyumbani kwao"
Mbegu zilizoanguka kando ya njia zililiwa na ndege.
Mbegu zilizoanguka juu ya mwamba ghafla zilichipuka lakini zilichomwa na jua na zilikauka.
wenye mbegu zilizoanguka katika miti yenye miiba zilisongwa na miti yenye miiba.
Mbegu zilizoanguka katika udongo mzuri zilizaa, zingine mar mia, zingine mara sitini na zingine thelathini.
Unabii wa Isaya ulisema watu wangesikia lakini wasiweze kuelewa na wangeona lakini wasiweze kutambua.
Watu waliomsikia Yesu wasiweze kumwelewa walikuwa na mioyo yenge giza na wagumu kusikia na walifumba macho yao.
Mbegu iliyopandwa kando ya njia ni yule ambaye husikia neno la ufalme lakini na halielewi, ndipo mwovu huja na kukinyakua kilichokwisha kupandwa ndani ya moyo wake.
Mbegu iliyopandwa kwenye ardhi yenye mwamba ni yule asikiaye neno na kulipokea haraka kwa furaha, lakini hujikwaa ghafla wakati mateso yanapotokea.
Mbegu iliyopandwa kwenye miiba ni yule mtu anayesikia neno la Mungu, lakini masumbufu ya dunia na udanganyifu wa utajiri hulisonga neno.
Mbegu iliyopandwa kwenye udongo mzuri ni yule mtu anayesikia neno la Mungu na kulielewa na kisha huzaa matunda.
Adui alipanda magugu katika shamba.
Mwenye shamba aliwaambia watumishi kuviacha vyote vikue pamoja hadi wakati wa mavuno, kisha kuyakusanya magugu na kuyachaoma na ngano kuikusanya kwenye ghala.
Mbegu ya haradari ilistawi kuwa mti mkubwa kuliko mimea ya bustani hivyo ndege hujenga viota vyao katika matawi yake.
Yesu alisema kuwa ufalme wa mbinguni ulikuwa kama hamira iliyochanganywa kwa vipimo vitatu vya unga hadi ilipoumuka.
Aliyepanda mbegu ni mwana wa Adamu, shamba ni ulimwengu, mbegu njema ni wana wa ufalme, magugu ni wana wa yule mwovu, na aliyepanda magugu ni mwovu.
Wavunaji ni malaika, na mavuno ni mwisho wa ulimwengu.
Katika mwisho wa dunia wale wanaofanya maovu watatupwa katika tanuru ya moto.
Katika mwisho wa dunia watendao haki watang'aa kama jua.
Mtu aliyepata hazina aliuza kila kitu alichakuwa nacho na kununua lile shamba.
Mtu yule aliyepata lulu ya thamani kuu aliuza kila kitu alichokuwa nacho na kuinunua.
Kama vile vitu vitu vibaya vilivyotengenishwa na vitu vizuri kutoka kwenye nyavu na vibaya vikatupwa, mwisho wa dunia watu waovu watatenganishwa kutoka miongoni mwa wenye haki na kutupwa katika tanuru ya moto.
Watu waliuliza, "Ni wapi mtu huyu alipopata hekima hii na miujiza hii?
Yesu aliisema nabii hapati heshima katika nchi yake.
Kwa sababu watu hawakuamini, Yesu hakufanya miujiza mingi katika mko wake.
1Kwa wakati huo, Herode alisikia habari juu ya Yesu.2Akawaambia watumishi wake, “Huyu ni Yohana Mbatizaji amefufuka kutoka katika wafu. Kwa hiyo nguvu hizi zipo juu yake.”3Kwa kuwa Herode alikuwa amemkamata Yohana akamfunga na kumtupa gerezani kwa sababu ya Herodia, mke wa Filipo kaka yake.4Kwa kuwa Yohana alimwambia, “Si halali kumchukua yeye kuwa mke wake.”5Herode angemwua lakini aliwaogopa watu kwa sababu walimwona Yohana kuwa nabii.6Lakini wakati siku ya kuzaliwa Herode ilipofika binti wa Herodia alicheza katikati ya watu na kumpendeza Herode.7Katika kujibu aliahidi kwa kiapo kwamba atampa chochote atakachoomba.8Baada ya kushauriwa na mama yake, alisema, “Nipe mimi hapa katika kombe kichwa cha Yohana Mbatizaji.”9Mfalme alikuwa na sikitiko kwa maombi ya binti, lakini kwa ajili ya kiapo chake, kwa sababu ya wote waliokuwa chakulani pamoja naye aliamuru kwamba inapaswa ifanyike.10Alituma Yohana aletwe kutoka gerezani11ili akatwe kichwa chake na kikaletwa juu ya sinia na akapewa binti na akakipeleka kwa mama yake.12Kisha wanafunzi wake wakaja kuuchukua ule mwili na kuuzika, baada ya hili walienda kumwambia Yesu.13Naye Yesu aliposika haya, akijatenga kutoka mahali pale akapanda ndani ya mashuka akaenda sehemu iliyotengwa. Wakati umati ulipo fahamu alikokuwa, walimfuata kwa miguu kutoka mijini.14Kisha Yesu alikuja mbele yao akauona umati mkubwa. Akawaonea huruma na kuponya magonjwa yao.15Jioni ilifika, wanafunzi wakaja kwake na kusema, “Hii ni sehemu ya jangwa, na siku tayari imepita. Watawanyishe makutano ili waende vijijini wakanunue chakula kwa ajili yao.16Lakini Yesu akawaambia, “Hawana haja ya kwenda zao. Wapeni ninyi chakula”17Wakamwambia, “Hapa tunayo mikate mitano na samaki wawili tu.”18Yesu akasema, “Ileteni kwangu.”19Kisha Yesu akauamuru umati kukaa chini kwenye nyasi. Akachukuwa mikate mitano na samaki wawili. Akatazama juu mbinguni, akabariki na kumega mikate akawapa wanafunzi. Wanafunzi wakaupatia umati.20Wakala wote na kushiba. Kisha wakavikusanya vipande vyote vya chakula na kujaza vikapu kumi na mbili.21Wale waliokula walikadiriwa kuwa wanaume elfu tano bila ya kusehabu wanawake na watoto.22Mara moja aliwaamuru wanafunzi waingie ndani ya mashua, wakati huo yeye akawaaga umati waende zao.23Baada ya kuwaaga umati kwenda zao, akapanda juu mlimani kuomba pekee yake. Wakati ilipokuwa jioni alikuwa huko pekee yake.24Lakini sasa mashua ilipokuwa katikati ya bahari ukiyumbayumba kwa sababu ya mawimbi, kwani upepo ulikuwa wa mbisho.25Katika usiku wa zamu ya nne Yesu aliwakaribia, akitembea juu ya maji.26Wakati wanafunzi wake walipomwona akiitembea juu ya bahari, walihofu na kusema, “Ni mzuka,” na kupaza sauti katika hali ya uoga.27Yesu akawaambia mara moja, akisema, “Jipeni moyo! Ni mimi! Msiogope.”28Petro alimjibu kwa kusema, “Bwana, kama ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.”29Yesu akasema, “Njoo.” Hivyo Petro akatoka ndani ya mashua na akatembea juu ya maji kwenda kwa Yesu.30Lakini Petro alipoona mawimbi, aliogopa, na kuanza kuzama, chini, akaita sauti na kusema, “Bwana, niokoe!”31Haraka Yesu akanyoosha mkono wake akamnyanyua Petro, na kumwambia, “Wewe mwenye imani ndogo, kwa nini ulikuwa na mashaka?”32Ndipo Yesu na Petro walipoingia katika mashua, upepo ulitulia kuvuma.33Wanafunzi mashuani wakamwabudu Yesu na kusema, “Kweli wewe ni Mwana wa Mungu.”34Na walipokwisha kuvuka, walifika katika nchi ya Genesareti.35Na watu katika eneo lile walipomtambua Yesu, walituma ujumbe kila sehemu za kando, na kuleta kila aliyekuwa mgonjwa.36Walimsihi kwamba waweze kugusa pindo la vazi lake, na wengi walioligusa waliponywa.
14:3-12 inataja matukio yaliyotokea hapo awali. Kwa hiyo, kuna mkatizo katika utaratibu wa matukio wa hadithi. Kusudi la mkatizo huu ni ufafanuzi; mtafsiri ataona umuhimu wa kuashiria mkatizo huu.
Herode aliamini kwamba kuvunja kiapo kulikuwa na aibu, hivyo aliamuru kuuawa kwa Yohana Mbatizaji. Hata hivyo, mauaji ambayo aliwajibika ilikuwa mbaya zaidi. Hii ni kinaya.
Mistari hii inaeleza jinsi Herode alivyopokea aliposikia habari za Yesu. Tukio hili linfuatia baada ya tukio linalofuata katika simulizi
"Katika siku hizo" au "wakati Yesu akiendelea na huduma huko Galilaya"
alaisikia juu ya uvumi wa Yesu
"Herode alisema"
amerudi kuishi
Baadhi ya Wayahudi waliamini kuwa kama mtu atarudikutoka wafu anaweza kuwa nanguvu za kufanya mambo makubwa.
Hapa mwandishi anaanza kueleza jinsi Herode alivyomnyonga Yohana mbatizaji. Matukio haya yanaanza kuonekana kabal y a matukio yaliyo kwenye mistari iliyopita
Mwandishi anaeleza upya habari ya kifo cha Yohana mbatizaji ili kuonesha kwa nini Herode aliitikia kwa jinsi alivyofanya aliposikia habari za Yesu
Kama inahitajika unaweza kurudia mpangilio wa tukio kama ulivyo 9:3 -4.
Inasemekana kuwa Herode alifanya mabo haya kwa sababu aliwaamuru wengine kufanya kwa ajili yake.
Filipo ni jina la kakawa Herode
Kwa kuwa Yohana alikuwa amemwambia kuwa siahali kwake kumchukua kama mke wake"
"Kwa kuwa Yohana aliendelea kumwambia Herode"
Filipo bado alikuwa hai wakati Herode anamwoa Herodia
Herode aliogopa
"walimwona Yohana
katikati ya wageni waliokuwa wamehudhuria ile sherehe ya kuzaliwa
baada ya mama yake kumpa maelekezo
"kumfundisha" au "kumwambia"
"binti wa Herodia alaisema kwa Herode"
sahani kubwa sana
ombilake lilimfanya mfalme asikitike
"mfalme Herode"
"aliwaamuru watu wake wafanye alichosema"
Hii inakamilisha habari ya Herode alivyomuua Yohana mbatizaji
mtu mmoja akaleta kichwa chake kwenye sinia akpeewa yule binti
sahani kubwa sana
binti ambaye hajaolewa
wanafunzi wa Yohana
maiti
wanafunzi wa Yohana walienda kumwambia Yesu kile kilichotokea kwa Yohana mbatizaji
Mistari hii inaeleza jinsi Yesu alivyopokea taarifa za kuuawa kwa Yohana mbatizaji.
Mistari hii inatoa historia yaju ya muujiza ambao Yesu anataka kuufanya wa kulisha watu elfu tano.
Neno hili limetumika hapa kama mwanzo wa habari mpya. Hapa Mathayo anaanza kueleza sehemu mpya ya habari hii.
" walposika kilichoteka kwa Yohana au waliposikia habari za Yohana
"aliondoka" au "alaienda mbali n a kundi
"kutoka eneo hilo"
"wakati umati waliposikia kule Yesu alikokuwa ameenda
"makutano ya watu" aua "kundi kubwa la watu"
Hii inamaanisha kuwa wale watu walikuwa wkitembea
Yesu alipokuja karibu na ufukwe akauona umati wa watu
Hii inaanzisha habari ya Yesu akiwalisha watu elfu tano kwa mikate mitano na samaki wawili
"wanafunzi wa Yesu wakaja kwake"
"watu hawana haja"
neno "ninyi" ni la wingi linalomaanisha wanafunzi
"wanafunzi wakamwambia Yesu
mkate ni bonge lenye sura kama donge lililookwa
"leteni mkate na samaki kwangu
Hii inahitimisha habari ya Yesu ya kuwalisha watu elfu tano
kaeni
akabeba mikononi mwake
kuivunja mikate
mikate mizima
maana zaweza kuwa 1) alipokuwa akitazama juu 2) baada ya kutazama juu
walishiba hadi walipokuwa hawana njaa
wanafunzi walikusanya aua waaaaatu walikusanya
vikapu 12 vilivyojaa
waliokula mikate na samaki
wanaume 5,000
Mistari ifuatayo inaelaza matukio yaliyotokea baada ya Yesu kuwalisha watu elfu tano
Mistari hii inatoa historia juu ya muujiza amabo Yesu anataka kuuonesha juu ya kutumbea juu ya maji
"Punde tu baada ya Yesu kuwalisha watu wote"
"baadaye jioni" au "giza lilipoingia"
"na wanafunzi hahawezi kuiongoza mashua kwa sababu ya mawimbi makubwa"
kwani upepo ulivuma kinyume nao
zamu ya inne ilikuwa kati ya saa 9 za usiku mpaka machweo
akaitembea juu ya maji
"waliogopa sana
Roho ile iliyotengana na mwili wa mtu baada ya kifo
Petro alimjibuYesu
Hapa "kuona mawimbki" maana yake ni kwamba ni kwamba alitambua kuwa kulikuwa na upepo
"wewe uliye na imani ndogo kiasi hicho
Haukupaswa kuwa na mashaka
Hii ni sifa ya muhimu ya Yesu inayoonesha mahusiano kati yake na Mungu
Mistari hii inaeelza kile kilichotokea baada ya Yesu kutembea juu ya maji. Mistari hii inatoa muhtasari wa jinsi watu walivyokuwa wakiitikia kwenye huduma ya Yesu
Wakati Yesu na wanafunzi walipokuwa wamevuka bahari
Huu ni mji mdogo ulioko Kaskazini Magharibi mwa mji wa bahari ya Galilaya
"wanaume wa eneohilo waltuma ujumbe
waagonjwa walimsihi
"chini yavazi" au "ncha ya vazi"
"joho" au "kile alichokuwa amevaa"
wakawa salama
Herode alifikiri kuwa Yesu ni Yohana Mbatizaji amefufuka kutoka katika wafu.
Herodealikuwa amemwoa mke wa ndugu yake
Herode hakumwua Yohana mbatizaji mara moja kwa sababu aliwahofia watu ambao walimtambua Yohana kuwa ni nabii
Herode aliahidi kwa kiapo kumpa Herodia chochote ambacho angeomba.
Binti wa Herodia aliomba kichwa cha Yohana Mbatizaji kiletwe kwenye sahani
Herode alimpatia Binti wa Herodia kwa sababu ya kiapo chake na kwa sababu ya watu waaliokuwapo kwenya sherehe hiyo.
Yesu aliwahurumia na kuwaponya wagonjwa wao.
Yesu aliwaambia wanafunzi wake kuwapa umati chakula.
Yesu alitazama juu mbinguni, akabariki na kumega mikate na akawapa wanafunzi wake, nao wakawapa umati.
Waliokula walikuwa wanaume elfu tano bila ya kuwahesabu wanawake na watoto, na vilibaki vikapu kumi na mbili.
Yesu alipanda yeye mwenyewe mlimani kuomba.
Ile mashua ya wanafunzi ilikuwa ikiyumbayumba kwa sababu y a upepo na mawimbi.
Yesu alikwenda kwa wanafunzi kwa kutembea juu ya maji.
Yesu aliwaambia wanafunzi wake wajipe moyo na wasiogope.
Yesu alimwambia Petro aje na atembee juu ya maji.
Petro alianza kuzama ndani ya maji alipoogopa.
Wakati Yesu na Petro walipoingia kwenye mashua upepo ulikoma kuvuma.
Wanafunzi walipoona jambo hili walimwabudu Yesu na kusema kweli alikuwa ni Mwana wa Mungu.
Wakati Yesu na wanafunzi walipokwenda upande mwingine wa bahari, watu walimletea Yesu wagonjwa wote.
1Ndipo Mafarisayo na waadishi walikuja kwa Yesu kutoka Yerusalemu. Na kusema,2“Kwa nini wanafunzi wanayaharibu mapokeo ya wazee? Kwa kuwa hawanawi mikono yao wanapokuwa wanakula chakula.”3Yesu akawajibu na kusema, “Nanyi, kwa nini mnaiharibu sheria ya Bwana kwa ajili ya mapokeo yenu?4Kwa kuwa Mungu alisema, ‘Mheshimu baba yako na mama yako;’ na ‘Asemaye uovu kwa baba yake na mama yake, hakika atakufa.’5Lakini ninyi husema, ‘Kila amwambiaye baba yake na mama yake, ‘Kila msaada ambao angepata kutoka kwangu sasa ni zawadi kwa Mungu,”6Mtu huyo hana haja ya kumuheshimu baba yake. Katika namna hii mmelitoa neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu.7Enyi wanafiki, ni vema kama Isaya alivyo tabiri juu yenu aliposema,8‘Watu hawa wananiheshimu mimi kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami.9Wananiabudu bure, kwa sababu wanafundisha mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu.”’10Ndipo akawaita umati na kuwaambia, “Sikilizeni na muelewe.11Hakuna kitu kiingiacho mdomoni mwa mtu na kumfanya najisi. Bali, kile kitokacho kinywani, hiki ndicho kimfanyacho mtu kuwa najisi.”12Ndipo wanafunzi wakamfuata na kusema na Yesu, “Je! Unafahamu Mafarisayo walipolisikia lile neno walikwazika?”13Yesu aliwajibu na kusema, “Kila mmea ambao Baba yangu wa mbinguni hajaupanda utang'olewa.14Waacheni pekee, wao ni viongozi vipofu. Kama mtu kipofu atamuongoza kipofu mwenzake, wote wawili wataanguka shimoni.”15Petro akajibu na kumwambia Yesu, “Tuelezee mfano huu kwetu.”16Yesu akajibu, “Nanyi pia bado hamuelewi?17Ninyi hamuoni kuwa kila kiendacho mdomoni hupitia tumboni na kwenda chooni?18Lakini vitu vyote vitokavyo mdomoni hutoka ndani ya moyo. Ndivyo vitu vimtiavyo mtu unajisi.19Kwa kuwa katika moyo hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushuhuda wa uongo, na matusi.20Haya ndiyo mambo yamtiayo mtu unajisi. Lakini kula bila kunawa mikono hakumfanyi mtu kuwa najisi.”21Ndipo Yesu akatoka mahali pale na akajitenga kuelekea pande za miji ya Tiro na Sidoni.22Tazama akaja mwanamke Mkanani kutoka pande hizo. Akapaza sauti akisema, “Nihurumie, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu anateswa sana na pepo.”23Lakini Yesu hakumjibu neno. Wanafunzi wake wakaja wakimsisitiza, wakisema, “Muondoe aende zake, maana anatupigia kelele.”24Yesu aliwajibu na kusema, “Sikutumwa kwa mtu yeyoye isipokuwa kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.”25Lakini alikuja na kuinama mbele yake, akisema, “Bwana nisaidie.”26Alimjibu na kusema, “Siyo vema kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.”27Akasema, “Ndiyo, Bwana, hata hivyo mbwa wadogo hula chakula kiagukacho mezani mwa Bwana wao.”28Ndipo Yesu akajibu na akisema, “Mwanamke, imani yako ni kubwa. Na ifanyike kwako kama utakavyo.” Na binti yake alikuwa ameponywa katika wakati huo.29Yesu aliondoka mahali pale na kwenda karibu na bahari ya Galilaya. Kisha alienda juu ya mlima na kuketi huko.30Kundi kubwa likaja kwake. Na kumletea viwete, vipofu, bubu, vilema na wengine wengi, waliokuwa wagonjwa. Waliwaweka katika miguu ya Yesu na akawaponya.31Nao umati wakashangaa walipoona mabubu wakiongea, na vilema wakifanywa wazima, viwete wakitembea, na vipofu wakiona. Walimsifu Mungu wa Israeli.32Yesu akawaita wanafunzi wake na kusema, “Nimewaonea huruma umati, kwa sababu wamekuwa nami kwa siku tatu bila kula kitu chochote. Sitawaaga waende kwao bila kula, wasije wakazimia njiani.”33Wanafunzi wake wakamwambia, “Ni wapi tunaweza kupata mikate ya kutosha hapa nyikani kushibisha umati mkubwa hivi?”34Yesu akawaambia, “Mna mikate mingapi?” Wakasema, “Saba, na samaki wadogo wachache.”35Yesu akawaamuru umati uketi chini.36Aliitwaa ile mikate saba na samaki, na baada ya kushukuru, akaimega na kuwapa wanafunzi. Wanafunzi wakawapa umati.37Watu wote wakala na kutosheka. Na wakakusanya mabaki ya vipande vya chakula vilivyosalia vipande vipande, vilijaa vikapu saba.38Wote waliokula walikuwa wanaume elfu nne bila wanawake na watoto.39Kisha Yesu akauaga umati waende zao na akaingia ndani ya mashua na kwenda sehemu za Magadani.
Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka mbele kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari yote ya 15: 8-9, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.
"Desturi za wazee," yaani, sheria zilizotamkwa, ni dhana muhimu katika sura hii. Hizi ndizo sheria ambazo viongozi wa kidini kati ya Wayahudi walikuza ili kuhakikisha kwamba Sheria ya Musa ilipata utii. Hata hivyo, sheria hizi mara nyingi zilikuwa muhimu zaidi katika vitendo kuliko Sheria ya Musa yenyewe. Yesu aliwakemea viongozi wa kidini kwa hili, na kwa sababu hiyo wao wakawa na hasira.
Imani ya mwanamke Mkanaani kwake Yesu ulikuwa tofauti sana na kutomkubali kwa viongozi wa Kiyahudi. Tofauti hii ilichangia kukemewa vikali kwa viongozi hao.
Watu mara nyingi huashiriwa kama kondoo katika maandiko. Katika sura hii, taswira ya kondoo inaonyesha kuwa Wayahudi walikuwa wamepotea kiroho bila ya kuwa na kiongozi mwafaka wa kuwaongoza.
Hapa Yesu anajibu hoja za Wayahudi
wanafunzi wako hawaziheshimu taratibu amabzo mababu zetu walitupa
Hizi si sawa na sheria za Musa. haya ni mafundisho na tafsiri za sheria zilizotolewa na viongozi wa dini baada ya Musa
kunawa huku siyo tu kwa kusafisha mikono. Hii inamaanisha kunawa kwa desturi kutokana na taratibu za wazee. Hawaoshi mikono yao vizuri
Nami n aona kwamba mnakataa kuzitii sheria za Mungu ili tu mweze kufuata kile ambacho mababu zenu waliwafundisha
Yesu anaendelea kwajibu Mafarisayo
Katika mstariwa 4, Yesu ananukuu m ara mbili kutoka kitabu cha kutoka ili kuonyesha jinsi Mungu anavyotegemea watu kuwatendea wazazi wao
watu watamuua
Lakini mnafundisha kuwa mtu hahitajio kuwaheshimu wazazi wake kwa kuwapa kitu ambacho kingeweza kuwasaidia kama mtu atawaambia wazazi wake hivyo tayari ameto zawadi kwa Mungu
inamaanisha kuwa baba yake ni mzazi wake. Hii inamaanisha kuwa viongozi wa dini waliwafundisha kuwa mtu hana haja ya kumheshimu mzazi wake kwa kumsaidia.
Mmezifanya desturi zenu kuwa za muhimu kulikko neno la Mungu
Yesu anahitimisha majibu yake kwa Mafarisayo
Katika mstari wa 8 na 9Yesu anamnukuu nabii Isaya kwa kuwakemea Mafarisayo na waandishi
Isaya alisema ukweli katika unabii wake juu ayenu
aliposema kile ambacho Mungu alisema
Watu hawa wanasema kweli kwangu
viwakilishi vya "kwang"u vinaanisha Mungu
watu hawjajitoa kwa ukweli kwa Mungu
"Ibaada zao hazina maana kwangu" au "wanaigiza kuniabudu mimi"
"shseria ambazo watu hutengeneza
Yesu anaanza kuwafundisha makutano na wanafunzi wake juu ya kile kinachomtia mtu unajisi na kwa nini mMafarisayo na waandishi walikuwa wamekosea kumkosoa Yesu
Sikilizeni kwa makini kile ninachosema ili muelewe maana yake.
Yesu anatofautisha kile ambacho mtu hula na kile asemacho. Yesu anamaanisha kuwa Mungu hujali zaidikile ambacho mtu husema kuliko kile ambacho hula
Usemi huu uliwafanya Mafarisayo wachukie
Hiki ni kirai kinachomaanisha kuwa Mafarisayo si watu wa Mungu, kwa hiyo Mungu atawatoa
Hiki ni cheo cha Yesu kinachoonesha uhusiano kati yake na Mungu
Baba yangu atawang'oa
neno pekee linamaanisha Mafrarisayo
Inamaanisha kuwa Mafarisayo hawajui amari za Mungu au jinsi ya kumpendeza Mungu Kwa hiyo, hawawezi kuwafundisha wengine jinsi ya kumpendeza Mungu
Yesu anaeleza mfano amabao amefundisha katika 15:12
kwetu wanafunzi
Yesu mfano kuwakemea wanafunzi kwa kutokuelewa mfano. Pia kwakilisha cha "hamu" kimesisitizwa. Yesu hawezi kuwaamini wanafunzi wake kwa kutokuelewa. Nimekatishwa tamaa na ninyi wanafunzi wangu kwa kuwa hamjaelewa kile ninachofundisha.
Yesu anatumia swli kuwakemea wanafunzi kwa kutokuelewa mfano. "hakika mnaelewa ... kwenda chooni"
hupitia mdomoni
Hii ni tafsida kwa eneo ambalo watu huzika uchafu wa mwili
Yesu anaendelea kufundisha mfano aliofundisha katika 15:12
Hii inamaanisha kile ambacho mtu husema
Hapa "moyo" inamaanisha akili za mtu au ndani ya mtu.
kuua mtu asiye na kosa
Kusema kitu juu ya mtu mwingine ambacho ni cha kuumiza na si cha kweli
Hii inamaansha mtu ambaye hajaosha mikono kwa desturi za wazee
Hii inaazisha habari y aYesu kumponya binti wa mwanamke Mkananayo
Inamaanisha kuwa wanafunzi waliondoka na Yesu
Kulikuwa na mwanamke Mkanaani aliyekuja kwa Yesu
"mwanamke kutoka kundi la watu aliyeitw Mkaanani anayeishi katika eneo hilo.
Kirai hiki kinamaanisha kuwa alikuwa akimuomba Yesu amponye binti yake.
Yesu hakuwa Mwana wa Daudi kimwili, hii inaweza kutafsiriwa kama "wa kizazi cha Daudi"
Pepo linamtesa sana binti yangu
Hapa "neno" linamaanisha kile mtu asemacho
Mungu hakunituma kwa yeyote
Tazama 10:5
mwanamke Mkanaani alikuja
Hii inaonesha kuwa yule mwanake alikuwa akinyeynyekeza mbele za Yesu
Yesu anamjibu mwanamke kwa kutumia mithali. Maana yake ni kwamba siyo sawa kuchukua kitu cha Wayahudi n a kuwapa watu wasio kuwa Wayahudi.
mkate unamaanisha chakula kwa ujumla
Wayahudi waliona mbwa kuwa ni wanyama najisi. hapa wanamanisha kama sura ya watu wasio Wayahudi
Yule Mwanamke akamjibu Yesu kwa kutumia mazingira yale yale aliyetumia Yesu kwenye mithali. Alimaanisha kuwa wasiokuwa Wayahudi waliweza kupata kiasi kidogo cha kile walichopata Wayahudi amabcho walikuwa wanatupa.
tazama 15"24
Nitafanya
Yesu alimponya yule binti
ghafla
Mstari huu unatoa histora ya muujiza amba Yesu anataka kuufanya wakulisha watu elfu nne
wale wasioweza kutembea, wale wasioona, wasiongea, na wale ambao miguu yao na mkono haifanyi kazi
waliwaweka katika mbele ya ya Yesu
vilema wakaw salama
watu viwete ... watu vilema ... watu vipofu.
Hii inaanzisha habari ya Yesu akiwalisha watu elfu nne
"kwa sababu wanaweza kuzimia njiani
hakuna mahali pa karibu tunapoweza kupata mikate ya kutosha huu umati mkubwa
mikate saba na samaki wachache wadogo
kaeni mkao wa kula
Yesu alibeba mkononi mwake
akaigawa mikate
akawapa mikate na samaki
wanafunzi walikusanya au watu walikusanya
watu waliokula
wanaume 4,000
lile eneo
Hili eneo wakati mwingine huitwa Magdala
Mafarisayo waliwazuia watoto kuwasaidia wazazi wao kwa kuchukua fedha kuwa "ni zawadi kutoka kwa Mungu"
Mafarisayo waliwazuia watoto kuwasaidia wazazi wao kwa kuchukua pesa na kuzifanya kuwa ni "zawadi toka kwa Mungu"
Isaya alitabiri kuwa mafarisyo watmheshimu Mungu kwa midomo yao, bali mioyo yao itakuwa mbali na Mungu
Isaya alitabiri kuwa Mafarisayo watamuheshimu Mungu kwa midomo y ao, lakini mioyo yao itakuwa mbali.
Mafarisayo walifundisha maagizo ya wanadamu kuwa ndiyo mafundisho
Yesu alisema kuwa kiingiacho mdomoni hakimtii mtu unajisi
Yesu alisema kile kitokachokinywani, ndicho kimfanyacho mtu kuwa najisi.
Yesu aliwaita Mafarisayo kuwa ni viongozi vipofu, na kwamba alisema kuwa watatumbukia shimoni.
Kutoka moyoni hukaa mawazo machafu, uuaji, uasherati, tamaa mbaya, wizi, ushuhuda wa uongo, na matusi
Yesu hakumjibu neno lolte
Yesu alieleza kuwa Yeye alikua ametumwa kwa kondoo wa nyumba Israeli waliokuwa waliopotea.
Yesu alisema kuwa yule mwanamke ana imani kubwa.
Yesu aliwaponya mabubu, viwete, vilema, na vipofu
Yesu aliwaponya mabubu, viwete, vilema, na vipofu
Wanafunzi walikuwa na mikate saba na samaki wadogo wachache?
Yesu aliichukua ile mikate na samaki halafu akashukuru, akaivunja ile mikate na akawapa wanafunzi.
Kulikuwa na vikapu saba vilivyojaa vilibaki baada ya kila mmoja kula.
Wanaume elfu nne, pamoja na wanawake na watoto walikula na walitosheka.
1Mafarisayo na Masadukayo walimjia na kumjaribu Yesu awaonyeshe ishara inayotoka angani.2Lakini Yesu aliwajibu na kuwaambia kuwa “Ikiwa ni jioni mnasema kuwa hali ya hewa ni nzuri, kwa kuwa anga ni jekundu.3Na asubuhi mnasema ‘Hali ya hewa leo si nzuri kwa kuwa anga ni jekundu na mawingu yameifunika anga yote.’ Mnajua kufafanua mwonekano wa anga, lakini hamwezi kufafanua ishara za nyakati.4Kizazi kiovu na cha uzinzi kinatafuta ishara, lakini hakuna ishara yoyote kitakachopewa, isipokuwa ile ya Yona.” Kisha Yesu akawaacha na akaenda zake.5Wanafunzi wakaja upande wa pili, lakini walikuwa wamesahau kuchukua mikate.6Yesu akawaambia “Jitahadharini na iweni makini na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.”7Wanafunzi wakahojiana miongoni mwao na kusema. “Ni kwa sababu hatukuchukua mikate.”8Yesu alitambua hilo na kusema, “Enyi wenye imani ndogo, kwa nini mmewaza na kusemezana miongoni mwenu na kusema kuwa ni kwa sababu hamkuchukua mikate?9Je bado hamtambui wala hamkumbuki ile mikate mitano kwa watu elfu tano, na vikapu vingapi mlivyokusanya?10Au mikate saba kwa watu elfu nne, na ni vikapu vingapi mlichukua?11Imekuwaje kuwa hata hamuelewi ya kuwa nilikuwa sizungumzi nanyi juu ya mikate? Jitunzeni na jihadharini na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.”12Kisha wakatambua kuwa alikuwa hawaambii juu ya kujihadhari na mikate iliyo na chachu, bali kujihadhari na mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo.13Wakati Yesu alipofika sehemu za Kaisaria ya Filipi, akawauliza wanafunzi wake, akisema, “Watu wanasema kuwa Mwana wa Adamu ni nani?”14Wakasema, “Wengine husema kuwa ni Yohana Mbatizaji; wengine, Eliya; na wengine, Yeremia, au mojawapo wa manabii.”15Akawaambia, “Ninyi mwasema mimi ni nani?”16Kwa akijibu, Simoni Petro akasema, “Wewe ni Kristo Mwana wa Mungu aliye hai.”17Yesu akamjibu na kumwambia, “Umebarikiwa wewe, Simoni Bar Yona, kwa kuwa damu na nyama havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.18Nami pia ninakwambia kuwa wewe ni Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu. Milango ya kuzimu haitalishinda.19Nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni. Chochote utakachokifunga duniani kitakuwa kimefungwa mbinguni, na chochote utakachokifungua duniani kitafunguliwa na mbinguni.”20Kisha Yesu akawaamuru wanafunzi wasimwambie mtu yeyote kuwa yeye alikuwa ni Kristo.21Tangu wakati huo Yesu alianza kuwaambia wanafunzi kuwa ni lazima aende Yerusalemu, kuteswa kwa mambo mengi katika mikono ya wazee na wakuu wa makuhani na waandishi, kuuawa na kufufuka siku ya tatu.22Kisha Petro akamchukua Yesu pembeni na kumkemea, na kusema, “Jambo hili na liwe mbali nawe, Bwana, hili lisitokee kwako.”23Lakini Yesu akageuka na kumwambia Petro, “Rudi nyuma yangu Shetani! Wewe ni kizuizi kwangu, kwa maana hujali mambo ya Mungu, bali mambo ya wanadamu.”24Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kama mtu yeyote akitaka kunifuata mimi, ni lazima ajikane yeye mwenyewe, auchukue msalaba wake, na anifuate.25Kwa kuwa anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, na kwa yeyote anayepoteza maisha yake kwa ajili yangu atayaokoa.26Je! Ni faida gani atakayopata mtu akipata dunia yote lakini akapoteza maisha yake? Je! Ni kitu gani atakachotoa mtu katika kubadilishana na maisha yake?27Kwa kuwa Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake na malaika wake. Naye atamlipa kila mtu kulingana na matendo yake.28Kweli nawaambieni kuna baadhi yenu mliosimama hapa ambao hawataonja mauti mpaka watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika ufalme wake.”
Mkate ni picha maalum katika 16:5-12. Yesu alitumia mjadala wa wanafunzi wake kuhusu mkate ili kuwaonya dhidi ya mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo. Aliyazungumzia mafundisho haya kana kwamba yalikuwa chachu, kiungo ambacho husababisha mkate kuinuka kabla ya kuokwa.
Wakati huo huo, kutajwa kwa mkate katika sura hii ni maana ya kuwakumbusha wasomaji kwamba Yesu alilisha watu elfu tano na mkate (tazama: Mathayo 14:13-21) na pia watu elfu nne (tazama: Mathayo 15:29-39 ). Maana ni kwamba Yesu hutoa mkate mzuri (mafundishoa), lakini Mafarisayo na Masadukayo hawafanyi hivyo.
Mathayo 16:21 huunda mkatizo katika maelezo haya. Katika hatua hii, Mathayo anatoa maoni kuhusu matendo ya Yesu ambayo yataendelea katika siku zijazo. Ni muhimu kwa mtafsiri kuashiria wazi wazi kwamba maoni haya ni kuhusu siku zijazo, yaliyoingizwa katika maelezo.
Kitendawili ni taarifa inayoonekana kuwa ya ajabu, ambayo ni kana kwamba inajikana yenyewe, lakini kwa hakika sio ya ajabu. Kitendawili kiko katika sura hii: "Yeyote anayetaka kuokoa maisha yake ataipoteza, na yeyote anayepoteza maisha yake kwa ajili yangu ataipata." (Mathayo 16: 24-28).
Hii inaanzisha mapambano kati y a Mafarisayo na Masadukayo
walimkosoa au walitaka kukamata
ni wakati wa siku ambapo juu huzama
hali nzuri, shwali na ya kuvutia
Wayahudi walijua kuwa, kama anaga litabarika na kuwa jekundu ilikuwa dalili ya kuwa siku inayofuat itakuwa nzuri
Yesu anaendelea kuwajibu Mafarisayo na Masadukayo
jua linapochomoza
hali ya mawingu na ya kimbunga
jekundu na zito
mwajua namna ya kutazama na kutambua aina ya hali ya hewa mtakayokuwa nanyo
lakini hamwezi kutambua kile kinachotokea sasa na kujua maana yake
watu amabao si waaminifu kwa Mungu
tazama 12:38
Mungu hatawapeni ishara
tazama 12:38
Mandhari yanabadilika nakuto eleka wakati wa mbale. Yesu anatumia nafasi ya kuwaonya wanafunzi juu ya Mafarisayo na Masadukayo
upande wa pili wa ziwa au upande wa pili wa bahari ya Galilaya
Hapa chachu inamaanisha mawazo macahfu na mafundisho yasiyo sahihi ya Mafarisayo Tazama 16:12.
wakajadiliana
Ninyi mlio na imani ndogo Tazama 6:30
Ninasikitika kuwa mnadhani kuwa mlisahau kuchukua mikate kwa sabasbu nimeongea juu ya chahu ya Mafarisayo na Masadukayo.
Yesu anaendelea kuwaonya wanafunzi juu ya Mafarisayo na Masadukayo
Kwa hakika mnakumbuka ... mlivyokusanya
"5,000 ... 4,000"
kwa hakika mnakumbuka ... mlivyokusanya!
Yesu anaendelea kuwaonya wanafunzi wake juu ya Mafarisayo na Masadukayo
"Inatakiwa muelewe kwamba siongei kumaanisha mikate kweli."
tazama 16:12
"wanafunzi"
Yesu anawauliza wanafunzi kama wanaelewa kuwa yeye ni nani
"Lakini ni ninyi ninaowauliza:mnasema kuwa mimi ni nani?"
Neno hili limetumika kuonesha mwanzo wa habari kuu au kumtambulisha mtu mwingine, Mathayo anaanza kueleza habari mpya.
Yesu anamaanisha yeye mwenyewe
Hapa neno "hai" linalinganisha Mungu wa Israeli na Miungu wengine wa uongo na masananu ambayo watu waliabudu. Mungu aliye ndiye Mungu pekee mwenye nguvu za kutenda.
"Simoni, mwana wa Yona"
damu na nyama inamaanisha binadamu
neno "hili" inamaanisha jibu la Petro kwamba Yesu ni Kristo mwana wa Mungu aliye juu
Hicho ni cheo cha muhimu kwa Mungu ambacho kinaelezea uhusiano kati ya Mungu na Yesu
hii inaongeza msisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye
jina Petro linamaanisha "mwamba"
hii inamaanisha kuwa Petro atakuwa kiongozi wa jamii ya watu wanomwamini Yesu
Maana zinazowezekana:1)"nguvu za kifo hazitaliweza kanaisa au 2) Kanaisa langu zitaivunja nguvu ya kifo kama jeshi liingiavyo katika mji
neno wewe linamaanisha Petro
Hapa "funguo" zinamaanisha Yesu akimpatia Petro mamlaka. Hii haimaanishi kuwa Petroni mmliki wa ufalme, lakini ana mamlaka ya kuamu nani ataiingia katika ufalme wa Mungu
Ufalme wa mbinguni limetumika katika Mathayo tu. tumia "mbingu"
kuwatangazia watu kusamehewa au kuhukumiwa kama ilivyofanyika mbinguni
kitu kinachotumika kufungua na kufunga milango
Mungu wa mbinguni ataruhusu maombi ya Petro kuruhusu au kufunga duniani
Mungu atafunga .. Mungu atafungua
Yesu antabiri kifochake na anaanza kuwambia wanafunzi wake gharama za kumfuata.
Baada ya Yesu kuwaamuru wanafunzi wake kutokumwambia yeyote kuwa yeye ni Kristo, alianza kushirikisha kile kitakachotokea Yerusakamu
Hapa "mikono " inamaanisha mamlaka. Ambapo wazee, makuhani na waandishi watamsababishia maumivu
watamuua
"hapana" au "halitatokea" au "Mungu alizuie"
"siku ya tatu, Mungu atamfanya aishi tena"
Yesu anamaanisha kuwa Petro anafanya kazi kama shatani kwa sababu Petro anajaribu kumzuia Yesu kukamilisha kile ambacho Mungu amemtuma Yesu. "Rudi nyuma yangu kwa sababu unafanya kama shetani! wewe ni kikwazo kwangu.
"uwe mwanafunzi wangu" au "uwe mmoja wa wanafunzi wangu"
msalaba unawakilisha mateso na kifo. lazima anitii hata kiasi cha kufa"
"na kunitii"
"Kwa yeyote anayetaka"
Hii haimanishi kuwa yule mtu lazima afe. inamaanisha kumwamini Yesu kuwa jambo la muhimu kuliko maisha yake.
"kwa sababu ananiamini mimi" au " kwa sababu yangu"
atapata maisha ya kweli
Haimpi mtu faida ...maisha yake
hakuna kitu cha thamani duniani kuliko kuishi na Mungu. " kama akipata kila kitu ulimwenguni"
"lakini akapoteza maisha yake"
"Hakuna kitu ambacho mtu atatoa ili kurudisha uhai wake"
Yesu alikuwa anajirejelea yeye mwenyewe katika nafsi ya tatu kama "Mwana wa mtu"
"kupata utukufu sawa na Baba yake"
"na malaika watakuwa pamoja naye" au "na malaika wa Baba watakuwa pamoja na mimi"
Hicho ni cheo kikubwa kwa Mungu ambacho kinaelezea uhusiano wa Mungu na Mwana wa mtu, Yesu
"Nawaambieni ukweli"
kiwakilishi cha wingi kinachomaanisha wanafunzi wa Yesu.
"kuonja" inamaanisha kupitia kifo" au "hawatapitia kifo" aua "hawatakufa"
"Ufalme" inamaanisha Mwana Adamu akitawala kama mfalme" aua "mpaka watakapomwona wa Adamu akija kutawala kama mfalme"
Yesu bado anaongelea wanafunzi. "mpaka mtakapomwona"
Walitaka awaonyeshe Ishara
Yesu alisema angewapatia Mafarisayo na Masadukayo ishara ya Yona.
Yesu aliwaambia wanafunzi wake wajitahadharishe na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.
Yesu alikuwa akiwaambia juu ya mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo
Watu wanasema kuwa Mwana wa Adamu ni nani?
Watu wengine walidhani kuwa Yesu alikuwaYohana Mbatizaji
Jibu la Petro lilikuwa hivi, "Wewe ni Kristo, mwana wa Mungu aliye hai".
Alifunuliwa na Baba wa mbiguni
Alipewa mamlaka ya kufunga chochote duniani, na kitakuwa kimefungwa mbinguni, na chochote atachokifungua duniani kitafunguliwa na mbinguni.
Ni lazima aende Yerusalemu, kuteswa kwa mambo mengi katika mikono ya wazee na wakuu wa makuhani na waandishi, kuuawa na kufufuka siku ya tatu.
Yesu alimwambia Petro, "Rudi nyuma yangu shetani"
Ni lazima ajikane yeye mwenyewe, auchukue msalaba wake, na amfuate Yesu.
Yesu alisema kuwa haimpii faida mwanadamu kuupata ulimwengu wote.
Yesu alisema kuwa Mwana Adamu atakuja katika utukufu wa baba yake na malaika wake.
Mwana wa Adamu atamlipa kila mtu kutokana na matendo yake atakapokuja
Yesu alisema kuwa baadhi yao waliokuwa wamesimama naye watamwona mwana wa Adamu akija katika ufalme wake.
1Siku sita baadaye Yesu aliwachukua pamoja naye Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, na akawachukua mpaka juu ya mlima mrefu wao wenyewe.2Alibadilishwa mbele yao. Uso wake ukang'aa kama jua, na nguo zake zilionekana zenye kung'aa kama nuru.3Tazama, pale walitokea Musa na Eliya wakiongea naye.4Petro akajibu na kumwambia Yesu, “Bwana, ni vema kwetu sisi kuwepo mahali hapa. Kama ukitamani, nitajenga hapa vibanda vitatu - kimoja chako, na kimoja kwa ajili ya Musa, na kimoja kwa ajili ya Eliya.”5Wakati anaongea, tazama wingu jeupe likawatia kivuli, na tazama, ikatokea sauti toka kwenye wingu, ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa ninayependezwa naye. Msikilizeni.”6Wanafunzi waliposikia hayo, wakaanguka kifudifudi na wakaogopa sana.7Kisha Yesu akaja akawagusa na kusema, “Inukeni wala msiogope.”8Nao wakainua nyuso zao juu lakini hawakumwona mtu isipokuwa Yesu pekee.9Na walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu akawaagiza, akasema, “Msitoe habari ya maono hayo mpaka Mwana wa Adamu atakapofufuka kutoka katika wafu.”10Wanafunzi wake wakamwuliza, wakisema, “Ni kwa nini waandishi wanasema kuwa Eliya atakuja kwanza?”11Yesu akawajibu na kusema, “Eliya atakuja kweli na atarudisha mambo yote.12Lakini naawaambieni ninyi, Eliya amekwisha kuja, lakini hawakumtambua. Badala yake, walimfanyia mambo watakayo wao. Na hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyoteswa katika mikono yao.”13Ndipo wanafunzi wakatambua kuwa alikuwa akiongea habari za Yohana Mbatizaji.14Walipofika katika umati, mtu mmoja alimwendea, akapiga magoti mbele zake, na kumwambia,15“Bwana, umhurumie mwanangu, maana amekuwa na kifafa na kuteseka sana. Kwa kuwa mara nyingi huanguka motoni au kwenye maji.16Nilimleta kwa wanafunzi wako, lakini hawakuweza kumponya.”17Yesu akajibu akisema, “Enyi Kizazi kisichoamini na kilichoharibika, nitakaa pamoja nanyi mpaka lini? Nitavumiliana nanyi hata lini? Mlete hapa kwangu.”18Yesu alimkemea, na pepo akamtoka. Kijana aliponywa tangu saa ile.19Kisha wanafunzi wakamjia Yesu kwa siri na kumwuliza, “Kwa nini hatukuweza kumfukuza?”20Yesu akawaambia, “Kwa sababu ya imani yenu ndogo. Kweli nawaambieni, kama mtakuwa na imani hata ndogo kama punje ya mbegu ya haradali, mtaweza kuuambia mlima huu, hama kutoka hapa uende kule, nao utahama na hakutakuwa na kitu chochote cha kushindikana kwenu.21122Wakati wakiwa bado Galilaya, Yesu akawaambia Wanafunzi wake, “Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa watu.23Na watamwua, na siku ya tatu atafufuka.” Wanafunzi walihuzunika sana.24Nao walipofika Kapenaumu, watu wakusanyao kodi ya nusu shekeli wakamwendea Petro na kusema, “Je mwalimu wenu hulipa kodi ya nusu shekeli?”25Akasema, “Ndiyo” Lakini Petro alipoingia ndani ya nyumba, Yesu akaongea na Petro kwanza na kusema, “Unafikiria nini Simoni? Wafalme wa dunia, hupokea kodi au ushuru kutoka nani? Kwa wale wanaowatawala au kutoka kwa wageni?26Na wakati Petro aliposema, “Kutoka kwa wageni” Yesu akamwambia, hivyo watawaliwa wameondolewa katika ulipaji.27Lakini tusije tukawafanya watoza ushuru wakatenda dhambi, nenda baharini, tupa ndoano, na umtwae yule samaki ajaye kwanza. Baada ya kuufungua mdomo wake, utakuta mle shekeli moja. Ichukue na uwape watoza ushuru kwa ajili yangu na wewe.
Nabii Malaki alitabiri kwamba siku moja Eliya atarudi kabla Masihi hajaja. Yesu anaelezea kwamba Yohana Mbatizaji alitimiza unabii huu kwa kumtumikia Mungu kwa namna ile ile kama Eliya. na )
Utukufu wa Mungu unaonekana kama mwanga mkubwa, katika maandiko. Utukufu wa Mungu daima humhofisha mtu anayeuona. Tukio hilo, lililoko katika sura hii, linaitwa "kubadilika," ambako Yesu anabadilika ili aonyeshe utukufu wake wa uungu. na )
Hii inazisha habariya Yesu kubadilika sura
"Petro, Yakobo, na kaka yake Yakobo Yohana"
"Mungu amembadilisha kabisa Yesu
"nguo"
Hii ni milinganyo inayosisitiza jinsi Yesu alivyong'aa.
Neno hili linatutayarisha kuwa tayari kwa taarifa za kushangaza zinazofuata.
kwa wanafunzi waliokuwa na Yesu amabao ni Petro, Yakobo na Yohana
"sema." Petro hajibu swali.
"pamoja na Yesu"
Maana zinazowezekana: 1)"ni vizuri kwamba sisi wanafunzi tuko hapa pamoja nawe, Musa, na Eliya au 2)"ni vizuri kuwa wewe, Musa, Eliya, na sisi wanafunzi wote tuko hapa pamoja"
Maana zinazowezekana: 1)mahali pa watu kuja kuabudia au 2)mahali pa muda pa watu kulala.
Hii hutahadharisha msomaji kuwa makini na maelezo ya kushangaza yanayofuata
"lilikuaj juu yao"
"Sauti inamaanisha Mungu aliogea" aua "Mungu aliongea noa kutoka kwenye wingu"
"wanafunzi walimsikia Mungu akiongea"
Wanafunzi waliinama kwa nyuso zao kugusa chini ardhini.
Tukio lifuatalo lilitokea mara tu baada ya wale wanafunzi watatu kushuhudia Yesu akibadilishwa
Na Yesu na wanafunzi wake
yeye anajinenea mwenyewe
Wanafunzi wanazingatia mafundisho ya kwamba Eliya atarudi kwanza kwa wana wa Israel kabla ya Masihi kurudi
"kuweka vitu katika mpangilio au utaratibu" au " waandae watu tayari kwa ajili kumpokea Masihi"
huu ni msisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye
Maana zinazowezekana: 1) viongozi wa wayahudi au 2) wayahudi wote
Hapa "mikono" inamaanisha nguvu. "watamfanya mwana wa Adamu kuteseka"
Yesu anajineneea mwenyewe.
Hii inaanzisha habari ya Yesu akimponya kijana aliyekuwa na roho mchafu.Tukio hili limetokea baada ya Yesu na wanafunzi wake kushuka kutoka mlimani.
inamanisha kuwa yule mtu alimtaka Yesu amponye mwanae. "umhurumie mwangu na umponye"
Hii inamaanisha kuwa wakati mwingine hupoteza fahamu
"Kizazi hiki hakimwani Mungu na hakijiui kitu kibaya na kizuri.
nimechoka kukaa pamojana nyi, nichoshwa na kutokuamni kwenu
kijana akawa mzima
mara moja
waongeaji na si wasikilizaji
"Kwa nini tusimfanye pepo amtoke kijana?"
"Mtaweza kufanya kitu chochote
"nawambia ukweli"
Yesu analinganisha ukubwa wa mbegu ya haradari na kiasi cha imani kinachotakiwa ili kufanya miujiza. inahitajika imani ndogo tu ili kufanya miujiza.
mtaweza kufanya kila kitu
Yesu anatabiri kifo chake na ufufuo
"wanafunzi na Yesu wamekaa"
"mmoja atamuua Mwana wa Adamu"
inamaanisha yeye yenyewe
"Mungu atamfufua" au" ataishi tena"
atatolewa
mikononi inamaanisha mamlaka ya kutwala. "katika utawala wa watu
siku ya tau
Mungu atamfufua
Yesu anamfundisha Petro juu ya kulipa ada ya hekalu
wakati yesu na wanafunzi wake
kodi juu ya wanaume wote wa kiyahudi ambayo ilitolewa ili kuwezesha kazi za hekaluni
mahali Yesu alipokaa
Yesu anauliza swali hili kumfundisha Simoni asitafute taarifa kutoka kwake. "Sikiliza Simoni, tunafahamu kuwawafalme wa dunia hukusanya kodi kutoka kwa wageni na wala si kwa raia wake.
viongozi kwa ujumla
watu chini ya kiongozi au mfalme
watu walio chini ya mfalme
Yesu anaendela kumfundisha Petro juu ya kulipa kodi
Huu ni mwisho wa habariinayoanzi 13:54 amabpo mwandishi amaeelza juu ya upinzani wa wa huduma ya Yesu kuhusu ufalme wa mbinguni
wakati Petro aliposema "ndiyo. hiyo ni sawa ,wafalme hukusanya kodi kutoka kwa wageni"
Nyakati hizi za leo. wafalme wanatoza kodi toka kwa raia wake, lakini katika nyakati za zamani wafalme walitoza kodi toka kwa watu waliokuwa wamewashinda na si raia wao.
Watu chini ya kiongozi au mfalme.
lakini tusiwafanye watoza ushuru kutenda kuwa na hasira
wavuvi hufunga ndoano mwisho wa uzi, na kisha huitupa majini ili kukamata samaki
"mdomo wa samaki"
sarafu iliyotosha malipo ya kibarau kwa siku moja
chukua shekeli
wewe inamaanisha Petro. Kila mwanamume alipaswa kulipa shekeli moja. kwa hiyo Shekel moja iliweza kutosha kwa kodi ya Peteo na Yesu
Petro, na Yakobo na Yohana kaka yake.
Yesu alibalishwasura kiasI kwamba sura yake iling'aa kama jua, na mavazi yake yaling'aa kama nuru.
Akawatokea Musa na Eliya wakaongea naye
Yesu alisema wajenge vibanda vitatu kwa ajili ya wale wanaume watatu.
Huyu ni mwanangu mpedwa, niliyependezwa naye.
Wasitoe habari ya maono hayo mpaka Mwana wa Adamu atakapofufuka kutoka kwa wafu.
Yesu akawajibu na kusema, Eliya atakuja kweli na atarudisha vitu vyote.
Yesu alisema kuwa Yohana Mbatizaji ndiye aliyekuwa Eliya ambaye tayari alikuwa amekwisha kuja, na walimfanyia kile walichotaka kumfanyia.
Yesu alisema Yohana Mbatizaji alikuwa Eliya ambaye tayari alikuwa amekwisha kuja, na walimfanyia chochote walichotaka kumfanyia.
Walikuwa wakiweza kumponya kijana mwenye kifafa.
Wanafunzi hawakuwa na uwezo wa kumponya yule mgonjwa wa kifafa.
Yesu alilikemea lile pepo, na yule kijana alipona tangu saa ile
Yesu alisema kuwa ni kwa sababu ya imani yao ndogo kwa hiyo wasingeweza kumponya yule kijana mwenye kifafa.
Kuwa Mwana wa Mtu atatiwa mikononi mwa watu, watamwua, na siku ya tatu atafufuka.
Yesu aliwaambia wanafunzi wake kuwa atatiwa mikononi watu ambao watamwua, na kwamba siku ya tatu atafufuliwa.
alimwambia Petro kwenda baharini, akatupe ndoano na kuchuku yule samaki wa kwanza, naye atakuwa na shekeli mdomoni mwake kwa ajili ya kodi.
1Muda huo huo wanafunzi wakaja kwa Yesu na kumwambia, “Ni nani aliye mkubwa katika ufalme wa mbinguni?”2Yesu akamwita mtoto mdogo, akamweka katikati yao,3na kusema, “Kweli nawaambieni, msipotubu na kuwa kama watoto wadogo hamtaweza kuingia katika ufalme wa Mungu.4Hivyo yeyote ajishushaye kama mtoto mdogo, mtu kama huyo ni mkuu katika ufalme wa mbinguni.5Na yeyote ampokeaye mtoto mdogo kwa jina langu anipokea mimi.6Lakini yeyote asababishaye mmoja kati ya wadogo hawa wanaoniamini kuasi, itakuwa vizuri kwa mtu huyo jiwe kuu la kusagia likafungwa shingoni mwake, na kuzamishwa kilindini mwa bahari.7Ole kwa dunia kwa sababu ya wakati wa kukwazwa! Kwa kuwa haina budi kwa nyakati hizo kuja, lakini ole kwake kwa mtu yule nyakati hizo zitakuja kwa ajili yake!8Kama mkono wako au mguu wako ukikusababishia kukwazika, ukate na uutupe mbali na wewe. Ni vizuri zaidi kwako wewe kuingia kwenye uzima ukiwa bila mkono au kilema, kuliko kutupwa kwenye moto wa milele ukiwa na mikono yote au miguu yote.9Kama jicho lako likikukwaza, uling`oe na ulitupe mbali na wewe. Ni vizuri zaidi kwako wewe uingie kwenye uzima na jicho moja, kuliko kutupwa kwenye moto wa milele ukiwa na macho yote.10Tazameni kwamba msije mkamdharau mmoja wa wadogo hawa. Kwa maana nawambieni kuwa mbinguni kuna malaika wao siku zote wakiutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni.11112Mnafikiri nini? Ikiwa mtu ana kondoo mia moja, na mmoja wao akapotea, je hatawaacha tisini na tisa mlimani na kwenda kumtafuta mmoja aliyepotea?13Na akisha kumpata, kweli nawaambieni, anamfurahia kuliko wale tisini na tisa wasiopotea.14Vivyo hivyo, siyo mapenzi ya Baba yenu wa mbinguni kuwa mmoja wa wadogo hawa aangamie.15Kama ndugu yako akikukosea, nenda, kamwonyeshe dosari iliyopo kati yako na yeye akiwa pekee yake. Kama akikusikiliza, utakuwa umemrejesha ndugu yako.16Lakini kama hatakusikiliza, mchukue ndugu mmoja au wawili zaidi pamoja nawe, kwa kuwa kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno linaweza kuthibitishwa.17Na kama akipuuza kuwasikiliza, liambie kanisa jambo hilo, kama akipuuza vilevile kulisikiliza kanisa, basi na awe kama mtu wa mataifa na mtoza ushuru.18Kweli nawaambieni, chochote kile mtakachokifunga duniani na mbinguni kitafungwa. Na chochote mtakachokifungua duniani na mbinguni kitafunguliwa.19Tena nawaambieni kwamba kama watu wawili kati yenu wakikubaliana juu ya jambo lolote duniani waliombalo, hilo Baba yangu wa mbinguni atalifanya.20Kwa kuwa wawili au watatu wakikusanyika pamoja kwa jina langu, Mimi niko katikati yao.21Tena Petro akaja na kumwambia Yesu, “Bwana, ni mara ngapi ndugu yangu akinikosea nami nimsamehe? Hata mara saba?”22Yesu akamwambia, “Sikuambii mara saba, lakini hata sabini mara saba.23Kwa sababu hiyo ufalme wa mbinguni ni sawa na mfalme fulani aliyetaka kusahihisha hesabu kutoka kwa watumwa wake.24Alipoanza kusahihisha hesabu, mtumwa moja akaletwa kwake ambaye alikuwa anamdai talanta elfu kumi.25Kwa kuwa hakuwa na njia ya kulipa, bwana wake aliagiza auzwe, mke wake pamoja na watoto wake na kila kitu alichokuwa nacho, na malipo yafanyike.26Hivyo mtumwa alianguka, akapiga magoti mbele yake, akisema, ‘Bwana, uwe na uvumilivu pamoja nami, na nitakulipa kila kitu.’27Hivyo bwana wa yule mtumwa, kwa kuwa alisukumwa sana na huruma, alimwachilia na kumsamehe deni hilo28Lakini mtumwa yule alitoka na kumpata mmoja kati ya watumwa wenzake, aliyekuwa anamdai denari mia. Alimvuta, akamkaba kooni, na kumwambia, ‘Nilipe kile ninachokudai.’29Lakini yule mtumwa mwenzake alianguka na kumsihi sana, akisema, ‘Uwe na uvumilivu nami, na nitakulipa.’30Lakini mtumwa yule wa kwanza alikataa. Badala yake, alienda na kumtupa gerezani, mpaka atakapo mlipa kile anachomdai.31Na walipoona watumwa wenzake kile kilichotokea. Walisikitishwa sana. Walikuja na kumwambia bwana wao kila kitu kilichotokea.32Ndipo yule bwana wa mtumwa yule alimwita, na kumwambia, ‘Ewe mtumwa mwovu, nilikusamehe wewe deni langu lote kwa sababu ulinisihi sana.33Je! Haukutakiwa kuwa na huruma kwa mtumwa mwenzio, kama mimi nilivyokuhurumia wewe?34Bwana wake alikasirika na kumkabidhi kwa wale watesaji mpaka atakapolipa kiasi chote alichokuwa anadaiwa.35Hivyo ndivyo Baba yangu wa Mbinguni atakavyowafanyia, kama kila mmoja wenu hatamsamehe ndugu yake kutoka moyoni mwenu.”
Katika sura hii, Yesu anafundisha kwamba ni muhimu kwa wafuasi wake kuacha ugomvi kati yao wenyewe. Anafundisha kwamba kikundi cha waumini lazima kiwe tayari kuwezesha hii kufanyika kwa njia "inayomheshimu Mungu.
Kanisa lina jukuma pia wa kuwahimiza waumini kutubu ikiwa wanafanya dhambi. na )
Hii ni mwanzo wa habari mpya inayoanzia 18:34, mahali Yesu anapofundisha juu ya maisha katika uflme wa mbinguni. Hapa Yesu anatumia mtoto mdogo kufundisha wanafunzi wake.
Nani ambaye ni wa muhimu zaidi"au "nani kati yetu atakuwa wa muhimu zaid
wakati Mungu wetu wa mbinguni atakapoanzisha utawala wake duniani
"nawambia ukweli" au hii inaongeza msisitizo kwa kile Yesu alichosema baadaye
lazima mbadilike .. ili kuingia"
lazima wawe wanyeyenyekevu kama watoto.
Mungu kutawala kama mfalme
Yesu anawafundisha wanafunzi wake kwamba wanahitaji kuwa wanyeyekevu kama watoto ili kuwa watu wa muhimu kwenye ufakme wa mbingini
ni wa muhimu zaidi aua atakuwa ni wa muhimu
katika ufalme wa mbinguni
kwa sababu yangu
ni kama ananipokea mimi
"kama wangemwekea jiwe la kusagia shingoni mwake na kumtupa kilindini mwa bahari"
Jiwe kubwa, zito iliyotengenezwa kama duara inayotumika kusagia nafaka kuwa unga .
Yesu anaendela kutumia watoto wadogo kuwafundisha wanafunzi wake na kuwaonya dhidi ya madhara makubwa ya kuwaangusha watoto
dunia inamaanisha watu
kwa sababu ya mambo yanyowafanya watu kukwazwa
Yesu anaongea na wanafunzi wake kama ni mtu mmoja.
kwamba mambo hayo huja yanayowafanya watu kufanya dhambi
mtu yeyote anayewafnya wengine kufanya dhambi
Yesu anamaanisha kuwa mtu lazima afanye kila linalolazimika ili kukitoa katika maisha kile kinachomfanya mtu kufanya dhambi
Yesu anaongea kwa watu wote kwa ujumla
uzima wa milele
kuliko kuwa na mikono miwil na miguu miwili wakati Mungu anakutupa kwenye moto wa milele.
Fungu hili linaonesha ukweli wa kutokuamini na ulazima wa kuizuia kwa gharama yoyote
"Ingia katika uzima wa milele"
Muwe waangalifu
"Msidhani kuwa hawa wadogo hawana umuhimu". onyesheni heshima kwa hawa wadogo
hii inatia msisitizo kwa kile Yesu alichosema baadaye
Yesu anammanisha kuwa malaika wa mbinguni humwambia Mungu juu ya wadogo hawa
"wapo karibu muda wote"
kila mara wako karibu na baba yangu"
Hiki ni cheo muhimu kwa Yesu kinachonesha uhsiano kati ya Yesu na Mungu
Yesu anaendele kuwatumia watoto wadogo kuwafundisha wanafunzi kueleza ulinzi wa Mungu kwa watu
"Fikiri watu wanavyofanya,"
viwakilishi vya wingi
Yesu anatumia mfano kuwafundisha wanafunzi
100 ...99
Yesu anatumia swali kuwafundisha wanafunzi
nawaambia ukweli
"Baba yenu mbinguni anataka wadogo wote hao waishi"
Yesu anaanza kuwafundisha wanafunzi wake juuy msamaha
waumini wenzake
"mtafanya mahusiano yenu mazuri tena na ndugu yako"
"mdomo" na "maneno" inamaanisha kile amabcho mtu anasema " ili kwamba wawili au watatu wanaweza kuthibitisha kile unachosema juu ya mwamini mwenzako"
Yesu anatumia moja katai ya sheria ambazo Musa alaiwapati watu
kama huyo nndugu akipuuza kuwasiliza mashahidiuliokuja nao
kwa waumini wote
"Mchukulie kama utakavyomchukulia mtu wa mataifa au "mtoza ushuru. Maana yake ni kwamba wamwondoe kati ya jamii ya waumini.
viwakilishi vyote hivi viko katka wingi
tazama 16:19
"Mungu atafunga...Mungu atafungua."
Msisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye
Hicho ni cheo cha muhimu kwa Mungu kinachoonesha uhusiano wa Mungu na Yesu.
anagalau wawili
"wawili au zaidi" au "angalau wawili"
"kutana"
inamaanisha "wawili wenu"
Hiki ni cheo muhimu cha Mungu kinachoonesha uhusiano kati ya Mungu na Yesu
"mara 7"
Maana zenye kufaa: 1) "70 mara 7". au 2) "mara 77." kama kutumia namba kutachanganya,unaweza kusema, "mara nyingi kuliko utakavyohesabu"
Yesu anatumia mfano kufundisha juuya msamaha na mapatano
Hii inatoa utangulizi wa mfano. Tazama 13:24
"ili awalipe watumwa wake kile walichostahili"
"mtu fulani akamleta mmoja wa watumishi wa wafalme"
"Talanta 10,000" au " fedha nyingi zaidi kuliko mtumishi alizoweza kulipa
"mfalme aliwaamuru watumishi wake kumuuza huyo mtu...na kulipa deni kwa fedha ya mauzo"
Hii inammanisha kuwa yule mtumwa aliongea na yule mfalme katika hali ua unnyenyekevu mkubwa.
"mbele ya mfalme"
"alimhurumia yulemtumwa"
alimwacha aende"
Yesu anaendelea kuwaambia mfano wanafunzi wake
"dinari 100" au "malipo ya kibarua ya siku miamoja"
"yulemtumwa wa kwanza alimkaba mtumwa mwenzake
kumung'ang'nia " au "kamata kwa nguvu"
Tazama 18:26
Yesu anaendelea kuwaambia mfano wanafunzi wake
"yule mtumwa wa kwanza alienda na kumtupa gerezani mtumwa mwenzake"
"watumwa wengine"
"walimwambia mfalme"
Yesu anaendelea kuwambia mfano wanafunzi wake
"Kisha mfalme akamwita mtumwa wa kwanza"
"uliniomba
Mfalme anatuma swalikumkalipia mtumwa wa kwanza. "ulitakiwa ... wewe"
Yesu anamalizia mfano wake juu ya msamaha na upatanishi
Huuni mwaisho wa shsemu y a simulizi iliyoanzia 18:1 mahali ambapo Yesu anafundisha juu ya maisha katika ufalme wa mbinguni.
"Mfalme"
"alimtoa kwa" inawezekena kuwa mfalme mwenyewe hakumkabidhi yule mtumwa wa kwanza kwa watesaji," "Aliwaagiza watumwa wake wamkabidhi"
"kwa wale ambao wangemtesa"
Hii inaweza kutafasiriwa kwa mafumo tendaji. Kile ambacho mfalme alimdai yule mtumwa wa kwanza"
Hiki ni cheo muhimu kwa Mungu kinachoonesha uhusiano kati ya Mungu ya Yesu.
Viwakilishi vyote hivi viko katika wingi. Yesu anaongea na wanafunzi wake, lakini mfanohuu unafundisha ukweli ambao unaweza kutumiwa na waamini wote
"ndugu yake"
Hii ni nahau. "kwa ukweli" au "kwa ukamilifu"
Yesu alisema lazima tutubu na kuwa kama watoto wadogo.
Yeye ajishushaye kama mtoto mdogo, mtu kama huyo ni mkuu katika ufalme wa mbinguni.
Yeyote anayemkosesha mtoto mdogo amwaminiye Yesu kufanya dhami, ni vizuri mtu huyo kufungiwa jiwe la kusagia shingono mwake na kutupwa baharini.
Yesu alisema lazima tukitupe kila kitu ambacho kinatukwaza.
Kwa maana huko mbinguni malaika wao huutazama uso wa Baba siku zote.
Ni kwa sababu si mapenzi ya Baba kwamba mmoja wa wadogo hawa kupotea
Ni kwa sababu kuwa si mapenzi ya Baba kwamba mmoja wa wadogo hawa kupotea
Nenda ukwamwonyeshe kosa lililopo kati yako na yeye mwenyewe.
Kitu cha pili, ni kumchukua mtu mmoja au wawili kwa ajili ya ushahidi.
Kama akipuuza kuwasikiliza, liambie kanisa jambo hilo. kwenu kama mtu wa mataifa na mtoza ushuru.
Mwisho, kama hatalisikiliza kanisa, anataikwa umchukulie kama mtu wa mataifa au mtoza ushuru.
Yesu anaahidi kuwepo pamoja nao wawili au watatu waliokusanyika kwa jina lake.
Yesu alisema hata saba mara sabini.
Yesu alisema tunatakiwa kuwasamehe saba mara sabini.
Yule mtumwa alikuwa anadaiwa talanta kumi, ambazo hakuweza kuzilipa.
Yule mtumwa alikuwa anadaiwa talanta kumi, ambazo hakuweza kuzilipa.
Yule Bwana alimhurumia mtumwa wake na kumsamehe deni lake
Alienda akamtupa gerezani mpaka atakapomlipa kile anachomdai.
Yule Bwana alimwambia yule mtumishi kuwa alipaswa kumhurumia mtumishi mwenzake.
Alimkasirikia na akamkabidhi kwa wale watesaji mpaka atakapolipa yote aliyokuwa anadaiwa.
Yesu alisema kuwa Baba atatufanya kama yule Bwana alivyomfanyia mtumishi wake kama hatutawasamehe ndugu zetu kutoka mioyoni mwetu.
1Ilitokea wakati Yesu alipomaliza maneno hayo, akaondoka Galilaya, na akaenda mpakani mwa Yudea mbele ya mto Jordani.2Umati mkubwa ukamfuata, na akawaponya huko.3Mafarisayo wakamjia, wakamjaribu, wakamwambia, “Je ni halali kwa mtu kumwacha mke wake kwa sababu yoyote?”4Yesu akajibu na kusema, “Hamkusoma, kwamba yeye aliyewaumba mwanzo aliwaumba mume na mke?5Na tena akasema, ‘Kwa sababu hiyo mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuungana na mke wake, nao wawili watakuwa mwili mmoja?’6Hivyo siyo wawili tena, bali mwili mmoja. Basi, kile alichokiunganisha Mungu, mtu yeyote asikitenganishe.”7Wakamwambia, “Sasa kwa nini Musa alituamuru kutoa hati ya talaka na kumwacha?”8Akawaambia, “Kwa ugumu wenu wa mioyo Musa aliwaruhusu kuwaacha wake zenu, lakini tangu mwanzo haikuwa hivyo.9Nawaambieni, kwamba yeyote atakayemwacha mke wake, isipokuwa kwa sababu ya uzinzi, na akamwoa mwingine, amezini. Na mwanaume atakayemwoa mke aliyeachwa amezini.”10Wanafunzi wakamwambia Yesu, “Kama ndivyo ilivyo kwa mume na mkewe, siyo vizuri kuoa.”11Lakini Yesu akawaambia, “Si kila mtu anaweza kupokea mafundisho haya, bali ni kwa wale tu walioruhusiwa kupokea.12Kwa vile wapo matowashi waliozaliwa tokea tumboni mwa mama zao. Na vile vile kuna matowashi waliofanywa na watu. Na kuna matowashi waliojifanya matowashi kwa ajili ya ufalme wa mbinguni. Awezaye kupokea mafundisho haya na ayapokee.”13Kisha akaletewa baadhi ya watoto wadogo ili awawekee mikono juu yao na kuomba, lakini wanafunzi wake wakawakemea.14Bali Yesu akasema, “Waruhusu watoto wadogo, wala msiwakataze kuja kwangu, kwa maana ufalme wa mbinguni ni wa watu kama wao.15Naye akaweka mikono yake juu yao, na kisha akaondoka pale.16Tazama mtu mmoja akaja kwa Yesu na kusema, “Mwalimu, ni kitu gani kizuri ninachotakiwa kufanya ili nipate kuwa na uzima wa milele?”17Yesu akamwambia, “Kwa nini unaniuliza ni kitu gani kizuri? Kuna mmoja tu aliye mwema, lakini kama ukitaka kupata uzima, shika sheria za Mungu.”18Yule mtu akamwuliza, “Ni sheria zipi?” Yesu akasema, “Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo,19waheshimu baba yako na mama yako, na mpende jirani yako kama nafsi yako.”20Mtu yule akamwambia, “Mambo yote hayo nimeyatii. Bado ninahitaji nini?21“Yesu akamwambia, “Kama ukitaka kuwa mkamilifu, nenda, ukauze ulivyo navyo, na uwape maskini, na utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo unifuate.”22Lakini kijana yule aliposikia yale Yesu aliyomwambia, akaondoka kwa huzuni, kwa sababu alikuwa amemiliki mali nyingi.23Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kweli nawaambieni, ni vigumu kwa mtu tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni.24Tena nawaambieni, ni rahisi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko kwa mtu tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.”25Wanafunzi waliposikia hivyo, wakashangaa sana na kusema, “Ni yupi basi atakayeokoka?”26Yesu akawatazama na kusema, “Kwa wanadamu hilo haliwezekani, lakini kwa Mungu yote yanawezekana.”27Kisha Petro akamjibu na kumwambia, “Tazama, tumeacha vyote na kukufuata wewe. Ni kitu gani tutakachopata?”28Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, yeye aliyenifuata mimi, katika uzao mpya wakati Mwana wa Adam atakapoketi katika kiti cha enzi cha utukufu wake, ninyi pia mtaketi juu ya viti kumi na viwili vya enzi, kuwahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.29Kila mmoja wenu aliyeacha nyumba, kaka, dada, baba, mama, watoto, au shamba kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia na kuurithi uzima wa milele.30Lakini wengi walio wa kwanza sasa, watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwa wa kwanza.
Katika sura hii, Yesu anafundisha kuhusu talaka. Ilikuwa jibu la changamoto lililotolewa na Mafarisayo. Mafundisho yake Yesu yanategemea nia ya awali ya Mungu katika kuunda ndoa. Yesu anaonyesha makosa ambayo viongozi wa dini walifanya katika desturi zao kuhusu ndoa.
Huu ni mwanzo wa simulizi jipyaamabalo linanaishia 22:45, ambayo inaonesha Yesu akihudumia huko Yudea
Mistari hii inatoa historia ya jinsi Yesu alivyokuja Yudea
Habari inaeleza jinsi Yesu alivyositisha mafundisho yake kwenda tukio lililofuata
kile Yesu alichofundisha kuanzi 18:1
"alitembea kutoka" au "akatoka"
Yesu anaanza kufundisha juu ya ndoa na talaka
"walikuja kwa Yesu
kujaribu limetumika kwa maana hasi. "wakamkosoa kwa kumuuliza" au "walitaka kumkamata kwa kumuuliza"
Yesu anatumia swali kuwajibu Mafarisayo. "Kwa hakika mmesoma kwamba mwanzo Mungu aliwaumba watu,aliwaumba"mume na mke
Katika mstari wa 5, Yesu ananukuu kutoka Mwanzo kuonesha kuwa Mume na mke hawatakiwi kuachana
Huu ni mwandelezo wa swali ambal oYesu alilitumia kuwaliza Mafarisayo katika 19:3. Hii nukuu ya moja kwa moja inaweza kuelezwa kama nukuu isyo ya moja kwa moja. Kwa hakika mnajua kuwa Mungu alisema kuwa kwa sababu hii...mwili mmoja.
sababu ya mwanamume kumwacha baba na mama ni kwamba Mungu alimuumba mwanamke kuwa msaidizi wa mwanamume
"Kaa na mke wake"
"watakuwa kama mwili mmoja"
Kwahiyo mwanamume na mwanake siwawil tena bali mwili mmoja"
"Mafarisayo walimwambia Yesu"
"Amuru sisi Wayahudi"
Waraka unaohalalisha kisheria mwisho wa ndoa
kwa sababu ninyi ni wasumbufu
wewe na yenu ziko katika wingi. Yesu anaongea na Mafarisayo, lakini Musa aliwapa shaeria hii miaka mingi iliyopita kwa mababu zao. amri ya Musa ilitumika kwa Wayahudi wote.
"Wakati Mungu alipomuumba mume mke hakupanga waachane"
anaongeza msisitizo
na kumwoa mwanamke mwingine
Maandishi mengi ya mwanzo hayajumuishi maneno haya.
wale ambao Mungu amewaruhusu au ambao Mungu huwaruhusu
kwa kuwa kuna wanaume waliozaliwa kuwa matowashi
kuna matowashi waliofanywa kuwa matowashi
inawweza kumaanisha 1)wanaume waliojifanya wenyewe kwa kutoa sehehmu zao za siri 2) wanaume waliochagua kutokuoana ni wasafi katika swala la zinaa.
ualame wa mbinguni inamaanisha Mungu kutawala kama mfalme
Anayeweza kupokea mafundisho haya na ayapokee."
Yesu anawapokea na kuwabariki wat.oto wadogo
watu baadhi wakaleta watoto wadogo kwa Yesu
"Ruhusu"
Msiwazuie kwa kuja kwangu
Mungu kuwa mfalme kwa watu anaowatawla
ni wa watu kama watoto
Yesu anaongelea habariya mtu tajiri na jinsi iwezavyo kumgharimuamafuatapo Yesu
Mwandishi anamweka mtu mpya kwenye habari.Lugha yako inaweza kuwa na njia nyingine ya kufanya hivyo.
kitu kinachompendeza Mungu
usiniulize juu ya kitu kilicho kizuri
"Mungu pekee ndiye mwema aliyekamilka"
"ikupokea uzima wa milele"
Wayahudi waliamni kuwa majirani zao ni wayahudi tu. Yesu alipanua maana ya jirani il kujuisha watu wote.
"kama unataka"
kwa wale amabao ni masikini
Mungu atakuzawadia mbinguni
Yesuanawaeleza wanafunziwake zawadi ya kutokutafuta mali ya hapa duniani na uhusianao wa kumfuata yeye.
nawaambia ukeli. huunimsisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye
kumpokea Mungu wa mbinguni kama mfalme wetu.
Yesu anatumia mbalagha kusisitiza kuwa ni vigumu kwa tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.
Tobo katika mwisho wa sindano kwa kupitishia uzi
"wanafunzi wameshtushwa au kushangazwa." walishangazwa kwa sababu waliamini kuwa na utajiri ilikuwa ishara ya kukubarika kwa Mungu
Kwa hiyo hakuna ambayae Mungu atamwokoa" au "hakuna ambaye atapokea uzima wa milele
"tumeacha utajiri wetu wote" au "tumeacha miliki yetu yote"
"Kitu gani kizuri Mungu atakachotupa?"
msisistizo wa kile kinachofuatia
"wakatimpya" inamaanisha wakatiMungu akirudisha kila ktu" au "wakati ule ambao Mungu atafanya kila kitu kuwa kipya.
Yesuanaonge juuyake mwenyewe
Kukaa katika enzi kunamaanisha kutawala kama mfalme. enzi yake kuwa tukufu minawakilisha "utawala wake kuwa wa utukufu" au "kutawala kwa utukufu kama mfalme"
Hapa "enzi" inamaanisha kutawala kama mfalme. Wanafunzi hawatakuwa sawa na Yesu ambaye pia yuko kwenye enzi.. Watapokeamamlaka kutoka kwake."kukaa kama kwenye enzi 12"
Hapa "makabila" inamaanisha wtu kutoka kabila hizo
hapa "jina" linamaanisha nafasi nzima. "kwa sababu yangu" au " kwa sababu ananiamini mimi"
Kupokea kutoka kwa Mungu mara 100 na vitu vingine vizuri kama walivyoacha
Hii ni nahau inayomaanisha "Mungu atawabariki na uzima wa milele" au "Mungu atawafanya kuishi milele
Yesu analinganisha kizazi hiki na kile kijacho. Wale ambao ni wa muhimu sasa Mungu atawafanya kuwa si wa muhimu atakapoanzisha utawala wake hapa duniani. Wale wanaoonekana si wa muhimu leo Mungu atawafanya kuwa wa muhimu atakapoanzisha utawala wake.
Je ni halali kwa mtu kumwacha mke wake kwa sababu yoyote?
Yesu alisema kuwa tokea mwanzo wa kuumbwa, Mungu aliwaumba mume na mke.
Yesu alisema kuwa mume atawaacha babana mama yake na kushikamana na mke wake.
Yesu alisema kuwa, mume anaposhikamana na mke wake wale wawili huwa mwili mmoja.
Yesu alisema kuwa alichokiunganisha Mungu mtu asikitenganishe.
Ni kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao
Ni kwa sababu y a ugumu wa mioyo yao
Yesu alisemayeyote amwachaye mke wake isipokuwa kwa uzinzi, na kuoa mwanake mwingine huyo afanya uzinzi, na kwamba mwanamumeanyeoa mwanamke aliyeachwa afanya uzinzi.
Ni kwa wale walioruhusiwa na Mungu kuipokea hali hiyo.
Ni kwa wale walioruhusiwa na Munga kuipokea hali hiyo.
Wanafunzi wake waliwakemea
Yesu aliseamawaacheni watoto wadogo waje, kwa kuwa ufalme wa mbinguni ni wa watoto kama hawa.
Alimwambia ashike sheria za Mungu
Yesu alimwambia yule kijana kuzishika amri ili kuingia kwenye uzima wa milele
Nenda ukauze ulivyo navyo, na uwape maskini, na utakuwa na hazina mbinguni.
Nenda ukauze ulivyo navyo, na uwape masikini, na utakuwa na hazina mbinguni
Yule kijana aliondoka akiwa amehuzunika sana kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
Ni rahisi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko kwa mtu tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.
Yesu alisema kuwa kwa wanadamu hilo haliwezekani, lakini kwa Mungu yote yanawezekana.
Katika uzao mpya wakati Mwana wa Adamu atakapoketi katika kiti cha enzi, wanafunzi nao wataketi naye wakiyahukumu makabila kumi na mbili ya Israel.
Yesu alisema kwamba ambao ni wa kwanza sasa watakuwa wa mwisho na wale ambao ni wa mwisho sasa watakuwa wa kwanza.
1Kwa maana ufalme wa mbinguni unafanana na mmliki wa shamba, aliyeamka asubuhi na mapema ili kuajiri wafanyakazi katika shamba lake la mizabibu.2Baada ya kuwa amekubaliana na wafanyakazi dinari moja kwa kutwa, aliwatuma kwenda katika shamba lake la mizabibu.3Alienda tena baada ya masaa matatu hivi na aliona wafanyakazi wengine wakiwa wamesimama bila kazi katika eneo la soko.4Akawaambia, ‘Ninyi pia, nendeni katika shamba la mizabibu, na chochote kilicho halali nitawapa.’ Hivyo wakaenda kufanya kazi.5Akaenda tena baada ya masaa sita na tena katika saa ya tisa, na alifanya hivyo hivyo.6Mara nyingine tena mnamo saa kumi na moja, alienda na kuwakuta watu wengine wamesimama bila kazi. Aliwaambia, ‘kwa nini mmesimama hapa bila kazi yoyote kwa siku nzima?7Wakamwambia, kwasababu hakuna mtu yeyote aliyetuajiri. Akawaambia, ‘Nanyi pia nendeni katika shamba la mizabibu.’8Wakati wa jioni ulipofika, mwenye shamba la mizabibu alimwambia msimamizi wake, ‘Waite wafanyakazi na uwalipe mishahara, kwa kuanza na wa mwisho hadi wa kwanza.’9Walipokuja wale walioajiriwa saa kumi na moja, kila mmoja wao alipokea dinari.10Walipokuja wafanyakazi wa kwanza, walifikiri kuwa watapokea zaidi, lakini walipokea pia kila mmoja dinari moja kila mtu.11Baada ya kupokea malipo yao, walimlalamikia mmiliki wa shamba.12Wakasema, ‘Hawa wafanyakazi wa mwisho wametumia saa moja tu katika kufanya kazi, lakini umewalinganisha na sisi, sisi tumebeba mzigo kwa siku nzima na kuungua na joto.’13Lakini mwenye shamba akajibu na kusema kwa mmoja wao, ‘Rafiki, sikutenda jambo baya. Je! Hatukukubaliana na mimi kwa dinari moja?14Pokea kile kilicho halali yako na uende zako. Ni furaha yangu kuwapa hawa wafanyakazi walioajiriwa mwisho sawa sawa na wewe.15Je! Si haki kwangu kufanya kile ninachotaka na mali zangu? Au jicho lako ni ovu kwa sababu mimi ni mwema?16Hivyo wa mwisho atakuwa wa kwanza na wa kwanza atakuwa wa mwisho”17Yesu alipokuwa akipanda kwenda Yerusalem, aliwachukuwa wanafunzi wake kumi na mbili pembeni, na njiani akawaambia,18“Tazama tunaelekea Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atatiwa katika mikono ya wakuu wa makuhani na waandishi. Watamhukumu kifo19na watamtoa kwa watu wa mataifa ili kumdhihaki, kumchapa na kumsulubisha. Lakini katika siku ya tatu atafufuka.”20Kisha mama wa wana wa Zebedayo alikuja kwa Yesu na wana wake. Alipiga magoti mbele yake na kumwomba kitu kutoka kwake.21Yesu akamwambia, “Unataka nini?” Akamwambia, “Amuru kuwa hawa wanangu wawili wakae, mmoja mkono wako wa kulia na mmoja mkono wako wa kushoto katika ufalme wako.”22Lakini Yesu akajibu na kusema, “Haujui kile unachoomba. Je! Unaweza kukinywea kikombe ambacho nitakinywea?” Wakamwambia, “Tunaweza.”23Akawaambia, “Kikombe changu hakika mtakinywea. Lakini kukaa mkono wangu wa kulia na mkono wangu wa kushoto si jukumu langu kuwapa, lakini ni kwa wale ambao wamekwisha kuandaliwa na Baba yangu.”24Wanafunzi wengine kumi waliposikia hivyo, wakahuzunishwa sana na wale ndugu wawili.25Lakini Yesu aliwaita mwenyewe na kuwaambia, “Mnafahamu ya kuwa watawala wa mataifa huwatiisha, na wakuu wao hutekeleza mamlaka juu yao.26Lakini isiwe hivyo kwenu. Badala yake, yeyote atakayetaka kuwa mkubwa miongoni mwenu lazima awe mtumishi wenu.27Na atakaye kuwa wa kwanza miongoni mwenu lazima awe mtumishi wenu.28Kama vile Mwana wa Adamu hakuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa uhai wake kuwa ukombozi kwa wengi.”29Wakati wakitoka Yeriko, umati mkubwa ulimfuata.30Na waliwaona vipofu wawili wameketi kando ya barabara. Waliposikia kuwa Yesu alikuwa anapita, walipaza sauti na kusema, “Bwana, Mwana wa Daudi, utuhurumie.”31Lakini umati ukawakemea, na kuwaambia nyamazeni. Hata hivyo, wao wakapaza sauti zaidi na kusema, “Bwana, Mwana wa Daudi, utuhurumie.”32Kisha Yesu alisimama na aliwaita na kuwauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”33Wakamwambia, “Bwana kwamba macho yetu yafumbuliwe.”34Basi Yesu, akiwa amevutwa na huruma, akayagusa macho yao, mara hiyo, wakapokea uwezo wa kuona na wakamfuata.
Yesu anatumia mfano huu (Mathayo 20:1-16) ili kuwafundisha wanafunzi wake kwamba kanuni za Mungu kuhusu kile kilicho sawa ni tofauti na kanuni za binadamu.
Yesu anaelzea mfano wa mtu mmoja aliyekuwa anamiliki shamba anayeajiri wafanya kazi, ili kufafanua jinsi atakavyowalipa watu wa ualme wake.
Tazama 13:24
"baada ya mmiliki wa shamba kukubaliana"
"malipo ya kibarau ya siku moja"
aliwatuma kwenda kufanya kazi katika shamba lake
Yesu anaendela kuelza mfano
"Mmiliki wa shamba alienda tena"
saa ya tatu ni sawa na saa tatu asubuhi
"Wamesisma eneo la soko pasipo kufanya kazi yeyote"
Hili ni eneokubwa la wazi ambapowatu huuza na kununua chakula na bidhaa zingine.
Yesu anaendelea kusimulia mfano
"Mmiliki wa shamba akaenda tena"
saa ya sita ni sawa na sasa sita mchana. saa ya tisa ni sawa na saa tisa mchana
Hii inamaanisha yule mmilikiwashamba alienda sokono kuaajiri atu wengine
Hii ni sawa na saa kumi na moja mchana
"bila kufanya chochote" au "bila kuwa na kazi yote"
Yesu anaendelea kueleza mfano
Waweza kuzi kuyafanya maelezo h aya yaeleweke kwa uwazi. "Kwa kuanza na wafanyakazi niliowaajiri mwishoni, kisha lipa wafanyakazi niliowaajiri kwanza"
Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. "wale aliowaajiri mwenye shamba"
"malipo kibarua ya siku moja"
Yesu anaendelea kueleza mfano
"pindi wafanyakazi waliofanya kazi kwa muda mrefu walipopokea"
"mmiliki shamba" au "mwenye mizabibu"
"umewalipa kiasi kilekile cha fedha sawa na ulivyotulipa"
Kirai "tumebeba mzigo kwa siku nzima" ni nahau inayomaanisha kuwa "sisi ambao tumefanya kazi kwa siku nzima tukiungua na joto la jua"
Yesu anaendelea kueleza mfano
"mmoja wa wafanyakazi waliofanyakazi kwa muda mrefu
Tumia neno ambalo mtu moja angelitumia kumtambulisha mtu mwingine ambaye anamkemea kwa upole
Mmilki wa shamba anatumia swali kumkemea mfanykazi aliyekuwa akilalamika. "tumeshakubaliana kuwa nitakulipa dinari moja"
"malipo ya kibarua ya siku moja"
Yesu anahitimisha mfano wake juu ya mmiliki wa shamba aliyeajili wafanya kazi
Yule mmiliki wa shamba anatumia swali kuwanyamazi wafanyakazi waliokuwa wakilalamika. "Ninaweza kufanya chochote ninachotakajuuya mali yangu"
Yule mmiliki wa shanba anaatumia swali kuwanyamazisha wale wafanyakazi waliokuwa wakilalamika. "Msiwe na wivu kwa sababu ya ukarimu wangu kwa watu wengine
Yule mmiliki w a shamba anatumia swali kuwanyamazisha wafanyakazi waliokuwa wakilalamika. "Msione wivu kwa sababu ya ukarimu kwa watu wengine"
Tazama 19:29
Yesu anasema kwa kuhitimisha kwa mfano huu. "Ndipo Yesu aliposema. 'wa mwisho atakuwa wa kwanza'"
Yesu anatabiri juu ya kifo na ufufuo wake kwa mara ya tatu wakati akisafiri na wanafunzi wake
Yesu alikuwa juu ya mlima kwa hiyo watu walipanda kwenda pale.
Yesu anatumia neno "tazama" ili kuwajengea usikivu wanafunzi wake juu kile anachotaka kuwaambia.
Kiwakilishi "tu" kinamaanisha Yesu na wanafunzi wake.
Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji "mtu fulani atamtoa Mwana wa Adamu"
Yesu anaongea juu yake akitumia nafsi ya tatu. Kama inawezekana unaweza kutafsiri hii kwa kutumia nafsi ya kwanza
Makuhani wakuu na waandishi watamhukumu na kumtoa kwa watu wa mataifa, na watu wa mataifa watamdhihaki.
"kumchapa" au "kumpiga kwa mijeredi"
siku ya 3
Hi inaweza kuelezwa kwa mfumo tendaji. "Mungu atamfufua"
Akijibu swali ambalo Yesu aliulizwa na mama wa wale wanafunzi wawili, Yesu anafundisha wanafunzi wake juu ya mamlaka na kuwatumikia wengine katika ufalme wa mbinguni
Hii inamaanisha Yakobo na Yohana
Maana yake ni uwezo wa kuwa na nguvu, mamlaka, na heshima.
Hapa "ufalme inamaanisha utawala wa Yesu kama mfalme. "utakapokuwa mfalme"
Hapa "ham" iko katika wingi na inamaanisha mama na watoto
Hapa "mna" ni wingi, lakini Yesu anasema na wale wana wawili.
Hii ni nahau inayomaanisha kupita katika mateso. "kupitia mateso ambayo punde nitayapitia"
"wale wana wa Zebebdayo walimwambia" au "Yakobo na Yohana walisema"
Hii ni nahau kupitia dhiki. "kwa hakika mtateseka kama nitakavyoteseka
tazama 20:20
Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "Baba yangu amekwisha kuyaandaa hayo maeneo, na atawapatia wale anaowachagua.
Hiki ni cheo muhimu kwa ajili ya Mungu kinachoonesha mahusiano kati ya Yesu na Mungu.
"Waliposikia ambacho Yakobo na Yohana walimwuliza Yesu"
Kama inawezekana unaweza kukiweka wazi kilichowahuzunisha wale wanafunzi kumi. "Walikasirishwa sana na wale ndugu wawili kwa sababu kilammoja wao alitaka kuketi kwenye upande wa heshima karibu na Yesu.
Yesu anamalizia kufundisha juu ya mamlaka na kuwatumikia wengine
"aliwaita wale thenashara"
watawala wa mataifa hulazimisha watu wa mataifa kufanya kile watawala wanataka.
"watawala wa watu wa mataifa"
"huwatawalawatu"
"yeyote atakaye" au "yeyote atamaniye"
"kuwa wa muhimu"
Yesu anaonge juu yake mwenyewe kwa kutumia nafsi ya tatu. kama inawezekana unaweza kuitafsiri hii katika nafsi ya kwanza.
Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo tendaji. "Hakuja ili kwamba watu wengine wamtumikie" au "sikuja ili kwamba watu wengine wanitumikie"
"bali kuwatumikia watu wengiine"
Hii ni nahau. "kufa"
Neno "ukombozi" htumika kwa maana ya kuwafanya wengine kuwa huru kutoka gerezani au utumwani. Hii ni sitiari ya Yesu kuwaokoa watu kutoka kwenye hukumu ya adhbu ya Mungu kwa ajili y a dhanbi zao
"kwa ajili ya watu wengi"
Hii inaanza na habari ya Yesu akiwaponya vipofu wawili
Hii inaongelea wanafunzi na Yesu
"ulimfuata Yesu"
Wakati mwingine jambo hili limetafsiriwa kama "Tazama kulikuwa na wanaume wawili weameketi." Mwandishi anatambulisha watu wawili kwenye hii habari. Lugha yako inaweza kuwa na namna ya kulifanya jambo hili.
"wale vipofu wawili waliposikia"
wakati mwingine hutafsiriwa , "Tazama" Mwandishi anamwambia msomaji kuwa makini kwa maelezo ya kushangaza yanayofuata. Lugha yako inaweza ikawa na njia fulani ya kufanya hivi.
Alikuwa akitembea kati yao
Yesu hakuwa mwana halisi wa Daudi, Kwa hiyoinaweza kutafsiriwa kama "kizazi cha mfalme wa Daudi." Hata hivyo "mwana wa Daudi " ni cheo cha Masihi, na huenda wale wanaume walikuwa wakimwita Yesu kwa cheo hiki.
Aliwaita vipofu
"je! mnataka"
Kirai cha "macho yetu yafumbuliwe" ni nahau inayomaanisha kuweza kuona tena. "tunataka utufanye kuona" au "tunataka uwezo wa kuona"
"kuwa na hurma" au "kusukumwa na huruma kwa ajili yao"
Dinari moja kwa kutwa
Dinari moja kwa kutwa
Atawalipa chochote kilicho halali
Dinari moja
Walilalamika kuwa wao walikuwa wamefanya kazi kwa siku nzima, lakini wamepokea kiasi sawa na wale waliofanya kazi kwa saa moja.
Walilalamika kuwa wao walikuwa wamefanya kazi kwa siku nzima, Lakini wa,epokes kiasi sawa na wale waliofanya kazi kwa saa moja.
Mwenye shamba aliwaambia kuwa hajawakosea chochote wafanyakazi na amewalipa kile walichostahili.
Mwenye shamba aliwaambia kuwa hajawakosea chochote wafanya kazi na amewalipa kile waliochostahili.
Yesu aliwaambia wanafunzi wake kuwa atatolewa kwa makuhani wakuu na waandishi, na kuhukumiwa kifo, atasulibiwa, na siku ya tatu atafufuka.
Yesu aliwaambia wanafunzi wake kuwa atatolewa kwa makuhani wakuu na waandishi, na kuhukumiwa kifo, atasulibiwa na siku ya tatu atafufuka.
Alimtaka Yesu aamuru kuwa watoto wake wawili wakae, mmoja mkono wake wa kushoto na mmoja mkono wake wa kuume.
Alimtaka Yesu aamuru kuwa watoto wake wawili wakae mmoja mkono wake wa kushoto na mmoja mko wake wa kuume
Yesu alisema kuwa Baba ameyaandaa maeneo hayo kwa ajili y a wale aliowachagua.
Yesu aliseam kuwa anayetaka kuwa mkuu lazima awe mtumwa.
Yesu alisema kuwa alikuja kutumika na kuyatoa maisha yake kuwa ukombozi kwa wengi.
Wale vipofu wawili walipiga kelele, "Bwana, Mwana wa Daudi, uturehemu."
Yesu aliwaponya wale vipofu wawili kwa sababu aliwaonea huruma.
1Yesu na wanafunzi wake wakafika karibu na Jerusalemu na wakaenda mpaka Bethania, katika mlima mizeituni, kisha Yesu akawatuma wanafunzi wawili,2akiwaambia, “Nendeni katika kijiji kinachofuata, na mara moja mtamkuta punda amefungwa pale, na mwanapunda pamoja naye. Wafungueni na kuwaleta kwangu.3Ikiwa mtu yeyote akiwaambia chochote kuhusu hilo, mtasema, ‘Bwana anawahitaji,’ na mtu huyo mara moja atawaruhusu mje pamoja nao.”4Jambo hili lilitokea ni lile lililosemwa kupitia kwa nabii lazima litimizwe. Akawaambia,5‘Waambie binti Sayuni, tazama, mfalme wako anakuja kwenu, mnyenyekevu na akiwa amempanda punda, na mwana punda mme.’6Kisha wanafunzi waliondoka na kufanya kama Yesu alivyowaagiza.7Wakamleta punda na mwanapunda, na kuweka nguo zao juu yao, naye Yesu akakaa pale.8Wengi katika mkusanyiko walitandaza nguo zao njiani, na wengine walikata matawi kutoka kwenye miti na kutandaza barabarani.9Umati uliomtangulia Yesu na wale waliomfuata walipaza sauti, wakisema, “Hosana kwa mwana wa Daudi! Ni mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana. Hosana juu zaidi!”10Yesu alipofika Yerusalemu, mji mzima ulishtuka na kusema, “Huyu ni nani?11“Umati ulijibu, “Huyu ni Yesu Nabii, kutoka Nazareti ya Galilaya.”12Kisha Yesu akaingia katika hekalu la Mungu. Akawafukuza nje wote waliokuwa wakinunua na kuuza hekaluni. Pia alipindua meza za wabadilishaji wa fedha na viti vya wauza njiwa.13Akawaambia, “Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya maombi,’ lakini ninyi mmeifanya pango la wanyang'anyi.”14Kisha vipofu na vilema wakamjia hekaluni, naye akawaponya.15Lakini wakati wakuu wa makuhani na waandishi walipoona maajabu aliyoyatenda, na waliposikia watoto wakipiga kelele hekaluni na kusema, “Hosana kwa Mwana wa Daudi,” walishikwa na hasira.16Wakamwambia, “Umesikia kile kinachosemwa na hawa watu?” Yesu akawaambia, “Ndiyo! Lakini hamjawahi kusoma, ‘Kutoka kwa midomo ya watoto na watoto wachanga wanyonyao mna sifa kamili?”17Kisha Yesu akawaacha na kwenda nje ya mji katika Bethania na kulala huko.18Asubuhi alipokuwa anarudi mjini, alikuwa na njaa.19Aliona mtini kandokando ya barabara. Akauendea, lakini hakupata kitu juu yake isipokuwa majani. Aliuambia, “Kusiwe na matunda kwako daima tena.” Na mara hiyo mtini ule ukanyauka.20Wanafunzi walipoona, wakastaajabu na kusema, “Imekuwaje mtini umenyauka mara moja?”21Yesu akajibu na kuwaambia, “Kweli nawaambieni, kama mkiwa na imani na bila wasiwasi, hamtafanya kile kilichofanyika kwa huo mtini tu, lakini mtauambia hata huo mlima, ‘Uchukuliwe na ukatupwe baharini,’ na itafanyika.22Chochote mtakachoomba kwa sala, huku mkiamini, mtapokea.”23Yesu alipofika hekaluni, wakuu wa makuhani na wazee wa watu wakamjia wakati alipokuwa akifundisha na kumwuliza, “Ni kwa mamlaka gani unafanya mambo haya? Na ni nani aliyekupa mamlaka haya?”24Yesu akajibu na kuwaambia, “Nami tena nitawauliza swali moja. Kama mkiniambia, nami vile vile nitawaambia ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.25Ubatizo wa Yohana- ulitoka wapi, mbinguni au kwa wanadamu?” Wakahojiana wenyewe, wakisema, “Tukisema, ulitoka mbinguni, atatuambia, ‘Kwa nini hamkumwamini?’26Lakini tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu,’ tunawaogopa makutano, kwa sababu wote wanamwona Yohana kama nabii.”27Kisha wakamjibu Yesu na kusema, “Hatujui” Akawaambia pia, “Wala mimi sitawaambia ni kwa mamlaka gani nafanya mambo haya.28Lakini mnafikiri nini? Mtu mwenye wana wawili. Akaenda kwa moja na kumwambia, ‘Mwanangu, nenda ukafanye kazi katika shamba la mizabibu29leo.’ ‘Mwana akajibu na kusema, ‘sitakwenda.’ Lakini baadaye akabadilisha mawazo yake na akaenda.30Na mtu yule akaenda kwa mwana wa pili na kusema kitu kile kile. Mwana huyu akajibu na kusema, ‘Nitakwenda, bwana.’ Lakini hakwenda.31Yupi kati ya wana wawili aliyefanya matakwa ya baba yake? Wakasema, “Mwana wa kwanza.” Yesu akawaambia, “Kweli nawaambieni, wakusanya ushuru na makahaba wataingia kwenye ufalme wa Mungu kabla yenu kuingia.32Kwa maana Yohana alikuja kwenu kwa njia iliyo nyoofu, lakini hamkumwamini, wakati wakusanya ushuru na makahaba walimwamini. Na ninyi, mlipoona hilo likitendeka, hamkuweza kutubu ili baadaye mumwamini.33Sikilizeni mfano mwingine. Kulikuwa na mtu mwenye eneo kubwa la ardhi. Alipanda mizabibu, akaiwekea uzio, akatengeneza na chombo cha kukamulia divai, akajenga na mnara wa walinzi, na akalikodisha kwa watunza zabibu. Kisha akaenda katika nchi nyingine.34Wakati wa mavuno ya mizabibu ulipokaribia, aliwatuma baadhi ya watumishi kwa wakulima wa mizabibu kuchukua mizabibu yake.35Lakini wakulima wa zabibu wakawachukua watumishi wake, wakampiga mmoja, wakamwua mwingine, na wakampiga mmoja kwa mawe.36Kwa mara nyingine, mmiliki aliwatuma watumishi wengine, wengi zaidi ya wale wa kwanza, lakini wakulima wa mizabibu waliwatendea vile vile.37Baada ya hapo bwana yule akamtuma kwao mwana wake, akisema, ‘Watamheshimu mwanangu.’38Lakini wakulima wa mizabibu walipomwona kijana yule, wakaambiana, ‘Huyu ni mrithi. Njooni tumuue na tumiliki urithi.’39Hivyo wakamchukua, wakamtupa nje ya shamba la mizabibu na kumwua.40Je mmliki wa shamba la mizabibu atakapokuja, atawafanya nini wakulima wa mizabibu?”41Wakamwambia, “Atawaharibu hao watu waovu katika njia ya ukali zaidi, na kisha atalikodisha shamba la mizabibu kwa wakulima wengine wa mizabibu, watu ambao watalipa kwa ajili ya mizabibu itakapoiva.”42Yesu akawaambia, “Hamkusoma katika maandiko, ‘Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la msingi. Hili lilitoka kwa Bwana, na inashangaza machoni petu?’43Hivyo nawaambieni, Ufalme wa Mungu utatwaliwa kutoka kwenu na kupewa taifa linalojali matunda yake.44Yeyote atakayeanguka juu ya jiwe hilo atavunjwa vipandevipande. Lakini kwa yeyote litakayemwangukia, litamsaga.”45Wakuu wa makuhani na mafarisayo waliposikia mifano yake, wakaona kuwa anawazungumzia wao.46Lakini kila walipotaka kunyosha mikono juu yake, waliogopa makutano, kwa sababu watu walimtazama kama nabii.
Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka kando kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari yote ya 21:5,16 na 42, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.
Hili ndilo neno ambalo watu walisema wakipiga kelele walipomkaribisha Yesu huko Yerusalemu. Ilikuwa ni tamko la sifa, ingawa pia ilikuwa neno la Kiebrania linalomaanisha, "Tuokoe!"
Wasomi wametofautiana kuhusu maana ya maneno haya. Swali muhimu ni hili: Je, tukio hili itakuwa la kudumu au la muda? Ikiwezekana, uziache wezekano zote mbili kuwa wazi katika tafsiri yako.
Hii inaanzisha habari ya Yesu akiingia Yerusalemu. Yesu anawapa maalekezo ya kile wanachopaswa kufanya.
Hikini kijiji kilichoko karibu na Yerusalemu
"mwanapunda ambaye amefungwa na mtu"
"amefungwa kwenye nguzo" au "amefungwa kwenye mti.
Hapa mwandishi anamnukuu nabii Zecharia kuonesha kuwa Yesu anataimiza unabii kwa kumpanda mwanapunda kuelekea Yerusalemu.
Hili neno limetumika hapa kuonesha mwanzo wa habari mpya. Hapa Mathayo anafafanua jinsi matendo ya Yesu yanatimiza maandiko
Jambo hili linaweza kutafsiriwa katika mfumo tendaji. "Hili lilitokea ili Yesu atimize kile alichosema Mungu kupitia manabii tangu zamani za kale"
"kupitia kwa nabii Zekaria"
Binti wa mji inamaanisha watu wa ule mji. "watu wa mji ule" au"watu waishio Sayuni"
Hili ni jina jingiine la Yerusalemu
Neno mwanapunda na mwanapunda mchanga inamaanisha mnyama yuleyule, haimaanishi wanyama wawili tofauti
dume changa la punda
Makutano wakatandaka mavazi yao chini, na wengine wakakata matawi ya miti wakayatandika barabarani
Neno la Kiebrania linalomaanisha "Tuokoe" lakini pia linaweza kumaanisha "Kumsifu Mungu!"
Yesu hakuwa mwana halisi wa Daudi, kwa hiyo hii inaweza kutafsiriwa kama "kizazi cha mfalme Daudi. Lakini pia, "Mwana wa Daudi" ni cheo cha Masihi, Huenda makutano walikuwa wakimwita Yesu kwa cheo hiki.
Hapa "kwa jina la Bwana" inamaanisha "kwa nguvu ya Bwana" au "kama mwakilish wa Bwana"
Neno "juu zaidi" linamaanisha Mungu atawalaye kutoka juu mbinguni. "Mungu asifiwe, ambaye yuko juu mbinguni" au "Sifa kwake Mungu"
Neno "mji" linamaanisha wakazi wa mji huo. "Watu wengi mjini kote walitaharuki"
Hii inaanzisha habari ya Yesu alipoingia Hekaluni
Katika msari wa 13, Yesu anamnukuu nabii Isaya kuwakememea wachuuzina wabadilishaji wa fedha.
Yesu hakuliingia lile hekalu halisi. Aliingia kwenye lile korido la hekalu
Wachhuzi waliokuwa wakiuza wanyama na bidhaa ziingine ambavyo wasafiri walinunua ili wapate sadaka halisi ya kutoa hekeluni.
"Yesu aliwaambia wale waliokuwa wanabadilisha fedha na kununua na kuuza vitu"
Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. "Nabii aliandika zamani za kale" au "Mungu alishasema tangu zamani
"Nyumba yangu itaitwa"
Kiwakilishi "yangu" kinamaanisha Mungu "Nyumba" inamaanisha hekalu
"mahali ambapo watu wataomba
Yesu anatumia sitiari kuwakemea watu wanouza na kununua bidhaa hekaluni. "Kama mahali ambapo wanyang'nyi hujificha"
wale waliokuwa vipofu na vilema"
kuwa na mguu ulioumia ambao unaosababisha kutembea kwa tabu"
Katika mstari wa 16,Yesu anatumia nukuu toka Zaburi kuthibitisha jinsi watu walivyokuwa wamemwitikia
"vitu vya kushangaza" au "miujiza." Hii inamaanisha Yesu alivyowaponya vipofu na vilema kati ka 21:12
Tazama 21:9
Tazama 21:9
Inamaanisha kuwa walishikwa na hasira kwa sababu hawakuamini kuwa Yesu ndiyo Kristo na hawakutaka watu wamsifu. "Walikasirika sana kwa sababu watu walikuwa wanamsifu"
Wakuu wa Makuhani na waandishi wanauliza swali hili kumkemea Yesu kwa sababu wanamchukia, "Usiwaruhusu watu kusema mambo haya juu yako"
Yesu anauliza swali hili kuwakumbusha wakuu wa makuhani na waandishi kile walichosoma kwenye maandiko. "Naam, nawasikia, lakini inawapasa mkumbuke mlichokisoma katika maandiko ... sifa"
"Ndiyo nimewasikia lakini mnatakiwa kukumbuka mlichokisoma katika maandiko matakatifu...sifu'."
Kirai hiki "kutoka kwenye midomo" kinamaanisha kuongea. "uliwafanya watoto na watoto wachanga kusema sifa kamili"
"Yesu aliwaacha makuhani wakuu na waandishi"
Yesu anatumia mtini kuwafundisha wanafunzi juu ya imani na maombi
Hili neno limetumika kuonesha mwanzo wa habari mpya. Mathayo anaeleza kuwa Yesu alikuwa na njaa na ndiyo sababu anasimama kwenye ule mtini.
"ukafa"
Wanafunzi wanatumia swali kuonesha mshangao wao. "Tumeduwaa kuona kuwa ule mtiini umenyauka haraka!"
"Nawaambia ukweli." Kirai hiki kinaonggeza msisitizo wa kile Yesu anachosema baadaye.
kama mtaamini kwa ukweli
"kukauka na kufa"
mtaweza kuumbia mlima huu kuondoka na kutupwa baharini"
itatokea
Hii inaanzisha habari ya viongozi wa dini wakimhoji Yesu
Inamaanisha kuwa Yesu hakuingia hekaluni ndani. Aliingia kwenye korido la hekalu
Hii inamaanisha mafundisho na uponyaji wa Yesu mle hekaluni. Pia inaweza kumaanisha tukio lililofanyika siku moja kabla la Yesu kuwafukuza wanunuzi na wachuuzi.
Yesu anaendelea kuwajibu viongozi wa dini
"alipata mamlaka toka wapi?"
"kama tukisema kuwa tunaamini kuwa Yohana alipokea mamlaka toka mbinguni, Yesu atatuuliza kuwa kwa nini hatukumwamini Yohana"
"mbinguni" inamaanisha Mungu."Kutoka kwa Mungu mbinguni"
Basi mngekuwa mmemwamini Yohana Mbatizaji"
"lakini kama tukisema kuwa tunaamini kuwa Yohana alipokea mamlaka kutoka kwa watu"
tunaogopa kile makutano watakachotufikiria au kile watakachotufanyia"
"Wanaamini kuwaYohana ni nabii"
Yesu anatumia mfano wa wana wawili kuwakemea viongozi wa dini na kufafanua kutokuamini kwao
Yesu anatumia swali ili kuwafanya viongozi wa dini wafikirie zaidi juu ya mfano aliotaka kuwaambia. "Niambieni mnafikiri nini juu ya kile ninachotaka kuwaambia"
Hii inamlenga yule mwana akifikiri kana kwamba alikuwa na fikra zaidi ili achague
"Makuhani wakuu na wazee walisema"
Yesu aliwaambia wakuu wa makuhani na wazee"
"Nawaambia ukweli." Kirai hiki kinaongeza msisitizo wa kile ambacho Yesu atasema baadaye
Neno "ufalme wa Mungu" linamaanisha utawala wa Mungu kama Mfalme. "Mungu atakaposimamisha utawalawake duniani, atawabariki watoza ushuru na makahaba kwa kuwatawala kabla ya kufanya hivyo kwenu"
Yaweza 1)Yesu atawapokea watoza ushuru na makahaba kabla ya kuwapokea viongozi wa dini 2) Mungu atawapokea watoza ushuru na makahaba badala ya kuwapokea viongozi wa dini wa Kiyahudi
Kiwakilishi cha "ninyi" ni cha wingi na kinamaanisha watu wote wa Israel na wala si viongozi wadini tu. "Yohana alikuja kwa watu wa Israel"
Hii ni nahau inayomaanisha kuwa Yohana aliwaonesha watu njia sahihi ya maisha. "na aliwaambia njia sahihi ambayo Mungu anataka ninyi muishi"
kiwakilishi cha"hamku.." ni cha wingi. nacho kinamaanisha viongoziwa dini.
Kuwakemea viongoziwa dini na kufafanua kutokuamini kwao, Yesu anaeleza mfano wa watumishi wapinzani.
"mtu anayemiliki sehemu ya mali"
"ukuta" au "kizuizi"
"alichimba shimo la kukamulia zabibu"
"kuwaweka wakulima wa mizabibu kuwa wasimamizi wa shamba la mizabibu" Mwenye shamba bado ni mmliki wa shamba.
watu waliojua jinsi ya kutunza mizabibu na divai
Yesu anaendelea kuelezea mfano
Watumwa wa "Mtu mwenye shamba kubwa"
Yesu anaendelea kuelezea mfano.
Neno "sasa" halimaanisha "wakati huu," bali limetumika kuvuta usikivu kwa ajili ya fundisho linalofuata.
"Watu wakamwambia Yesu"
Yesu anaanza kuelezea mafano wa watumishi wapinazani
Yesu anamnukuu nabii Isaya kuonesha kwamba Mungu atamheshimu yule ambaye viongozi wa dini wanamkataa.
Tazama 21:40
"Fikiria juu ya kile ambacho mmesoma ... macho"
Yesu ananukuu kutoka Zaburi. Hii ni sitiari inamaanisha viongozi wa dini, kama wajenzi, watamkataa Yesu, lakini Mungu atamfanya kuwa wa muhinmu katika ufalme wake, kama jiwe kuu la pembeni katika ujenzi.
"limekuwa jiwe kuu la pembeni"
"Bwana ndiye aliyefanya haya mabadiliko
Kirai cha "machoni petu" kinamaanisha kuona. "ni maajabu kuona"
Hii inaongeza msisitizo juu ya kile ambacho Yesu anasema baadaye
Kiwakilishi cha wa... ni cha wingi. Yesu alikuwa anaongea na viongozi wa dini na Wayahudi pia katika ujumla wao.
Neno "ufalme wa Mungu" inamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. "Mungu atawakataa, Wayahudi, na atakuwa mfalme wa watu toka mataifa mengine watakaozaa matunda"
Hii ni nahau inayomaanisha utii. "wale wanaotii amri za Mungu"
Neno "jiwe hili" nijiwe sawa na lile la 21:42. Hii ni sitiari inayomaanisha kuwa Kristo atamharibu mtu yeyote anayempinga. "Jiwe litamvunjavunja yeyote anayeanguka juu yake"
Hiki ni krai kinachoonesha kuwa Kristo ndiye atakuwa hakimu wa mwisho na atamharibu kila mtu atakayempinga.
Viongozi wa dini wanamwinukia Yesu juu ya mfano ambao Yesu alifundisha
Mifano ya Yesu
Yesu aliseama watamwona punda amefunwa, na mwanapunda pamoja naye.
Nabii alitabri kuwa mfalme anawaijieni, akiwa amempanda punda na mwanapunda.
Nabii alikuwa ametabiri kuwa Mfalme anawaijieni, akiwa amempanda punda na mwanapunda.
Makutano walitandika mavazi yao juu yake na waliweka matawi ya miti njiani
walisema Hosana kwa mwana wa Daudi! Ni mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana. Hosana juu!!
Aliwavurumisha nje wote waliokuwa wakinunua na kuuza hekaluni. Pia alipindua meza za wabadilisha fedha na viti vya wauza njiwa.
Yesu aliwaambia, "Ndiyo!" Hajasoma ilivyoaandikwa kuwa katika midomo ya watoto kuna sifa kamili?
Aliulaani mtini, ukakauka, kwasababu haukuwa na matunda.
Kweli nawaambieni kama mkiwa na imanin na hamna wasiwasi yoyote, hamtafanya kile kilichofanyika kwa huo mtini tu, lakini mtasema hata kwa huo mlima, uchukuliwe na utupwe bahrini, na itafanyika hivyo.
walimuuliza juu ya mamlaka gani alikuwa anayafanya hayo?
Ubatizo wa Yohana ulitoka wapi? mbinguni au kwa wanadamu?
Yule wa kwanza alisema hataweza kufka, lakini baadaye akaenda.
Yule mtoto wa kwanza alisema hataenda lakini baadaye akaenda
Yule mtoto wa pili alisema atakwenda, halafu hakwenda.
Mtoto wa kwanza
Ni kwasababu watoza ushuru na makahaba walimwamini Yohana, lakini Wakuu wa Makuhani na waandishi hawakumwamini Yohana.
Waliwachukua wake, wakawapiga, na kuwaua.
Wakulima wa mizabibu walimwua mtoto wa mwenye shamba.
wakulima wa mizabibu walimwua mtoto wa mwenye shamba.
Watu walisema kuwa mmiliki anapaswa kuwaangamiza wale wakulima wa kwanza wa mizabibu na kulipangasha shamba kwa wakulima wengine
Watu walisema kuwa mmiliki anapaswa kuwaangamiza wale wakulima wa kwanza wa mizabibu na kulipangasha shamba kwa wakulima wengine
Jiwe lililokataliwa na waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni/msingi
Ufalme wa Mungu utatwaliwa kutoka kwa wakuu wa Makuhani na Mafarisayo na wapea taifa linalojali matunda yake.
Waliwaogopa makutano, kwa sababu makutano walimwona Yesu kuwa ni nabii.
1Yesu alisema nao tena katika mifano, akisema,2“Ufalme wa mbinguni unafanana na mfalme aliyeandaa sherehe ya harusi ya mwanawe.3Akawatuma watumishi wake kuwakaribisha waliokuwa wamealikwa kuja katika sherehe ya harusi, lakini hawakufika.4Mfalme aliwatuma tena watumishi wengine, akisema. “Waambieni wote walioalikwa, ‘Angalieni, nimeandaa chakula. Fahali na ndama wangu wanono wamechinjwa, na mambo yote yako tayari. Njoni katika sherehe ya harusi.”5Lakini watu hao hawakuzingatia kwa dhati mwaliko wake. Baadhi walirejea katika mashamba yao, na wengine walirudi katika sehemu zao za biashara.6Wengine waliwainukia watumishi wa mfalme na kuwadhalilisha na kuwaua.7Lakini mfalme alikasirika. Alituma jeshi lake, akawaua wale wauaji na kuuteketeza mji wao kwa moto.8Kisha aliwaambia watumishi wake, ‘Harusi iko tayari, lakini walioalikwa hawakustahili.9Kwa hiyo nendeni kwenye makutano ya njia kuu, waalikeni watu wengi kadri iwezekanavyo waje kwenye sherehe ya harusi.’10Watumishi walienda njia kuu na kuwakaribisha watu wowote waliowaona, wema na wabaya. Hivyo ukumbi wa harusi ulijaa wageni.11Lakini mfalme alipoingia kuwatazama wageni, alimuona mtu mmoja ambaye hakuvaa vazi rasmi la harusi!12Mfalme alimwuliza, ‘Rafiki, ulipataje kufika hapa ndani bila vazi la harusi?’ Na mtu huyo hakujibu chochote.13Ndipo mfalme alipowaambia watumishi wake, ‘Mfungeni mtu huyu mikono na miguu na mtupeni nje katika giza, huko ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.14Kwa kuwa watu wengi wanaitwa, lakini wateule ni wachache.’”15Ndipo Mafarisayo waliondoka na kupanga jinsi ya kumkamata Yesu katika maneno yake mwenyewe.16Ndipo walipowatuma wanafunzi wao pamoja na Maherode. Na walimwambia Yesu, “Mwalimu, tunajua kuwa wewe ni mtu wa kweli, na kwamba unafundisha matakwa ya Mungu katika ukweli. Haujali maoni ya mtu mwingine na hauoneshi upendeleo kwa watu.17Kwa hiyo tuambie, unafikiri nini? Je, ni sahihi kisheria kulipa kodi kwa Kaisari au hapana?”18Yesu alifahamu uovu wao na akasema, “Kwa nini mnanijaribu, enyi wanafiki?19Nionesheni pesa itumikayo kulipia kodi.” Ndipo wakamletea dinari.20Yesu akawauliza, “Sura na jina hili ni vya nani?”21Wakamjibu, “Vya Kaisari.” Ndipo Yesu akawaambia, “Mpeni Kaisari vitu vilivyo vyake na vya Mungu mpeni Mungu.”22Waliposikia hivyo walishangaa. Kisha walimwacha na kwenda zao.23Siku hiyo baadhi ya Masadukayo walikuja kwa Yesu, wale wasemao kuwa hakuna ufufuo wa wafu. Wakamwuliza,24wakisema, “Mwalimu, Musa alisema, ikiwa mtu amefariki bila kuzaa watoto, ndugu yake na amrithi huyo mwanamke na ampatie mtoto kwa ajili ya ndugu yake.25Walikuwapo ndugu saba. Wa kwanza alioa na kisha akafariki bila kuzaa watoto. Akamwachia mke nduguye.26Kisha ndugu yake wa pili naye akafanya vivyo hivyo, kisha yule wa tatu, ikawa hivyo hadi kwa yule wa saba.27Baada ya kufanya hivyo wote, yule mwanamke naye alifariki.28Sasa katika ufufuo huyo mwanamke atakuwa mke wa nani katika ndugu hao saba? Kwa sababu wote walimuoa.”29Lakina Yesu aliwajibu na kuwaambia, “Mnakosea, kwa sababu hamjui Maandiko wala nguvu za Mungu.30Kwa kuwa katika ufufuo, watu hawaoi wala kuolewa. Badala yake watu huwa kama malaika huko mbinguni.31Lakini kuhusu ufufuo wa walio kufa, hamjawahi kusoma kile ambacho Mungu alikisema kwenu, akisema,32“Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? Mungu si Mungu wa waliokufa, bali ni Mungu wa walio hai.”33Wakati umati waliposikia hili, waliyashangaa mafundisho yake.34Lakini Mafarisayo waliposikia kuwa Yesu amewanyamazisha Masadukayo, walijikusanya wao wenyewe kwa pamoja.35Mmoja wao, akiwa mwana sheria, alimwuliza swali kwa kumjaribu.36“Mwalimu, ni amri ipi iliyo kuu kuliko zote katika sheria?”37Yesu akamjibu, “Lazima umpende Bwana kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.38Hii ndiyo amri iliyo kuu na ya kwanza.39Na ya pili inafanana na hiyo. Ni lazima kumpenda jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.40Sheria zote na Manabii hutegemea amri hizi mbili.”41Na Mafarisayo walipokuwa bado wamejikusanya pamoja, Yesu aliwauliza swali.42Akisema, “Je, mwafikiri nini juu ya Kristo? Yeye ni Mwana wa nani?” Nao wakamjibu, “Ni mwana wa Daudi.”43Yesu akawajibu, “Ni kwa namna gani Daudi katika Roho anamwita Bwana, akisema,44‘Bwana alimwambia Bwana wangu, ‘Kaa mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowafanya maadui zako wawekwe chini ya miguu yako.”45Kama Daudi anamwita Kristo ‘Bwana,’ jinsi gani atakuwa mtoto wake?”46Hakuna aliyeweza kumjibu neno tena, na hakuna aliyethubutu tena kumwuliza maswali zaidi tangu siku hiyo na kuendelea.
Some translations set poetry farther to the right than the rest of the text to show that it is poetry. The ULB does this with the poetry in verse 44, which is from the Old Testament.
In the parable of the wedding feast (Matthew 22:1-14), Jesus taught that when God offers to save a person, that person needs to accept the offer. Jesus spoke of life with God as a feast that a king prepares for his son, who has just gotten married. In addition, Jesus emphasized that not everyone whom God invites will properly prepare themselves to come to the feast. God will throw these people out from the feast.
Kama waandishi wengine wa Injili, Mathayo anadhani kwamba wasomaji wake wataelewa hali nyingi ambazo anawasilisha, kwa hiyo hatoi maelezo mengi. Anasema, kwa mfano, katika Mathayo 22:15-22, kwamba Wafarisayo walijaribu kumdanganya Yesu ili aseme mambo mabaya, lakini anadhani kwamba wasomaji wataelewa kwa nini swali lao kwa Yesu lilikuwa la hatari kujibu (Mathayo 22:16) ). Walitarajia kwamba Yesu katika jibu lake angewakasirisha Wayahudi au mamlaka ya Kirumi.
Kitendawili ni taarifa inayoonekana kuwa ya ajabu, ambayo ni kana kwamba inajikana yenyewe, lakini kwa hakika sio ya ajabu. Katika sura hii, Yesu ananukuu Zaburi ambapo Daudi anamwita mwanawe "bwana," yaani, mkuu. Wayahudi daima walitarajia kwamba mababu wangekuwa wakubwa kuliko wazao wao. Katika kifungu hiki, Yesu anajaribu kuwaongoza wasikilizaji hatua kwa hatua kuelewa ukweli kwamba Masihi mwenyewe atakuwa Mungu, na kwamba yeye, Yesu, kwa hakika ndiye Masihi. (Mathayo 22:43-44)
Kuwakemea viongozi wa dini na kuonesha kutokuamini kwao, Yesuanafundisha mfano wa sherehe ya harusi
"watu"
Tazama 13:24
"Watu ambao mfalme alikuwa amewaalika."
Yesuanaendelea kuelezea mfano
akawaamuru, watumishi wawaambie wale aliowaalika.
"Angalia" au "Sikiliza" au "Kuwa msikivu kwa kile ninachotaka kukuambia."
Inamaanisha kuwa wale wanyama wameshapikwa na wako tayari kwa kuliwa. "Watumishi wangu wamechinja na wamewapika mafahali na ndama wangu wanono"
"Mafahali wangu na ndama wangu walio wazuri kwa kula"
Yesu anaendelea kuelezea mfano
"Lakini wale wageni walioalikwa na mfalme walipuuzia"
Inamaanisha kuwa, askari wa mafalme waliawaua wale wauaji.
Yesu anaendelea kuelezea mfano
"Wale ambao nimewaalika"
"Mahali ambapo barabara hukutana." mfalme anawatuma watumishi kwenye maeneo ambayo wana uhakika mkubwa wa kupata watu.
"watu wabaya na watu wema"
"kwa hivyo wageni waliujaza ukumbi wa harusi"
chumba kikubwa
Yesu anaendelea kuelezea mfano
"haujavaa vazi rasmi kwa ajili ya harusi. haupaswi kuwa hapa"
"yule mtu alikuwa kimya"
Yesu anahitimisha mfano wa harusi
"mfungeni kiasi kwamba hawezi kusogeza mikono na miguu"
Tazama 8:11
Tazama 8:11
"Kwa kuwa Mungu huwakaribisha watu wengi, lakini huchagua wachache"
Neno hili linamaaisha mpito. Yesu anamaliza mfano na sasa ataeleza maana ya mfano
Hii inaanzisha habari ya viongozi wa dini wakipanga jinsi ya kumkamata Yesu kwa kutumia maswali mengi magumu. Hapa Mafarisayo wanamuuliza Yesu juu ya kulipa kodi kwa Kaisari.
"Jinsi ambavyo wangeweza kumsababisha Yesu kukosea katika kauli ili wamkamate"
Wanafunzi wa Mafarisayo walikubaliana na swala kulipa kodi kwa mamlaka za Kiyahudi. Maherode walikubaliana na swala la kulipa kodi kwa mamlaka za Kirumi. kwa maana hiyo, Mafarisayo waliamini kuwa kwa vyote ambavyo Yesu angejibu; angelikosea moja ya makundi hayo.
Hawa walikuwa wafuasi na maofisa wa Herode mfalme wa Wayahudi. Alikuwa rafiki wa mamlaka za Kirumi.
"Huoneshi heshima ya kipekee kwa baadhi ya watu" au " haujali tu watu maarufu zaidi."
Watu hawakulipa kodi moja kwa moja kwa Kaisari lakini kwa mmoja wa maofisa wake. "Kulipa kodi ambayo Kaisari alilitaka"
"msinijaribu mimi enyi wanafiki" au "Najua kuwa ninyi wanafiki mnajaribu kunijaribu!"
Sarafu ya kirumi yenye thamani ya ujira wa siku.
kiwakilishi "wa" kinamaanisha Maherode na wanafunzi wa Mafarisayo.
Niambieni sura na jina mnavyoviona kwenye hii sarafu ni vya nani?
"Sarafu hii ina sura na jina la Kaisari"
"Vitu ambavyo ni mali ya Kaisari"
"Vitu ambavyo ni mali ya Mungu."
Masadukayo wanajaribu kumkamata Yesu kwa kumtega kwa swali gumu kuhusu ndoa na ufufuo wa wafu.
Walikuwa wakimuuliza kuhusu alichoandika Musa katika Maandiko. "Musa alisema kwamba ikiwa mtu amekufa."
Kimilikishi "yake" inamaanisha yule mfu
Mafarisayo wanaendelea kumwuliza Yesu swali
namba za mpangiliio
"Baada ya kila ndugu kuwa amemuoa" au " Baada ya kila ndugu kuwa amefariki."
"baada ya kila ndugu kufa"
Hapa Masadukayo wanabadilisha habari ya ndugu yule wa saba na kuuliza swali halisi
"Mnakosea juu ya ufufuo"
"Kile ambacho Mungu anaweza kufanya."
"wakati wafu watapofufuka"
"watu hawataoa"
"wala watu hawataruhusu watoto wao kuolewa"
Katika 22:32, Yesu ananukuu kutoka kitabu cha Kutoka ili kuhakikisha kuwa watu wataishi tena baada ya kifo
"Najua mmekwisha soma, Lakini inaonekana hamkuelewa ambacho...Yakobo.'
"Kile alichowaambia Mungu"
"Mungu alimwambia Musa kwamba Yeye, Mungu, ni Mungu wa Abramu,Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo."
wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai"
Farisayo mwanasheria alimtega Yesu kwa swali kwa kumwuliza swali gumu juu ya amri kuu
Farisayo ambaye alikuwa na ujuzi maalum katika kuelewa sheria ya Musa.
Yesu ananukuu ile amri kuu kutoka Kumbukumbu la torati
Virai vyote vitatu vinamaanisha kitu kilekile. Vinamaanisha kuwa mtu lazima ampende Mungu kwa pendo la ndani na kwa kujito kwa ukweli.
Neno "kuu" na ya "kwanza" yanamaanisha kitu kilekile. vinasisitiza kuwa hii ni amri ya muhimu
Yesu ananukuu mstari toka Walawi kama amri kuu ya pili
Yaweza kumaanisha 1) "kuna amri ya pili ambayo inafuatia kwa umuhimu" au 2) "kuna amri ya pili ambayo nayo ni ya muhimu." Kwa namna yeyote ile, Yesu anamaanisha kuwa amri hizi zote ni za muhimu kuliko amri zingine zote.
Ya pili ni katika kupangilia
Tazama 2:37
Neno "jirani" inamaana zaidi ya mtu aliye karibu na wewe. inamaanisha kuwa mtu lazima awapende watu wote
Neno "sheria zote na manabii" limzznisha maandiko yote. "Kila kitu ambacho Musa na Manabii waliandika katika maandiko zinategemea amri hizi zote mbili"
Yesu anawauliza Mafarisayo swali gumu ili kuzuia mpango wao wa kumkamata.
Neno hili limetumika ili kuonesha mwanzo wa habari mpya. Mathayo anaanza kueleza sehemu mpya ya simulizi wakati Yesu alipowauliza viongozi wa dini swali.
vyote hivi "mwana" vinamaanisha "kizazi"
Yesu ananukuu toka Zaburi kuonesha kuwa Kristo ni zaidi ya "mwana wa Daudi"
"Yesu anatumia swali kuwafanya viongozi wa dini kufikiri kwa undani zaidi juu ya Zaburi anyotaka kuinukuu "Niambieni kwa nini Daudi katika Roho anamwita Bwana"
"Daudi ambaye anavuviwa na Roho. "Hii inamaanisha kuwa Roho Mtakatifu anamwezesha Daudi kusema.
Hapa "mwi" inasimama badala ya Kristo, ambaye pia ni kizazi cha Daudi.
Neno "Bwana" inamaanisha Mungu Baba
Kiwakilishi "wangu" kinamaanisha Mungu Baba. "Mkono wa kuume" huwa inatumika kuonesha sehemu ya heshima
Hii ni nahau. "hadi nitakapowashinda adui zako" au hadi nitakapowafanya maadui zako kukuinamia"
Huu nu mwisho wa jitihada za viongozi wa dini kutaka kumkamata Yesu kwa maswali mengi
Huu ni mwisho wa sehemu ya habari hii inayoanzia 19:1, ambayo inaelezea habari za Yesu akihudumia Yuda
"Daudi anamwita Yeye Bwana, kwa hiyo Kristo lazima awe zaidi kuliko mzao wa Daudi."
Daudi amemrejea Yesu kama "Bwana" kwa sababu Yesu hakuwa tu mzao wa Daudi, lakini pia alikuwa bora kuliko Daudi.
"Neno" inamaanisha kile amabacho watu husema. "kumjibu yeye chochote" au " kumjibu"
Inamaanisha kuwa hakuna aliyemuuliza maswali ya jinsi hiyo ambayo yalikusudiwa kuwaYesu angeyajibu kimakosa ili viongozi wa dini wamkamate
Baadhi yao hawakuizingatia ile mialiko na kuendelea na shughuli zao, na wengine waliwanyoshea mikono wale watumishi wa mfalme na kuwaua.
Baadhiyao hawakuzingatia hiyo mialiko na kuendelea na shughuli zao, na wengine waliwanyoshea mikono hao watumishi wa mfalme na kuwaua.
Mfalme alituma jeshi, na kuwaua wale wauuaji, na kuichoma miji yao
Basi, malme alikarisha watu wengi kadri watumishi wake walivyoweza kuwapata. wote wema na wabaya.
Basi, mfalme aliwakaribisha watu wengi kadri watumishi wake walivyoweza kuwapata. Wote wema na wabaya.
Mfalme aliamuru afungwe na atupwe nje kwenye giza.
Mafarisayo walijaribu kumnasa Yesu katika mazungumzo yake.
Walimwuliza Yesu kama ilikuwa halali kulpa kodi kwa Kaisari.
Yesu aliseam kumpa Kaosari kilicho chake, na kumpa Mungu kilicho cha Mungu.
Masadukayo waliamini kwamba hakutakuwaepo na ufufuo wa wafu.
Yule mwanamke alikuwa na waume saba
Yule mwanamke alikuwa na waume saba
Yesu alisema kwamba Mafarisayo hawakujua Maandiko Matakatifu wala nguvu za Mungu.
Yesu alisema katika ufufuo hakuna kuolewa wala kuoa
Yesu alinukuu maandiko ambayo Mungu anasema kuwa yeye ni Mungu wa Ibrahimu, wa Isaka, na Mungu wa Yakobo - Mungu wa walio hai.
Yule mwanasheria alimwuliza Yesu kuwa sheria iliyo kuu ni ipi?
Yesu alisema lazima, kumpenda Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote na kwa akili zako zote, na kumpenda jirani yako kama nafsi yako, hizo ndizo amri kuu mbili.
Yesu alisema lazima, umpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kumpenda jirani yako kama nafsi yako, hii ndiyo amri iliyo kuu na ya kwanza.
Yesu alisema kumpenda jirani yako kama nafsi yako, hiyo ndiyo amri ya pili.
Yesu aliwauliza kuwa, Kristo ni mwana wa nani?
Mafarisayo walimjibu Yesu kuwa Kristo alikuwa Mwana wa Daudi.
Baadaye Yesu aliwauliza jinsi gani Daudi angeweza kumwita mwana wake, Kristo, Bwana,
Mafarisayo hawakuweza kumjibu Yesu neno lolote.
1Baadaye aliongea na umati na wanafunzi wake. Akasema,2“Waandishi na Mafarisayo wanakalia kiti cha Musa.3Kwa hiyo chochote wanacho waamuru kufanya, fanyeni huku mkiwachunguza. Lakini msije mkaiga matendo yao, kwa sababu wao hutamka mambo wasiyoyafanya.4Kweli, wao hufunga mizigo mizito ambayo ni vigumu kuibeba, na kisha huwabebesha watu mabegani mwao. Lakini wao wenyewe hawasogezi hata kidole kuibeba.5Matendo yao yote, huyafanya ili watazamwe na watu. Kwa sababu wao hupanua masanduku yao na huongeza ukubwa wa mapindo ya mavazi yao.6Wao hupendelea kukaa maeneo ya kifahari katika sherehe na katika viti vya heshima ndani ya masinagogi,7na kusalimiwa kwa heshima maeneo ya sokoni, na kuitwa ‘Walimu’ na watu.8Lakini ninyi hampaswi kuitwa “Walimu,” Kwa kuwa mnaye Mwalimu mmoja, na ninyi wote ni ndugu.9Msimuite mtu yeyote hapa duniani kuwa baba yenu, kwa kuwa mnaye Baba mmoja tu, naye yuko mbinguni.10Wala msije kuitwa ‘walimu,’ kwa kuwa mnaye Mwalimu mmoja tu, yaani Kristo.11Bali aliye mkubwa miongoni mwenu atakuwa mtumishi wenu.12Yeyote ajiinuae atashushwa. Na yeyote anaye jishusha atainuliwa.13Lakini ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Mnawafungia watu ufalme wa mbinguni. Nanyi hamwezi kuuingia, na hamwaruhusu wanaoingia kufanya hivyo.14115Ole wenu Waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Mnavuka ng'ambo ya bahari na kufika kumfanya mtu mmoja aamini yale mnayoyafundisha, na anapokuwa kama ninyi, mnamfanya mara mbili mwana wa jehanamu kama ninyi wenyewe mlivyo.16Ole wenu viongozi vipofu, ninyi msemao, ‘Yeyote aapaye kwa hekalu, si kitu. Lakini anayeapa kwa dhahabu ya hekalu, amefungwa na kiapo chake.’17Enyi vipofu wapumbavu, kipi ni kikubwa kuliko kingine, dhahabu au hekalu ambalo limeweka wakfu dhahabu kwa Mungu?18Na, yeyote aapaye kwa madhabahu, si kitu. Bali anayeapa kwa sadaka iliyo juu yake, amefungwa na kiapo chake.19Enyi watu vipofu, kipi ni kikubwa kuliko kingine, sadaka au madhabahu ambayo huweka wakfu sadaka zinazotolewa kwa Mungu?20Kwa hiyo, yeye aapaye kwa madhabahu huapa kwa hiyo na kwa vitu vyote vilivyo juu yake.21Naye aapaye kwa hekalu, huapa kwa hilo na kwa yeye akaaye ndani yake.22Na yeye aapaye kwa mbingu, huapa kwa kiti cha enzi cha Mungu na kwa yeye aketie juu yake.23Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnalipa zaka kwa bizali, mnaanaa na mchicha, lakini mnaacha mambo mazito ya sheria- haki, rehema, na imani. Lakini haya mnapaswa kuwa mmeyafanya, na siyo kuacha mengine bila kuyatekeleza.24Enyi viongozi vipofu, ninyi ambao mnachuja mdudu mdogo lakini mnameza ngamia!25Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnasafisha nje ya vikombe na nje ya sahani, lakini ndani pamejaa dhuluma na kutokuwa na kiasi.26Enyi Mafarisayo vipofu, safisheni kwanza ndani ya kikombe na ndani ya sahani, ili upande wa nje nao pia uwe safi.27Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnafanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, ambayo kwa nje huonekana mazuri, lakini kwa ndani yamejaa mifupa ya waliokufa na kila kitu kilicho kichafu.28Vivyo hivyo, nanyi kwa nje mwaonekana wenye haki mbele ya watu, lakini kwa ndani mmejaa unafiki na udhalimu.29Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mwajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya wenye haki.30Ninyi mwasema, kama tungeishi siku za baba zetu, tusingekuwa tumeshiriki pamoja nao kumwaga damu za manabii.31Kwa hiyo mwajishuhudia wenyewe kwamba ninyi ni watoto wa hao waliowaua manabii.32Pia ninyi mnakamilisha kujaza sehemu inayostahili dhambi ya baba zenu.33Enyi nyoka, wana wa majoka, kwa namna gani mtaikwepa hukumu ya jehanamu?34Kwahiyo, tazama, nawatuma kwenu manabii, watu wenye hekima, na waandishi. Baadhi yao mtawaua na kuwasulubisha. Na baadhi yao mtawachapa ndani ya masinagogi yenu na kuwafukuza kutoka mji mmoja hadi mwingine.35Matokeo ni kwamba juu yenu patatokea damu zote za wenye haki zilizomwagwa duniani, kuanzia damu ya Habili mwenye haki hadi kwa damu ya Zakaria mwana wa Barakia, mliye muua kati ya patakatifu na madhabahu.36Kweli, nawaambieni, mambo haya yote yatakipata kizazi hiki.37Yerusalemu, Yerusalemu, wewe unayewaua manabii na kuwapiga mawe wale ambao wanatumwa kwako! Mara ngapi nimewakusanya watoto wako pamoja kama vile kuku awakusanyavyo vifaranga wake chini ya mabawa yake, lakini haukukubali!38Tazama, nyumba yako imebaki ukiwa.39Nami nakuambia, kuanzia sasa na kuendelea hautaniona, hadi utakaposema, ‘Amebarikiwa yeye ajaye kwa jina la Bwana.”’
Unafiki wa Wafarisayo ni neno kuu katika sura hii. Yesu anazungumzia kwa kina kuhusu unafiki huu. Wafarisayo waliunda sheria ambayo hakuna mtu angeweza kutii, na kisha wakawashawishi watu kwamba walikuwa na hatia kwa sababu ya kutotii sheria. Pia, sheria za Wafarisayo ziliwapa sababu za kutotii amri za asili za Mungu za Sheria ya Musa.
Katika tamaduni nyingi, ni makosa kuwaalumu watu. Maneno mengi katika sura hii yaliyowalenga Wafarisayo yanaweza kuchukuliwa kama matusi. Wanaitwa "wanafiki," "viongozi vipofu," "wajinga," na "nyoka." Yesu anatumia maneno haya kuelezea na kuhukumu tabia zao.
Kitendawili ni taarifa inayoonekana kuwa ya ajabu, ambayo ni kana kwamba inajikana yenyewe, lakini kwa hakika sio ya ajabu. Kwa mfano, "aliye mkuu kati yenu atakuwa mtumishi wenu" (Mathayo 23:11-12).
Huu ni mwamnzowa habari mpya inyoenedelea hadi 25:44, amabpo Yesu anafundisha juu ya wokovu na hukumu ya mwisho. Anaanza kuwaonya watu juu ya Mafarisayo na waandishi
Kiti kinamaanisha mamlaka ya kutawala na kuhukumu. "Wanayo mamlaka kama aliyokuwanayo Musa." au "wanayo mamlaka ya kusema maana ya sheria Musa."
"Yoyote" au "kila kitu."
"Wanawawekea ninyi kanuni nyingi ambazo ni ngumu kufuata."
"Wao hawatatoa msaada hata msasada kidogo"
wanafanya mataendo yao kwa kusuadi la kutazamwa na watu
Hivi vyote ni vitu ambavyo Mafarisayo huvifanya ili waonekane kuwa wanamtii Mungu kuliko watu wengine
Haya ni makasha madogo ya ngozi yenye karatasi za maandiko
Mafarisayo huweka mapindo marefu chini ya kanzu zao kuonesha uchaji wao kwa Mungu.
Yesu anaendelea kuongea na makutano kuhusu Mafarisayo
Maeneo yaote haya na yale amabayo watu muhimu hukaa
Maeneo makubwa ya wazi amabyo watu huuza na kununua bidhaa
"ili watu wawaite rabi"
"Msimruhusu mtu yeyote awaite"
viwakilishi vyote vya "ninyi" viko katka wingi na vinamaanisha wafauasi wote wa Yesu
Neno "ndugu" linamaanisha "waumini wenzenu"
"msiseme kwamba mtu yeyote hapa duniani ni baba yenu"
"baba" ni cheo muhimu cha Mungu
"pia msimruhusu mtu kuwaita"
Wakati Yesu aliposema "Kristo" alikuwa anasema juu yake mwenyewe katika nafsi ya tatu. AT: "Mimi, Kristo ndiye mwalimu wenu pekee."
"mtu maarufu miongono mwenu"
kiwakilishi "mwenu" ni cha wingi na kinamaanisha wafuasi wa Yesu
"ajifanyaye mwenyewe kuwa maarufu."
"Mungu atamshusha
Mungu atamuheshimu
Yesu anaanza kuwakemea viongozi wa dini kwa sababu ya unafiki wao
tazama 11:20
"Mnawazuia watu kumpokea Mungu wetu wa mbinguni kuwa mfalme wao"
"Hamumruhusu Mungu kuwa mfalme wenu"
"wala hamuwarusu wale wanaotaka kumpokea Mungu kuwa mfalme wao kufanya hivyo"
"mnasafiri umbali mrefu"
"kumfanya mtu mmoja aamini dini yenu"
"Mtu ambaye mahali pake ni kuzimu." au mtu ambaye hanabudi kwenda kuzimu."
"Kuiba kila kitu kutoka kwa wanawake wasio na wanaume wa kuwalinda."
Tazama 15:12
"kwa hekalu hawezi kulinda kiapo chake
"Lazima atende kile alichoahidi kufanya."
Hekalu amablo limetumika kuweka wakfu dhahabu kwa Mungu ni la muhimu kuliko dhahabu ile"
"Hekalu ambalo hutengeneza dhahabu ni mali ya Mungu pekee"
"na ninyi pia husema"
"hakuna haja ya kulinda kiapo chake"
ni mnyama au nafaka ambayo mtu anaweza kuileta kwa Bwana na kuiweka madhabahuni
"lazima afanye kile alichoahidi kufanya"
Viongozi wa Kiyahudi walikuwa vipofu kiroho. Ingawa walijidhania kuwa walimu, hawakuwaeza kuuelewa ukweli wa Mungu
"Madhabahu ambayo huzifanya sadaka kuwa takatifu ni kuu kuliko sadaka
madhabahu ambayo huziweka sadaka kuwa rasmi kwa Mungu"
"kwa vitu vyote ambvyo sadaka zote huwekwa juu yake"
virai vyote hivi vinamaanisha Mungu Baba.
Tazama 11:20.
Majani na mbegu zinazotumika kuungia chakula.
"hamkutii
"mambo y a muhimu zaidi"
"mnapaswa kuwa mmeziheshimu hizi sheria za muhimu"
"wakati pia mnatii zile sheria ndogondogo"
Tazama 15:12
Kuwa mwaangalifu kufuatilia sheria zenye uzito kidogo na kupuuzia sheria zenye uzito mkubwa, hiyo ni upumbavu sawa na kuwa mwangalifu kwa kutokumeza mnyama mdogo aliye najisi, bali unakula nyama ya mnyama mkubwa sana aliye najisi pengine kwa makusudi au kwa kutokujuwa. AT: "Wewe ni mpumbavu kama mtu ambaye anachuja mdudu aliyeangukia ndani ya kinywaji chake lakini akimeza ngamia."
Kujucha kwa kutumia ktambaa ili kuondoa mdudu katika kinywaji
Mdudu mdogo arukae.
Tazama 11:20
"Waandishi" na "Mafarisayo" kwa wengine wanaonekana "safi kwa nje, lakini ndani ni wachafu
"Wanachukua vitu vya watu kwa ubinafsi
Mafarisayo walikuwa vipofu kiroho. Ingawa wao wenyewe walijidhania kuwa walimu. hawakuwa na uwezo wa kuelewa ukweli wa Mungu
Hii ni sitiari inayomaanisha kuwa kama wangekuwa safi mioyoni mwao, basi matokeo yake wangekuwa safi kwa nje pia
hii ni kejeli inayoonesha kuwa Mafarisayo na waandishi wanaonekana kuwa safi nje, lakini ndani ni wachafu
"makaburi ambayo mtu ameyapaka chokaa" Wayahudi walipakaa makaburi kwa chokaa ili kuepusha kuyagusa. Kugusa kaburi ilihesabiwa kuwa ni unajisi.
"ya watu wenye haki"
"wakati wa mababu zetu"
"tusingekuwa tumeshirikiana nao"
Damu inamaanisha uhai. kumwaga damu inamaanisha kuua. "kuua" au "mauaji"
"watoto inamaanisha uzao"
"Ninyi mna kamilisha dhambi ambazo babu zenu walizianzisha,"
"Ninyi ni waovu na hatari kama nyoka wenye sumu."
tazama 3:7
"Hakuna njia mnayoweza kutumia kuepuka hukumu ya jehanamu!"
"nitawatuma." Hapa "ni" inamaanisha Yesu.
"Mungu atawahukumu kwa mauaji ya watu wenye haki"
"kutoka mauji hadi ... mauaji"
Abeli alikuwa mhanga wa kwanza katika mauaji, na Zakaria huenda akafikiriwa kuwa wa mwisho kuuwawa na Wayahudi hekaluni.Watu hawawaili wanawakilisha mauaji ya watu wote wenye haki
Siyo baba yake na Yohana Mbatizaji.
Yesu hamaanisha watu wale aliokuwa akisema nao kuwa ndio waliomua Zekaria. Anamaanisha kuwa mababu zao ndio waliomuua.
"Nawaambia ukweli." Hii inaongeza msisitizo wa kile Yesu atakachosema baadye.
Yesu anaomboleza juuya watu wa Yerusalemu kwa sababu wanamkataa kila aliyetumwa na Mungu kwao
Yesu anazungumza na watu wa Yerusalemu kana kwamba wao wenyewe ndio walikuwa mji.
wale ambao Mungu huwatuma kwako
"watu wako" au 'kizazi chako"
Huu ni usemi unaosisitiza upendowa Yesu kwa watu n a jinsi alivyotaka kuwajali.
"Mungu ataiacha nyumba yako, na itabaki tupu."
Maana yake ni : (1). Mji wa Yerusalemu au (2). Hekalu.
Huu ni msisitizo wa kile Yesualichosema baadaye
Tazama 21:9
Yesu aliwaambia watu kufanya na kuyasikiliza mafundisho ya Mafarisayo waliyofundisho toka kwenye kiti cha Musa.
Yesu aliwaaambia watu kufanya na kuyasikiliza mafundisho ya Mafarisayo waliyofundisha toka kwenye kti cha Musa.
Yesu alisema wasiyafuate matendo yao kwa sababu walikuwa wakisema vitu ambavyo wao wenyewe hawavifanyi.
Walifanya matendo yao kusudi watazamwe na watu.
Yesu alisema kwamba, Baba yetu aliye mmoja ni Yeye Mwenyewe aliye mbinguni, na mwalimu wetu pekee ni Kristo.
Yesu alisema kwamba, Baba yetu aliye mmoja ni yeye mwenyewe aliye mbinguni, na mwalimu wetu pekee ni Kristo.
Mungu atamshusha mtu yule ajikwezaye mwenyewe na kumwinua mtu yule ajishushaye.
Mara kwa mara Yesu aliwaita waandishi na Mafarisayo wanafiki.
Mafarisayo na waandishi walipopata mfuasi mpya alikuwa mwana wa kuzimu mara mbili.
Mara kwa mara Yesu aliwaita waandishi na Mafarisayo wanafiki
Yesu alisema kwamba waandishi na Mafarisayo walikuwa viongozi vipofu na vipofu wapumbavu.
Yesu alisema kwamba waandishi na Mafarisayo walikuwa viongozi vipofu na vipofu wapumbavu.
Waandishi na Mafarisayo walishindwa kufanya mambo makubwa ya sheria haki, rehema, na imani.
Waandishi na Mafarisayo walishindwa kusafisha ndani ya kikombe chao, ili upande wa nje pia uwe safi.
Waandishi na Mafarisayo walishiindwa kusafisha ndani ya kikombe chao, ili upande wa nje pia uwe safi.
Waandishi na Mfarisayo ndani yao walikuwa wamejaa majivuno, udhalimu, unafiki na uovu.
Waliwaua manabii
Wazazi wa waandishi na Mafarisayo waliwaua manabii wa Mungu.
Hukumu ya Jehanamu
Yesu alisema watawaua na kuwasulibisha baadhi yao, kuwapiga baadhi yao, na wengine kuwafukuza kutoka mji mmoja hadi mwingine.
Hatia ya kumwagika kwa damu ya wenye haki katika duniani itakuja juu ya waandishi na Mafarisayo.
Yesu alisema kuwa haya yote yatatokea kwenye kizazi hiki.
Yesu alitamani kuwakusanya watoto wa Yerusalemu pamoja, lakini hawakukubali.
Nyumba za Yerusalemu zitabaki ukiwa.
1Yesu alitoka hekaluni na kwenda zake. Wanafunzi wake walimwendea na kumuonesha majengo ya hekalu.2Lakini aliwajibu na kusema, “Je, hamuyaoni mambo haya yote? Kweli nawaambia, hakuna jiwe litalobaki juu ya lingine bila kubomolewa.”3Na alipokaa katika lima wa Mizeituni, wanafunzi wake walimwendea kwa faragha na kusema, “Tuambie, mambo haya yatatokea lini? Kitu gani kitakuwa dalili ya kuja kwako na mwisho wa ulimwengu?”4Yesu aliwajibu na kuwaambia, “Iweni makini kwamba asije mtu akawapotosha.5Kwa kuwa wengi watakuja kwa jina langu. Watasema, ‘Mimi ndiye Kristo,’ na watawapotosha wengi.6Mtasikia vita na taarifa za vita. Angalieni msije mkawa na wasiwasi, kwa kuwa mambo haya hayabudi kutokea; lakini ule mwisho utakuwa bado.7Kwa kuwa taifa litainuka dhidi ya taifa jingine, na ufalme dhidi ya ufalme. Kutakuwa na njaa na matetemeko ya ardhi katika sehemu mbalimbali.8Lakini mambo haya yote ni mwanzo tu wa uchungu wa kujifungua.9Ndipo watawatoa kwa ajili ya mateso na kuwaua. Mtachukiwa na mataifa yote kwa sababu ya jina langu.10Ndipo wengi watajikwaa na kusalitiana na watachukiana wenyewe kwa wenyewe.11Manabii wengi wa uongo watatokea na kuwadanganya wengi.12Kwa sababu uovu utaongezeka, upendo wa wengi utapungua.13Lakini atakaye vumilia mpaka mwisho, ataokolewa.14Hii Injili ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu mzima kama ushuhuda kwa mataifa yote. Na ndipo ule mwisho utafika.15Kwa hiyo, mtakapoona chukizo la uharibifu, lililosemwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu (asomaye na afahamu),16ndipo walioko Yuda wakimbilie milimani.17Na yule aliyeko juu ya paa la nyumba asiweze kuteremka chini kuchukua kitu chochote kutoka ndani ya nyumba yake,18naye aliyeko shambani asirudi kuchukua vazi lake.19Lakini ole wao ambao wana mtoto na wale ambao wananyonyesha katika siku hizo!20Ombeni kwamba kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato.21Kwa kuwa kutakuwa na dhiki kuu, ambayo haijawahi kuwapo tangu kuumbwa kwa ulimwengu hadi sasa, na wala haitakuwapo tena.22Kama siku hizo zisingefupishwa, hakuna ambaye angeokoka. Lakini kwa sababu ya wateule, siku hizo zitafupishwa.23Kisha ikiwa mtu yeyote atawaambia ‘Tazama, Kristo yuko hapa! Au, ‘Kristo yuko kule’ msiamini maneno hayo.24Kwa kuwa Makristo wa uongo na manabii wa uongo watakuja na kuonesha ishara kubwa na maajabu, kwa kusudi la kupotosha, kama ingewezekana hata na wateule.25Tazameni, nimewatahadharisha kabla ya mambo hayo kutokea.26Kwa hiyo, ikiwa watawaambia, “Kristo yuko jangwani,’ msiende huko jangwani. Au, ‘Tazameni, yuko ndani ya nyumba,’ msiamini maneno hayo.27Kama vile radi inavyomulika kutokea mashariki na kuangaza hadi magharibi, ndivyo itakavyokuwa kuja kwa Mwana wa Adamu.28Popote ulipo mzoga, huko ndiko tai wakusanyikapo.29Lakini mara baada ya dhiki kuu ya siku zile, Jua litatiwa giza, mwezi hautatoa mwanga wake, nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za mbinguni zitatikisika.30Ndipo ishara ya Mwana wa Adamu itaonekana angani, na makabila yote ya dunia wataomboleza. Watamwona Mwana wa Adamu akija katika mawingu ya angani kwa nguvu na utukufu mkuu.31Atawatuma malaika wake kwa sauti kuu ya tarumbeta, nao watawakusanya pamoja wateule wake kutoka pande nne za dunia, kutoka mwisho mmoja wa mbingu hadi mwingine.32Jifunzeni somo kutokana na mti mtini. Mara tu tawi linapochipuka na kutoa majani, mnajua kwamba kiangazi kinakaribia.33Hivyo pia, mtakapoona mambo haya yote, mnapaswa kujua kwamba amekaribia, karibu na malango.34Kweli nawaambia, kizazi hiki hakitapita, hadi mambo yote haya yatakuwa yametokea.35Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.36Lakini kuhusu siku ile na saa hakuna mtu ajuaye, hata malaika wa mbinguni, wala Mwana, bali Baba peke yake.37Kama vile ilivyokuwa katika siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa kuja kwa Mwana wa Adamu.38Kwa kuwa katika siku hizo kabla ya gharika watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa hadi siku ile ambayo Nuhu aliingia katika safina,39na hawakujua kitu chochote hadi gharika ilipokuja na kuwasomba wote - ndivyo itakavyokuwa kuja kwa Mwana wa Adamu.40Ndipo watu wawili watakuwa shambani- mmoja atachukuliwa, na mmoja ataachwa nyuma.41Wanawake wawili watakuwa wanasaga pamoja - mmoja atachukuliwa, na mmoja atabaki.42Kwa hiyo, kuweni macho kwa sababu hamjui ni siku gani ambayo atakuja Bwana wenu.43Lakini mjue kwamba, ikiwa bwana mwenye nyumba angejua ni saa ipi ambayo mwizi angekuja, angekesha na asingeruhusu nyumba yake kuvamiwa.44Kwa hiyo, pia mnapaswa kuwa tayari, kwa kuwa Mwana wa Adamu atakuja katika saa msiyoitarajia.45Hivyo ni nani aliye mwaminifu, mtumwa mwenye akili, ambaye bwana wake amempa madaraka juu ya walio katika nyumba yake, ili awape chakula kwa wakati unaofaa?46Amebarikiwa mtumishi huyo, ambaye bwana wake atamkuta akifanya hivyo wakati ajapo.47Kweli nawaambia kwamba bwana atamweka juu ya kila kitu kilicho chake.48Lakini kama mtumwa mwovu akisema moyoni mwake, ‘Bwana wangu amekawia,’49na akaanza kuwapiga watumishi wake, na akala na kulewa vileo,50Bwana wa mtumwa huyo atakuja katika siku ambayo haitarajii, na katika saa ambayo haijui.51Bwana wake atamkata vipande viwili na kumweka katika nafasi moja sawa na wanafiki, ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
Katika sura hii, Yesu anaanza kutabiri kuhusu wakati ujao kutoka wakati huo hadi atakaporudi kama mfalme wa ulimwengu.
Katika sura hii, Yesu anatoa jibu kwa wanafunzi wake wakati wanauliza jinsi watakavyojua wakati atakapokuja tena.
Katika wakati wa Nuhu, Mungu alituma gharika kuu kuwaadhibu watu kwa dhambi zao. Aliwaonya mara nyingi kuhusu kuja kwa mafuriko hayo, lakini kwa hakika yalianza ghafla. Katika sura hii, Yesu analinganisha mafuriko hayo na siku za mwisho.
ULB hutumia neno hili kuanzisha amri kadhaa za Yesu, kama "wacha wale walio Yudea wakimbilie milimani" (24:16), "yule aliye juu ya nyumba asije akashuka kuchukua chochote kutoka kwa nyumba yake "(24:17), na" aliye mashambani asirudi kuchukua nguo yake "(24:18). Kuna njia nyingi za kuunda amri. Watafsiri wanapaswa kuchagua njia za asili zaidi katika lugha zao wenyewe.
Yesu anaanza kueleza matukio amabayo yatakuja tokea kabla hajarudi mara ya pili
Inaonesha kuwa Yesu hakuwa ndani ya hekalu. alikuwa kwenye korido la hekalu.
"Ngoja niwaambie kitu fulani kuhusu majengo haya yote."
"Nawaambia ukweli." huu ni msisitizo wa kile alichosema Yesu badaye
"wakati maaskari walio adui watakapokuja, watabomoa kila jiwe juu ya majengo haya"
Neno "kuja kwako" linamaanisha wakati Yesu atakapokuja katika nguvu, kuanzisha utawala wa Mungu duniani na kukifikisha kizazi hiki mwisho wake.
"Mwe waangalifu kwamba msiamini yeyote ambaye atawaongopea kuhusu mambo haya."
Neno "jina" linamaanisha "katika mamlaka" au " kama mwakilishi" wa mwingine. "Wengi watadai kuwa wamekuja kama wawakilishi wangu" au "wengi watasema kuwa wanaongea kwa niaba yangu"
"Msije mkaruhusu mambo haya kuwapa wasiwasi."
Hii inamaanisha kitu kilekile. na msisitizo wake ni kwamba kutakuwa na mapigano kila mahali
Hii inamaanisha maumivu mwanamke huyapata wakati anapotaka kujifungua mtoto. Sitiari hii inamaanisha kuwa haya matetemeko, njaa na vita ni mwanzo tu wa matukio yatakayotuongoza kuelekea mwisho wa dunia
"watuwatawatoa kwa mamlaka amaboa watawatesa na kisha kuwaua"
"watu kutoka kilataifa watawachukia"
"kwa sababu mnaniamini "
"watakuja"
"watu watafanya dhambi zaidi na zaidi"
Maana ya karibu: 1."watu wengi hawatawapenda wenzao." au 2."watu wengi hawatampenda Mungu."
"yeyote atayebaki na uvumilivu"
haieleweki kama "mwisho" inamaanisha mtu anapokufa, au wakati dhiki itakapokoma, au mwisho wa nyakati wakati Mungu atakapojionesha kuwa mfalme. jambo l a kuzingatia hapa ni uvumilivu usiokoma
"Mungu atamwokoa mtu huyo"
"Watu watahubiri ujumbe juu ya utawala wa Mungu"
"Watu wote katika sehemu zote."
"mwisho wa ulimwengu" aua "mwisho wa nyakati"
"mtu wa aibu atakayevinajisi vitu vya Mungu"
"Kuhusu ambacho nabii Danieli aliandika."
Haya maneno hayakusemwa na Yesu. Matahayo aliongezea haya ili kupata usikivu
mapaa wakati wa Yesu yalikuwa tambarare, kiasi kwamba watu wangeweza kusimama
"wanawake wenye mimba"
"wakati huo"
"kwamba msikimbie"
"Majira ya baridi."
"kama Mungu hatazifupisha siku zadhiki watu wote wangekufa"
Watu.
"Mungu atazifupisha siku za dhiki"
Yesu anaendelea kuwaambia wanafunzi wake
"Msiamini mambo ya uongo wanayowaambia."
"ili kuwafanya watu wasitii"
"kupotosha, kama ingeliwezekana, watawafanya hata na wateule kutotii"
"au, kama mtu atawambia kuwa Kristo yumo ndani ya nyumba"
"ndani ya chumba cha siri"
Hiiinamaanisha mwana wa mtu atakuja kwa kasi sana na itakuwa rahisi kumwona
Atakuja kwa kasi na itakuwa rahisi kuonekana.
Yesu anaongea juu yake katika nafsi ya tatu
Maana ya karibu ni: (1). Mwana wa Adamu atakapokuja, kila mtu atamuona na kujua kwamba amekuja; (2). Popote walipo watu aliokufa kiroho, manabii wa uongo watakuwepo huko kuwaambia uongo.
Ndege ambao wanakula mizoga au wanyama wanaokaribia kukata roho.
"wakati huo"
"wakati huo wa dhiki"
"Mungu atalifanya jua liwe giza."
" Mungu atatikisa vitu katika mbingu na juu ya anga."
Yesu anaongea juu yake katika nafsi ya tatu.
watu wa makabila yote
"wakati tarumbeta itakapolia atawatuma malaika wake"
"Malaika wake watakusanya."
Watu ambao Mwana wa Adamu amewachagua.
kutoka kila upande
"wakati wangu wa kuja umekaribia"
karibu na malango
"Nawaambia ukweli" huu ni msisitizo wa kile kinachosemwa baadaye
"Watu wanaoishi kipindi hiki hawatafariki wote."
"Mpaka Mungu asababishe mambo haya yote yatimie."
"Mbingu na nchi hazitaendelea kuwapo."
"kile ninachosema daima kitabaki kuwa ukweli"
hapa "siku" na "saa" vinamaanisha muda halisi ambao mwana wa Adamu atarudi
"Hakuna hata mwana"
Hiki ni cheo muhimu cha Yesu, Mwana wa Mungu
Hiki ni cheo muhimu cha Mungu
"Siku ambayo Mwana wa Adamu atakuja tena itakuwa kama ilivyokuwa siku za Nuhu,"
Yesu anaongea juu yake akaitumia nafsi ya tatu
"katika safina. Na watu hawakuju kuwa kuna kitu kilikuwa kinaenda kutokea"
"Hivyo ndivyo itakavyokuwa wakati wa kuja kwa Mwana wa Adamu"
Yesu anaanza kuwaambia wanfunzi wake kuwa tayari kwa ajili ya kurudi kwake
Wakati Mwana wa Adamu ajapo.
Maana za karibu: 1. Mungu atamchukuwa mmoja kwenda mbinguni na ataacha mmoja duniani kwa ajili ya adhabu, au 2. Malaika watamchukua mmoja kwa ajili ya adhabu na kumuacha mwingine kwa ajili ya baraka.
Chombo cha kusagia.
"Kwa sababu ya kile nilicho waambia."
Kaa tayari.
Yesu anaatumia mfano wa bwana na mtumwa kufafanua kuwa wansfunzi wake wanatakiwa kujiandaa kwa ajili ya kurudi kwa Yesu
Yesu anasema atakuja wakati ambao watu hawamtarajii, siyo kwamba atakuja kuiba.
"Angelinda nyumba yake" kuisalimisha.
"Asingeruhusu mtu yeyote kuingia ndani ya nyumba yake aibe vitu."
Yesu anatumia nafasi ya tatu kujisemea yeye
Yesu anaendelea na mithali yake ya bwana na mtumwa kufafanua kuwa wanafunzi wake wanapaswa kujiandaa kwa ajili y a kurudi kwa Yesu.
"Hivyo ni nani mwaminifu, mtumwa mwenye akili? Ndiye yule ambaye bwana wake...wakati."
"Awape watu chakula chao katika mji wa bwana wake"
"Nawaambieni ukweli" Hii inaongeza msisitizo wa kile ambacho Yesu atakuja kusema baadaye.
Yesu anahitimisha mithali yake ya bwana na mtumwa ...
"Anafikiri akilini mwake."
Bwana wangu hafanyi haraka kuja
Virai hivi vyote vinamaanisha kitu kilekile. vinasisitiza kuwa bwana atakuja wakati ambao mtumwa wake hamtarajii kuja.
"Kumtendea"
"kumtendea"
kumfanya mtu aumie sana
Tazama 8:11
Yesu alitabiri kuwa haltabakijiwe juu ya jiwe ambalo halitabomolewa.
Wanafunzi walimuuliza ni lini mambo haya yangetokea, na ni nini dalili za kuja kwake na mwisho wa ulimwengu?
Yesu alisema kuwa wengi watakuja wakisema wao ni makristo, watawapotosha wengi.
Yesu alisema kwamba vita, njaa, na matetemeko yatakuwa mwanzo wa utungu.
Yesu alisema kuwa vita njaa, na matetemeko yatakuwa mwanzo wa utungu
Yesu alisema kwamba wanafunzi watapata mateso ya dhiki kuu, baadhi watajikwaa na kusalitiana, na mioyo ya watu wengi itapoa.
Yesu alisema kuwa wanafunzi wangepata mateso ya dhiki kuu, baadhi watajikwaa na kusalitiana,na mioyo ya watu wengi itapoa
Yesu alisema kwamba atakayevumilia mpaka mwisho ndiyo atakayeokoka?
Injil ya ufalme itahubiriwa duniani kote kabla mwisho kuja.
Yesu alisema waumini watakimibilia milimani.
Yesu alisema waumini watakimblia milimani.
Katika siku zile, ile dhiki itakuwa kubwa sana kuliko ambavyo ilishawahi kutokea tangu kuumbwa kwa dunia.
Makristo wa uongo na manabii wa uongo watawapotosha watu kwa kufanya ishara na maajabu.
Kuja kwa Mwana wa Adamu kutakuwa kama radi inavyomulika kutokea mashariki na kuangaza hadi magharibi.
Jua na mwezi vitatiwa giza, na nyota zitaanguka kutoka mbinguni.
Makabila ya duniani watapigapiga vifua vyao.
Sauti kuu ya tarumbeta itasikika malaika watakapowakusanya wataeule.
Yesu alisema kwamba kizazi hiki hakitapita mpaka mambo haya yote yatimie.
Yesu alisema kuwa mbingu na dunia zitapita, lakini neno lake halitapita kamwe.
Ni Baba peke yake ajuae lini matukio haya yatatokea.
Watu watakuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, bila kujua hukumu itawajilia kuwaangamiza.
Watu watkuwa wakila na kunywa, wakioa na kuolewa, bila kujua hukumu itawajilia kuwaangamiza.
Yesu alisema kuwa waumini wake lazima wawe tayari, kwa sababu hawajui ni siku gani Bwana atakapokuja.
Mtumwa mwaminifu na mwenye busara alitunza mali yote ya bwana wake wakati bwana wake alipokuwa amesafiri.
Mtumwa mwaminifu na mwenye busara alitunza mali yote ya bwana wake wakati bwana wake aliokuwa amesafiri
Takapokuja, bwana wake atamweka mtumwa mwaminnifu na mwenye busara juu ya kila kitu anachokimiliki.
Mtumwa mwovu aliwapiga wafanyakazi wake na akala na kunywa pamoja na walevi wakati bwana hajarudi.
Mtumwa mwovu aliwapiga wafnyakazi wake na akala na kunywa pamoja na walevi wakati bwana hajarudi.
Bwana atakaporudi, atamkata yule mtumwa mwovu katika vipande viwili na kumpeleka mahali ambapo kutakuwa na kilo na kusaga meno.
1Ndipo ufalme wa mbinguni utafananishwa na wanawali kumi waliochukua taa zao na kuondoka kwenda kumpokea bwana harusi.2Watano miongoni mwao walikuwa wapumbavu na watano wengine walikuwa werevu.3Wanawali wapumbavu walipochukua taa zao, hawakuchukua mafuta yoyote.4Bali wanawali welevu walichukua vyombo vyenye mafuta pamoja na taa zao.5Sasa wakati bwana harusi amechelewa kufika, wote walishikwa usingizi na wakalala.6Lakini wakati wa usiku wa manane kulikuwa na yowe, ‘Tazama, bwana harusi! Tokeni nje mkampokee.’7Ndipo hao wanawali waliamka wote na kuwasha taa zao.8Wale wapumbavu waliwaambia wale werevu, ‘Mtupatie sehemu ya mafuta yenu kwa sababu taa zetu zinazimika.’9Lakini wale werevu waliwajibu na kuwaambia, ‘Kwa kuwa hayatatutosha sisi na ninyi, badala yake nendeni kwa wanaouza mjinunulie kiasi kwa ajili yenu.’10Wakati wameenda huko kununua, Bwana harusi alifika, na wote waliokuwa tayari walienda naye kwenye sherehe ya harusi, na mlango ulifungwa.11Baadaye wale wanawali wengine pia walifika na kusema, ‘Bwana, bwana, tufungulie.’12Lakini alijibu na kusema, ‘Kweli nawaambia, Mimi siwajui.’13Kwa hiyo angalieni, kwa kuwa hamjui siku au saa.14Kwa kuwa ni sawa na mtu alipotaka kusafiri kwenda nchi nyingine. Aliwaita watumwa wake na kuwakabidhi utajiri wake.15Mmoja wao alimpatia talanta tano, mwingine alimpa mbili, na yule mwingine alimpa talanta moja. Kila mmoja alipokea kiasi kulingana na uwezo wake, na yule mtu alisafari kwenda zake.16Mapema yule aliyepokea talanta tano alienda kuziwekeza, na kuzalisha talanta zingine tano.17Vile vile yule aliyepokea talanta mbili, alizalisha zingine mbili.18Lakini mtumwa aliyepokea talanta moja, alienda zake, akachimba shimo ardhini, na kuificha fedha ya bwana wake.19Na baada ya muda mrefu, bwana wa watumwa hao alirudi na kutengeneza mahesabu nao.20Yule mtumwa aliyepokea talanta tano alikuja na kuleta talanta zingine tano, akasema, ‘Bwana, ulinipa talanta tano. Tazama, nimepata faida ya talanta zingine tano.’21Bwana wake akamwambia, ‘Hongera, mtumwa mzuri na mwaminifu! Umekuwa mwaminifu kwa vitu vidogo. Nitakupa madaraka juu ya vitu vingi. Ingia katika furaha ya bwana wako.’22Mtumwa aliyepokea talanta mbili alikuja na kusema, ‘Bwana, ulinipa talanta mbili. Tazama, nimepata faida ya talanta zingine mbili,’23Bwana wake akamwambia, ‘Hongera, mtumwa mzuri na mwaminifu! Umekuwa mwaminifu kwa vitu vichache. Nitakupa madaraka juu ya vitu vingi. Ingia katika furaha ya bwana wako.’24Baadaye mtumwa aliyepokea talanta moja alikuja na kusema, ‘Bwana, najua kuwa wewe ni mtu mkali. Unachuma mahali ambapo hukupanda, na unavuna mahali ambapo hukusia.25Mimi niliogopa, nikaenda zangu na kuificha talanta yako katika udongo. Tazama, unayo hapa ile iliyo yako.’26Lakini bwana wake alijibu na kusema, ‘Wewe mtumwa mwovu na mzembe, ulijua kwamba ninachuma mahali ambapo sijapanda na kuvuna mahali ambapo sikusia.27Kwahiyo ulipaswa kuwapa fedha yangu watu wa benki, na wakati wa kurudi kwangu ningeipokea ile yangu pamoja na faida.28Kwa hiyo mnyang'anyeni hiyo talanta na mpeni yule mtumwa aliye na talanta kumi.29Kila mtu aliye nacho, ataongezewa zaidi-hata kwa kuzidishiwa sana. Lakini kwa yeyote asiye na kitu, hata alicho nacho atanyang'anywa.30Mtupeni nje gizani huyo mtumwa asiyefaa, ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.’31Wakati Mwana wa Adamu atakapokuja katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye, ndipo atakapokaa juu ya kiti chake cha utukufu.32Mataifa yote yatakusanyika mbele zake, naye atawatenganisha watu, kama vile mchungaji anavyowatenganisha kondoo na mbuzi.33Atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, bali mbuzi atawaweka mkono wa kushoto.34Kisha mfalme atawaambia wale walio mkono wake wa kulia, ‘Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme ulioandaliwa kwa ajili yenu tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu.35Kwa kuwa nilikuwa na njaa na mlinipa chakula; Nilikuwa mgeni na mlinikaribisha;36Nilikuwa uchi, na mlinivika nguo; Nilikuwa mgonjwa na mkanitunza; Nilikuwa kifungoni na mkaniijia.’37Ndipo wenye haki watamjibu na kumwambia, ‘Bwana, lini tulikuona ukiwa na njaa, na kukulisha? Au una kiu na tukakupa maji?38Na lini tulikuona ukiwa mgeni, na tukakukaribisha? Au ukiwa uchi na tukakuvisha nguo?39Na lini tulikuona ukiwa mgonjwa, au katika kifungo, na tukakujia?40Na mfalme atawajibu na kuwaambia, ‘Kweli nawaambia, mlichotenda hapa kwa mmoja wa ndugu zangu wadogo, mlinitendea mimi.’41Ndipo atawaambia hao walio mkono wake wa kushoto, ‘Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, nendeni katika moto wa milele ulioandaliwa kwa ajili ya shetani na malaika zake,42kwa sababu nilikuwa na njaa lakini hamkunipa chakula; Nilikuwa na kiu lakini hamkunipa maji;43Nilikuwa mgeni lakini hamkunikaribisha; nikiwa uchi lakini hamkunipa mavazi; nikiwa mgonjwa na nikiwa kifungoni, lakini hamkunitunza.’44Ndipo wao pia watamjibu na kusema, ‘Bwana, lini tulikuona ukiwa na njaa, au una kiu, au u mgeni, au ukiwa uchi, au ukiwa mgonjwa, au ukiwa mfungwa, na hatukukuhudumia?45Kisha atawajibu na kusema, ‘Kweli nawaambia, kile ambacho hamkutenda kwa mmoja wa hawa wadogo, hamkunitendea mimi.’46Hawa watakwenda katika adhabu ya milele bali wenye haki katika uzima wa milele.”
Sura hii inaendeleza mafundisho ya sura ya awali.
Miongoni mwa Wayahudi, wakati ndoa ilipangwa, kulikuwa na muda kabla ya harusi. Mwisho wa muda huo, kijana huyo angeenda nyumbani kwa bibi arusi, ambako alikuwa anamngojea. Sherehe ya harusi basi ingefanyika. Kwa furaha kubwa wangeweza kusafiri hadi nyumba ya bwana harusi, ambako kungekuwa na sikukuu.
Yesu anatumia desturi hii kwa kuwaambia mfano wa bikira kumi (Mathayo 25:1-13).
Yesu anaongea mfano wa wanawali wenyebusara na wale wanawali wajinga kufundisha kuwa wanafunzi wake wanapaswa kujiandaa kwa ajili y a kurudi kwa Yesu
Tazama 13:24
Hizi ziliweza kuwa, 1.taa zenyewe au mienge iliyotengenezwa kwa kuwekewa kitambaa kuzunguka mwisho wa mti na hulowanishwa na mafuta.
Watano kati ya wanawali.
"Waliyokuwa nayo ni yale tu yaliyokuwa katika taa zao."
Neno linaloonesha kuanzisha habari mpya. Yesu anaanza kueleza sehemu ya habari hii.
"wakati bwana harusi alipochukua muda mrefu kuwasili"
Wanawali wote kumi walianza kusinzia.
"mtu mmoja alianza kupiga kelele"
Yesu anaendelea kueleza mfano
"Wakarekebisha taa zao ili ziwake kwa mng'ao."
"Wanawali wapumbavu walisema na wanawali welevu."
"Moto katika taa zetu unaelekea kuzima."
Yesu anahitimisha mfano wa wanawali kumi
"Wanawali wapumbavu waliondoka."
"kununua mafuta zaidi"
Wanawali waliokuwa na mafuta ya ziada.
"watumishi walifunga mlango."
"Fungua mlango kwa ajili yetu ili tuingie ndani"
"Nawaambia ukweli" Hiiinatia msisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye
"Si watambui ninyi ni akina nani" au 'si wajui ninyi ni akina nani."
"Hamjui muda halisi ambao Mwana wa Adamu atakuja"
Yesu anaeleza mfano wa mtumishi mwaminifu na asiye mwaminifu ili kuwafundisha wanafunzi wake kubaki waaminifu wakati yeye hatakuwepo na wawe tayari kwa ajili ya kurudi kwa Yesu.
"Ufalme wa mbinguni ni unafanana na."
"Alipokuwa tayari kuondoka" au mara alipotaka kuondoka."
"Akawapa usimamizi wa mali yake." au "akawapa usimamizi wa utajiri wake."
"Mali yake."
"Talanta moja" ilikuwa na thamani ya mishahara wa miaka ishirini. Epuka kutafsiri jambo hili katika pesa za siku hizi. Mfano huo unalinganisha uwiano wa kiasi cha tano, cha mbili na kiasi cha moja sawia na kiasi kikubwa cha utajiri uliotumika. "mifuko mitano ya dhahabu."
"kulingana na uwezo wa kila mtumishi wa kusimsmia mali"
"Kutokana na uwekezaji wake, alipata faida ya talanta zingine tano."
"kutokana na uwekezaji wake, akazalisha talanta zingine tano"
Yesu anaendelea mafano wa watumishi na talanta
"Alipata faida ya talanta zingine mbili.'
Yesu anaendelea kueleza mfano wa watumishi na talanta
Kirai hiki kimetumika kuonesha mwanzo wa habari mpya. Yesu anaanza kueleza sehemu mpya ya simulizi.
"Nimepata faida ya talanta tano zaidi."
Mali yenye thamani kubwa. talanta moja ilikuwa sawa na mishahara ya miaka ishirini.Tazama tafsiri katika. 25:14--15.
"Umefanya kazi vizuri." au "Umefanya vema." Katika utamaduni wako pengine mnao usemi ambao mkuu (mtu mwenye mamlaka) angetumia kuthibitisha kile ambacho mtumishi wake (au yeyote chini yake) amekitekeleza.
"Njoo ufurahie na mimi"
Yesu anaendelelea kueleza mfano wa watumishi na talanta
"Nimepata fada ya talanta mbili zaidi"
umefanya vema.
Tazama 25:19
Yesu anaendelea kueleza mfano wa watumishi na talanta
Maelezo haya mawili yanamaanisha kitu kilekile. Mtumwa anamlaumu bwana kwa kukusanya mazao ambayo siyo yake. "Unakusanya mazao ya bustani kutoka katika bustani ambazo huna haki ya kukusanya mazao hayo."
Siku hizo walizoea kutupa kiasi kidogo cha mbegu pande zote badala ya kupanda katika mistari.
"Angalia, hii n"diyo yako"
Yesu anaenedelea kueleza mfano wa watumishi na talanta.
"wewe ni mtumwa mwovu ambaye hutaki kufanya kazi."
Tazama 25:24
"Kupokea tena fedha yangu mwenyewe"
Malipo yanayotolewa na benki kutokana na matumizi yasiyo ya kudumu ya pesa ya bwana.
Yesu anaendelea kueleza mfano wa watumishi na talanta
Bwana anawaambia wale watumishi wengine
Tazama 25:14
"anayetumia vizuri alicho nacho"
"Mungu atampa zaidi"
"hata zaidi"
"Kwa yeyeote asiyetumia vizuri hicho alicho nacho.
"Mahali ambapo watu watalia na kusaga meno yao."
nitakiondoa
"nje gizani ambako kuna kilio na kusaga meno"
Yesu anaanza kuwaambia wanafunzi wake jinsi atakavyowahukumu watu atakaporudi wakatiwa mwisho
Yesu anatumia nafsi ya tatu kuongea juu yake mwenyewe
"Atayakusanya mataifa yote mbele zake."
"Mbele za uso wake."
"Watu wote kutoka kila nchi."
Yesuanatumia msemo kuonesha jinsi atakavyowatenganisha watu
atawaweka watu wenye haki upande wake wa kuume na atawaweka wenye dhambi upande wake wa kushoto
"Mimi mfalme, ... mkono wangu wa kulia"
Yesu alijisema yeye mwenyewe katka nafsi ya tatu. AT: "Mimi, Mfalme...mkono wangu wa kulia."
"Njoni, ninyi ambao baba yangu amewabariki."
Hili ni jina mashuhuri la Mungu linaloonesha uhusiano kati ya Mungu na Yesu
"Urithini ufalme ambao Mungu ameufanya tayari kwa ajili yenu."
"pokeeni baraka za utawala wa Mungu ambazo Mungu alipanga kuwapeni"
"Tangu hapo alipouumba ulimwengu"
watu wenye haki
"au ni lini tulipokuwa ukiwa na kiuau nilini tulipokuona u uchi"
Hiki ni cheo kingine cha Mwana wa Mungu
"Akasema na wale walio mkono wa kulia."
"Nawaambia ukweli, "Huu ni msisitizo wa kile ambacho Yesu alikuja kusema baadaye"
"mmoja wa wasio wa muhimu"
"kaka zangu na dada" au "hawa ambao ni kama kaka zangu na dada zangu
"Ninajali kwamba mlifanya hivyo kwa ajili yangu."
"Ndipo mfalme atawaambia"
"enyi watu ambao Mungu amewalaani."
"Moto wa milele ambao Mungu ameandaa."
Wasaidizi wake.
"Nilikuwa uchi lakini hamkunipa nguo."
"Nilikuwa mgonjwa na nilikuwa kifungoni."
"nilikuwa mgonjwa na nilikuwa gerezani"
Yesu anahitimisha kuwaambia wanafunzi wake jinsi atakavyowahukumu watu atakapokuja mara ya pili
Huu ni mwisho wa sehemu ya habari inayoanzaia 23:1, mahali ambapo Yesu anafundisha juu ya wokovu na hukumu ya mwisho.
"Hao walioko kushoto pia watamjibu"
"Kwa yeyote kati ya watu wangu walio wadogo."
"Nina jali kuwa hamkufanya kwa aajili yangu" au "Mimi ndiye hasa yule ambaye hamkumsaidia"
"Mfalme atawapeleka hawa kwenye eneo amablo watapata adhabu ambayo haitakoma"
"Watu wenye haki wataenda katika uzima wa milele."
"lakini mfalme atawapeleka hawa mahali ambapo wataishi milele pamoja na Mungu"
"watu wenye haki"
Wale wanawali wapumbavu walipochukua taa zao hawakuchukua mafuta.
Wale wanawali wenye busara walichukua vyombo vyenye mafuta pamoja na taa zao.
Bwana arusi alifika usiku wa manane, baada ya muda uliotarajiwa.
Bwana Harusi alifika usiku wa manane, baada ya muda uliotarajiwa.
Wanawali welevu walienda pamoja na bwana arusi katika sherehe ya harusi.
Wale wanawali wapumbavu walienda kununua mafuta, na walipokuja ule mlango wa kuingia kwenye sherehe ulikuwa umefungwa.
Wale wanawali wapumbavu walienda kunua mafuta, na walipokuja ule mlango wa kuingia kwenye sherehe ulikuwa umefungwa.
Yesu alisema kuwa waumii wanapaswa kuwa tayari kwa kuwa hawajui siku wala saa.
Yule mtumishi mwenye talanta tano alizalisha talanta zingine tano na yule mwenye talanta mbili alizalisha zingine mbili.
Yule mwenye moja alichimba shimo na kuifukia ile talanta ya bwana wake .
Huyo bwana alikaa huko safarini kwa muda mrefu.
Yule bwana alisema, "hongera, watumwa wazuri na waamiinifu" na aliwaweka kuwa wasimamizi wa mambo mengi.
Yule bwana alisema, "hongera, watumwa wazuri na waamiinifu" na aliwaweka kuwa wasimamizi wa mambo mengi.
Tule bwana alisema, "wewe mtumwa mwovu na mzembe," alimnyanga'nya ile talanta moja, na kumtupa katika giza la nje.
Mwana Adamu atayakusanya mataifa yote na atawatenganisha watu kundi moja kutoka kundi jingine.
Mwana Adamu atayakusanya mataifa yote na atawatenganisha watu kundi moja kutoka kundi jingine.
Wale wa upande wa kulia wa Mfalme kupokea ufalme ulioandaliwa kwa ajili yao tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu.
Wale wa upande kushoto wa Mfalme watapokea moto wa milele ulioandaliwa kwa ajili ya shetani na malaika zake.
Wale wa upande wa kushoto wa mfalme hawakuwapa chakula wenye njaa, wala kinywaji wenye kiu, hawakuwakaribisha wageni, hawakuwapa nguo walio uchi, hawakuwajali wagonjwa, wala kuwatembelea wafungwa.
Wale wa upande wa kushoto wa mfalme hawakuwapa chakula wenye njaa, wala kinywaji wenye kiu, hawakuwakaribisha wageni, hawakuwapa nguo walio uchi, hawakuwajali wagonjwa, wala kuwatembelea wafungwa.
1Wakati Yesu alipomaliza kusema maneno yote hayo, aliwaambia wanafunzi wake,2“Mnajua kwamba baada ya siku mbili kutakuwa na sikukuu ya pasaka, na mwana wa Adamu atatolewa ili asulibiwe.”3Baadaye wakuu wa makuhani na wazee wa watu walikutana pamoja katika makao ya Kuhani Mkuu, aliye kuwa anaitwa Kayafa.4Kwa pamoja walipanga njama ya kumkamata Yesu kwa siri na kumuua.5Kwa kuwa walisema, “Isifanyike wakati wa sikukuu, kusudi isije ikazuka ghasia miongoni mwa watu.”6Wakati Yesu alipokuwa Bethania katika nyumba ya Simoni mkoma,7alipokuwa amejinyoosha mezani, mwanamke mmoja alikuja kwake akiwa amebeba mkebe wa alabasta iliyokuwa na mafuta yenye thamani kubwa, na aliyamimina juu ya kichwa chake.8Lakini wanafunzi wake walipoona jambo hilo, walichukia na kusema, “Nini sababu ya hasara hii?9Haya yangeweza kuuzwa kwa kiasi kikubwa na kupewa maskini.”10Lakini Yesu, akiwa anajua hili, akawaambia, “Kwa nini mnamsumbua mwanamke huyu? Kwa kuwa amefanya kitu kizuri kwangu.11Masikini mnao siku zote, lakini hamtakuwa pamoja nami daima.12Kwa sababu alipomimina mafuta haya juu ya mwili wangu, alifanya hivyo kwa ajili ya maziko yangu.13Kweli nawaambieni, popote Injili hii itakapohubiriwa katika ulimwengu mzima, kitendo alichofanya huyu mwanamke, pia kitakuwa kinasemwa kwa ajili ya kumkumbuka.”14Ndipo mmoja wa wale Kumi na wawili, aliyeitwa Yuda Iskariote, alienda kwa wakuu wa makuhani15na kusema, “Mtanipatia nini nikimsaliti?” Wakampimia Yuda vipande thelathini vya fedha.16Tangu muda huo alitafuta nafasi ya kumsaliti.17Hata siku ya kwanza ya mikate isiyotiwa chachu, wanafunzi walimwendea Yesu na kusema, “Wapi unataka tukuandalie ule chakula cha Pasaka?”18Akawaambia, “Nendeni mjini kwa mtu fulani na mwambieni, Mwalimu anasema, ‘Muda wangu umekaribia. Nitaitimiza Pasaka pamoja na wanafunzi wangu katika nyumba yako.’”19Wanafunzi walifanya kama Yesu alivyowaagiza, na waliandaa chakula cha Pasaka.20Ilipofika jioni, aliketi kula chakula pamoja na wale wanafunzi kumi na wawili.21Walipokuwa wanakula chakula, alisema, “Kweli nawaambia kwamba mmoja wenu atanisaliti.”22Walihuzunika sana, na kila mmoja alianza kumuuliza, “Je, hakika siyo mimi, Bwana?”23Akawajibu, “Yule ambaye anachovya mkono wake pamoja nami katika bakuli ndiye atakaye nisaliti.24Mwana wa Adamu ataondoka, kama alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu ambaye atamsaliti Mwana wa Adamu! Ingekuwa vizuri kwa mtu huyo kama asingezaliwa.”25Yuda, ambaye angemsaliti alisema, “Je, ni mimi Rabi?” Yesu akamwambia, “Umesema jambo hilo wewe mwenyewe.”26Walipokuwa wakila chakula, Yesu aliutwaa mkate, akaubariki, na kuumega. Akawapa wanafunzi wake akisema, “Chukueni, mle. Huu ni mwili wangu.”27Akatwaa kikombe na kushukuru, akawapa na kusema, “Kunyweni wote katika hiki.28Kwa kuwa hii ni damu ya agano langu, inayomwagwa kwa ajili ya wengi kwa msamaha wa dhambi.29Lakini nawaambieni, sitakunywa tena matunda ya mzabibu huu, hadi siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.”30Walipokuwa wamemaliza kuimba wimbo, walitoka kwenda Mlima wa Mizeituni.31Kisha Yesu akawaambia, “Usiku huu ninyi nyote mtajikwaa kwa sababu yangu, kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji na kondoo wa kundi watatawanyika.32Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”33Lakini Petro alimwambia, “Hata kama wote watakukataa kwa sababu ya mambo yatakayokupata, mimi sitakukataa.”34Yesu akamjibu, “Kweli nakuambia, usiku huu kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”35Petro akamwambia, “Hata kama ingenipasa kufa na wewe, sitakukana.” Na wanafunzi wengine wote wakasema vivyo hivyo.36Baadaye Yesu alienda nao mahali panapoitwa Gethsemane na aliwaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa wakati nikienda huko na kuomba.”37Akamchukua Petro na wana wawili wa Zebedayo na akaanza kuhuzunika na kusononeka.38Kisha akawaambia, “Roho yangu ina huzuni kubwa sana, hata kiasi cha kufa. Bakini hapa na mkeshe pamoja nami.”39Akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, na kuomba. Akasema, “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki kiniepuke. Isiwe kama ninavyotaka mimi, bali kama utakavyo wewe.”40Akawaendea wanafunzi na akawakuta wamelala usingizi, na akamwambia Petro, “Kwa nini hamkuweza kukesha nami kwa saa moja?41Kesheni na kuomba kusudi msiingie majaribuni. Roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.”42Akaenda zake mara ya pili na kuomba, akasema, “Baba yangu, kama jambo hili haliwezi kuepukika na ni lazima nikinywee kikombe hiki, mapenzi yako yatimizwe.”43Akarudi tena na kuwakuta wamelala usingizi, kwa kuwa macho yao yalikuwa mazito.44Kisha akawaacha tena akaenda zake. Akaomba mara ya tatu akisema maneno yaleyale.45Baadaye Yesu aliwaendea wanafunzi wake na kuwaambia, “Bado mmelala tu na kujipumzisha? Tazameni, saa imekaribia, na Mwana wa Adamu anasalitiwa mikononi mwa wenye dhambi.46Amkeni, tuondoke. Tazama, yule anaye nisaliti amekaribia.”47Wakati alipokuwa bado anaongea, Yuda mmoja wa wale kumi na wawili, akafika. Kundi kubwa lilifika pamoja naye likitokea kwa wakuu wa Makuhani na wazee wa watu. Walikuja na mapanga na marungu.48Tena mtu aliyekusudia kumsaliti Yesu alikuwa amewapa ishara, akisema, “Yule nitakayembusu, ndiye yeye. Mkamateni.”49Mara hiyo alikuja kwa Yesu na kusema, “Salamu, Mwalimu!” Na akambusu.50Yesu akamwambia, “Rafiki, lifanye lile ambalo limekuleta.” Ndipo wakaja, na kumnyoshea mikono Yesu, na kumkamata.51Tazama, mtu mmoja wa wale waliokuwa pamoja na Yesu, alinyosha mkono wake, akachomoa upanga wake, na akampiga mtumishi wa kuhani mkuu, na kumkata sikio lake.52Ndipo Yesu akamwambia, rudisha upanga wako pale ulipoutoa, kwa kuwa wote watumiao upanga wataangamizwa kwa upanga.53Mnadhani kuwa siwezi kumwita Baba yangu, naye akanitumia makundi ya majeshi zaidi ya kumi na mawili ya malaika?54Lakini basi jinsi gani maandiko yangeweza kutimizwa, hivi ndivyo inapasa kutokea?”55Wakati huo Yesu akauambia umati, “Je! Mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kama mnyang'anyi? Kila siku nilikaa hekaluni nikifundisha, na hamkunishika!56Lakini yote haya yametendeka ili Maandiko ya manabii yatimie.” Ndipo wanafunzi wake wakamwacha na kukimbia.57Wale waliomkamata Yesu walimpeleka kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, mahali ambapo waandishi na wazee walikuwa wamekusanyika pamoja.58Lakini Petro alimfuata nyuma kwa mbali hadi katika ukumbi wa Kuhani Mkuu. Aliingia ndani na kukaa pamoja na walinzi aone kitakachotokea.59Basi wakuu wa makuhani na Baraza lote walikuwa wakitafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu, kusudi wapate kumuua.60Ingawa walijitokeza mashahidi wengi, lakini hawakupata sababu yoyote. Baadaye mashahidi wawili walijitokeza mbele61na kusema, “Mtu huyu alisema, “Naweza kulivunja hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.”62Kuhani Mkuu alisimama na kumwuliza, “Hauwezi kujibu? Hawa wanakushuhudia nini dhidi yako?”63Lakini Yesu alikaa kimya. Kuhani Mkuu akamwambia, “Kama Mungu aishivyo, nakuamuru utwambie, kama wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu.”64Yesu akamjibu, “Wewe mwenyewe umesema jambo hilo. Lakini nakuambia, toka sasa na kuendelea utamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kulia wenye nguvu, na akija katika mawingu ya mbinguni.”65Ndipo Kuhani Mkuu alirarua mavazi yake na kusema, “Amekufuru! Je, twahitaji tena ushahidi wa nini? Angalia, tayari mmesikia akikufuru.66Je! Mnawaza nini? Wakajibu na kusema, “Anastahili kifo.”67Kisha walimtemea mate usoni na kumpiga ngumi, na kumchapa makofi kwa mikono yao,68na kusema, “Tutabirie, wewe Kristo. Ni nani amekuchapa?”69Wakati huo Petro alikuwa amekaa nje katika ukumbi, na mtumishi wa kike alimwendea na kusema, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”70Lakini alikana mbele yao wote, akisema, “Sijui kitu unachosema.”71Alipoenda nje ya lango, mtumishi mwingine wa kike alimwona na kuwaambia waliokuwepo hapo, “Mtu huyu pia alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti.”72Akakana tena kwa kiapo, “Mimi simjui mtu huyu.”73Muda mfupi baadaye, wale waliokuwa wamesimama karibu, walimwendea na kusema na Petro, “Kwa hakika wewe pia ni mmoja wao, kwa kuwa hata lafudhi yako inaonesha.”74Ndipo alianza kulaani na kuapa, “Mimi simfahamu mtu huyu,” na mara hiyo jogoo akawika.75Petro alikumbuka maneno aliyoambiwa na Yesu, “Kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu.”
Baadhi ya tafsiri zinaingiza nukuu kutoka kwa Agano la Kale. ULB inafanya hivyo kwa mistari iliyonukuliwa katika 26:31.
Hii ni taswira ya kawaida inayotumiwa katika Maandiko ya kutaja watu wa Israeli. Lakini, katika Mathayo 26:31, "kondoo" inawakilisha wanafunzi wa Yesu, ambao walikimbia wakati alikamatwa.
Kifo cha Yesu kilitokea kwa uhusiano na Sikukuu ya Pasaka kwa sababu yeye ndiye timizo la mwanakondoo wa Pasika. Ni kifo chake cha dhabihu ambacho kinatuokoa kutokana na hukumu ya Mungu.
Sherehe hii, ambayo mara nyingi huitwa "Meza ya Bwana," "Ekaristi", au "Ushirika Mtakatifu," hufanyika katika karibu makanisa yote hadi siku hii kwa ukumbusho wa dhabihu ya Kristo kwa ajili ya dhambi za binadamu. Hufanyika kwa kutii maagizo ya Yesu kwa wanafunzi wake katika Mathayo 26:26-28.
Kote katika sura hii, matendo ya viongozi wa Kiyahudi ni ya aibu na ya woga. Waliwaogopa watu waliopaswa kuwaongoza. Matendo yao ya aibu na ya uoga yanaweza kuwa vigumu kueleza katika kutafsiri.
Yuda amenakiliwa katika Mathayo 26:49 kumbusu Yesu ili kutoa ishara kwa askari ili kumtambua yule watakaomkamata. Miongoni mwa Wayahudi, kubusu ilikuwa njia ya kawaida ya kumsalimu mtu. Walikuwa na busu za aina mbalimbali kati ya watu wa tabaka mbalimbali. Kwa kuwa Yesu alikuwa mwalimu wa Yuda, labda alibusu mkono wake kama ishara ya heshima na utii.
Katika Mathayo 26:61, watu wawili wanamshtaki Yesu kwa kutaka hekalu la Yerusalemu liangamizwe ili aweze kulijenga kwa "siku tatu." Labda walikuwa wakimshtaki Yesu kwa kutukana hekalu na kwa hiyo, kwa njia nyingine, kumtukana Mungu. Mathayo hana rekodi ya Yesu akitamka haya, lakini maneno haya yapo katika Yohana 2:19.
Maneno "katika siku tatu" yanapaswa kueleweka kwa njia ya Kiyahudi kama "ndani ya siku tatu," wala sio "baada ya siku tatu."
Huu ni mwanzo wa sehehmu mpya wa simulizi amablao linaelezea kusulibiwa kwa Yesu, kufa na kufufuka. Hapa anawaeleza wanafunzi wake jinsi atakavyoteseka
"kisha " au"baadaye"
Tazama 24:3
"Baadhi ya watu watamtoa Mwana wa Adamu kwa watu wengine ambao watamsulibisha."
Yesu anatumia nafsi ya tatu kuongea juu yake
Mstari huu unatoa historia ya mpango wa viongozi wa Wayahudi wa kumkamata na kumwua Yesu
"walikutana"
"Bila kujulikana kwa wengi"
"Tusimuue Yesu wakati wa sikukuu"
Sikukuu ya kila mwaka ya Pasaka.
Hii inaanza na habari ya mwanamke akimwaga manukato ya gharama kabla ya kifo cha Yesu
Hil ni neno linalotumika kuazisha habari mpya. Mathayo anaanza kuelezea habari mpya
Inamaanisha kuwa huyu ndiye mtu ambaye Yesu alimponya kwa ukoma
"Yesu alikuwa amekaa upande wake". Unaweza kutumia neno la lugha yako kwa mkao wa watu ambavyo huwa wakati wa kula.
Mwanamke alikuja kwa Yesu.
chombo ambacho hugharimu sana kwa kukinunua kilicho tengenezwa na jiwe laini.
Mafuta ambayo yana harufu nzuri.
Yule mwanamke alifanya hivi kuonesha heshima kwa Yesu
"Mwanamke huyu amefanya jambo baya kwa kuharibu mafuta haya"
"angweza kuyauza kwa thamani kubwa ya pesa na kuitoa ile pesa
"kwa watu masikini"
"Hamkupaswa kumsumbua mwnamke huyu"
viwakilishi vyote vya "mna" viko katika wingi
"watu masikini"
Tazama 26:6
"nawambia ukweli" huu ni msisitizo wa kile kilichofuata
"popote pale watu watakapohubiri injili hii"
"watakumbuka kile ambacho mwanamke huyu amefanya na wataambiwa wengine juu yake"
Yuda Iskaariote anakubali kuwasaidia viongozi wa Wayahudi kumkamata na kumwua Yesu
"kuwasaidia kumkamata Yesu."
Kwa kuwa maneno haya ni sawa na yale ya unabii katika Agano la Kale, endeleza muundo huu badala ya kuugeuza katika pesa ya leo.
"Kuwasaidia wakuu wa makuhani kumkamata Yesu."
"vipande 30"
Hii inaazisha hanari y a Yesu akisherehekea Pasaka pamoja na wanafunzi wake
Hili ni neno amablo limetumika kuonesha mwazo wa habari mpya. Matahyo anaanza kueleza sehemu mpya ya habari
"Aliwaambia wanafunzi wake kuingia mjini kwa mtu fulani na kumwambia kwamba Mwalimu anamwambia, 'Muda wangu umekaribia. Nitaitimiza Pasaka pamoja na wanafunzi wangu nyumbani mwako.'" au "Aliwaambia wanafunzi wake kwenda mjini kwa mtu fulani na kumweleza mtu huyo kwamba Mwalimu anasema muda wake umekaribia na atatimiza Pasaka pamoja na wanafunzi wake katika nyumba ya mtu huyo."
Maana yake yaweza kuwa: 1) " Muda ambao niliwahi kuwajulisha" au 2 "Muda ambao Mungu amepanga kwa ajili yangu."
Maana yake yaweza kuwa: 1) "uko karibu" au 2) "Umefika."
"Kula chakula cha Pasaka" au "sherekea sikukuu ya Pasaka kwa kula chakula maalum."
Tumia neno kwa mkao ambao watu katika utamaduni wako daima hukaa wakati wa kula.
"Nawaambia ukweli." Huu ni msisitizo wa kile kilichofuata
"Nina hakika mimi siye, Je, ni mimi?"
Yesu anatumia nafsi ya tatu kuongea juu y ake mwenyewe
"akufa"
"kama vile manabii walivyoandika juu yake katika maandiko"
"Mtu ambaye amsaliti Mwana wa Adamu."
"Rabi, kwa hakika si mimi nitakayekusaliti"
"wewe ndiye unayesema"
Yesu anakula chakula na wanafunzi kwa kusherehekea Pasaka na wanafunzi wake
Tazama 14:19
Tazama14:19
Kikombe kinamaanisha kikombe kikiwa na divai ndani yake
"kunywa divai kutoka kikombe hiki"
"kwa kuwa hii divai ni damu yangu"
"Damu ambayo huonesha kwamba agano linafanya kazi" au "damu ambayo hufanya agano liwezekane.
"Inamwagwa kwa ajili ya kifo" au "hivi punde itachuruzika kutoka mwilini mwangu." au "itachuruzika kutoka katika majeraha yangu nitakapo kufa."
"mvinyo"
Hii inaongeza msisitzo
Baba atakapoanzisha ufalme wake duniani "hapa"
Hiki ni cheo muhimu cha Mungu kinachoonesha uhusiano muhimu kati ya Mungu na Yesu.
Yesu anaendelea kuwafundisha wanafunzi wake wakati wakielekea mlima wa Mizeituni
Katika mstari wa 31, Yesu anamnukuu Nabii Zekaria kuonesha kuwa ili kutimiza unabii, wanaaafunzi wake wataondoka.
Wimbo wa sifa kwa Mungu.
"mtaniacha"
"Kuniacha."
Kwa kuwa nabii zekaria aliandika tangu awali katika maandiko"
kiwakilishi "ni" kinamaanisha Mungu. Inamaanisha kuwa Mungu atasababisha au kuruhusu watu kumwumiza na kumwua Yesu
Yesu na wanafunziwake
"Watawatawanya kondoo wote wa kundi"
"Baada ya Mungu kunifufua"
Tazama 26:30
"Ninakuambia ukweli" Hiiinaongeza msisitizo wa kile kilichofuata baadaye
"Kabla jua halijachomoza."
Ndege ambaye huwika kwa sauti kubwa karibu na majira ya jua kuchomoza.
Sauti ambayo jogoo hufanya anapowika.
"utasema mara tatu kuwa wewe si mfuasi wangu"
Hii inaazisha habariy a Yesu akiomba Gethsemane
"na akawa na huzuni sana"
Hapa roho inamaanisha nafsi nzima ya mtu. "Nina huzuni sana"
"Najihisi kama nataka kufa"
Kwa makusudi kuweka uso chini ili upate kuomba.
Hili ni jina maarufu la Mungu ambalo huonesha uhusiano kati ya Mungu na Yesu.
Usemi huu, "kikombe hiki" huashiria mateso ambayo Yesu atapitia.
Hii inaweza kuelezwa kama sentensi iliyo kamilika. "Lakini usifanye kile nitakacho bali kile utakacho."
Yesu anamwambia Petro, kiwakilishai cha "hamku" ni cha wingi kinamaanisha Petro, Yakobo na Yohana.
"Ninasikitaka kuwa hamkuweza kukesha nami hata kwa saa moja"
"mtu yeyote asiwajaribu mtende dhambi"
Roho inamaanishahamu ya nafsi. Na "mwili" inamaanisha mwanadamu kamili. Yesu anamaanisha wanaweza kuwa na hamu ya kufanya mapenzi ya Mungu, Lakini kama wanadamu ni wadhaifu na wanaweza kushindwa
"Yesu alienda zake."
mpangilio kwa nafasi za namba
"Isipokuwa kukinywea kikombe hiki cha mateso."
Hili ni jina mashuhuri la Mungu ambalo hueleza uhusiano kati ya Mungu na Yesu.
"Walikuwa wakisinzia- sinzia sana."
"lazima nikinywee"
J"ambo hili" inamaanisha kikombe na kile kilichomo.
"lazima nikinywee" lazima nikinywee kikombe cha mateso"
"kile utakacho kifanyike"
"walikuwa na usingizi mzito"
Ninasikitika kwamba bado mmelala na kupumzika"
"Muda umefika."
"kuna mmoja wenu anamsaliti mwana wa Aadamu"
Neno "mikono" linamaanisha mamlaka ya kutawala. "Watu wenye dhambi."
"Zingatia kile ambacho nataka kuwaambia."
Hii inaazisha habari ya Yuda wakati alipomsaliti Yesu na viongozi wa dini wakamkamata
"Wakati Yesu alipokuwa bado akiongea."
vipande vikubwa vya miti vya kupigia watu
Neno "sasa" linaonesha kuanza kwa habari mpya. Mathayo anaeleza jinsi Yuda atakavyotoa ishara atakayotoa kwa nia ya kumsaliti.
"Akasema kwamba yule aliye mbusu ndiye waliyepaswa kumkamata."
"Yule nitakaye mbusu" au "Mtu ambaye nita mbusu."
Namna ya heshima ya kumsalimia mwalimu wa mtu mwingine.
"Yuda alimtokea Yesu."
"Akakutana naye kwa kumbusu."
"Kiwakilishi "waka.." kinamaanisha wale watu waliokuja na Yuda wakiwaa na marungu na mapanga pamoja na viongozi wa dini
Wakamkamata Yesu"
Neno "tazama" linatuvuta usikivu kwa ajili ya taarifa ya kugusa inayofuatia.
"aliyechukua upanga ili aue wengine"
"watakufa kwa njia ya upanga" au "mtu atawaua kwa upanga"
"Mlipaswa kujua kwamba ningeweza kumwita Baba yangu, na angenitumia majeshi zaidi ya kumi na mawili ya malaika."
hapa "mna" neno la umoja linlomaanisha yule mtu aliye na upanaga.
Hili ni jina mashuhuri la Mungu ambalo hueleza uhusiano kati ya Mungu na Yesu.
Neno "jeshi" ni neno la kijeshi linalojumuisha wanajeshi 6,000. Yesu anamaanisha kuwa Mungu angeweza kutuma malaika wa kutosha kuwazuia wale waliokuwa wanamkamata. Zaidi ya makundi 12 ya malaika.
"Lakini kama nkifanya hivyo, nisingeweza kutimiza,kile Mungu alichosema kwenye maandiko kitokee"
"Mnajua kwamba mimi siyo mnyang'anyi, hivyo ni makosa yenu kuniijia mkiwa na mapanga na marungu.
Vipande vikubwa vya miti migumu kwa ajili ya kupigia watu.hekaluni
Inaoneshakuwa Yesu hakuwa hekaluni. alikuwa kwenye korido la hekalu
"napenda kutimiza kile ambacho manabii waliandika kwenye maandiko"
Kujitenga naye au walijitenga naye.
Hii inaanzisha habari ya majaribu ya Yesu kwenye baraza la viongozi wa dini ya Wayahudi
"Petro alimfuata Yesu
Sehemu ya uwazi karibu na nyumba ya Kuhani Mkuu.
"Petro aliingia ndani"
Hili neno linaonesha kuazisha habari mpya kwenye simulizi. Matahyo anaanza kueleza habari mpya ya simulizi
kiwakilisi "wa" kinamaanisha wale wakuu wa Makuhani na wale wajumbe wa baraza.
"Wanaume wawili walikuja mbele" au "mashahidi wawili walitokeza mbele."
"Walishuhudia kwamba walimsikia Yesu akisema angeweza kuvunja hekalu la Mungu na kulijenga upya kwa muda wa siku tatu."
"Mtu huyu Yesu alisema."
"unajibu nini juu ya ushuhuda huu dhidi yako?"
Hili ni jina mashuhuri ambalo hueleza uhusiano kati ya Kristo na Mungu.
Tazama 16:13
Yesu anathibitisha kwamba yeye "ndiye Kristo, Mwana wa Mungu. "Kama ulivyosema, Mimi ndiye" au "Umekubaliana na ukweli huo"
Neno "wewe" ni la wingi. Yesu anamwambia kuhani mkuu na kwa wengine waliokuwapo hapo.
Maana zinaweza kuwa: 1) Watamuona Mwana wa Adamu baadaye kwa wakati ujao au 2) kwa "sasa" Yesu anamaanisha wakati wa kifo chake, kule kurudi kwake kutoka kwa wafu, na kupaa kwake kwenda mbinguni.
Yesu anatumia nafsi ya tatu kuongea juu yake
"Upande wa mkono wa kulia wa Mungu mwenyezi"
"Akisafiri kuja duniani katika mawingu ya mbinguni."
Kuchana mavazi ilikuwa ni ishara ya huzuni na hasira.
kwa kufuru hii, inamaanisha kuwa Yesu alikuwa akidai kuwa yeye ni sawa na Mungu
"hatuhitaji kusikia ushahidi mwingine"
kiwakilishi cha "mme" kikokatika wingi kinamaanisha wajumbe wa baraza.
Maana yaweza kuwa: "Kisha baadhi ya watu" au "Kisha askari"
Hili ni tendo la kufedhehesha.
Hapa "tutabirie" humaanisha, "tuambie kwa kutumia uwezo wa Mungu." Haimaanishi, "tuambie kitu gani kitatokea kwa wakati ujao."
Wale waliokuwa wakimpiga Yesu. Walimwita kwa kumdhihaki
Hii ni habri ya Petro akimkana mara tatu kuwa anamjua Yesu, kama vile Yesu alivypkuwa amaesema kuwa atafanya.
Matukio haya yanatokea sambamba na majaribu ya Yesu kwa viongozi wa dini
Hili neno linaonesha kuanza kwa habari nyingine. Mathayo anaanza kuwaambia sehemu ya habari.
Petro aliweza kufahamu alichosema mjakazi. Alitumia maneno haya kukana kwamba alikuwa pamoja na Yesu.
"Petro alipo..."
Uwazi katika ukuta kwenye ukumbi.
"akakana tena na kusema, 'Naapa simjui mtu huyu'"
"Mmoja wa hao waliokuwa pamoja na Yesu."
"Tunaweza kukuambia kwamba unatoka Galilaya kwa sababu unaongea kama Mgalilaya."
"Kujitakia laana iwe juu yake mwenyewe."
Tazama 26:33
Ptro alikumbuka kuwa Yesu alikuwa amemwambia kuwa kabla jogoo hajawika atakuwa amemkana mara tatu"
Yesu alisema Pasaka ilikuwa inawadia baada ya siku mbili.
Walikuwa wanapanga kumkamata Yesu kwa siri na kumuua.
Walikuwa wanaogopa kumwua Yesu wakati wa Pasaka kwa hofu ya watu wasije kuzua ghasia.
Wanafunzi walikasirika na walitaka kujua kwa nini mafuta yasingeuzwa na pesa zake wakapewa maskini.
Wanafunzi walikasirika na walitaka kujua kwa nini mafuta yasingeuzwa na pesa zake wakapewa maskini.
Yesu alisema mwanamke alimimina mafuta juu yake kwa ajili ya maziko yake.
Yuda alilipwa vipande thelathini vya fedha ili kumkabidhi Yesu katika mikono ya wakuu wa makuhani.
Yuda alilipwa vipande thelathini vya fedha ili kumkabidhi Yesu katika mikono ya wakuu wa makuhani.
Yesu alisema kuwa mmoja wa wanafunzi wake angemsaliti.
Yesu alisema kuwa ingekuwaafadhali kwa mtu atakayemasaliti kama asingezaliwa.
Yesu alisema "wewe wasema"
Yesu alisema, "Twaeni, mle. Huu ni mwili wangu."
Yesu alisema kuwa kile kikombe ni damu yake ya agano ambayo inamwagwa kwa ajili ya wengi kwamsamaha wa dhambi.
Yesu aliwaambia wanafunzi wake kwamba wote wangetawanyika usiku ule kwa sababu yake.
Yesu aliwote wangetawanyika usiku ule kwa sababu yake.waambia wanafunzi wake kwamba
Yesu alisema kwamba Petro angemkana Yesu usiku ule mara tatu kabla jogoo hajawika.
Yesu alisema kwamba Petro angemkana Yesu usiku ule mara tatu kabla jogoo hajawika.
Yesu aliwaambia kaeni hapa na kukusha naye.
Yesu aliwaambia kaeni hapa na kukusha naye.
Yesu aliomba kwamba, kama ingewezekana kikombe hiki kimwepuke.
Wanafunzi walikuwa wamesinzia Yesu aliporudi toka kwenye maombi
Yesu aliomba kwamba mapenzi ya Baba yatimie, kuliko mapenzi yake mwenyewe.
Yesu aliwaacha wanafunzi wake mara tatu naye akaenda kuomba
Yesu aliwaacha wanafunzi wake mara tatu naye akaenda kuomba
Wanafunzi walikuwa wamesinzia wakati Yesu akirudi kutoka maombini.
Yuda alimbusu kama ishara kwa kikosi kwamba Yesu ndiye wa kukamatwa.
Yuda alimbusu kama ishara kwa kikosi kwamba Yesu ndiye wa kukamatwa.
Mmoja wa wanafunzi wa Yesu alichomoa upanga wake na kumkata sikio mtumishi wa Kuhani Mkuu.
Mmoja wa wanafunzi wa Yesu alifuta upanga wake na kumkata sikio mtumishi wa kuhani mkuu.
Yesu alisema kuwa maandiko yalikuwa yanatimizwa kwa matukio hayo
Wanafunzi wote walimwacha na kukimbia
Walikuwa wakitafuta ushahidi wa uongo dhidi ya yake ili kumuua Yesu.
Kuhani mkuu alimwamuru Yesu asema kama yeye ndiye Kristo, Mwana wa Mungu
Yesu alisema "wewe wasema"
Yesu alimwambia kuhani mkuu atamwona Mwana wa Adamu amekaa mkono wa kuume wa mamlaka, na akija katika mawingu ya mbinguni.
Kuhani Mkuu alimshitaki Yesu kwa kosa la kukufuru.
Walimtemea Yesu usoni, wakampiga, na kumchapa makofi kwa mikono yao.
Petro alijibu kuwa hakumfahamu Yesu
Baada tu ya Petro kujibu mara ya tatu, jogoo aliwika.
Petro alijibu kuwa hakumfahamu Yesu
Petro alikumbuka kuwa Yesu alikuwa amesema kuwa, kabala jogoo hajawika atakuwa amemkana mara tatu..
1Muda wa asubuhi ulipofika, wakuu wote wa makuhani na wazee wa watu walikula njama dhidi ya Yesu wapate kumuua.2Walimfunga, walimwongoza, na kumfikisha kwa Liwali Pilato.3Kisha wakati Yuda, ambaye alikuwa amemsaliti, aliona kwamba Yesu amekwisha kuhukumiwa, alijuta na kurudisha vipande thelathini vya fedha kwa mkuu wa makuhani na wazee,4na akasema, “Nimefanya dhambi kwa kuisaliti damu isiyo na hatia.” Lakini wakajibu, “Inatuhusu nini sisi? Yaangalie hayo mwenyewe.”5Kisha alivirusha chini vile vipande vya fedha katika hekalu, na kuondoka zake na kujinyonga mwenyewe.6Mkuu wa makuhani alivichukua vile vipande vya fedha na kusema, “Si halali kuiweka fedha hii katika hazina, kwa sababu ni gharama ya damu.”7Walijadiliana kwa pamoja na fedha ikatumika kununulia shamba la mfinyazi la kuzika wageni.8Kwa sababu hii shamba hilo limekuwa likiitwa, “Shamba la damu” hadi leo hii.9Kisha lile neno lililokuwa limenenwa na nabii Yeremia lilitimia, kusema, “Walitwaa vipande thelathini vya fedha, gharama iliyopangwa na watu wa Israel kwa ajili yake,10na waliitumia kwa shamba la mfinyanzi, kama Bwana alivyokuwa amenielekeza.”11Sasa Yesu alisimama mbele ya Liwali, na Liwali akamwuliza, “Je! Wewe ni mfalme wa Wayahudi?” Yesu alimjibu, “Wewe wasema hivyo.”12Lakini wakati aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu chochote.13Kisha Pilato akamwambia, “Hujayasikia haya mashitaka yote dhidi yako?”14Lakini hakumjibu hata neno moja, hivyo Liwali alijawa na mshangao.15Sasa katika sikukuu ilikuwa desturi ya Liwali kumfungua mfungwa mmoja anayechaguliwa na umati.16Wakati huo walikuwa na mfungwa sugu jina lake Baraba.17Hivyo wakati walipokuwa wamekusanyika pamoja, Pilato aliwauliza, “Ni nani mnataka tumfungue kwa ajili yenu?” Baraba au Yesu anayeitwa Kristo?”18Kwa sababu alijua kwamba wamekwisha kumkamata kwa sababu ya chuki.19Wakati alipokuwa akiketi kwenye kiti chake cha hukumu, mke wake alimtumia neno na kusema, “Usitende jambo lolote kwa mtu huyo asiye na hatia. Kwani nimeteswa mno hata leo katika ndoto kwa sababu yake.”20Ndipo wakuu wa makuhani na wazee waliwashawishi makutano wamwombe Baraba, na Yesu auawe.21Liwali aliwauliza, “Ni yupi kati ya wawili mnataka mimi nimwachie kwenu?” Walisema, “Baraba.”22Pilato akawaambia, “Nimtendee nini Yesu anayeitwa Kristo?” Wote wakajibu, “Msulibishe”23Naye akasema, “Kwa nini, ni kosa gani ametenda?” Lakini walizidi kupaza sauti hata juu mno, “Msulibishe.”24Hivyo wakati Pilato alipoona hawezi kufanya lolote, lakini badala yake vurugu zilikuwa zimeanza, alitwaa maji akanawa mikono yake mbele ya umati, na kusema, “Mimi sina hatia juu ya damu ya mtu huyu asiye na hatia. Yaangalieni haya wenyewe.”25Watu wote wakasema, “Damu yake iwe juu yetu na watoto wetu.”26Kisha akamfungulia Baraba kwao, lakini alimpiga mijeredi Yesu na kumkabidhi kwao kwenda kusulibiwa.27Kisha askari wa Liwali wakamchukua Yesu mpaka Praitorio na kundi kubwa la maaskari wote wakakusanyishwa.28Wakamvua nguo zake na kumvika kanzu ya rangi nyekundu.29Kisha wakatengeneza taji ya miiba na kuiweka juu ya kichwa chake, na walimwekea mwanzi katika mkono wake wa kuume. Walipiga magoti mbele yake na kumkejeli, wakisema, “Salamu, Mfalme wa Wayahudi?”30Na walimtemea mate, na walitwaa mwanzi na kumpiga kichwani.31Wakati walipokuwa wakimkejeli, walimvua ile kanzu na kumvika nguo zake, na kumwongoza kwenda kumsulibisha.32Walipotoka nje, walimwona mtu kutoka Krene jina lake Simeoni, ambaye walimlazimisha kwenda nao ili apate kuubeba msalaba wake.33Walipofika mahali paitwapo Galigotha, maana yake, ‘Eneo la fuvu la Kichwa.’34Walimpa siki iliyochanganywa na nyongo anywe. Lakini alipoionja, hakuweza kuinywa.35Wakati walipokuwa wamemsulubisha, waligawana mavazi yake kwa kupiga kura.36Na waliketi na kumwangalia.37Juu ya kichwa chake waliweka mashitaka dhidi yake yakisomeka, “Huyu ni Yesu, mfalme wa Wayahudi.”38Wanyang'anyi wawili walisulubiwa pamoja naye, mmoja upande wa kulia wake na mwingine wa kushoto.39Wale waliokuwa wakipita walimdhihaki, wakitikisa vichwa vyao40na kusema, “Wewe uliyekuwa unataka kuliharibu hekalu na kulijenga katika siku tatu, jiokoe mwenyewe! Kama ni Mwana wa Mungu, shuka chini utoke msalabani!”41Katika hali ile ile wakuu wa makuhani walikuwa wakimkashifu, pamoja na waandishi na wazee, na kusema,42“Aliokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe. Yeye ni Mfalme wa Wayahudi. Na ashuke chini toka msalabani, ndipo tutakapomwamini.43Alimtumaini Mungu. Acha Mungu amwokoe sasa kama anataka, kwa sababu alisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu.’”44Na wale wanyang'anyi waliokuwa wamesulubiwa pamoja naye pia walisema maneno ya kumdhihaki.45Sasa kutoka saa sita kulikuwa na giza katika nchi yote hadi saa tisa.46Ilipofika saa tisa, Yesu akalia kwa sauti kuu, “Eloi, Eloi, lama thabakithan?” akimaanisha, “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”47Wakati huo baadhi yao waliokuwa wamesimama pale walisikia, wakasema, “Anamwita Eliya.”48Mara moja mmoja wao alikimbia kuchukua sifongo na kuijaza kinywaji kichungu, akaiweka juu ya mti na kumpa apate kunywa.49Nao waliosalia wakasema, “Mwacheni peke yake, acheni tuone kama Eliya atakuja kumwokoa.”50Kisha Yesu akalia tena kwa sauti kuu na akaitoa roho yake.51Tazama, Pazia la hekalu lilipasuka sehemu mbili kutokea juu hadi chini. Na ardhi ikatetemeka na miamba ikapasuka vipande.52Makaburi yalifunguka, na miili ya watakatifu wengi waliokuwa wamelala usingizi walifufuliwa.53Walitoka kwenye makaburi baada ya ufufuo wake, waliingia mji mtakatifu, na wakaonekana na wengi.54Basi yule akida na wale ambao walikuwa wakimtazama Yesu waliona tetemeko na mambo yaliyokuwa yakitokea, walijawa na woga sana na kusema, “Kweli huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”55Wanawake wengi waliokuwa wakimfuata Yesu kutoka Galilaya ili kumhudumia walikuwa pale wakitazama kutoka kwa mbali.56Miongini mwao walikuwa Mariamu Magdarena, Mariamu mama yake Yakobo na Joseph, na mama wa watoto wa Zebedayo57Ilipofika jioni, alikuja mtu tajiri kutoka Arimathayo, aliyeitwa Yusufu, ambaye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.58Alimwendea Pilato na kuuomba mwili wa Yesu. Kisha Pilato aliagiza apate kupewa.59Yusufu aliuchukua mwili akaufunga na sanda ya sufi safi,60na akaulaza katika kaburi jipya lake alilokuwa amelichonga mwambani. Kisha akavingirisha jiwe kubwa likafunika mlango wa kaburi na akaenda zake.61Mariamu Magdalena na Mariamu mwingine walikuwa pale, wamekaa kuelekea kaburi.62Siku iliyofuata ambayo ilikuwa siku baada ya maandalio, wakuu wa makuhani na Mafarisayo walikusanyika pamoja kwa Pilato.63Wakamwambia, “Bwana, tunakumbuka kuwa wakati yule mdanganyifu alipokuwa hai, alisema, ‘Baada ya siku tatu atafufuka tena.’64Kwahiyo, agiza kwamba kaburi lilindwe salama mpaka siku ya tatu. Vinginevyo, wanafunzi wake wanaweza kuja kumwiba na kusema kwa watu, ‘Amefufuka kutoka kwa wafu.’ Na udanganyifu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa kwanza.”65Pilato akawaambia, “Chukueni walinzi. Nendeni mkafanye hali ya usalama kama muwezavyo.”66Hivyo walikwenda na kufanya kaburi kuwa salama, jiwe liligongwa mhuri na kuweka walinzi.
Wayahudi walikuwa chini ya utawala wa Ufalme wa Kirumi, na Warumi hawakuwaruhusu watoe uhai wa mhalifu yeyote bila kupata ruhusa kwanza. Kwa hivyo viongozi wa Kiyahudi walimuomba Pontio Pilato athibitishe hukumu yao juu ya Yesu. Pilato alijaribu kuepuka kuthibitisha uamuzi wao. Alijaribu kuwafanya viongozi wa Kiyahudi kuchagua kati ya kumkomboa Yesu au mfungwa mbaya sana aliyeitwa Baraba.
Kaburi ambamo Yesu alizikwa (tazama: Mathayo 27:59-60) ilikuwa ni aina ya kaburi ambamo Wayahudi tajiri walizikwa. Ilikuwa na chumba halisi ambacho kilichombwa kwenye mwamba, ambapo miili ilikuwa imefungwa na kuwekwa kwenye miamba ilivyokuwa kwenye kuta. Baadaye, wakati miili imeharibika na kubakia mifupa iliyo wazi, mifupa hiyo ilikusanywa na kuingizwa kwenye mitungi maalum inayoitwa mabasi. Makaburi hayo yalifungwa na mwamba mmoja mkubwa wa kutosha kuufunga mlango. Mwamba huu ulikuwa umevingirwa au kuwekwa mahali pa mlango mwa kaburi.
Kifungu hiki, kinachopatikana katika Mathayo 27:29, ni mfano wa kinaya. Katika takwimu hii ya matamshi, kitu kinasemwa ili kuashiria kitu kingine, mara nyingi maana yake ikiwa ni kinyume. Tamko "Shikamoo" ilikuwa salamu iliyotumiwa na watu nyakati maalum, mara nyingi mbele ya wafalme na malkia. Hata hivyo, askari waliomdhihaki Yesu hawakutaka kumheshimu.
Hii inaanzisha kujariwa kwa Yesu mbele ya Pilato
neno linamaanisha kuazisha habari mpyakataika simulizi. Matahyo anaanza kueleza habari mpya katika sehemu hii
Viongozi wa Wayahudi walikuwa wakipanga jinsi ya kuwashawishi viongozi wa Rumi jinsi ya kumuua Yesu
"walimkabidhi" au "walimpeleka"
Mwanadishi amekoma kueleza habari ya kuhojiwa kwa Yesu na anaeleza jinsi Yuda alivyojiua
Tukio hili limeanza baada ya Yesu kuhojiwa mbele ya baraza la viongozi wa Wayahudi, lakinni hatujui kama hii ilitokea baada au kabla ya mahojiano ya Yesu kwa Pilato
Kama lugha yako ina namna ya kuonesha habari mpya inapoanza, unaweza kuitumia hapa.
"Viongozi wa Wayahudi wameshamhukumu Yesu"
Tazam 26:14
"mtu ambaye hakustahili kufa"
"hilo siyo tatizo letu" au "hilo ni tatizo lako"
Hii inamaanisha 1) alivitupa vile vipande vya fedha akiwa kwenye korido la hekalu, au 2) alikuwa amesimama kwenye korido la hekalu na akavitupa vile vipande vya fedha hekaluni.
"Sheria zetu hazituruhusu kuiweka hii"
"kuiweka fedha hii"
ahaili ni eneo ambalo waliweka ile fedha waliyotumia kwa mahitaji ya hekaluni nakwa makuhani.
Hii ni nahau inayomaanisha pesa i;iyotumika kumlipa mtu aliyeua mtu. "Pesa iliyolipwa kwa ajili ya kuuawa kwa mtu"
Hili n ishamba ambalo lilikuwa limenunuliwa kwa ajili ya kuwazikia wageni waliofia Yerusalemu
"watu huliita shamba hilo"
Hadi wakati ambao Mathayo alikuwa anaandika kitabu hiki.
Mwandishi ananukuu toka maandiko ya Agano Jipya kuonesha kuwa kujinyonga kwa Yuda kulikuwa kutimiza unabii
"Hili liltimiza unabii ambao nabii Yeremia alisema"
"Gharama ambayo watu wa Isrel walimpngia"
Hii inamaanisha baadhi ya watu wa Isrel waliolipa ili Yesu auawe. "baadhi ya watu wa Israel" au "viongozi wa Israel"
kiwakilishi "ni" kinamaanisha Yeremia
Ni habari inayoanzi 27:1
Kama lugha yako ina maneno yanyotumika kuendeleza mazungumzo baada ya pumziko la hadithi kubwa, waweza kuyatumia hapa
"Pilato"
Hii ni nahau ambayo Yesu anatumia kumaanisha "ndiyo" lenye lengo lakumaanisha kutoweka wazi alichokuwa anasema "wewe ndiye unayesema" au "unaonesha kukiri"
"Lakini wakati wakuu wa makuhani na wazee walipomshitaki"
Pilatoanauliza swali kwa sababu anashangazwa na ukimya wa Yewsu. "Ninashangazwa kwamba huwajibu hawa watu wanokushitaki kwa kutenda mabaya"
"neno moja; hii ilimshangaza sana liwali"
Hili ni neno linalotumika kuosha mwanzo wa habari kuu ili kwamba mwandishi aweze kutoa taarifa za kumsaidia msomaji kinachotokea kuanzia 27:17
Hii ni sikuu ya kusherehekea Pasaka
"mfungwa ambaye umati utamchagua"
"kulikuwa na funwa sugu"
anayejulikan vizuri kwa kutenda makosa makubwa
"umati ulikuwa umekusanyika"
ambaye watu baadhi humwita Kristo
viongozi wa Wayahudi walikuwa wamemleta Yesu kwake. "walifanya haya ili kwamba Pilato amhukumu Yesu.
"Pilato alopokuwa ameketi"
"Kuketi kwenye kiti cha hakimu." Hapa ndipo hakimu huketi anapokuwa akifanya maamuzi.
"neno" inamaanisha ujumbe. "alituma ujumbe"
"Nimeteseka san leo"
Neno "ndipo" limetumika kumaanisha mwanzo wa habari. Yesu anaeleza kwa nini umati ulimchagua Baraba.
Askari wa Rumi wamuue Yesu"
"aliuliza umati"
"ambaye watu baadhi humwita Kristo"
"ambalo Yesu ametenda"
"walipiga kelele"
Pilato alifanya hivi kama ishara ya kuwa yeye hawajibiki kwa kifo cha Yesu
"damu" inamaanisha damu ya mtu "kifo"
"huu ni wajibu wenu"
damu inamaanisha kifo cha mtu. Kirqai cha "iwe juu yetu na watoto wetu" ni nahau inayomaanisha kuwa wanakubali kuajibika kwa kile kinachotokea. "Ndiyo! Sisi na wa watoto wetu tutaajibika kwa kifo cha Yesu"
Maaskari wa Pilato walimpiga mijeredi Yesu.
kumpiga mtu kwa kutumia mjeredi
"na Pilato akaamuru Yesu asulibiwe"
Hii inaanzisha habari ya kusulibiwa kwa Yesu
"kikosi cha maaskari
"kumvulisha nguo"
"nyekundu yenye mng'ao
"taji iliyotengenezwa kwa matawi ya miiba" au "taji ilitengenezwa ka matawi yalyo na miiba"
Walimpa Yesu ashikilie fimbo kuonesha kuwa wafalme hushilia fimboya enzi. walifanya hivi kumkejeli.
walisema hivi kumkejeliYesu. walikuwa wakimwita Yesu "mfalme, wa Wayahudi," lakini kwa hakika hawakuamini kuwa Yesu alikuwa mfalme. Lakini walichokuwa wakisema kilikuwa kweli.
"maaskari walimtemea Yesu"
Hii inamaanisha Yesu na maaskari walitoka nje ya mji, "walipokuwa wakitoka nje ya Yerusalaem"
"maaskari walimwona mtu"
"amabye maaskari walimlazimisha kwenda naye ili kwamba abebe msalaba wa Yesu"
"eneo ambalo watu waliliita Golgotha"
"walimpa siki, ambayo walikuwa wameichanganya na nyongo"
kinwaji kichungu cha njano ambacho miili hukitumia kwa mmeng'enyo wa chakula
Hili ni vazi ambalo Yesu alikuwa akilivaa
"mashitaka" inamaanisha waliandika ili kuonesha sababu za kumsulibisha Yesu
Maskari walimsulibishaYesu pamoja na wanyanga'nyi wawili
walifanya hivi kumcheka Yesu
Kama wewe ni mwana wa Mungu thibitisha kwa "kushuka msalabani"
Hiki ni cheo cha muhimu amabcho kinaonesha uhusiano kati ya Kristo na Mwanawa Mungu
Maana yake yaweza kuwa 1) viongozi wa Wayahudi hawakuamini kuwa Yesu aliwaokoa wengine au kwamba anaweza kujiokoa wenyewe au 2) waliamini kuwa Yesu aliwaokoa wengine na sasa wanamcheka kwa sababu sasa hawezi kujiokoa mwenyewe
Viongozi wanamkejeli Yesu. Wanamwita "Mfalme wa Israel," Lakini kwa uhalisia hawaamini kuwa yeye ni Mfalme. "Anasema kuwa yeye ni mfalme wa Israel"
Viongozi wa Wayahudi wanaendelea kumkejeli Yesu
"Kwa sababu Yesu alisema kuwa yeye ni Mwana wa Mungu"
Hiki ni cheo cha maalumu cha Yesu ambacho kinaelezea uhusiano na Mungu
"Na wale wanyanga'nyi ambao maaskari waliwasulibisha pamoja na Yesu"
Neno hili limetumika kuonesha kuanza kwa habari nyingine. Mathayo anaanza kueleza sehemu mpya ya habari
Kuanzia mnamo adhuhuri ... kwa muda wa saa tatu" au "kuazia mnamo muda wa saa sita mchana ... hadi mnamo muda wa saa tisa mchana"
Neno "giza" ni nomino. "ilikuwa giza nchi yote"
"Yesu akaita" au "Yesu alipiga kelele"
Haya ndiyo maneno amabyo Yesu aliita kwa sauti kuu katika lugha ya.ke
inaweza kumaanisha 1)mmoja wa maaskari au 2) mmoja wale waliokuwa wamesimama karibu wakitazama
Huyu ni mnyama wa majini ambaye anapokuwa amevuliwa lile ganda lake liliweza kutumika kwa kuwekea vitu kama maji na kinywaji ambacho kinaweza kusukumwa nje.
"akampa Yeu
"akafa akiitoa roho yake kwa Mungu" au "akapumua pumzi ya mwisho"
Hii inaanza na matukio ambayo yalitokea baada ya Yesu kufa
Neno "tazama" linatutaka kuwa makini kwa taarifa za kushangaza zinazofuata.
"lile pazia la hekaluni lilipasuka katika sehamu mbili" au "Mungu alilifanya pazia la hekalu ligawanyike mara mbili"
"Mungu alifunua makaburi na kuifufua miili ya watu wengi wa Mungu waliokuwa wamekufa"
Hii ni tafsida yenye maana ya kufa "waliokuwa wamekufa"
Mpangilio wa matukio haya hauko wazi sana. Baada ya tetemeko la ardhi wakati Yesu alipokufa na makaburi kufunuka 1)Watu watakatifu walikuwa hai tena, kisha baada ya Yesu kufufuka, watakatifu wakauingi mji wa Yerusalemu na watu wengi waliwaona, au 2)Yesu alifufuka, kisha watakatifu nao wakafufuka na kuuingia mji ambapo watu wengi waliwaona.
Hili neno limetumika kuonesha mwanzo wa habari mpya. Mathayo anaaza kueleza sehemu nyingine ya habari
"na wale maaskari waliokuwa wakimtazama Yesu"
Hiki ni cheo maalumucha Yesu kinachoonesh uhusiano na Mungu
"Mama wa Yohana na Yakobo" au "mke wa Zebedayo"
Hii inaanza na habari ya kuzikwa Kwa Yessu
Hili jina la mji ulioko Israel
"Pilato aliwaagiza maaskari kumpa Yusufu mwili wa Yesu"
Nguo laini ya thamani
Inamaanisha kuwa Yusufu aliajiri watu ambao waliochonga hilo akaburi
Yawekana Yusufu alikuwa na watu wengine pale waliomsaidia kulivingirisha lile jiwe
"karibu na kaburi"
Hii ni siku ambayyo watu waliandaa mabo yao kwa sababu ya sabato
"walikutana na Pilato"
"wakati mdanganyifuYesu alipokuwa hai"
"alisema kwamba baada ya siku tatu atafufuka tena"
"waagize maaskari wako kulilinda kaburi"
siku ya 3
"kuiba mwili wake"
"na kuwaambia watu kwamba amefufuka kutoka wafu"
"kama watawadanganya watu kwa kusema hivyo, itakuwa vibaya kuliko alivyowadanganya watu kwa kusema kuwa yeye ni Kristo"
kwa Warumi Ilimaanisha maaskari wanne hadi kumi na sita
Inaweza kumaanisha 1) waliweka kamba karibu na jiwe na kuliunganishana kuta za lile jiwe katika pande zote za lango la kaburi au 2) waliweka mihuri katkati ya jiwe na kuta
"kuwaambia walinzi wasimame mahali ambapo wataweza kuwazuia watu ambao watadirika kufanya chochote kaburini.
Asubuhi walimpeleka Yesu kwa Liwali Pilato
Yesu alikiri kuisaliti damu isiyo hatia, akazirudisha zile fedha, akatoka nje, akajinyonga.
Yesu alikiri kuisaliti damu isiyo hatia, akazirudisha zile fedha, akatoka nje, akajinyonga.
Walinunua shamba la mfinyanzi kwa ajili ya maziko ya wageni.
Walinunua shamba la mfinyanzi kwa ajili ya maziko ya wageni
Matukio haya yanatimiza unabii wa Yeremia.
Matukio haya yanatimiza unabii wa Yeremia.
Pilato alimwuliza Yesu kama yeye alikuwa ni maflme wa Wayahudi, na Yesu alimjibu, "wewe wasema".
Yesu hakujibu hata neno moja.
Yesu hakujibu hata neno moja.
Pilato alitamani kumwachia huru Yesu. kwa mjibu watamaduni za Wayahudi.
Pilato alitamani kumwachia huru Yesu. kwa mjibu watamaduni za Wayahudi.
Alimwambia Pilato kuwa asimfanyechochote huyo mtu asiyekuwa na hatia.
Wkuu wa makuhani nawazee waliwashawishi makutano wamwombe baraba afunguliwe badala ya Yesu.
Makutano walipiga kelele wakiomba Yesu asulibiwe.
Pilato alinawa mikona yake, alikuwa hana hatia kwa damu ya mtu asiyekuwa na hatia, na kisha akamtoa Yesu kwa makutano.
Watu waalisema hivi, "damu yake na iwe juu yetu na watoto wetu".
Wale maaskari walimvalisha kanzu ya rangi nyekundu, na taji ya miiba kichwani mwake.
Wale maaskari walimvalisha kanzu ya rangi nyekundu, na taji ya miiba kichwani mwake.
Simon alilazimishwa kubeba msalaba wa Yesu.
Walimpeleka Golgotha, maana yake "fuvu la kichwa".
Maaskari walipiga kura ili kugawana mavazi yake na waliketi na kumwangalia".
Maaskari walipiga kura ili kugawana mavazi yake na waliketi na kumwangalia".
Waliandika, "HUYU NDIYE YESU MFALME WA WAYAHUDI".
Wanyang'anyi wawili walisulibuwa pamoja na Yesu, mmoja upande wa kushoto na mwingine upande wa kulia.
Wote walimtaka Yesu ajiokoe nakushuka msalabani?
Giza lilikuja juuya dunia kuanzia saa sita mpaka saa tisa.
"Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?"
Yesu aliitoa nafsi yake.
Lile pazia la hekalu lilipasuka sehemu mbili kutoka juu hadi chini baada ya Yesu kufa.
Watakatifu wengi aliokuwa wamelala usingizi walifufuka nao wakawatokea wengi baada ya Yesu kufa.
Watakatifu wengi aliokuwa wamelala usingizi walifufuka nao wakawatokea wengi baada ya Yesu kufa.
Yule akida alishuhudia kuwa, "Hakika huyu alikuwa mwana wa Mungu".
Mwanafunzi tajiri wa Yesu, Yusufu, alimwomba Yesu mwili wa Yesu, aliufunga sanda ya sufi, na kuulaza kwenye kaburi lake jipya.
Mwanafunzi tajirialimwomba Yesu mwili wa Yesu, aliuzonga kwenye sanda ya kitani, na kuulaza kwenye kaburi lake jipya. wa Yesu, Yusufu,
Jiwe kubwa liliwekwa kwenye mlango wa lile kaburi ambamo mwili wa Yesu ulikuwa umelazwa.
Wakuuwa makuhani na Mafarisayo walitaka kuhakikisha kuwa kaburi la Yesu liko salama ili mtu asije akauiba mwili wa Yesu.
Wakuuwa makuhani na Mafarisayo walitaka kuhakikisha kuwa kaburi la Yesu liko salama ili mtu asije akauiba mwili wa Yesu.
Pilato aliwaruhusu waweke mhuri kaburini na kulilinda.
Pilato aliwaruhusu waweke mhuri kaburini na kulilinda.
1Baadaye jioni siku ya Sabato, jua lilipokuwa likichwa kuelekea siku ya kwanza ya juma, Mariamu magadalena, na yule Mariam mwingine walikuja kuliona kaburi.2Tazama kulikuwa na tetemeko kubwa, kwa sababu malaika wa Bwana alishuka na kulivingirisha lile jiwe, kisha akalikalia.3Sura yake ilikuwa kama ya umeme, na mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji.4Wale walinzi walijawa na hofu na kuwa kama wafu.5Yule malaika akawafafanulia wale wanawake akisema, “Msiogope kwa maana najua kuwa mnamtafuta Yesu, aliyesulubiwa.6Hayupo hapa, lakini amefufuka kama alivyowaambia. Njooni muone mahali ambapo Bwana alilala.7Nendeni haraka mkawaambie wanafunzi wake, ‘Amefufuka toka wafu, tazama amewatangulia Galilaya. Huko ndiko mtamwona.’ Tazama mimi nimewaambia.”8Wale wanawake waliondoka pale kaburini haraka wakiwa na hofu na furaha kubwa, na wakakimbia kuwaambia wanafunzi wake.9Tazama Yesu akakutana nao na kusema, “Salamu.” Wale wanawake walikuja na kushika miguu yake, na kisha wakamwabudu.10Kisha Yesu akawaambia, “Msiogope, nendeni mkawaambie ndugu zangu watangulie Galilaya. Huko wataniona.”11Wakati wale wanawake walipokuwa wakienda, tazama baadhi ya walinzi walienda mjini na kuwaambia wakuu wa makuhani mambo yote yaliyokuwa yametokea.12Nao makuhani walipokuwa wamekutana na wazee na kulijadili jambo hilo pamoja nao, walitoa kiasi kikubwa cha pesa kwa wale askari13na kuwaambia, “Waambieni wengine kuwa, ‘Wanafunzi wa Yesu walikuja usiku wakauiba mwili wa Yesu wakati sisi tulipokuwa tumelala.’14Kama taarifa hii itamfikia Liwali, sisi tutamshawishi na kuwaondoleeni ninyi mashaka yote.”15Kwa hiyo wale askari wakazichukua zile pesa na kufanya kama walivyokuwa wameelekezwa. Habari hii ikaenea sana kwa Wayahudi na imekuwa hivyo hadi leo.16Lakini wale mitume kumi na mmoja walienda Galilaya, kwenye ule mlima aliokuwa amewaelekeza.17Nao walipomwona, walimwabudu. Lakini baadhi yao waliona shaka.18Yesu akaja kwao akawambia akisema, “Nimepewa mamlaka yote duniani na mbinguni.19Kwa hiyo enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi. Wabatizeni katika jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtatkatifu.20Wafundisheni kuyatii mambo yote niliyowaagiza, na tazama, mimi niko pamoja nanyi daima, hata mpaka mwisho wa dunia.
Aya mbili za mwisho (Mathayo 28:19-20) zinajulikana kama "Tume Kubwa" kwa sababu zina amri muhimu sana iliyotolewa kwa Wakristo wote. Wakristo wanapaswa "wafanye wanafunzi" kwa kwenda kwa watu, kuwapa injili na kuwafundisha kuishi kama Wakristo.
Mathayo, Marko, Luka, na Yohana wote waliandika juu ya malaika waliovalia nguo nyeupe wakiwa pamoja na wanawake kwa kaburi la Yesu. Waandishi wawili kati yao waliwaita wanaume, lakini ni kwa sababu tu malaika walikuwa katika hali ya kibinadamu. Waandishi wawili waliandika kuhusu malaika wawili, lakini waandishi wengine wawili waliandika juu ya moja tu. Ni bora kutafsiri kila moja ya vifungu hivi kama inavyoonekana katika ULB bila kujaribu kufanya vifungu vyote kufanana. (Angalia: Mathayo 28:1-2, Marko 16: 5 na Luka 24: 4 na Yohana 20:12)
Hii ni habari ya ufufuo wa Yesu kutoka wafu
Baada ya Sabato kuisha, jua lilipokuwa likichomoza Jumapili asubuhi"
Hili ni nenolinaloonesha kuanza kwa habari mpya. Mathayo anaanza kueleza sehemu mpya ya habari hii
Huyu ni Mariamu mama wa Yakobo na Yusufu Tazma (27:54)
Neno "tazama" linatutahadharisha kuwa tayari kwa ajili ya taarifa kushanagaza ambazo zinafuata. Lugha yako inaweza kuwa namna ya kulisema hili.
Yaweza kumaanisha yafatayo 1) tetemeko lilitokea kwa sababu alishuka na kulivingirisha lile jiwe au 2) matukio yote haya yalitokea kwa wakati mmoja.
kutetemeka ghafla kwa ardhi
"Sura ya malaika"
"ilikuwa inang'aa kama ya umeme"
"mavazi yake yalikuwa meupe sana kama theluji"
Huu ni msemo unaomaanisha kuwa wale maaskari walianguka chini na hawakuweza hata kutikisika. "na walianguka chini na kulala pale kama watu waliokufa"
"Mariamu Magadalena na yule Mariamu mwingine"
"yule ambaye watu na maaskari walimsulibisha" au "yula ambaye walimsulibisha"
kirai cha "toka wafu" kinamaanisha eneo ambalo roho za wale waliokufa huenda. 'Lakini amefufuka"
waambieni wanafunzi wake kuwa amefufuka wafu na kwamba Yesu amewatangulia kwenda Galilaya ambako mtamwona"
kiwakilishi cha "mta" ni cha wingi. kinamaanisha wale wanawake na wanafunzi
kiwakilishi "wa" ni cha wingi. kinamaanisha wale wanawake
"Mariamu Magedalena na Mariamu yule mwingine"
neno "Tazama" linatuandaa kusikiliza taarifa zinazofuata. Lugha yako yaweza kuwa namfumo wa kulisema hili.
Hii ni salamu ya kawaida
"walipiga magoti na kugusa miguu yake"
Hii inamaanisha wanafunzi wa Yesu.
Hii inaanza kwa habari ya mwitikio wa viongozi wa dini waliposikia habari ya kufufuka kwa Yesu
Hili neno linaonesha mwanzo wa habari kuu. Mathayo anaanza kusimuliasehemu ya habari
Inamaanisha Mariamu Magadelena na yula Mariamu mwingine
Hii inaonesha mwanzo wa tukio lingine katika habari kuu. Inaweza kujumuisha watu tofauti katika matukio yalitangulia. Lugha yako inaweza kuwa na namna ya kulifanya hilo.
"walipanga mpango wao wenyewe." Makuhani na wazee waliamua kuwapa zile fedha wale maaskari
Wambieni wengine kuwa wanafunzi wa Yesu waikuja ... wakati mlipokuwa mmelala"
"Kama liwali atasikia haya kuwa mlikuwa mmesinzia wakati wanafunzi wa Yesu walipouchukua mwili"
"Pilato"
"msihuzunike. tutongea naye ili asiwaadhibu"
"walifanya kile ambacho makuhani waliwaambia kufanya"
"Wayahudi wengi waliisikia habari hii na wanaeendelea kuwaambia wengine hadi leo"
Hii inamaanisha wakati Mathayo alipokuwa akiandika kitabu.
Hii inaanzisha habari ya Yesu kukutana na wanafunzi wake
Maana zake zaweza kuwa 1) wote walimwabudu Yesu ingawa baadhi yao waliona shaka au) Baadhi yao walimwabudu Yesu, lakini wengine hawakumwabudu kwa sababu waliona shaka
"Wengine wlions shaka kuwa ni kweli yeye ndiye aliyekuwa Yesu na kwamba amefufuka
"Baba yangu amaenipa mamlaka yote"
"Mbingini" na "duniani"zimetumika pamoja kumaanisha kila kitu na kila mmoja duniani na mbinguni.
Hapa "mataifa" inamaanisha watu. "kwa watu wote kwa kila taifa"
Hapa "jina" linamaanisha mamlaka. 'kwa mamlaka"
hIvi ni vyeo maalumu vinavyoonesha uhusiano wa Yesu na Mungu.
"Sikilizeni" au "iweni tayari"
"mpaka mwisho wa nyakati" au "mpaka mwisho wa ulimwengu"
Jua lilipokuwa likichwa kuelekea siku ya kwanza ya Juma, walienda kwenye kaburi la Yesu.
Malaika wa Bwana alishuka na kulivingirisha lile jiwe.
Wale walinzi waloishikwa na hofu wakawa kama wafu walipomwona malaika.
Malaika alisema kuwa Yesu alikuwa amefufuka naye alikuwa anawatangulia kwenda Galilaya
Malaika alisema kuwa Yesu alikuwa amefufuka naye alikuwa anawatangulia kwenda Galilaya
Wale wanawake walikutana na Yesu na kumshikilia miguu yake na kisha kumwabudu.
Wale wanawake walikutana na Yesu na kumshikilia miguu yake na kisha kumwabudu.
Wakuu wa Makuhani waliwalipa wale askari kiasi kikubwa cha pesa na kuwaambia waseme kuwa wanafunzi wa Yesu waliuiba mwili wa Yesu
Wakuu wa Makuhani waliwalipa wale askari kiasi kikubwa cha pesa na kuwaambia waseme kuwa wanafunzi wa Yesu waliuiba mwili wa Yesu
Wale wanafunzi walimwabudu Yesu, japo wengine waliona shaka.
Yesu alisema kuwa alikuwa amepewa mamlka yote yaliyo mbinguni na duniani.
Yesu aliwaamuru wanafunzi wake kwenda na kuwafanya watu kuwa wanafunzi wake na kuwabatiza.
Yesu aliwaambia wanafunzi wake kubatiza katika jina la Baba na la mwana na la Roho mtakatifu.
Yesu aliwaamuru wanafunzi wake kuwafundisha mataifa kutii mambo yote aliyoamuru.
Yesu aliahidi kuwa nao mpaka mwisho wa Ulimwengu
Abiya ni jina la watu mbalimbali katika agano la kale. Wafuatao ni watu hao:
Abiya lilikuwa jina la Mfalme wa Yuda aliyetawala tangu 915-913 BC. Alikuwa mtoto wa mfalme Rehoboamu. Walikuwepo watu wengine walioitwa Abiya katika agano la kale. Watoto wa Samweli Abiya na Yoeli walikuwa viongozi wa wana wa Israeli huko Belisheba. Kwa kuwa Abiya na kaka yake hawakuwa waaminifu watu walimuomba Samweli ateue mfalme mwingine wa kuwaongoza. Abiya mwingine ni yule aliyekuwa kwenye hekalu la kinabii wakati wa mfalme Daudi. Abiya lilikuwa jina la mtoto wa mfalme Yeroboamu. Abiya pia lilikuwa jina la kuhani mkuu aliyerudi na Zerubabeli Yerusalemu toka utumwani Babiloni.
Abramu alikuwa Mkalidayo toka mji wa Urialiyechaguliwa na Mungu kuwa baba wa Waisraeli. Mungu alibadilisha jina lake na kuwa "Abrahamu."
Adamu alikuwa binadamu wa kwanza aliyeumbwa na Mungu. Yeye na mke wake Hawa walitengenezwa kwa mfano wa Mungu.
"Adui" ni mtu au kundi lililo kinyume na mtu au kitu fulani.
Ahazi alikuwa mfalme muovu aliyetawala ufalme wa Yuda toka 732-716 BC. Hii ilikuwa yapata miaka 140 kabla ya wakati ambao wana wa Israeli na Yuda walichukuliwa mateka Babiloni.
Neno "Amina" hutumika kusisitiza au kuweka mkazo jambo ambalo mtu amesema. Mara nyingi hutumika mwisho wa sala. Mara nyingine hutafsiriwa kama "kweli."
"Waamoni" lilikuwa kundi la watu walioishi Kaanani. Walikuwa uzao wa Benyamini, aliyekuwa mtoto wa Lutu.
Andrea alikuwa mmoja kati ya wanafunzi kumi na wawili aliowachangua Yesu kuwa karibu naye ambao baadaye waliitwa Mitume.
"Angalia" inamaanisha kuwa kutazama kitu kwa ukaribu na kwa makini. "Mlinzi" ni mtu ambaye kazi yake ni kuulinda mji kwa kuangalia kwa makini vyote vinavyomzunguka kama kuna hatari yoyote kwa watu wa mji ule.
Asa alikuwa mfalme aliyetawana ufalme wa Yuda kwa miaka arobaini. toka 913-873 BC.
Babeli ulikuwa mji mkuu katika eneo lililoitwa Shinari kusini mwa Mesopotamia. Shinari ulikuja baadaye kuitwa Babiloni.
"Bahari ya Galilaya" ni jina la ziwa mashariki mwa Israeli. Katika Agano la Kale liliitwa "Bahari ya Shinerethi."
Baraba alikuwa mfungwa huko Yerusalemu wakati Yesu anakamatwa.
Boazi alikuwa mwisraeli aliyekuwa amemwoa Ruthi, babu wa mfalme Daudi, na babu wa Yesu Kristo.
Neno "Bwana" linamaanisha mtu anayemiliki na mwenye mamlaka juu ya watu wengine. Inapokuwa na herufi kubwa, ni jina linalomaanisha Mungu. (Noti hata hivyo inapotumika kama njia ya kumtambua mtu mwanzo mwa sentesi inaweza kuwa na herufi kubwa na kuwa na maana ya "mkuu.")
Katika Agano la Kale, msemo huu pia unatumika maneno kama, "Bwana Mungu Mkuu" au "Bwana Yahwe" au "Yahwe Bwana wetu." Katika Agano Jipya, mitume walitumia neno hili katika misemo kama, "Bwana Yesu" na "Bwana Yesu Kristo," illiyoonyesha kuwa Yesu ni Mungu. Neno "Bwana" katika Agano Jipya pia linatumika peke yake kama njia ya moja kwa moja ya kumtambua Mungu, hasa katika nukuu za kutoka Agano la Kale. Kwa mfano, maandishi ya Agano la Kale ya, "Amebarikiwa ajaye kwa jina la Yahwe" na Agano Jipya lina, "Amebarikiwa ajaye kwa jina la Bwana." Katika ULB na UDB, jina "Bwana" linatumika tu kutafsiri maneno halisi ya Kihebrania na Kigriki yanayomaanisha "Bwana." Halitumiki kama tafsiri ya jina la Mungu (Yahwe), kama inavyofanywa na tafsiri zingine.
Bwana harusi ni mtu anayemwoa bibi arusi katika sherehe ya harusi.
Dani alikuwa mwana wa tano wa Yakobo na alikuwa mmoja wa makabila kumi na mawili ya Israeli. Eneo lililokaliwa na kabila la Dani sehemu ya kaskazini ya Kaanani pia lilipatiwa jina hili.
Katika kipindi cha Abrahamu, kulikuwa na mji ulioitwa Dani uliokuwa magharibi mwa Yerusalemu.
Miaka ya baadaye, katika kipindi ambapo taifa la Israeli lilipoingia katika nchi ya ahadi, mji tofauti ulioitwa Dani ulikuwa kama maili 60 kaskazini mwa Yerusalemu.
Msemo "Wadani" una maana ya vizazi vya Dani, ambao pia ni wanajumuiya wa ukoo wake.
Danieli alikuwa nabii wa Kiisraeli ambaye alikuwa kijana mdogo aliyechukuliwa mateka na mfalme wa Babeli Nebukadreza mnamo wa 600 KK.
Huu ulikuwa wakati ambapo Waisraeli wengine wengi kutoka Yuda walishikwa mateka huko Babeli kwa miaka 70.
Danieli alipewa jina la Kibabeli la Belteshaza.
Danieli alikuwa kijana aliyeheshimika na mwenye haki aliyemtii Mungu.
Mungu alimwezesha Danieli kutafsiri ndoto kadhaa au maono kwa wafalme wa Babeli.
Kwa sababu ya uwezo huu na kwa sababu ya hulka yake ya heshima, Danieli alipewa nafasi ya juu ya uongozi katika ufalme wa Kibabeli.
Miaka mingi baadaye, maadui wa Danieli walimdanganya mfalme wa Babeli Dario kutunga sheria inayokataza kumwabudu mtu yeyote isipokuwa mfalme. Danieli aliendelea kuomba kwa Mungu, kwa hiyo alikamatwa na kutupwa katika tundu la simba. Lakini Mungu alimkomboa na hakudhuriwa kabisa.
Daudi alikuwa mfalme wa pili wa Israeli na alimpenda na kumtumikia Mungu. Alikuwa mwandishi mkuu wa kitabu cha Zaburi.
Daudi alipokuwa mvulana mdogo akichunga kondoo wa familia yake, Mungu alimchagua kuwa mfalme afuataye wa Israeli.
Daudi alikuwa mpiganaji hodari na aliongoza jeshi la Israeli katika vita dhidi ya maadui zake. Kumshinda kwake Goliati na Wafilisti kunajulikana sana.
Mfalme Sauli alijaribu kumuua Daudi, lakini Mungu alimlinda, na kumfanya awe mfalme baada ya kifo cha Sauli.
Daudi alitenda dhambi mbaya sana, lakini alitubu na Mungu alimsamehe.
Yesu, Masihi, anaitwa "Mwana wa Daudi" kwa sababu ni uzao wa Mfalme Daudi.
Eliakimu lilikuwa jina la wanamume wawili katika Agano la Kale.
Mwanamume mmoja aliyeitwa Eliakimu alikuwa msimamizi wa kasri chini ya Mfalme Hezekia.
Mwanamume mwingine aliyeitwa Eliakimu alikuwa mwana wa Mfalme Yosia. Alifanywa mfalme wa Yuda na farao wa Misri, Necho.
Necho alibadili jina la Eliakimu kuwa Yehoyakimu.
Eliya alikuwa mmoja wa manabii muhimu sana wa Yahwe. Eliya alitabiri katika wakati wa tawala za wafalme kadhaa wa Israeli au Yuda, akiwemo Mfalme Ahabu.
Mungu alifanya miujiza mingi kupitia Eliya, ikiwemo kumfufua mvulana mfu kurudi katika uhai.
Eliya alimkaripia Mfalme Ahabu kwa kuabudu mungu wa uongo Baali.
Aliwapa changamoto manabii wa Baali katika mtihani ambao ulithibitisha ya kwamba Yahwe ni Mungu mmoja wa kweli.
Katika mwisho wa maisha ya Eliya, Mungu alimchukua kimuujiza juu mbinguni angali bado yu hai.
Miaka mia moja baadaye, Eliya, pamoja na Musa, walijitokeza na Yesu juu ya mlima na waliongea pamoja juu ya kurudi, kuteseka na kufa kwa Yesu Yerusalemu.
Filipi ulikuwa mji muhimu na koloni la Rumi lililokuwa Makedonia kaskazini mwa Ugiriki ya kale.
Katika kanisa la kwanza huko Yerusalemu Filipo alikuwa mmoja wa viongozi saba waliochaguliwa ili kuwajali masikini, Wakristo wenye uhitaji hasa wajane.
Mtume Filipo alikuwa mmoja wa wanafunzi kumi na mbili wa Yesu alikuwa anatoka mji wa Bethsaida.
Galilaya ni eneo la kaskazini ya Israeli, kaskazini ya Samaria. "Mgalilaya" alikuwa mtu ambaye aliishi Galilaya.
Galilaya, Samaria, na Yudea ilikuwa miji mitatu ya msingi ya Israeli wakati wa Agano Jipya.
Galilaya imepakana upande wa mashariki na ziwa kubwa liitwalo "Ziwa la Galilaya".
Yesu alikua na kuishi katika mji wa Nazareti Galilaya.
Miujiza mingi na mafundisho ya Yesu yalifanyika katika eneo la Galilaya.
Gethsemane ilikuwa bustani ya mizeituni mashariki mwa Yerusalemu mbali ya bonde la Kidroni karibu na Mlima wa Mizeutuni.
Bustani ya Gethsemane ilikuwa sehemu ambapo Yesu na wafuasi wake walienda kuwa wenyewe na kupumzika, mbali na mikusanyiko.
Ilikuwa Gethsemane ambapo Yesu aliomba kwa huzuni kubwa, kabla ya kukamatwa pale na viongozi wa Kiyahudi.
Gomora ilikuwa mji katika bonde lenye rutuba, karibu na Sodoma ambapo mpwa wa Abrahamu Lutu alichagua kuishi.
Mahali haswa pa Gomora na Sodoma hapajulikani, lakina kuna viashiria ya kwamba inaweza kuwa mahali moja kwa moja kusini mwa Bahari ya Chumvi, karibu na Bonde la Sidimu.
Kulikuwa na wafalme wengi vitani katika eneo ambapo Sodoma na Gomora na ilikuwepo.
Familia ya Lutu ilipokamtwa katika ugomvi kati ya Sodoma na miji mingine, Abrahamu na wanamume wake waliwakomboa.
Sio muda baada ya hapo, Sodoma na Gomora ziliteketezwa na Mungu kwa sababu ya uovu wa watu walioishi pale.
Habili alikuwa mtoto wa Adamu na Hawa. Alikuwa ndogo wake na Kaini.
Habili alikuwa mfugaji.
Habili alitoa sadaka ya baadhi ya mifugo yake kwa Mungu.
Mungu alipendezwa na sadaka ya Habili.
Mtoto wa kwanza wa Adamu na Hawa, Kaini alimuua Habili.
Hamu ni mtoto wa pili kati ya wana watatu wa Nuhu. katika gharika kuu la kidunia ambalo liliigharikisha dunia yote, Hamu na ndugu zake pamoja na wake zao walikuwa pamoja na baba yao, Nuhu katika safina. Baada ya gharika, kulikuwa na tukio la Hamu kutomweshimu baba yake, Nuhu. Na matokeo yake, Nuhu alimlaani mtoto wa Hamu alilyeitwa Kanaani pamoja na uzao wake wote, ambao baadaye walijulikana kama Wakanaani.
Hili lilikuwa jina la mwanamke wa kwanza. Jina lake linamaanisha "uhai" au "kuishi".
Mungu alimuumba Hawa kutoka kwa ubavu ambao aliuchukua kutoka kwa Adamu.
Hawa aliumbwa kuwa "msaidizi" wa Adamu. Alikuja kando ya Adamu kumsaidia katika kazi ambayo Mungu aliwapa kufanya.
Hawa alijaribiwa na Shetani (kwa mfano wa nyoka) na alikuwa wa kwanza kufanya dhambi kwa kula tunda ambalo Mungu aliwaambia kutokula.
Herodia alikuwa ni mke wa Herode Antipa huko Uyahudi kipindi cha Yohana Mbatizaji. Herodia alikuwa mke halali wa kaka yake na Antipa, aliyeitwa Philipo, lakini baadaye aliolewa na Herodi Antipa kinyume na sheria. Yohana mbatizaji aliwakemea Herode na Herodia kwa sababu ya ndoa yao haramu. Na kwasababu hiyo, Yohana alifungwa gerezani na baadaye aliuawa kwa kukatwa kichwa.
Hezekia alikuwa ni mfalme wa 13 wa ufalme wa Yuda. Alikuwa ni mfalme aliyemtumaini Mungu na kumtii. Tofauti na baba yake, Ahazi aliyekuwa mfalme mwovu, Mfalme Hezekia alikuwa ni mfalme mzuri aliyeharibu maeneo yote ya ibada ya miungu katika Yuda. Wakati Hezekia alipougua na alipokuwa karibu kufa, alimwomba Mungu sana ili alinde na kuhifadhi maisha yake. Mungu alimponya na alimruhusu kuishi miaka 15 zaidi. Mungu alifanya muujiza kwa Hezekia kwa kurudisha muda nyuma. Mungu alijibu maombi ya Hezekia kwa kuwaokoa watu wake kutoka mikononi mwa Mfalme Senakaribu wa Siria, aliyekuwa akiwashambulia.
maneno haya "Kama ilivyoandikwa" au "kilichoandikwa" yametokea mara nyingi katika agano jipya na yameelezea amri au unabii ulioandikwa katika maandiko ya Kiebrania.
Isaka alikuwa mwana pekee wa Abrahamu na Sara. Mungu aliwaahidi kuwapa mwana wa kiume ingiwa walikuwa wazee sana.
Jina "Isaka" linamaanisha "kicheko." Mungu alipomuambia Abrahamu kuwa Sara atazaa mwana wa kiume, Abrahamu alicheka kwa sababu wote walikuwa wazee sana. Baada ya muda, Sara pia alicheka aliposikia taarifa hii. Lakini Mungu alitimiza ahadi yake na Isaka alizaliwa kwa Abrahamu na sara katika uzee wao. Mungu alimuambia Abrahamu kuwa agano alilofanya na Abrahamu itakuwa pia ya Isaka na vizazi vyake milele. Wakati Isaka alikuwa kijana, Mungu aliijaribu imani ya Abrahamu kwa kumuamuru kumtoa isaka kama sadaka. Mwana wa Isaka, Yakobo, alikuwa na wana kumi na mbili ambao uzao wao baadaye ukawa makabila kumi na mbili ya taifa la Israeli.
Isaya alikuwa nabii wa Mungu aliyetabiri wakati wa utawala wa wafalme wanne wa Yuda: Uzia, Yothamu, Ahazi, na Hezekia.
Aliishi Yerusalemu wakati Waashuri walipokuwa wakivamia mji, wakati wa utawala wa Hezekia. Kitabu cha Agano la Kale cha Isaya ni moja ya vitabu vikuu vya Biblia. Isaya aliandika unabii mwingi ulitokea wakati wa uhai wake. Isaya anajulikana zaidi kwa unabii alioandika kumhusu Masihi uliotimia miaka 700 baadaye wakati Yesu alipoishi duniani. Yesu na wanafunzi wake walinukuu utabiri wa Isaya kuwafundisha watu kuhusu Masihi.
Neno "Israeli" ni jina ambalo Mungu alimpa Yakobo. Linamaanisha, "anashindana na Mungu."
Uzao wa Yakobo walijulikana kama "watu wa Israeli," "taifa la Israeli" au "Waisraeli." Mungu aliunda agano lake na watu wa Israeli. Walikuwa watu wake aliowachagua. Taifa la Israeli liliundwa na makabila kumi na mbili. Mara baada ya mfalme Sulemani kufa, Israeli iligawanyika katika falme mbili: ufalme wa kusini, uliitwa "Yuda" na ufalme wa kaskazini, uliitwa "Israeli."
Jehanamu ni sehemu ya mwisho iliyo na maumivu na mateso yasiyokoma, mahali ambapo Mungu atamhukumu kila mmoja anayemwasi Yeye na kuukataa mpango wake wa kuwaokoa kupitia kwa sadaka ya Yesu. Pia inarejelewa kama 'ziwa la moto. Jehanamu au Kuzimu kunatajwa kama sehemu ya moto na mateso makali. Shetani na roho chafu zinazomfuata zitatupwa katika Jehanamu kwa ajli ya hukumu ya milele. Watu wasioamini sadaka ya Yesu kwa ajili ya ondoleo la dhambi zao, na wasiomtumaini Yeye, watahukumiwa Jehanamu milele
Mapendekezo ya tafsiri Maneno haya yanapaswa kutafsiriwa tofauti tofuauti kwasababu yanatokea tofauti katika muktadaha tofauti. Katika baadhi ya lugha haziwezi kutumia neno 'ziwa' kwa sababu kwao ziwa ni 'maji' Neno Jehanamu laweza kutafsiriwa kama 'sehemu ya mateso au sehemu yenye giza na maumivu' Maneno 'ziwa la moto' yanaweza pia kutafsiriwa kama 'bahari ya moto' au 'moto mkubwa.'
Neno "Kaisari" lilikuwa jina au jina la heshima lililotumika kwa watawala wengi wa Dola ya Rumi. Katika Biblia, hili neno linahusisha kwa tawala tatu tofauti tofauti.
Katika majina kama Kaisari Agustino au Tiberia Kaisari, "Kaisari" inaweza kutamkwa karibia na vile lugha ya taifa inavolitamka.
Kaisaria ulikuwa mji wa muhimu katika pwani ya Bahari ya Meditrania, kama 39 kilomita kusini mwa Mlima Karmeli Kaisaria Filipi ulikuwa mji unaoonyesha kusinimagharibi sehemu ya Israeli, karibu na Mlima Herimoni.
Katika Biblia neno 'kichwa' lilmetumika kama tamathali ya semi likiwa lina maana nyingi: Mara nyingi neno hili limetumika kurejelea hali ya kuwa na mamlaka juu ya watu , kwa mfano, "mmenifanya kichwa cha mataifa" Sentensi hiyo yaweza kutafsiriwa kuwa "mmenifanya kuwa mtawala" au "mmenipa mamlaka juu ya..." Yesu anaitwa 'kichwa cha kanisa.' Kama ambavyo kichwa cha mtu huongoza viungo vingine vya mwili, hivyo na Yesu huongoza na huelekeza viungo vingine vya mwili wake, yaani kanisa. Agano la Jipya linatufundisha kuwa mme ni "kichwa'' au mwenye mamlaka kwa mkewe. Amepewa wajibu wa kumwongoza na kumwelekeza mkewe na familia. Maneno yanayosema "wembe hautagusa kich chake" maana yake ni kwamba" hatakata au hatanyoa nywele zake. Neno 'kichwa' laweza pia kurejelea mwanzo au asili ya kitu fulani, mfano 'kichwa cha mtaa" Maneno kama "kichwa cha nafaka" hurejelea sehemu ya juu ya ngano au mche wa shayiri ambao una mbegu ndani yake. Mfano mwingine wa 'kichwa' ni pale unapotumika kuwakilisha mtu mzima. Mfano, 'kichwa cheupe' humrejelea mtu mzee au tunaposema ' kicha cha Yusufu, tunamaanisha Yusufu mwenyewe. Msemo unaosema 'acha damu yao iwe juu ya kichwa chake' humaanisha kuwa mtu yule anawajibika kwa vifo vyao na atapokea adhabu/hukumu yake.
Mapendekezo ya tafsiri Neno 'kichwa' laweza kutafsiriwa kama 'mamlaka' au 'mtu anayeongoza na kuelekeza' au 'mtu anayewajibika kwa..' kwa kutegemea na muktadha wenyewe. Maneno kama ' kichwa cha' hurejelea mtu mwenyewe mzima, na hivyo maneno hayo yaweza kutafsiriwa kwa kutumia jina la mtu husika. kwa mfano ''kichwa cha Yusufu'' ina maana ya 'Yusufu' Maelezo kama ' itakuwa juu ya kichwa chake' yanaweza kutafsiriwa kama " itakuwa juu yake'' au 'ataadhibiw'a kwa ajili ya' au 'atawajibika kwa ajili ya... Kwa kutegemea na muktadha wenyewe, maana zingine za neno kichwa zaweza kuwa "mwanzo' au "asili'' au ''chanzo'' au "mtawala" au ''juu ya''
Krene ulikuwa mji wa Kigiriki kaskazini mwa pwani ya Afrika kwa upande wa bahari ya Mediteraniani, moja kwa moja kusini mwa kisiwa cha Krene.
Masihi na Kristo inamaana ya mpakwa mafuta na inamuelezea Yesu mwana wa Mungu.
Katika Biblia Kuhani alikuwa mtu aliyechaguliwa kutoa sadaka ya kuteketezwa kwa Mungu kwa niaba ya watu wa Mungu. Ukuhani lilikuwa jina au masharti ya kuwa kuhani.
Pamoja na maana yake ya kawaida maji yaweza kuwelezea vyanzo vya maji kama vile bahari, mto au ziwa.
Malaika ni kiumbe chenye roho na chenye nguvu kilichoumbwa na Mungu. Malaika wanamtumikia Mungu kwa kufanya yale wanayoagizwa kuyafanya na Mungu. Malaika mkuu ni malaika anayewaongoza malaika wengine.
Malkia ni kiongozi mwanamke wa nchi fulani au mke wa mfalme.
Hawa walikuw wanaume watano kwa jina Manase katika Agano la Kale:
Mariamu alikuwa mwanamke mdogo aliye ishi katika mji wa Nazarethi aliye poswa kuolewa na Yusufu. Mungu alimchagua Mariamu kuwa mama wa Yesu Mesia, Mwana wa Mungu.
Mariamu Magdalena alikuwa miongoni mwa wanawake waliyo muamini Yesu na kumfuata katika huduma yake. Alijulikana kama kama Yesu aliye mponya kutoka kwa mapepo saba waliyo mtawala.
Msemo "mataifa" una maana ya mtu yeyote ambaye sio Myahudi. Watu wa mataifa ni watu ambao sio uzao wa Yakobo.
Katika Biblia, msemo "kutotahiriwa" pia hutumika kitamathali kumaanisha watu wa Mataifa kwa sababu wengi wao hawakutahiri watoto wao wa kiume kama Waisraeli walivyofanya.
Kwa sababu Mungu aliwachagua Wayahudi kuwa watu maalumu, walifikiria juu ya watu wa mataifa kama watu wa nje ambao wasingeweza kuwa watu wa Mungu.
Wayahudi pia waliitwa "Waisraeli" au "Waebrania" katika vipindi tofauti vya historia. Waliwajua wengine wote kama "watu wa Mataifa".
Watu wa mataifa pia inaweza kutafsiriwa kama "asiye Myahudi" au "asiye Muisraeli" (Agano la Kale).
Kitamaduni, Wayahudi hawakula na watu wa mataifa au kujihusishanao, ambapo mara ya kwanza ilisababisha matatizo miongoni mwa kanisa la kwanza.
Mathayo alikuwa mmoja wa wanaume kumi na mbili Yesu aliyo wachagua kuwa mitume wake. Alijulikana kama pia kama Lawi, mwana wa Alfayo.
Usemi, "Mfalme wa Wayahudi" ni jina linalomaanisha Yesu, Masihi.
Mara ya kwanza Biblia inaandika hili jina wakati linapotumika na wanaume wenye hekima waliosafiri kwenda Bethlehemu wakimtafuta mtoto aliye "Mfalme wa Wayahudi." Malaika alimfunulia Mariamu kuwa mwanaye, mzawa wa mfalme Daudi, atakuwa mfalme ambaye ufalme wake utadumu milele. Kabla Yesu hajasulibishwa, askari Wakirumi walimdhihaki Yesu kwa kumuita "Mfalme wa Wayahudi." JIna hili liliandikwa pia katika kipande cha mbao na kupigwa msumari juu ya msalaba wa Yesu. Yesu kweli ni Mfalme wa Wayahudi na mfalme wa viumbe vyote.
Mara nyingi katika Agano la Kale, wakati Mungu akijizungumzia, hutumia jina lake badala ya nomino kiwakilishi.
Kwa mfano, badala ya kusema, "Niheshimu mimi," husema "Mheshimu Yahwe." Kuiweka wazi kuwa ni Mungu anayejizungumzia, ULB kawaida hutafsiri hii kwa kuongezea nomino kiwakilishi kama, "Niheshimu mimi, Yahwe" au "Mimi, Yahwe ninasema." Kwa kuongeza nomino kiwakilishi "mimi", ULB inaashiria kwa msomaji kuwa Mungu ndiye anayezungumza.
Misri ni nchi katika sehemu ya kaskazini ya Afrika, kusini mashariki mwa nchi ya Kaanani. Mmisri ni mtu ambaye anatoka katika nchi ya Misri.
Katika miaka ya zamani, Misri ilikuwa nchi yenye nguvu na utajiri.
Misri ya zamani iligawanyika katika sehemu mbili, Misri ya Chini (sehemu ya kaskazini ambapo mto hutiririka chini kuelekea baharini) na Misri ya Juu (sehemu ya kusini). Katika Agano la Kale, sehemu hizi zinajulikana kama "Misri" na "Pathrosi" katika lugha ya maandishi asili.
Wakati mwingine ambapo kuna chakula kichache Kaanani, wakuu wa koo walisafiri kwenda Misri kununua chakula kwa ajili ya familia zao.
Kwa miaka mia moja hivi, Waisraeli walikuwa watumwa Misri.
Yusufu na Mariamu walishuka chini Misri na mtoto mdogo Yesu kutoroka kwa Herode Mkuu.
Mkuu ni mtoto wa kiume wa mfalme. Binti wa mfalme ni mtoto wa kike wa mfalme.
"Mkuu" ni kiongozi wa muhimu na mwenye nguvu sana katika kundi fulani.
Mlima wa Mizeituni ni mlima au kilima kikubwa karibu na mashariki mwa mji wa Yerusalemu. Una mita787 kwenda juu.
Neno 'mnafiki' humrejelea mtu ambaye hufanya mambo ili aonekane mwema, ingawa kwa siri hufanya mambo maovu. Neno 'unafiki' hurejelea tabia ambayo huwahadaa watu kwa kufikiri kuwa mtu huyo ni mwenye haki. Wanafiki wanapenda kuonekana wakiwa wanafanya mambo mazuri, hivyo watu hufikiri kuwa ni watu wazuri. Mara kwa mara watu wanafiki huwakosoa watu wengine kwa kufanya mambo yale yale ya dhambi ambayo wao wenyewe huyafanya. Yesu aliwaita Mafarisayo kuwa ni wanafiki kwasababu walifanya matendo ya kidini kama vile kuvaa aina fulani ya nguo na kula chakula fulani, lakini hawakuwa wema na wenye haki kwa watu. Mtu mnafiki huweka wazi makosa ya watu wengine, lakini yeye mwenyewe hakubali makosa yake.
Mapendekezo ya tafsiri Baadhi ya lugha huwa na maneno kama "sura mbili" ambayo hutumika kumrejelea mnafiki au matendo ya mnafiki. Namna nyingine ya kutafsiri neno mnafiki ni "mdanganyifu, mtu anayejifanya, mwongo,"
Katika Biblia, msemo "Mungu" una maana ya kiumbe wa milele ambaye aliumba ulimwengu bila chochote. Mungu alikuwepo kama Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu. Jina binafsi la Mungu ni "Yahwe".
Mungu mara zote alikuwepo; alikuwepo kabla ya kitu chochote kuwepo, na ataendelea kuwepo milele.
Yeye ni Mungu mmoja wa kweli na ana mamlaka juu ya kila kitu ulimwenguni.
Mungu ana haki timilifu, hekima isiyo na mwisho, mtakatifu, bila dhambi, wa haki, wa rehema, na upendo.
Ni Mungu wa kutunza agano, ambaye hutimiza ahadi zake daima.
Watu waliumvwa kumwabudu Mungu na ni yeye pekee wanaopaswa kumwabudu.
Mungu alifunua jina lake kama "Yahwe" ambayo ina maana ya "yeye ni" au "Mimi ni" au "Yule anayekuwepo daima".
Biblia pia hufundisha kuhusu "miungu" wa uongo ambao ni sanamu wasioishi ambao watu huabudu kwa makosa.
Musa alikuwa nabii na kiongozi wa watu wa Israeli kwa miaka 40.
Jina, "Mwana wa Adamu" lilitumika na Yesu akijieleza. Mara nyingi alitumia hili jina badala ya kusema "mimi."
Neno "Mwana wa Mungu la husu Yesu, Neno la Mungu aliye kuja duniani kama binadamu. Anajulikana kama "Mwana."
"Nabii ni mtu anayesema ujumbe wa Mungu kwa watu. Mwanamke anayefanya hivi anaitwa "nabii mwanamke."
Naftali alikuwa mwana wa sita wa Yakobo. Uzao wake uliunda kabila la Naftali, ambalo lilikuwa moja ya kabila la Israeli.
Ninawi ilikuwa mji mkuu wa Asyria. Mninawi alikuwa mtu aliye ishi Ninawi.
Nuhu alikuwa mwanaume aliye ishi miaka 4,000 iliyo pita, kipindi ambacho Mungu alipotuma garika duniani kuharibu watu waovu. Mungu alimwambia Nuhu ajenge meli kubwa ambayo yeye na familia yake waliweza kuishi wakati mafuriko yalipo funika dunia.
Istilahi 'nyumba' hutumika kama tamathali ya semi (mfano) katika Biblia. Mara nyingine hutumika kumaanisha 'kaya' kurejelea watu wanaoishi pamoja katika nyumba. Mara zote neno 'nyumba' humaanisha wazao au watoto au ndugu wengine. Mfano, nyumba ya Daudi huwa na maana ya uzao wa Daudi. Maneno kama 'nyumba ya Mungu' au 'nyumba ya Yahweh' huwa na maana ya hekalu au hema la kukutania au sehemu Mungu alipo. Katika Waebrania 3, "Nyumba ya Mungu" ni sitiari ikimaanisha Watu wa Mungu. Kifungu cha maneno ' nyumba ya Israeli" kwa ujumla huwa na maana ya taifa laote la Israeli au hasa hasa kwa makabila ya ufalme wa Kasikazini wa Israeli.
Mapendekezo ya tafsiri kwa kutegemeana na muktadha, neno, nyumba linaweza kuwa na maana ya 'kaya' ' watu, familia, uzao, hekalu au sehemu ya kukaa.'' "Nyumba ya Daudi' in maana ya ''ukoo wa Daudi, familia ya Daudi au uzao wa Daudi. "Nyumba ya Israeli' ina maana ya watu wa Israeli au wazao wa Israeli au waisraeli. 'Nyumba ya Yahweh' ina maana ya hekalu au sehemu ya kumwabudia Mungu.
"Pasaka " ni jina la sherehe ya kidini ambayo Wayahudi walisherehekea kila mwaka kukumbuka mi kwa namna gani Mungu aliwaokoa mababu zao Waisraeli toka utumwani Misri.
Katika Biblia pazia ni kitu kinene, chenye nyenzo nzito kinachotumika kutengenezea maskani na hekalu.
Petro alikuwa mmoja wa mitume wa Yesu. Alikuwa kiongozi wa muhimu katika kanisa la kwanza.
Pilato alikuwa kiongozi wa serikali ya Rumi katika Yudea aliyumuhukumu Yesu kifo.
Rabi ina maana ya bwana wangu au mwalimu wangu.
Rahabu alikuwa mwanamke aliyeishi Yeriko Waisraeli walipovamia mji. Alikuwa kahaba.
Raheli alikuwa mmoja wa wake wa Yakobo. Yeye na dada yake Lea walikuwa watoto wa mjomba wake Yakobo.
Rama ulikuwa mji wa zamani wa Israeli uliokuwa kilometa 8 toka Yerusalemu. Ulikuwa mji ambao Benyamini aliishi.
Rehoboamu alikuwa mmoja wa wana wa mfalme Sulemani na alikuja kuwa mfalme baada ya Sulemani kufa.
Maneno haya yote humrejelea Roho Mtakatifu ambaye ni Mungu. Mungu mmoja na wa kweli aishiye milele katika nafsi tatu, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu. Roho Mtakatifu mara zingine hutajwa kama 'Roho' na 'Roho ya Yahweh' au 'Roho wa ukweli' Roho Mtakatifu ni mtakatifu kwa sababu yeye ni Mungu. Yeye yuko kamili na mwadilifu katika kila jambo alifanyalo. Roho Mtakatifu alishiriki kikamilifu katika uumbaji wa ulimwengu pamoja na Baba na Mwana. Wakati Mwana wa Mungu, Yesu aliporudi mbinguni, Mungu alimtuma Roho Mtakatifu kwa watu ili awaongoze, kuwafundisha, kuwafariji na kuwawezesha kufunya mapenzi ya Mungu. Roho Mtakatifu alimwongoza Yesu na pia anawaongoza wale wanaomwamini Yesu.
Mapendekezo ya tafsiri Neno hili laweza kutafsiriwa tu kwa kutumia maneno yenye kumaanisha 'roho' na 'mtakatifu' Lakini maneno mengine ambayo yaweza kutumika ni kama 'Roho Safi' au 'Roho aliye Mtakatifu' au 'Mungu Roho.'
Neno "rudi" linamaanisha kurudi au kurudisha kitu.
Neno "Sabato" la husu siku ya saba ya wiki, ambayo Mungu aliwaamuru Waisraeli waitenge kama siku ya kupumzika na kutofanya kazi.
Sauti hutumika kumaanisha kuongea au kuwasiliana kitu au jambo.
Hapo awali, neno "Sayuni" au "Mlima Sayuni" lilimaanisha ngome ambayo Mfalme Daudi aliiteka kutoka kwa Wayebusi. Majina haya yakawa njia nyingine ya kuitaja Yerusalemu.
Ibilisi ni roho hai Mungu aliyo umba, lakini aliasi dhidi ya Mungu na kuwa adui wa Mungu. Ibilisi anaitwa "Shetani" na "yule muovu."
Sidoni alikuwa mwana wa kwanza wa Kanani. Pia kuna mji wa Kikanani unao itwa Sidoni, labda uliitwa baada ya mwana wa Kanani.
Katika Biblia, kuna wanaume kadhaa wenye jina Simeoni.
Simoni alikuwa mmoja wa wanafunzi kumi na mbili wa Yesu.
Sodoma ulikuwa mji kusini mwa kanani ambapo mpwa wa Ibrahimu Lutu aliishi na mke na watoto wake.
Sulemani alikuwa mmoja wa wana wa Mfalme Daudi. Mama yake alikuwa ni Bathsheba.
Tamari ni jina la wanawake kadhaa katika Agano la Kale. Ni jina la miji ya maeno kadhaa katika Agano la Kale.
Thomaso alikuwa mmoja wa wanaume kumi na mbili Yesu aliye wachagua kuwa wanafunzi na baadae, mitume. Alijulikana kama "Didimasi" yenye maana ya "pacha."
Neno ufalme linawaelezea watu au vitu ambavyo vinahusiana na mfalme au malkia.
Uri ulikuwa mji muhimu pembeni mwa Mto Frati katika mji wa zamani wa Kalidea, ambao ulikuwa sehemu ya Mesopotamia. Hili eneo lilikuwa ambapo sasa ni Iraqi.
Uria alikuwa mwanaume mwenye haki na mmoja wanajeshi hodari wa Mfalme Daudi. Utajwa kama "Uria Mhiti"
Neno "Uyahudi" inamaanisha dini inayofuatwa na Wayahudi. Inajulikana piakama "dini ya Kiyahudi."
Katika Agano la Kale, neno "dini ya Kiyahudi" inatumika wakati katika Agano Jipya neno "Uyahudi" ndio linatumika. Uyahudi inajumuisha sheria zote za na maelekezo ya Agano la Kale ambayo Mungu aliwapa Wasiraeli kutii. Inajumuisha pia desturi na tamaduni zilizoongezwa katika dini ya Kiyahudi kadri muda ulivyoenda. Wakati wakutafsiri, usemi "dini ya Kiyahudi" au "dini ya Wayahudi" zinaweza kutumika katika Agano la Kale au Jipya. Lakini, neno "Uyahudi" linapaswa kutumika tu kwenye Agano Jipya, kwa sababu neno hilo halikuwepo kabla ya wakati huo
Uzia alikuwa mfalme wa Yuda akiwa ni umri wa miaka 16 na akatawala miaka 52, ambao ulikuwa utawala mrefu. Uzia alijulikana kama "Azaria."
Katika Biblia mtoto limetumika kwa namna ya jumla kuelezea mtu ambaye ni mdogo kwa umri. Watoto ni wingi wa neno mtoto.
Yakobo alikuwa pacha mdogo aliyekuwa mwana wa Isaka na Rebeka.
Jina la Yakobo linamaanisha "anakamata kisigino" ambao ni usemi unaomaanisha, "hudanganya." Wakati yakobo alipozaliwa, alikuwa akishilia kisigino cha pacha wake Esau. Miaka mingi baadaye, Mungu alibalisha jina la Yakobo kuwa "Israeli," inayomaanisha, "anashindana na Mungu." Yakobo alikuwa mjanja na muongo. Alipata njia ya kupata baraka za mwana wa kwanza na kurithi haki kutoka kwa kaka yake, Esau. Esau alikasirika na kupanga kumuua, kwa hiyo Yakobo akaondoka nchini mwake. Lakini baada ya miaka Yakobo alirudi na wake zake na watoto katika nchi ya Kanaani ambamo Esau alikuwa akiishi, na familia zao ziliishi kwa amani zikiwa jirani. Yakobo alikuwa na wana kumi na mbili. Uzao wao ukawa makabila kumi na mbili ya Israeli. Mwanaume tofauti aitwaye Yakobo ameorodheshwa kama baba wa Yusufu katika ukoo wa Mathayo.
Yehoshafati ni jina la angalua watu wawili katika Agano la Kale.
Mtu anayejulikana vizuri zaidi kwa hili jina ni Mfalme Yehoshafati ambaye alikuwa mfalme wa nne kutawala ufalme wa Yuda. Alirejesha amani kati ya Yuda na Israeli, na kuangamiza madhabahu ya miungu wa uongo. Yehoshafati mwingine alikuwa "mtunza kumbukumbu" wa Daudi na Sulemani. Kazi yake ilikuwa pamoja na kuandika nyaraka kwa ajili ya mfalme kusaini na kurekodi historia ya matukio muhumi yaliyotokea katika ufalme.
Yeremia alikuwa nabii wa Mungu katika ufalme wa yuda. Kitabu cha Agano la Kale cha Yeremia kina unabii wake.
Kama manabii wengi, Yeremia mara nyingi ilimbidi kuwaonya watu wa Israeli kuwa Mungu atawaadabisha kwa dhambi zao. Yeremia alitabiri kuwa Wababeli wataiteka Yerusalemu, jambo lililowafanya baadhi ya watu wa Yuda kukasirika. Kwa hiyo walimuweka katika kisima kilichokauka na kumuacha humo kufa. Lakini mfalme wa Yuda aliwaamuru watumishi wake kumuokoa Yeremia kutoka katika kisima. Yeremia aliandika kuwa alitamani macho yake yawe "chemchemi ya machozi," kuonesha masikitiko yake makali kuhusu uasi na mateso ya watu wake.
Yeriko ulikuwa mji wenye nguvu katika nchi ya Kanaani. Ulikuwa magharabi mwa mto wa Yordani na kaskazini mwa Bahari ya Chumvi.
Kama Wakanaani wote, watu wa Yeriko waliabudu miungu ya uongo. Yeriko ulikuwa mji wa kwanza katika nchi ya Kanaani ambao Mungu aliwaambia Waisraeli kuuteka. Wakati Yoshua alipowaongoza Waisraeli dhidi ya Yeriko, Mungu alifanya muujiza mkubwa kuwasaidia kuushinda huo mji.
Yerusalemu mwanzoni ulikuwa mji wa zamani wa Kikanaani ambao baadaye ulikuwa mji muhimu zaidi katika Israeli. Inapatikana karibu kilomita 34 magharibi mwa Bahari ya Chumvi na kaskazini mwa Bethlehemu. Bado ni mji mkuu wa Israeli ya leo.
Jina "Yerusalemu" imetajwa kwa mara ya kwanza katika kitabu cha Yoshua. Majina mengine ya mji huu katika Agano la Kale ni pamoja na "Salemu", "mji wa Yebusi," na "Sayuni." "Yerusalemu" na "Salemu" zote zina msingi wa "amani" katika maana. Yerusalemu mwanzoni ilikuwa ngome ya Yebusi iitwayo "Sayuni" amabyo mfalme Daudi aliikamata na kuifanya kuwa mji wake mkuu. Mwana wa Daudi Sulemani alijenga hekalu la kwanza Yerusalemu, katika mlima Moria, ambao ulikuwa mlima ambao Abrahamu alimtoa Isaka kama sadaka kwa Mungu. Hekalu lilirudiwa kujengwa hapo baada ya kutetezwa na Wababeli. Kwa sababu hekalu lilikuwa Yerusalemu, sherehe kuu za Kiyahudi ziliadhimishwa huko. Watu kawaida husema kwenda "juu" Yerusalemu kwa sababu palikuwa mlimani.
Yese Yese alikuwa baba wa mfalme Daudi, na mjukuu wa Ruthu na Boazi.
Yesu ni mwana wa Mungu. Jina "Yesu" linamaanisha, "Yahwe anaokoa." Neno "Kristo" ni jina linalomaanisha "mtiwa mafuta" na ni jina jingine la Masihi.
Majina mawili mara nyingi yanaunganishwa kama "Yesu Kristo" au "Kristo Yesu." Majina haya yanasisitiza kuwa mwana wa Mungu ndiye Masihi aliyekuja kuwaokoa watu kutoadhibiwa milele kwa dhambi zao. Katika njia za kimiujiza, Roho Mtakatifu alisababisha mwana wa milele wa Mungu kuzaliwa kama binadamu. Wazazi wake wa duniani waliambiwa na malaika kumuita "Yesu" kwa sababu alikusudiwa kuwaokoa watu kutoka katika dhambi zao. Yesu alifanya miujiza mingi iliyoonesha kuwa yeye ni Mungu na ni Kristo, au Masihi.
Yona alikuwa nabii wa Kihebrania katika Agano la Kale.
Kitabu cha Yona kinaelezea hadithi ya wakati Mungu alipomtuma Yona kuhubiri kwa watu wa Ninawi. Yona alikataa kwenda Ninawi na badala yake akapanda katika meli iliyokuwa inaelekea mji mwingine. Mungu alisababisha dhoruba kali kuilemea meli. Watu waliukuwa wakidafiri katika meli walipogundua kuwa Yona hakuwaanamtii Mungu, walimtupa katika bahari na dhoruba ikakoma. Yona alimezwa na samaki mkubwa na akawa tumboni mwake kwa siku tatu, mchana na usiku. Baada ya hayo, Yona alienda Ninawi na kuwahubiri watu wa huko, na wakaziacha dhambi zao.
Yoramu mwana wa Ahabu alikuwa mfalme Israeli. Wakati mwingine anajulikana kama "Yehoramu."
Mfalme Yoramu wa Israeli alitawala wakati mmoja kama Yehoramu wa Yuda. Yoramu alikuwa mfalme muovu aliyeabudu miungu ya uongo na kusababisha watu wa Israeli kutenda dhambi. Mfalme Yoramu wa Israeli pia alitawala wakati wa nabii Eliya na Obadia. Mwanamme mwingine aitwaye Yoramu alikua mwana wa mfalme wa Hamathi wakati Daudi ni mfalme.
Yosia alikuwa mfalme mcha Mungu aliyetawala juu ya ufalme wa Yuda kwa miaka thelathini na moja. Aliwaongoza watu wa Yuda kutubu na kumuabudu Yahwe.
Baada ya baba yake mfalme Amoni kuuwawa, Yosia akawa mfalme juu ya Yuda akiwa na miaka minane. Katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wake, mfalme Yosia alimuamuru kuhani mkuu Hilkia kulijenga tena hekalu la Mungu. Wakati hili likifanyika, vitabu vya Sheria vilipatikana. Vitabu vya Sheria viliposomwa kwa Yosia, alisikitishwa na jinsi watu wake walivyokuwa hawamtii Mungu. Aliamuru kwamba sehemu zote za kuabudia sanamu ziteketezwe na makuhani wa miungu wa uongo wauwawe. Pia aliwaamuru watu kuanza kuadhimisha sherehe ya Pasaka tena.
Katika Agano la Kale kuna wanaume watatu wenye jina Yothamu.
Mwanaume mmoja aitwaye Yothamu alikuwa mwana wa mwisho wa Gideoni. Yothamu alisaidia kumshinda kaka yake mkubwa Abimeleki, ambaye aliwauwa ndugu zake wengine wote. Mwanamme mwingine aitwaye Yothamu alikuwa mfalme juu ya Yuda kwa miaka kumi na sita baada ya kifo cha baba yake Uzia (Azaria). Kama baba yake, Yothamu alimtii Mungu na likuwa mfalme mzuri. Lakini hakuondoa sehemu za kuabudia sanamu na hii ilisababisha watu wa Yuda baadaye kumgeuka Mungu tena.
Yuda alikuwa mmoja wa wana wakubwa wa Yakobo. Mama yake alikuwa Lea. Uzao wake uliitwa "kabila la Yuda."
Alikuwa ni Yuda aliyewaambia ndugu zake kumuuza mdogo wao Yusufu kama mtumwa badala ya kumuuacha afe katika shimo. Mfalme Daudi na wafalme wote baada yake walikuwa uzao wa Yuda. Yesu pia alikuwa uzao wa Yuda. Utawala wa Sulemani ulipoisha na taifa la Israeli kugawanyika, ufalme wa Yuda ulikuwa wa sehemu ya kusini mwa nchi. Katika kitabu cha Agano Jipya cha Ufunuo, Yesu anaitwa "Simba wa Yuda." Maneno "Yahudi" na mji wa "Yuda" yametoka katika jina "Yuda."
Kabila la Yuda lilikuwa kubwa zaidi kati ya makabila kumi na mbili ya Israeli. Ufalme wa Yuda uliundwa na makanila ya Yuda na Benyamini.
Baada ya mfalme Sulemani kufa, taifa la Israeli liligawanyika katika falme mbili: Israeli na Yuda. Ufalme wa Yuda ulikuwa ufalme wa kusini, uliokuwa magharabi mwa Bahari ya Chumvi. Mji mkuu wa ufalme wa Yuda ulikuwa Yerusalemu. Wafalme wanane wa Yuda walimtii Yahwe na kuwaongoza watu kumwabudu yeye. Wafalme wengine wa Yuda walikuwa waovu na kuwaongoza watu kuabudu sanamu. Zaidi ya miaka 120 baada ya Ashuru kuishinda Israeli (ufalme wa kaskazini), Yuda ilitekwa na taifa la Babeli. Wababeli waliangamiza mji na hekalu, na kuwachukua watu wengi wa Yuda kwenda Babeli kama watekwa.
Neno "Yuda" linamaanisha sehemu katika nchi ya Israeli ya zamani. Wakati mwingine linatumika katika maana finyu na wakati mwingine katika maana pana.
Wakati mwingine"Yuda" inatumika katika maana finyu kumaanisha jimbo lililo sehemu ya kusini ya Israeli ya zamani magharibi tu mwa Bahari iliyo Kufa. Wakati mwingine "Yuda" inamaana pana na inamaanisha majimbo yote ya Israeli ya zamani, ikiwemo Galilaya, Samaria, Perea, Edomu na Yuda. Maana pana ya Yuda (mfano. Luka 1:5) inaweza kutafsiriwa kama "nchi ya Yuda" na katika maana finyu (mfano Luka 1:39) inaweza kutafsiriwa kama "jimbo la Yuda" kwa sababu hii ndio sehemu ya nchi ya Israeli ya zamani ambapo kabila la Yuda ya lilikuwepo.
Yuda Iskariote alikuwa mmoja wa mitume wa Yesu. Alikuwa ndiye aliyemsaliti Yesu kwa viongozi wa Kiyahudi.
Jina "Iskariote" inaweza kumaanisha "kutoka Keriothi", labada kuashiria kuwa Yuda alikulia katika huo mji. Yuda Iskariote alitunza fedha ya mitume na mara kwa mara aliiba kutumia kwa ajili yake. Yuda alimsaliti Yesu kwa kuwaambia viongozi wa dini mahali alipo Yesu ili wamkamate. Baada ya viongozi wa dini kumhukumu Yesu kifo, Yuda alijuta kuwa alimsaliti Yesu kwa hiyo akarudisha fedha ya usaliti kwa viongozi wa Kiyahudi na kisha kujiua. Mtume mwingine pia aliitwa Yuda na alikuwa mmoja wandugu wa Yesu. Kuna wanaume wengi waitwao Yuda katika Biblia, kama vile ndugu yake Yesu na mtume mwingine.
Zabuloni alikuwa mwana wa mwisho wa Yakobo na Lea na ni jina la mojawapo wa makabila kumi na mbili ya Israeli
Zakaria alikuwa nabii aliyetabiri wakati wa utawala wa Mfalme Dario I wa Uajemi. Kitabu cha Zakari katika Agano la Kale kina unabii wake, ambacho kinawasihi mateka waliorudi kulijenga tena hekalu.
Zebedayo alikuwa mvuvi kutoka Galilaya anayejulikana kwa sababu ya wanawe, Yakobo na Yohana, waliokuwa wanafunzi wa Yesu. Hawa wamekuwa wakitajwa katika Agano Jipya kama "wana wa Zebedayo."
Zerubabeli lilikuwa jina la Waisraeli wawili katika Agano la Kale.
Agizo ni sharti au sheria ya hadhara inayo toa amri au maelekezo ya watu kufuata. Hili neno lina maana sawa na "kisimika"
Msemo wa "aibisha" una maana ya kufanya kitu ambacho si cha heshima kwa mtu. Hii inaweza pia kumsababishia mtu huyo aibu au fedheha.
Msemo "ya kuaibisha" inaelezea tendo ambalo ni la aibu au litasababisha mtu kupungukiwa na sifa.
Mara nyingine "kuabisha" inatumika kumaanisha vyombo ambavyo havina kazi kwa jambo lolote muhimu.
Watoto wanaamuriwa kuwaheshimu na kuwatii wazazi wao. Pale ambapo watoto hawatii, wanakuwa hawaheshimu wazazi wao. Wanawafanya wazazi wao kwa njia ambayo haiwapi heshima kwao.
Waisraeli walipunguza sifa kwa Yahwe walipoabudu miungu ya uongo na kutenda mwenendo muovu.
Wayahudi hawakumheshimu Yesu kwa kusema ya kwamba alikuwa amepagawa na pepo.
Hii inaweza kutafsiriwa kama "kutoheshimu" au "kutenda bila heshima.
Nomino ya "kutoheshimu" inaweza kutafsiriwa kama "kutoheshimu" au "kupotea kwa sifa".
Kutegemea na muktadha, "ya kuaibisha" inaweza kutafsiriwa kama "siyo na heshima" au "ya aibu" au "haifai" au "haina thamani".
Neno "aina" linamaanisha makundi ya vitu vilivyoungana kwa kugawana tabia.
Katika Biblia, usemi huu unatumika bayana kumaanisha aina tofauti za mimea na wanyama ambao Mungu alivyotengeza alipoumba ulimwengu. Mara nyingi kuna tofauti nyingi za spishi katika kila "aina." Kwa mfano, farasi, punda milia, na punda zote ni sehemu ya "aina" moja lakini ni spishi tofauti. Kitu kikuu kinachotofautisha kila "aina" kama kundi tofauti ni kwamba kila mmoja wa hilo kundi anaweza kuzaa zaidi wa "aina" hiyo. Viumbe wa aina tofauti hawawezi kufanya hivyo pamoja.
Kuamuru ni kutoa amri kwa mtu afanye jambo fulani. Amri ni jambo ambalo mtu ameamriwa afanye.
Amri ni sheria maalumu iliyo andikwa inayo toa muongozo watu kuishi.
Amri ni tamko au sheria ambayo inatolewa kwa umma kwa watu wote.
Sheria za Mungu pia zinajulikana kama makataa, maagizo au amri.
Kama sheria na amri, makataa lazima yanapaswa kufuatwa.
Mfano wa makataa ya mtawala wa kibinadamu ulikuwa ni tangazo la Kaisari Augusto ya kwamba kila mmoja aliyeishi katika milki ya Roma alipaswa kurudi nyumbani kwake ili ahesabiwe katika sensa.
Kutoa amri juu ya jambo ina maana ya kutoa amri ambayo ilikuwa lazima kuitii. Hii inaweza kutafsiriwa kama, "kuamuru" au "kuamrisha" au "kutaka rasmi" au "kuweka sheria kwa umma".
Jambo linalofanywa kuwa "amri" kufanyika ina maana ya kwamba "lazima ifanyike" au "imeamuliwa na haitabadilishwa" au "kutamkwa kwa uhakika ya kuwa itafanyika"
Katika Biblia, "Bahari Kuu" au " bahari ya magharibi" inaelezea ile ambayo sasa ujulikana "Bahari ya Medeterenia," ambayo ilikuwa ni eneo la maji lilokulikana na watu wa Biblia.
Msemo "baya" na "uovu" yote ina maana ya chochote ambacho kinapingana na tabia takatifu na mapenzi ya Mungu.
Wakati "ubaya" unaweza kuelezea tabia ya mtu, "ovu" unaweza kumaanisha zaidi ya tabia ya mtu. Hata hivyo, misemo yote inafanana maana.
Msemo "uovu" una maana ya hali ambayo watu hufanya maovu.
Matokeo ya uovu yanaonywesha kwa uwazi kwa jinsi watu wanavyotenda vibaya wengine kwa kuwaua, kuiba, kusengenya au kuwa katili na kutokuwa mwema.
Mapendekezo ya Tafsiri
Kulingana na muktadha, misemo "uovu" na "ovu" inaweza kutafsiriwa kama "ubaya" au "dhambi" au "kinyume na maadili".
Njia zingine za kutafsiri hii zinaweza kujumuisha "isiyo nzuri" au "sio takatifu" au "sio adilifu".
Hakikisha maneno au misemo ambayo inatumika kutafsiri misemo hii kutosha muktadha ambayo ni kawaida katika lugha husika.
Neno "bwana" linamaanisha mtu anayemiliki na mwenye mamlaka juu ya watu wengine.
Neno hili wakati mwingine linatafsiriwa kama "mkuu" wakati wakumuita Yesu au wakati wakumaanisha mtu anayemiliki watumwa.
Katika Biblia, neno "chafu" utumika kama fumbo kueleza vitu ambavyo Mungu alitangaza sio sahihi kwa watu wake kugusa,kula, au kutoa dhabihu.
Msemo "chukiza" unaelezea jambo ambalo linapaswa kutopendwa na kukataliwa. "Kuchukia" kitu ina maan ya kutokipenda kabisa.
Mara nyingi Biblia huzungumzia kuhusu kuchukia uovu. Hii ina maana kuchukia uovu na kuukataa.
Mungu alitumia neno "chukiza" kuelezea matendo maovu ya wale waliomwabudu miungu ya uongo.
Waisraeli waliamriwa "kuchukia" matendo ya dhambi, na kinyume na maadili ambayo baadhi ya makundi ya watu majirani waliyafanya.
Mungu aliyataja matendo yote ya uasherati kuwa "chukizo".
Uaguzi, uchawi, na sadaka za mtoto yote yalikuwa "chukizo" kwa Mungu.
Msemo "chukizo" unaweza kutafsiriwa kama "uovu mbaya" au "inayochukiza" au "inayostahili kukataliwa".
Inapotumika na kiumbe takatifu "chukizo kwa" waovu, hii inaweza kutafsiriwa kama "kuchukuliwa kutotamanika kwa" au "kutokuwa na ladha" au "kukataliwa na"
Mungu aliwaambia Waisraeli "kuchukia" aina kadhaa ya wanyama ambao Mungu alitamka kuwa "wachafu" na kutofaa kwa chakula. Hii inaweza kutafsiriwa kama "kuchukia kwa uzito" au "kukataa" au "kuchukua kama kutokubalika".
Dada ni mtu wa jinsi ya kike anaye shiriki wastani wa mzazi mmoja na mtu mwingine.
Neno "damu" linamaanisha kimiminika chekundu kinachotoka katika ngozi ya mtu panapokuwa na jeraha au kidonda. Damu inaleta viini lishe vya uhai katika mwili wote wa mtu.
Neno "desturi" la eleza tamaduni na mapokeo yaliyo tunzwa kwa muda na yanayo pokelewa na vizazi vijavyo.
Katika Biblia, maneno "dhabihu" na "sadaka" ya husu zawadi maalumu anazopewa Mungu kama kitendo cha kumuabudu. Watu pia walitoa sadaka kwa miungu ya uongo.
Dhahabu ni chuma cha manjano, cha ubora wa juu sana kinachotumika kutengeneza vito na vyombo vya dini. Ilikuwa chuma ya thamani zaidi katika kipindi cha zamani.
Katika kipindi cha Biblia, aina nyingi tofauti ya vyombo vilitengezwa kwa dhahabu ngumu au kufunikwa na safu nyembamba ya dhahabu.
Vyombo hivi vilijumuisha heleni na vito vingine, sanamu, madhabahu, na vyombo vingine vilivyotumika katika tabenakulo au hekalu, kama vile sanduku la agano.
Katika Agano la Kale, dhahabu ilitumika kama njia ya kubadilishana katika kununua na kuuza. Ilipimwa juu ya mizani kupata thamani yake.
Baadaye, dhahabu na vyuma vingine kama vile fedha vilitumika kutengeneza sarafu kutumiwa kununua na kuuza.
Pale inapomaanisha kitu ambacho sio dhahabu ngumu, lakini ina safu nyembamba tu ya dhahabu, msemo "ya dhahabu" au "kufunikwa kwa dhahabu" inaweza kutumika.
Mara nyingi chombo kinaelezewa kama "rangi ya dhahabu" ambayo ina maana ina rangi ya njano ya dhahabu, lakini haijatengenezwa kwa dhahabu.
Maneno "dhalimu" na "kwa dhalimu" yanaeleza kutendea watu pasipo haki, na mara nyingi, namna ya kudhuru.
Neno "dhambi" la husu matendo, mawazo, na maneno yaliyo kinyume dhidi ya mapenzi ya Mungu na Sheria. Dhambi yaweza maanisha kutofanya kitu Mungu alicho tuambia tufanye.
Neno kudhihaki ni kumtania mtu, kwa namna mbaya.
Neno "dhiki" la husu kipindi cha ugumu, mateso, na msongo wa mawazo.
Msemo "dunia" una maana ya dunia ambayo wanadamu wanaishi, pamoja na kila aina ya viumbe hai.
"Dunia" pia inaweza kumaanisha ardhi au udongo ambayo hufunika nchi.
Msemo huu mara kwa mara hutumika kitamathali kumaanisha watu wanaoishi juu ya dunia.
Misemo, "acha dunia iwe na furaha" na "Atahukumu dunia" ni mifano ya matumizi ya tamathali ya msemo huu.
Msemo "kidunia" mara kwa mara humaanisha vitu vya kimwili kinyume na vitu vya kiroho.
Mapendekezo ya Tafsiri
Msemo huu unaweza kutafsiriwa kwa neno au msemo ambao lugha ya taifa hutumia kumaanisha sayari ya dunia ambayo tunaishi.
Kulingana na muktadha, "dunia" pia inaweza kutafsiriwa kama, "ulimwengu" au "ardhi" au "udongo".
Unapotumika kitamathali, "dunia" inaweza kutafsiriwa kama, "watu wa dunia" au "watu wanaoishi juu ya dunia" au "kila kitu juu ya dunia".
Njia za kutafsiri "kidunia" zinaweza kujumuisha, "kimwili" au "vitu vya dunia hii" au "vinavyoonekana".
Usemi "elekeza" na "maelekezo" yanamaanisha kutoka uongozo bayana ya nini cha kufanya.
"Kutoa maelekezo" inamaanisha kumuambia mtu bayana kitu anachotakiwa kufanya. Yesu alipowapa wanafunzi wake mikate na samaki kuwapa watu, aliwapa maelekezo bayana ya jinsi ya kuifanya. Kulingana na mazingira, neno "elekeza" inaweza kutafsiriwa kama "kumuambia" au "kuongoza" au "kufundisha" au "kutoa maelekezo kwa." Neno "maelekezo" inaweza kutafsiriwa kama "uongozo" au"ufafanuzi" au "kitu alichokuambia kufanya." Mungu akikupa maelekezo, huu usemi wakati mwingine unatafsiriwa kama "kuamuru" au "kuamrisha."
Neno "erevu" la elezea mtu enye akili na mahiri, hususani katika mambo ya utendaji.
Neno "fahamu" lina maana ya kusikia ua kupokea taarifa na kuelewa ina maana gani.
Fedha ya ng'aa, ni ya chuma ya kijivu inayo tumika kufanya sarafu, mikufu, vyombo, na mapambo.
Katika kipindi cha Biblia, zumari ilikuwa vyombo vya muziki iliyotengenezwa kwa mfupa au mbao na mashimo inayoruhusu sauti kutoka nje. Filimbi ilikuwa aina ya zumari.
Zumari nyingi ilikuwa na matete yaliyotengenezwa kutoka kwa nyasi nene ambayo hutikisika pale hewa inapopulizwa kwake.
Zumari bila matete mara kwa mara ilijulikana kama "filimbi".
Mfugaji alicheza filimbi kutuliza mifugo yao ya kondoo.
Zumari na filimbi ilitumika kucheza muziki wa huzuni na furaha.
Haya maneno "fundisha" na "kufundisha" yanaeleza kuambia watu wengine taarifa wasiyo ijua kabla. Mara nyingi maelezo utolewa rasmi au kwa utaratibu.
Neno "funga" linamaanisha kukaza kitu kwa usalama. Kitu kilichofungwa au kuunganishwa pamoja kinaitwa "muungano". Neno "kufunga" ni sehemu ya neno hili katika wakati uliopita.
Neno "funga" laweza pia kutafasiriwa kama "kaza" au "zungushia"
Msemo "kufunga" una maana ya kuacha kula chakula kwa kipindi fulani, kama vile siku moja au zaidi. Mara nyingi inajumulisha kutokunywa.
Kufunga kunaweza kusaidia watu kumlenga Mungu na kuomba bila kutolewa mawazo kwa kuandaa chakula na kula.
Yesu aliwalaani viongozi wa dini wa Kiyahudi kwa kufunga kwa sababu ambazo sio sahihi. Walifunga ili kwamba wengine wafikiri kuwa wao ni watakatifu.
Mara nyingi watu walifunga kwa sababu walikuwa na huzuni sana au majonzi juu ya jambo.
Kitenzi cha "kufunga" kinaweza kutafsiriwa kama "kujizuia kula" au "kutokula".
Nomino ya "funga" inaweza kutafsiriwa kama "muda wa kutokula" au "muda wa kujizuia na chakula"
Msemo "funga" una maana ya kufunga kitu kuzunguka kitu kingine. Mara kwa mara humaanisha kutumia mkanda kuzunguka kiuno kuweka kanzu au gwanda mahali pake.
Msemo wa kibliblia unaojulikana, "funga kiuno" una maana ya kuchomekea chini ya vazi ndani ya mkanda kuruhusu mtu kusogea kwa uhuru zaidi, mara nyingi kufanya kazi.
Msemo una maana ya kujiweka tayari kufanya kazi au kujiandaa kufanya kitu kigumu.
Msemo "funga kiuno" unaweza kutafsiriwa kutumia msemo katika lugha husika yenye maana moja. Au inaweza kutafsiriwa bila tamathali kama "jiandae kwa ajili ya tukio" au "jiandae"
Msemo "kufngwa na" inaweza kutafsiriwa kama "kuzungushwa na" au "kufungwa na".
Furaha ni hisia ya kupendezwa au kuridhika inayotoka kwa Mungu. Maana inayokaribiana, "mwenye furaha" inaelezea mtu anayejisikia vizuri sana na mwenye furaha nyingi.
Mtu anasikia furaha anapokua anahisi kuwa anachopitia ni chema sana. Mungu ndiye anayegawa furaha ya kweli kwa watu. Kuwa na furaha hakutegemei hali nzuri. Mungu anaweza kuwapa watu furaha hata kama vitu vigumu kabisa vinatokea katika maisha yao. Sehemu zingine zinaelezwa kama za furaha, kama nyumba na miji. Hii inamaanisha kuwa watu waiishio humo ni wenye furaha.
Neno "fuvu" la eleza kichwa cha mifupa kisicho na nyama cha mtu au mnyama
"Kugeuka" kuna maana ya kubadili mwelekeo wa mwili au kusababisha kitu kingine kubadilisha muelekeo.
Ghadabu ni hasira kali ambayo mara nyingine hudumu kwa mda mrefu. Hii maranyingi huelezea hukumu ya Mungu ya haki na adhabu ya watu walioasi dhidi yake.
Msemo "injili" una maana ya "habari njema" na una maana ya ujumbe au tangazo ambalo linawaambia watu jambo ambalo lina manufaa kwako na kuwapa furaha.
Katika Biblia, msemo huu humaanisha ujumbe kuhusu wokovu wa Mungu kwa watu kupitia sadaka ya Yesu msalabani.
Katika Biblia nyingi za Kiingereza, "habari njema" mara nyingi hutafsiriwa kama "injili" na pia hutumika katika misemo kama vile "injili ya Yesu Kristo" au "injili ya Mungu" na "injili ya ufalme".
Mapendekezo ya Tafsiri
Njia tofauti za kutafsiri msemo huu zinaweza kujumuisha "jumbe mzuri" au "tangazo zuri" au "ujumbe wa Mungu wa wokovu" au "mambo mazuri Mungu anayofundisha kuhusu Yesu".
Kulingana na muktadha, njia za kutafsiri msemo "habari njema ya" inaweza kujumuisha "ujumbe/havbari njema" au "ujumbe mzuri kutoka" au "mambo mazuri Mungu husema juu ya" au "kile Mungu anasema kuhusu jinsi anavyookoa watu".
Maneno haya yanamaanisha kuwatendea watu vyema kulingana na sheria za Mungu. Sheria za binadamu zinazo onesha kiwango cha Mungu cha tabia sawa kwa watu wengine.
Kuwa wa "haki" ni kutenda ya haki na mema kwa mtu mwingine. Pia inaashiria uaminifu na msimamo kufanya kilicho adilifu machoni pa Mungu. Kutenda kwa "haki" inamaanisha kuwatendea watu kwa njia iliyo sawa, nzuri na ya kufaa kulingana na sheria za Mungu. Kupokea "haki" inamaanisha kutendewa vyema chini ya sheria, aidha kulindwa kwa sheria au kuadhibiwa kwa kuvunja sheria. Wakati mwingine neno "haki" lina maana pana ya "utakatifu"au "kufuata sheria za Mungu."
Hakimu ni mtu anayeamua nini kiko sawa au la ukiwepo ugomvi kati ya watu, mara nyingi katika mambo yanayofungamana na sheria.
Katika Biblia, Mungu mara nyingi anatajwa kama hakimu kwa sababu yeye ndiye hakimu aliye kamili anayefanya maamuzi ya mwisho kuhusu nini kiko sawa au kisicho sawa. Baada ya watu wa Israeli kuingia nchi ya Kanaani na kabla hawajawa na wafalme wa kuwatawala, Mungu aliwapa viongozi waitwao "waamuzi" kuwaongoza nyakati za shida. Mara nyingi waamuzi hao walikuwa viongozi wa kijeshi waliowaokoa Waisraeli kwa kuwaangamiza maadui zao. Neno "hakimu" linaweza pia kuitwa "muamuzi" au "kiongozi" au "mkombozi" au "gavana," kutegemea na mazingira.
Msemo "halali" unamaanisha kitu kinachoruhusiwa kufanywa kulingana na sheria au mahitaji mengine. Kinyume cha hiki ni "kinyume na sheria" inyomaanisha "sio halali."
Katika Biblia, kama kitu kinasemwa kuwa "halali" inamaanisha inaruhusiwa na sheria ya kimaadili ya Mungu, au kwa sheria ya Musa au sheria zingine za Kiyahudi. Kitu ambacho "sio halali" "hakiruhusiwi" na sheria hizo. Kufanya kitu "ipasavyo" inamaanisha kuifanya "sawa" au "katika njia sahihi." Mambo mengi Wayahudi waliyoona ni halali au sio halali hayakuwa kwenye makubaliano na sheria za Mungu kuhusu kuwapenda wengine. Kulinga na mazingira, njia za kuafsiri "halali" ni pamoja na, "kuruhusu" au "kulingana na sheria ya Mungu" au "kufuatana na sheria zetu" au "sawa" au inafaa." Msemo "Je ni halali" inaweza pia kutafsiriwa kama "Je, sheria zetu zinaruhusu" au "Hilo ni jambo ambalo sheria zetu zinaruhusu?"
Zamani za kale, hati ilikuwa aina ya kitabu kilicho tengenezwa kwa karatasi ndefu ya mafunjo au ngozi.
Msemo "hatia" una maana ya ukweli wa kufanya dhambi au kutenda kosa.
Kuwa na "hatia" ina maana ya kuwa umefanya kitu kiouvu kimaadili, yaani, kutomtii Mungu.
Kinyume cha "mwenye hatia" ni "asiye na hatia".
Mapendekezo ya Tafsiri
Baadhi ya lugha zinaweza kutafsiri "hatia" kama "uzito wa dhambi" au "hesabu ya dhambi".
Njia za kutafsiri "kuwa na hatia" inaweza kujumuisha neno au msemo ambayo ina maana ya "kuwa katika kosa" au "kuwa umefanya jambo ovu kimaadili" au "kuwa umefanya dhambi".
Neno "haya" la husu hali ya maumivu ya kuumizwa kihisia kwa kuaibishwa kwasababu ya kitu cha fedheha ambacho yeye au mtu mwingine amefanya.
Hekalu lilikuwa ni jengo lililo zungukwa na kuta za nyuani ambapo Waisraeli walikuja kuombaa na kutoa dhabihu kwa Mungu. Lilikuwa Mlima Moria katika mji wa Yerusalemu.
Hema ni hifadhi linalo hama lililo tengenezwa na uzi uliyo zungushiwa kwenye nguzo pamoja.
Istilahi 'heshima' na 'kuheshimu' hurejelea kitendo cha kumpa mtu heshima au kumstahi mtu. Heshima mara kwa mara hutolewa kwa mtu mwenye hadhi ya juu na umuhimu wa juu kama vile mfalme au Mungu. Mungu pia huwaagiza Wakristo wote kuwaheshimu watu wengine, lakini si kutafuta heshima zao wenyewe. Watoto wameagizwa kuwatii wazazi wao na kuwatii. Maneno kama 'heshima' na 'utukufu' ni maneno yanayoenda kwa pamoja hasa yanapomrejelea Yesu. Heshima kwa Mungu inajumuisha kumshukuru na kumsifu Mungu, na kuonesha heshima kwa kumtii Mungu na kuishi katika njia inayoonesha kuwa Mungu ni Mkuu.
Mapendekezo Njia nyingine za kutafsiri neno 'heshima' linajumuisha 'staha' Neno 'kuheshimu' laweza kutafsiriwa kama 'kuonesha heshima maalumu kwa au kuonesha mtu thamani ya juu.
Neno "hukumu" mara nyingi humaanisha kufanya maamuzi kama jambo liko sawa kimaadili au kama haliko sawa.
"Hukumu ya Mungu" mara nyingi humaanisha uamuzi wake kulaani kitu au mtu muovu. Hukumu ya Mungu mara nyingi huhusisha kuwaadhibu watu kwa dhambi zao. Neno "hukumu" inaweza pia kumaanisha "kulaani." Mungu anawaagiza watu wake kutowahukumu wengine kwa naamna hii. Maana nyingine ni "uamuzi kati ya" au "kuhukumu kati ya", yaani kuchagua ni mtu gani yuko sahihi katika ugomvi kati yao. Katika mazingira mengine, "hukumu" za Mungu ni yale aliyeamua ni mema na yenye haki. Zinafanana na amri, sheria na maagizo yake. "Hukumu" inaweza kumaanisha uwezo wa busara wa kufanya maamuzi. Mtu anayekosa "hukumu" hana hekima kufanya maamuzi ya busara.
Msemo "huru" au "uhuru" una maana ya kutokuwa katika utumwa au aina yoyote ya kifungo.
Msemo "kumweka mtu huru" au "kumweka huru mtu" ina maana ya kutoa njia kwa mtu ili asiwe katika utumwa au kifungo.
Katika Biblia, misemo hii mara kwa mara hutumika kitamathali kumaanisha jinsi gani muamini katika Yesu hayupo chini ya nguvu ya dhambi.
Kuwa "huru" au "uhuru" inaweza kumaanisha kutohitajika kutii Sheria ya Musa, lakini badala yake kuwa huru kuishi kwa mafunzo na uongozi wa Roho Mtakatifu.
Mapendekezo ya Tafsiri
Msemo "huru" unaweza kutafsiriwa kwa neno au msemo ambao una maana ya "kutofungwa" au "kutokuwa katika utumwa" au "kutokuwa katika kifungo".
Msemo "ukuru" unaweza kutafsiriwa kwa neno au msemo ambao una maana, "hali ya kuwa huru" au "hali ya kutokuwa mtumwa" au "kutofungwa".
Msemo "kuweka huru" unaweza kutafsiriwa kama "kusababisha kuwa huru" au "kukomboa mtu kutoka utumwani" au "kumwachia kutoka kifungoni".
Mtu ambaye "amewekwa huru" atakauwa "ameachiliwa" au "kutolewa kutoka" katika kifungo au utumwa.
Maneno "iga" na "mwigaji" yanamaanisha kumuiga mtu mwingine na kuigiza sawa na mtu huyu afanyavyo.
Wakristo wanafundishwa kumuiga Yesu Kristo kwa kumtii Mungu na kuwapenda wengine, kama Yesu alivyofanya. Mtume Paulo aliliambia kanisa la awali kumuiga yeye, kama yeye alivyomuiga Yesu.
Neno "imani" la eleza kuamini kwamba kitu au mtu ni wa kweli au tegemeo. Mtu "mwaminifu" na weza kuwa tegemevu kufanya kitu na kusema kilicho sawa na kweli.
Kwa ujumla, msemo "imani" una maana ya imani, au matumaini ndani ya mtu au jambo.
"Kuwa na imani" na mtu ni kuamini ya kwamba kile anachosema na kufanya ni kweli na kuaminika.
"Kuwa na imani na Yesu" ina maana ya kuamini mafundisho yote ya Mungu kuhusu Yesu. Ina maana haswa ya kwamba watu wanamuamini Yesu na sadaka yake kuwasafisha kutoka kwa dhambi zao na kuwakomboa kutoka na adhabu wanayostahili kwa sababu ya dhambi yao.
Imani ya kweli kwa Yesu itamsababisha mtu kuzaa matunda mazuri ya kiroho au tabia kwa sababu ya Roho Mtakatifu anayeishi ndani yake.
Mara kwa mara "imani" kwa ujumla ina maana ya mafundisho yote kuhusu Yesu, yaani kama msemo, "ukweli wa imani".
Katika muktadha kama wa "tunza imani" au "telekeza imani", msemo "imani" una maana ya hali ya kuamini mafundisho yote kuhusu Yesu.
Mapendekezo ya Tafsiri
Katika baadhi ya muktadha, "imani" inaweza kutafsiriwa kama "imani" au "hatia" au "kujiamini" au "kuamini".
Kwa baadhi ya lugha misemo hii inaweza kutafsiriwa kutumia aina za kitenzi cha "imani".
Inua, inua juu inamaana ya kuinua kitu juu au kukuweka juu.
Ishara ni kitu, tukio, au kitendo kinacho wasilisha maana maalumu.
jangwa, au nyika, ni sehemu iliyokauka, isiyokuwa na mazao ambayo mimea na miti michache inaweza kuota pale.
Jangwa ni eneo la ardhi lenye tabia ya nchi ya ukavu na mimea na wanyama wachache.
Kwa sababu ya mazingira magumu, watu wachache sana wanaweza kuishi katika jangwa, kwa hiyo pia inajulikana kama "nyika".
"Nyika" inaleta maana ya sehemu iliyojitenga, ya kipekee mbali na watu.
Neno hili pia linaweza kutafsiriwa kama "sehemu ya jangwa" au "sehemu iliyojitenga" au "sehemu isiyokaliwa".
Maneno yote haya yanamaanisha kuwa na ujasiri na ushujaa kwa kuongea ukweli kuhusu jambo halali hata kama ni vigumu na hatari.
Neno "jikwaa" lina maana ya "karibu kuanguka" wakati wakutembea au kukimbia. Kujikwaa juu ya kitu.
Katika Biblia, neno "jina" linatumika kwa mifano kadhaa.
Neno "jirani" mara kwa mara la mueleza mtu anaye ishi karibu. Pia yaweza kueleza kwa ujumla mtu anaye ishi katika jamii moja au kundi la watu.
Jitu mara nyingi ilimaanisha mtu ambaye alikuwa na ukubwa usio wa kawaida wa urefu na nguvu.
Goliati, mwanajeshi wa Kifilisti aliyepigana na Daudi, aliitwa Daudi kwa sababu alikuwa mrefu sana, mkubwa, na mtu mwenye nguvu.
Wapelelezi wa Israeli waliotafiti nchi ya Kaanani walisema ya kwamba watu wanaoishi pale walikuwa kama majitu.
Jiwe ni mwamba mdogo. Neno "kupiga jiwe" la husu kurusha mawe na majabali makubwa kwa mtu kuweza kumuua.
Katika Biblia, neno "joho" uleza vazi lililo valiwa chini ya ngozi, chini nguo nyingine.
Neno "juma" kwa kawaida lamaanisha kipindi cha kuishia siku saba.
Maneno " juu" na " juu sana" ni misemo inayo maanisha, "mbinguni."
Kabila ni kundi la watu waliyo toka kwa babu mmoja.
Neno "kaburi" ni sehemu watu wanapo weka mwili wa mtu aliye kufa.
Misemo "kama" na "mfano" inamaanisha kitu kuwa sawa au kufanana na kitu kingine.
Neno "kama" pia inatumika katika mithali zinazoitwa "mfanano" ambapo kitu kinalinganishwa na kitu kingine, kawaida huonyesha tabia zinazolingana. Kwa mfano, "nguo zake zinang'aa kama jua" na "sauti ilivuma kama ngurumo." "Kuwa kama" au "kusikika kama" au "kuonekana kama" kitu au mtu inamaana kuwa na sifa zinazofanana na kitu anacholinganishwa nacho au mtu anayelingishwa naye. Watu waliumbwa katika "mfano" wa Mungu. Inamaanisha wana sifa au tabia ambazo ni "kama" au "zizafanana" na sifa ambazo Mungu anazo, kama uwezo wakufikiri, kuhisi na kuwasiliana. Kuwa na "mfano" wa kitu au mtu inamaana kuwa na tabia zinazofanana na hicho kitu au mtu.
Neno "kamata" la maanisha kuchukuwa au kumteka mtu au kitu kwa nguvu. Inaweza maanisha ya kumzidi nguvu au kumtawala mtu.
"Kanyaga" ina maana ya kukanyaga kitu na kukisaga kwa mguu. Neno pia utumika kimfano katika Biblia kumaanisha "haribu" au "shinda" au "aibisha."
Katika Biblia maneno kazi, vitendo, matendo ni vitu ambavyo Mungu au watu hufanya.
Neno "kazi" linamaanisha kufanya kazi ngumu ya aina yoyote.
Kwa ujumla, kazi ni shughuli inayotumia nguvu, mara nyingi inaashiria kuwa shughuli ni ngumu. Mfanyakazi ni mtu afanyae aina yoyote ya kazi.
Katika Biblia, kiapo ni ahadi rasmi ya kufanya kitu. Mtu anaye kiapo anapswa kutimiza hiyo ahadi. Kiapo kinahusu kuwa mwaminifu na wa kweli.
Kiasi ni uwezo wa kutawala tabia ya mtu ili kuepusha kutenda dhambi.
Msemo huu unatumika kumaanisha vyote kifo cha kimwili na kiroho. Kimwili, ina maana ya mwili wa kihalisia wa mtu kukoma kuishi. Kiroho, ina maana ya wenye dhambi kutengwa na Mungu mtakatifu kwa sababu ya dhambi yao.
Mapendekezo ya Tafsiri
Kutafsiri msemo huu, ni vyema kutumia neno la kila siku au usemi ambao una maana ya kifo katika lugha husika.
Katika baadhi ya lugha, "kufa" inaweza kuelezwa kama "kutokuishi". Msemo "kufa" unaweza kutafsiriwa kama "kutokuwa hai" au "kutokuwa na uhai wowote" au "kutokuishi".
Lugha nyingi zinatumia msemo wa tamathali kuelezea kifo, kama "kuondoka" kwa Kiingereza. Ila katika Biblia ni bora kutumia msemo wa moja kwa moja kwa ajili ya kifo ambao unatumika kila siku katika lugha.
Katika Biblia, uhai na kifo wa kimwili mara kwa mara hulinganishwa na uhai na kifo cha kiroho. Ni muhimu katika tafsiri kutumia neno moja au msemo kwa ajili kifo cha kimwili na kifo cha kiroho.
Katika baadhi ya lugha inaweza kuwa wazi zaidi kusema, "kifo cha kiroho" ambapo muktadha unahitaji maana hiyo. Watafsiri wengine wanaweza kuhisi ni bora kusema, "kifo cha kimwili" katika muktadha ambapo unalinganishwa na kifo cha kiroho.
Msemo wa "wafu" ni kivumishi chenye maana ya watu waliokufa. Baadhi ya lugha zitatafsiri hili kama, "watu waliokufa" au "watu ambao wamekufa"
Neno "kikapu" linamaanisha chombo kilichotengenezwa kwa kusukwa.
Kiti cha enzi ni kiti ambacho mfalme ana keti kuamua mambo muhimu na kusikiliza maombi ya watu wake.
Msemo "kizazi" una maana ya kundi la watu ambao wote wamezaliwa katika kipindi cha kufanana.
Kizazi pia kinaweza kumaanisha kipindi cha muda. Katika kipindi cha Biblia, kizazi kilichukuliwa kuwa kama miaka 40.
Wazazi na watoto waoo wanatoka katika vizazi viwili tofauti.
Katika Biblia, msemo "kizazi" pia hutumika kitamathali kumaanisha kwa ujumla watu ambao huwa na tabia za kufanana.
Mapendekezo ya Tafsiri
Msemo " kizazi hiki" au "watu wa kizazi hiki" unaweza kutafsiriwa kama "watu wanaoishi sasa" au "nyie watu".
"Kizazi hiki kiovu" inaweza kutafsiriwa kama "watu hawa waovu wanaoishi sasa".
Msemo "kutoka kizazi hadi kizazi" au "kutoka kizazi kimoja hadi kingine" inaweza kutafsiriwa kama "watu wanaoishi sasa, pamoja na watoto na wajukuu wao" au "watu katika kipini chote" au "watu wa kipindi hili na vipindi vya baadaye" au "watu wote na uzao wao".
"Kizazi kinachokuja kitamtumikia; watawaambia kizazi kifuatacho juu ya Yahwe" inaweza kutafsiriwa kama "Watu wengi hapo baadaye watamtumikia Yahwe na kuwaambia watoto na wajukuu wao juu yangu".
"kondoo" ni mnyama wa saizi ya kati wa miguu minne mwenye manyoya mwili mzima.
Neno "kubeba" linamaanisha "kubeba" kitu fulani. Lakini pia kuna kuna matumizi ya tamathari mbalimbali ya neno hili.
Neno la "kufuru" lina maana ya kuharibu au kuchafua sehemu takatifu au kitu katika namna ambayo haikubaliki kutumika katika kuabudu.
Mara kwa mara kukufuru kitu inahusisha kuonyesha okosefu mkubwa wa keshima kwake.
Kwa mfano, wafalme wa kipagani walikufuru vyombo maalumu kutoka hekalu la Mungu kwa kuvitumia kwa ajili ya sherehe katika kasri zao.
Mifupa kutoka watu waliokufa ilitumika na maadui kukufuru madhabahu katika hekalu la Mungu.
Msemo huu unaweza kutafsiriwa kama, "kusababisha kutokuwa mtakatifu" au "kumvunjia heshima kwa kufanya asiwe mtakatifu" au "kukufuru kwa kuvunja heshima" au "kusababisha kutokuwa msafi".
Neno 'kuhani mkuu' hurejelea kuhani maalumu aliyekuwa ameteuliwa kutumika kwa mwaka mmoja kama kiongozi wa makuhani wote wa Wayahudi. Kuhani mkuu alikuwa na majukuu mahususi. Alikuwa ni mtu pekee aliyeruhusiwa kuingia mahali patakatifu sana katika hekalu ili kutoa sadaka maalumu mara moja kwa mwaka. Waisraeli walikuwa na makuhani wengi sana, lakini walikuwa na kuhani mkuu mmoja kwa muda fulani. Kipindi alichokamatwa Yesu, Kayafa alikuwa kuhani mkuu. Anasi, Baba mkwe wa Kayafa anatajwa mara kadhaa kwasababu alikuwa kuhani mkuu hapo awali, huenda alikuwa bado na mamlaka na nguvu fulani juu ya watu.
Mapendekezo ya tafsiri 'Kuhani mkuu" tunaweza kutafsiri kama "kuhani wa daraja la juu"
"Kujua" inamaanisha kuelewa kitu au kuwa na ufahamu wa jambo. Usemi "kufanya kujulikana" ni usemi unaomaanisha kutoa taarifa.
Neno "ufahamu" linamaanisha taarifa ambazo watu wanajua. Inaweza kuwa kujua vitu katika dunia ya kimwili na kiroho. "Kujua kuhusu" Mungu inamaanisha kuelewa mambo kumhusu kwa sababu ya yale aliyotufunulia. "Kumjua" Mungu inamaanisha kuwa na uhusiano naye. Hii inamaanisha pia kuwajua watu wake. Kujua mapenzi ya Mungu inamaanisha kuwa na ufahamu wa yale aliyetoagiza, au kuelewa ni nini anataka mtu afanye. "Kujua Sheria" inamaanisha kuwa na ufahamu wa yale Mungu aliyoagiza au kuelewa yale Mungu aliyoagiza katika sheria alizompa Musa. Wakati mwingine "ufahamu" unatumika kama neno lingine la "hekima," linalojumuisha kuishi katika njia inayompendeza Mungu. "Ufahamu wa Mungu" wakati mwingine unatumika kama njia nyingine ya kusema hofu ya Yahwe.
Katika nyakati za Biblia, "kukesha" ulikuwa wakati wa usiku ambao katika huo mlinzi au mwangalizi wa mji alikuwa kazini akiangalia hatari yoyote kutoka kwa maadui.
Katika Biblia, haya maneno ni tafsida yanayo eleza kufanya ngono.
Msemo "kulewa" ina maana ya kuleweshwa kutokana na kunywa kileo.
"Mlevi" ni mtu ambaye hulewa mara kwa mara. Mtu wa aina hii anajulikana kama "mlevi".
Biblia inawaambia waumini kutolewa na vilevi, lakini kutawaliwa na Roho Mtakatifu wa Mungu.
Biblia inafundisha ya kwamba ulevi sio busara na inamshawishi mtu kutenda dhambi kwa njia zingine.
Njia zingine za kutafsiri "kulewa" zinaweza kujumuisha "levya" au "kulewa" au "kupata kilevi kingi sana" au "kushiba kwa kinywaji chachu"
Neno "kumwaga damu" linamaanisha kifo cha mwanadamu kwa sababu ya mauaji, vita, au sababu nyingine ya kikatiri.
Katika Biblia "kundi" ina maana ya kundi la kondoo na mbuzi na "mifugo" ina maana ya kikundi cha ng'ombe, maksai, au nguruwe.
Lugha tofauti zinaweza kuwa na njia tofauti za kutaja makundi ya wanyama au ndege.
Kwa mfano, katika Kiingereza msemo "kundi" unaweza pia kutumika kwa ajili ya kondoo au mbuzi, lakini katika maandishi ya Biblia haitumiki kwa njia hii.
Msemo "kundi" katika Kiingereza pia hutumika kwa ajili ya kundi la ndege, lakini unaweza kutumika kwa ajili ya nguruwe, maksai au ng'ombe.
Fikiria ni misemo gani inatumika katika lugha yako kumaanisha makundi tofauti ya wanyama.
Kwa mistari ambayo ina maana ya "makundi au mifugo" inaweza kuwa bora kuongeza "ya kondoo" au "ya ng'ombe" kwa mfano, kama lugha haina maneno tofauti kumaanisha aina tofauti za makundi ya wanyama.
Neno "kuomba" lamaanisha kumwomba mtu kitu fulani kwa umuhimu. Mara kwa mara inamaanisha kuomba pesa, lakini pia limetumika kuonesha kuombeleza jambo fulani.
"Kura" ni kitu kilichowekwa alama kinachochaguliwa miongoni mwa vitu vya kufanana kama naamna ya kuamua jambo. "Kupiga kura" inamaanisha kurusha vitu vilivyo wekwa alama kwenye sakafu au ardhi yoyote.
Mara nyingi kura yalikuwa mawe madogo yenye alama au vipande vidogo vilivyovunjika vya udongo. Tamaduni zingine zinafanya "bahati nasibu" au "kuvuta" kura kwa kutumia majani makavu. Mtu anayashikilia majani makavu ili asiwepo wakuona yana urefu gani. Kila mtu anavuta jani na yule atakayepata jani kavu refu zaidi (au fupi) ndiye atakayekuwa amechaguliwa. Zoezi la kupiga kura lilitumika na Waisraeli kujua ni nini Mungu aliwataka wafanye. Kama nyakati za Zekaria na Elisabeti, ilitumika pia kuchagua ni kuhani yupi atatenda jukumu bayana hekaluni katika muda maalumu. Askari walio msulubisha Yesu walipiga kura kuamua ni nani atakaa na joho la Yesu. Usemi "kupiga kura" inawezakutafsiriwa kama "kufanya bahati nasibu" au "kurusha kura". Kulinga na mazingira, neno "kura" inaweza pia kutafsiriwa kama "jiwe lenye alama" au "kipande cha udongo" au "kijiti" au "kipande cha jani." Kama maamuzi yakifanyika "kwa kura" hii inaweza kutafsiriwa kama "kufanya bahati nasibu (au kurusha) ya kura."
Neno "kusaliti" lamaanisha tendo la kumdanganya na kumdhuru mwingine. "Msaliti" ni mtu amsalitiye rafiki yake mwenye kumwamini.
Msemo "kusanya" una maana ya kupita katika shamba au shamba la matunda kuokota nafaka yoyote au tunda ambao wavunaji wameacha nyuma.
Mungu aliwaambia Waisraeli kuruhusu wajane, watu maskini, na wageni kukusanya mabaki ya nafaka ili kwamba wapate chakula kwa ajili yao.
Mara nyingine mmiliki wa shamba angeruhusu wakusanyaji kwenda moja kwa moja nyuma ya wavunaji kukusanya, ambayo iliwawezesha wao kukusanya nafaka zaidi.
Mfano wa wazi ni jinsi hii ilivyofanya kazi katika simulizi ya Ruhtu, ambaye aliruhusiwa kwa ukarimu kukusanya miongoni mwa wavunaji katika mashamba ya ndugu wa Boazi.
Neno "kuza" lina maana ya kufanya kitu au mtu mkubwa au kuvuta umakini kwa ukuu wa mtu.
katika Biblia kuna maneno mawili yametumika, neno la Kiebrania 'sheol' na neno la Kigriki 'hades.' Maneno haya yametumika katika Biblia kumaanisha kifo na sehemu ambako roho za watu waliokufa huenda. katika Kiebrania neno 'sheol' limetumika katika Agano la Kale kurejelea sehemu ya watu waliokufa au sehemu ya kifo. katika agano jipya, neno la Kigriki 'hades" limetumika kumaanisha sehemu ya roho za watu waliomwasi Mungu. Roho hizi hurejelewa kama zinaenda "chini." Wakati mwingine linaweza kutofautishwa na 'kwenda juu' mbinguni mahali ambako roho za watu za watu wanaomwamini Yesu zinaishi.
Mapendekezo ya tafsiri Katika Agano la Kale neno "sheol" linaweza kutafsiriwa kama " sehemu ya wafu" au "sehemu kwa ajli ya roho za wafu" Baadhi ya tafsiri hufasiri neno hili kama "shimo" au "kifo" kwa kutegemea na muktadha. Neno "hades" limetumika sana katika Agano Jipya ambalo laweza kutafsiriwa kama "sehemu kwa ajili ya roho za wafu za watu wasioamini" au " sehemu ya mateso na adhabu ya kwa roho za wafu wasioamini." Baadhi ya tafsiri hutunza neno ''sheol" au ''Hades'' kwa kutumia herufi ambazo zinakubaliana katika mfumo wa sauti wa lugha husika. kwa kiswahili twaweza kusema 'sheoli" na 'hadesi'
Maneno "kweli" na "ukweli" yana eleza mambo ambyo ni halisi, matukio yaliyo tukia, na maneno yaliyo semwa.
Maneno "la kumi" na "zaka" yanaeleza "asilimia ya kumi" au "moja-kati-ya -sehemu- ya-kumi" ya pesa, mazao, mifugo, au mali za mtu anazo mpa Mungu.
Haya maneno yana maana ya kimafumbo kuhusu kifo.
"Lango" ni kizuizi chenye bawaba katika njia ya kufikia ya uzio au ukuta ambao huzunguka nyumba au mji. "Nguzo ya lango" ina maana ya nguzo ya chuma au mbao ambayo inaweza kusogezwa katika sehemu kufunga lango.
Lango la mji linaweza kufunguliwa kuruhusu watu, wanyama, na mizigo kusafiri ndani na nje ya mji.
Kulinda mji, kuta zake na malango ilikuwa nene na imara. Malango yalifungwa na kukazwa na nguzo ya chuma au mbao kuzuia wanajeshi wa maadui kuingia mji.
Lango la mji mara kwa mara ilikuwa kiini cha habari na katikati ya jamii ya kijiji. Pia ilikuwa mahali ambapo mihamala ya kibiashara hufanyika na hukumu kufanyika, kwa sababu kuta za mji zilikuwa na unene wa kutosha kuwa na njia ambayo ilitoa kivuli cha baridi kutoka kwa jua kali. Raia walifurahia kukaa chini ya kivui na kufanya biashara zao na pia kuhumu masuala ya kisheria.
Mapendekezo ya Tafsiri
Kulingana na muktadha, njia zingine za kutafsiri "lango" inaweza kuwa "mlango" au "uwazi wa ukuta" au "kizuizi" au "njia ya kuingia".
Msemo "nguzo za lango" unaweza kutafsiriwa kama "komeo za lango" au "mihimili ya mbao ya kufunga lango" au "chuma cha kufunga lango"
Msemo "mafuriko" ina maana ya kiasi kikubwa cha maji ambacho kinafunika juu ya nchi.
Msemo huu pia hutumika kitamathali kumaanisha kiasi kikubwa cha kitu, haswa kitu ambacho hutokea ghafla.
Katika kipindi cha Nuhu, watu walikuwa waovu hadi Mungu akasababisha mafuriko duniani kote kuwa juu ya uso wote wa dunia, hata kufunika juu za milima. Kila mtu ambaye hakuwa katika mtumbwi pamoja na Nuhu alizama. Mafuriko yote mengine hufunika eneo dogo la nchi.
Msemo huu pia unaweza kuwa tendo kama, "nchi ilifurika na maji ya mto".
Mapendekezo ya Tafsiri
Njia za kutafsiri maana halisi ya "mafuriko" inaweza kujumuisha, "maji yanayomwagikia" au "kiasi kikubwa cha maji"
Mlinganisho wa kitamathali, "kama mafuriko" unaweza kukaa na msemo halisi, au msemo mbadala unaweza kutumika ambao una maana ya kitu ambacho kina hali ya kutiririka kwake, kama vile mto.
Kwa msemo "kama mafuriko ya maji" pale ambapo maji yametajwa tayari, neno "mafuriko" linaweza kutafsiriwa kama "kiasi kikubwa sana" au "yanayomwagikia".
Msemo huu unaweza kutumika kama sitiari kama, "usiruhusu mafuriko kunizoa juu yangu", ambayo ina maana ya "usiruhusu maafa haya makubwa kutokea kwangu" au "usiniache niteketezwe kwa maafa" au "usiache hasira yako initeketeze".
Mafuta ni maji mazito yanayo chukuliwa kutoka kwenye mimea au matunda. Katika Biblia, mafuta yalito kwenye mizeituni.
Maneno haya yote yanamaanisha kuwa hai kimwili, sio kufa. Yanatumika pia kimafumbo kumaanisha kuwa hai kiroho. Yanayofuata yanaelezea nini kinamaanishwa na "maisha ya kimwili" na "maisha ya kiroho."
Kulingana na mazingira, "maisha" inaweza kuetafsiriwa kama "kuwepo" au "mtu" au "roho" au "kuwa" au "kupitia." Neno "uhai" inaweza kutafsiriwa kama "kuishi" au "kukaa" au "kuwepo." Msemo "mwisho wa maisha yake" inaweza kutafsiriwa kama, "alipoacha kuishi." Msemo "alinusuru maisha yao" unaweza kutafisiri kama, "aliwaruhusu waishi" au "hakuwaua." Msemo "walihatarisha maisha yao" unaweza kutafsiriwa kama, "walijiweka hatarini" au "walifanya kitu ambacho kingiweza kuwaua." Bibilia inapozungumzia kuwa hai kiroho, "maisha" yanaweza kutafsiriwa kama "maisha ya kiroho" au "maisha ya milele," kulingana na mazingira. Wazo la "maisha ya kiroho" linaweza pia kutafsiriwa kama, "Mungu kutufanya kuwa hai katika roho zetu" au "maisha mapya kwa Roho wa Mungu" au "kufanywa hai ndani yetu." Kulingana na mazingira, msemo "toa maisha" unaweza kutafsiriwa kama, "kusababisha kuishi" au "kutoa uzima wa milele" au "kusababisha kuishi milele."
Majivu ni vumbi la kijivu linalobaki baada ya kuni kuungua. Hutumika pia kama lugha ya picha kuonesha kitu kisicho na thamani.
Makapi ni ganda kavu linalolinda mbegu ya nafaka. Makapi sio mazuri kwa chakula hivyo watu hutenganisha na mbegu na kuyatupa.
Manemane ni mafuta au manukato yanayo tengenezwa kwa majani ya manemane yanayo ota Africa na Asia.
Mbegu ni sehemu ya mmea unao oteshwa kwenye ardhi kuzalisha aina moja zaidi ya mmea huo. Pia ina maana kadha ya mafumbo.
Neno linalotafsiriwa kama "mbingu" hurejelea mahali anapoishi Mungu. Neno hilo hilo laweza kumaanisha " anga" kwa kutegemea na muktadha. Neno 'mbingu' hurejelea kila kitu tunachokiona juu mawinguni kama vile jua, mwezi, na nyota. Inaweza pia kujumuisha vitu vingine vya anga la mbali kama vile sayari, vitu ambavyo hatuwezi kuviona tukiwa hapa duniani. Neno "anga' hurejelea anga la bluu lililo juu ya dunia ambalo lina mawingu na hewa tunayopumua. Mara kwa mara, jua na mwezi husemwa kuwa ziko 'juu angani. Neno 'mbingu' laweza kumaanisha 'anga' au sehemu ambako Mungu anaishi' hii hutegemea na muktadha mbalimbali. Wakati neno 'mbingu' linapotumika kama tamathali ya semi, humrejelea Mungu mwenyewe. Kwa mfano, Mathayo anapoandika juu ya 'ufalme wa mbinguni' anarejelea ufalme wa Mungu.
Mapendekezo ya tafsiri Wakati neno 'mbingu' linapotumika kimfano laweza kutafsiriwa kama 'Mungu" Maneno 'mbingu' au " vitu vya kimbingu' yaweza kutafsiriwa kama 'jua, mwezi na nyota. Kirai "nyota za mbinguni" chaweza kutafsiriwa kama " nyota za angani."
Mbuzi ni mnyama wa ukubwa wa kati, mwenye miguu minne ambaye analingana na kondoo na hukuzwa kimsingi kwa ajili ya maziwa yake na nyama. Mtoto wa mbuzi huitwa "mwanakibuzi".
Kama kondoo, mbuzi walikuwa wanyama muhimu wa sadaka, haswa wakati wa Pasaka.
Ingawa mbuzi na kondoo wanaweza kufanana, kuna namna ambavyo wako tofauti.
Mbuzi wanya manyoya ya kukwaruza; kondoo wana sufu.
Mkia wa mbuzi husimama juu; mkia wa kondoo huning'inia chini.
Kondoo mara kwa mara hupenda kukaa katika kundi lake, lakini mbuzi wanajitegemea zaidi na kutembea mbali na kundi lao.
Katika kipindi cha Biblia, mbuzi walikuwa chanzo kikuu cha maziwa Israeli.
Ngozi ya mbuzi ilitumika kwa ajili ya kufunika mahema na kutengeza mifuko ya kubeba divai.
Pote katika Agano la Kale na Jipya, mbuzi alitumika kama ishara ya ukosefu wa utakatifu wa watu, labda kwa sababu ya mazoea yao ya kutangatanga mbali na yule aliyekuwa akiwatunza.
Waisraeli pia walitumia mbuzi kama mfano wa mtu mwenye dhambi. Mbuzi mmoja anapotolewa sadaka, kuhani huweka mikono yake juu ya mbuzi wa pili aliye hai na kumwachilia jangwani kama alama ya mnyama kubeba dhambi ya watu.
Mbwa mwitu ni mnyama mkali, anayekula nyama na anafanana na mbwa.
Mchungaji ni mtu anaye linda kondoo. Kitenzi "kuchunga" ina maana ya kulinda kondoo na kuwapa chakula na maji.
Msemo wa "meza" una maana ya kula au kutumia kwa hali ya fujo.
Kutumia neno hili kwa hisi ya tamathali, Paulo anatahadharisha waumini kutojimeza wao kwa wao, akimaanisha kutojishambulia au kuangamizana wao kwa wao kwa maneno au matendo (Wagalitia 5:15).
Pia katika hisi ya tamathali, msemo "kumeza" mara kwa mara hutumika kwa maana ya "kuangamiza kabisa" kama kuzungumzia juu ya mataifa kumeza mengine au moto kumeza majengo na watu.
Msemo huu pia unaweza kutafsiriwa kama "kumeza kabisa" au "kuangamiza kabisa".
Neno "mfalme" linamaanisha mwanamme ambaye ni mtawala mkuu wa mji, jimbo, au nchi.
Mfalme kawaida huchaguliwa kutawala kwa sababu ya uhsiano wake kifamilia na wafalme wa nyuma. Mfalme anapokufa, kawaida mwana wake mkubwa ndiye anayekuwa mfalme mpya. Katika nyakati za zamani, mfalme alikuwa na mamlaka yote juu ya watu katika ufalme wake. Neno "mfalme" halitumiki sana kwa mtu asiye mfalme wa kweli, kama "mfalme Herode" katika Agano Jipya. Katika Biblia, Mungu anajulikana kama mfalme anaye tawala juu ya watu wake. "Ufalme wa Mungu" unamaanisha utawala wa Mungu juu ya watu wake. Yesu aliitwa "Mfalme wa Wayahudi," "mfalme wa Israeli," na "mfalme wa wafalme." Yesu atakaporudi, atatawala kama mfalme wa dunia. Neno hili linaweza kutafsiriwa kama, "mkuu" au "kiongozi kamili" au "mtawala mwenye nguvu." Usemi "mfalme wa wafalme" unaweza kutasiriwa kama "mfalme anayetawala juu ya wafalme wengine wote" au "kiongozi mkuu aliye na mamlaka juu ya viongozi wengine wote."
Msemo, "mgeni" una maana ya mtu anayeishi katika nchi ambayo sio yake.
Katika Agano la Kale, msemo huu haswa humaanisha mtu yeyote ambaye alikuja kutoka kwa kundi tofauti la watu na watu ambao anaishi miongoni mwao.
Mgeni pia ni mtu ambaye lugha yake na utamaduni ni tofauti na ya kwako.
Kwa mfano, Naomi na familia yake alipohama kwenda Moabu, walikuwa wageni kule. Naomi na mkwe wake Ruthu walipohamia Israeli baadaye, Ruthu aliitwa "mgeni" kule kwa saba hakuwa wa Israeli kiasili.
Mtume Paulo aliwaambia Waefeso ya kuwa kabla hawajamjua Kristo, walikuwa "wageni" kwa agano la Mungu.
Mara nyingi, "mgeni" hutafsiriwa kama "mgeni" mtu ambaye hajulikani au hajazoeleka.
Msemo huu "milele" una maana ya kitu ambacho kitaendelea kuwepo au kutadumu daima.
Msemo "milele" una maana ya hali ya kutokuwa na mwanzo au mwisho. Pia inaweza kumaanisha maisha ambayo hayana mwisho.
Baada ya maisha haya ya sasa ya duniani, binadamu wataishi milele aidha mbinguni na Mungu au jehanamu kutengana na Mungu.
Misemo "maisha ya milele" inatumika katika Agano Jipya kumaanisha kuishi milele pamoja na Mungu mbinguni.
Msemo "milele na milele" ina wazo la muda ambao hauna mwisho na huelezea nini milele au maisha ya milele yakoje.
Mapendekezo ya Tafsiri
Njia zingine za kutafsiri "milele" zinaweza kujumuisha "kutokuwa na mwisho" au "kuendelea siku zote".
Msemo "maisha ya milele" unaweza kutafsiriwa kama "maisha ambayo hayana mwisho" au "maisha ambayo yanaendelea bila kikomo" au "kufufua miili yetu kuishi milele".
Kulingana na muktadha, njia tofauti za kutafsiri "milele" zinaweza kujumuisha "kuwepo nje ya muda" au "maisha yasiyo na mwisho" au "maisha mbinguni".
Pia fikiria namna neno hili linatafsiriwa katika Biblia katika lugha ya taifa.
Katika Biblia, msemo "milele" una maana ya muda usiofika mwisho. Mara kwa mara hutumika kitamathali kumaanisha, "muda mrefu sana".
Msemo "milele na milele" unasisitiza ya kwamba jambo litakuwepo milele.
Msemo "milele na milele" ni njia ya kuelezea maisha ya milele yakoje. Pia una wazo la muda ambao hauishi.
Mungu alisema ya kwamba ufalme wa Daudi utakuwepo "milele". Hii inamaanisha ukweli ya kwamba uzao wa Daudi Yesu atatawala kama mfalme milele.
Mapendekezo ya Tafsiri
Msemo huu unaweza kutafsiriwa kama "mara zote" au "kutokuwa na mwisho". Msemo, "utadumu milele" unaweza kutafsiriwa kama "kuwepo mara zote" au "hautakoma" au "utaendelea mara zote". Msemo wa kishindo, "milele na milele" unaweza kutafsiriwa kama "kwa mara zote na zote" au "kutomalizika" au "ambayo haifiki mwisho". Ufalme wa Daudi kudumu milele unaweza kutafsiriwa kama, "uzao wa Daudi atatawala milele" au "uzao wangu ataendelea kutawala".
Neno, "mjumbe" la husu mtu anaye pewa ujumbe kuwa ambia wengine.
Neno 'mkono' limetumika katika Biblia kama lugha ya picha kwa njia mbalimbali Kuweka kitu katika mikono ya mtu fulani inamaana ya kukabidhi kitu hicho. Neno 'mkono' limetumika kurejelea uweza au nguvu ya Mungu na matendo yake. kwa mfano, Mungu anaposema "je si mkono wangu uliyoyafanya haya?" Neno "kabidhi" hurejelea maana ya kuweka kitu katika mkono au utawala wa mtu fulani. Kuweka mikono juu ya mtu fulani mara nyingi huambatana na utoaji wa baraka kwa mtu huyo. Pia kitendo cha 'kuweka mikono" juu ya mtu kinamaanisha kumweka mtu huyo wakfu kwa ajili ya kazi ya Mungu au kwa ajili ya kumwombea mtu huyo uponyaji. Baadhi ya lugha za picha za neno mkono ni: Kunyosha mkono juu ya mtu maana yake ni kumdhuru. ''kumwokoa kutoka katika mkono wa..." ni kumzuia mtu ili asimdhuru mtu mwingine. matumizi mengine ya mkono ni kama: "kunyosha mkono" ina maana ya 'kudhuru' au kuumiza" "kumwokoa mtu mikononi mwa" ina maana ya kumzuia mtu ili asimdhuru mtu mwingine. "kuwa karibu na mkono " kuwa 'karibu' "kuwa mkono wa kuume" humaanisha kuwa 'nafasi'' au ''sehemu ya'' au "upande wa kulia" Maelezo yanayosema "kwa mkono wa'' au ''kupitia mkono'' ina maana kuwa kitendo kimefanya na mtu huyo. kwa mfano, "kwa mkono wa Bwana'' ina maana kuwa Bwana ndiye amefanya tendo hilo. Wakati Paulo anasema " imeandikwa kwa mkono wangu" ina maana kuwa sehemu hii ya barua iliandikwa kwa mkono wake kabisa, badala tu kusema na mtu mwingine akayaandika.
Mapendekezo ya tafsiri. Maelezo haya na tamathali hizi za semi zaweza kutafsiriwa kwa kutumia lugha zingine za picha ambazo zina maana sawa. Au maana inaweza kutafsiriwa kwa kutumia lugha ya moja kwa moja.
Moto ni joto, mwanga na miale ambayo hutokana pale kitu kinapochomwa.
Kuchoma mbao kwa moto hugeuza mbao kuwa majivu.
Msemo "moto" pia hutumika kitamathali, mara kwa mara kumaanisha hukumu au utakaso.
Hukumu ya mwisho ya wasioamini ipo katika moto wa jehanamu.
Moto hutumika kusafisha dhahabu na vyuma vingine. Katika Biblia, hatua hii hutumika kuelezea jinsi Mungu husafisha watu kupitia mambo magumu ambayo hutokea katika maisha yao.
Msemo "kuwabatiza kwa moto" unaweza kutafsiriwa kama "kukusababisha upitie mateso ili kwamba yakusafishe"
Neno "mpendwa" ni kifungu cha kitabia kinachomweleza mtu anayependa na mwingine.
Msemo "mpumbavu" una maana ya mtu ambaye mara kwa mara hutengeneza uchaguzi mbaya, haswa kuchagua kutokutii. Msemo "upumbavu" unaelezea mtu au tabia ambayo siyo ya hekima.
Katika Biblia, msemo "mpumbavu" mara kwa mara una maana ya mtu ambaye haamini au kumtii Mungu. Mara nyingi hii hutofautishwa na mtu mwenye hekima, ambaye humwamini Mungu na kumtii.
Katika Zaburi, Daudi anaelezea mtu mpumbavu kama mtu ambaye hamwamini Mungu, ambaye hupuuza ushahidi wote wa Mungu na uumbaji wake.
Kitabu cha Agano la Kale cha Mithali pia hutoa maelezo mengi ya mpumbavu ni nani, mtu mpumbavu yukoje.
Msemo "upuuzi" una maana ya tendo ambao sio la hekima kwa sababu ni kinyume na mapenzi ya Mungu. Mara nyingi "upuuzi" pia hujumuisha maana ya kitu ambacho ni cha kudharaulika au hatari.
Mapendekezo ya Tafsiri
Msemo "mpumbavu" unaweza kutafsiriwa kama "mtu mpumbavu" au "mtu asiye na hekima" au "mtu asiyejitambua" au "mtu asiyemcha Mungu"
Njia za kutafsiri "mpumbavu" zinawvza kujumuisha "upungufu wa uelewa" au "kutokuwa na hekima" au "kutojitambua".
Neno "msimamizi" la husu mtu aliye mwangalizi wa kazi na maendeleo ya watu wengine.
Kitenzi cha "kuanzishwa" ina maana ya kujengwa juu ya au kutokana na kitu. Msingi ni sehemu ya chini ambapo kitu kunajengwa.
Msingi wa nyumba or jengo lazima uwe na nguvu na kutegemewa ili kuimarisha umbo lote.
Msemo "msingi" unawvza kumaanisha mwanzo wa jambo au muda ambao kitu kiliumbwa.
Kwa kitenzi cha kitamathali, waumini katika Kristo wanalinganishwa na jengo ambalo limejengwa juu ya mafunzo ya mitume na manabii, na Kristo mwenyewe kuwa jiwe la pembeni la jengo.
"Jiwe la msingi" lilikuwa jiwe ambalo lililazwa kama sehemu ya msingi. Mawe haya yalijaribiwa kuhakikisha yalikuwa na nguvu ya kutosha kuimarisha jengo kamili.
Mapendekezo ya Tafsiri
Msemo "kabla ya msingi wa dunia" inaweza kutafsiriwa kama "kabla ya uumbaji wa ulimwengu" au "kabla ya muda ambapo dunia ilianza kuwepo".
Msemo "kujengwa juu ya" inaweza kutafsiriwa kama "kujengwa kwa imara juu ya" au "kujengwa kwa imara kwa".
Kulingana na muktadha, "msingi" inaweza kutafsiriwa kama "msingi imara" au "uimara wa kudumu" au "mwanzo" au "uumbaji"
Neno "mtakatifu'' ni jina ambalo katika Biblia mara zote humrejelea Mungu. Katika Agano la kale, jina hili mara kwa mara lilitokea katika kirai ''mtakatifu wa Israeli" Katika Agano Jipya, jina mtakatifu lilitumika kumrejelea Yesu Mara nyingine katika Biblia, neno mtakatifu hutumika kumrejelea malaika.
Tini ni tunda dogo, laini, tamu ambalo huota juu ya miti. Linapoiva, tunda hili linaweza kuwa na rangi nyingi, ikiwemo kahawia, njano na zambarau.
Mitini inaweza kuota kuwa urefu wa mita 6 na matawi yao makubwa hutoa kivuli kizuri. Tunda hili lina urefu wa sentimita 3-5.
Adamu na Hawa walitumia majani ya mtini kutengeneza mavazi kwa ajili yao baada ya kutenda dhambi.
Mitini inaweza kuliwa mibichi, ikiwa imepikwa, au kukaushwa. Watu pia walikata katika vipande vidogo vidogo na kuzikandamiza kuwa keki kuliwa baadaye.
Katika kipindi cha Biblia, mitini ilikuwa muhimu kama chanzo cha chakula na kipato.
Uwepo wa mitini inayozaa mara kwa mara hutajwa katika Biblia kama ishara ya mafanikio.
Mara kadhaa Yesu alitumia mitini kama mfano wa kufundisha wanafunzi wake kweli za kiroho.
Neno "mtumishi" la weza pia maanisha "mtumwa" na kumueleza mtu anaye mfanyia mtu mwingine kazi, iwe kwa uwamuzi au kwa lazima. Muktadha wa maneno yaliyo zunguka yanaweka dhahiri kuwa kama mtumishi au mtumwa ndiye anaye tajwa.
Katika Biblia neno "muda" utumika sana kama fumbo kueleza wakati maalumu au kipindi cha muda fulani matukio yametokea. Lina maana sawa na "umri" au "wakati."
"Muujiza" ni kitu kinacho shangaza ambacho hakiwezekani pasipo Mungu kusababisha kitokee.
Mwalimu ni mtu anaye toa taarifa mpya. Waalimu wanasaidiana kupata na kutumia maarifa na ujuzi.
Katika Biblia, neno "mwamini" larejerea mtu anayeamini na kumtegemea Yesu Kristo kama Mwokozi.
Kuwa "mwaminifu" kwa Mungu ina maana kuwa na desturi ya kuishi kulingana na mafunzo ya Mungu. Ina maana ya kuwa mwaminifu kwake na kumuamini. Hali ya kuwa mwaminifu ni "uaminifu".
Mtu ambaye ni mwaminifu anaweza kuaminiwa kuweza kushika ahadi zake na kutimiza majukumu yake daima kwa watu wengine.
Mtu mwaminifu huvumilia katika kutenda kazi, hata pale ambapo ni ndefu au ngumu.
Uaminifu kwa Mungu ni matendo ya daima ya kutenda ambacho Mungu anatutaka kufanya.
Mapendekezo ya Tafsiri
Katika muktadha nyingi, "mwaminifu" inaweza kutafsiriwa kama "uaminifu" au "kujitolea" au "kutegemea".
Katika muktadha zingine, "mwaminifu" inaweza kutafsiriwa kwa neno au msemo ambao una maana ya "kuendelea kuamini" au "kuvumilia katika kuamini na kumtii Mungu".
Njia ambazo "uaminifu" inaweza kutafsiriwa inaweza kumaanisha "kuvumilia katika kuamini" au "uaminifu" au "kuamini na kumtii Mungu".
Neno "mwana" la husu mvulana au mwanaume na wazazi wake. La weza eleza mzao wa kiume wa mwanaume au mwana aliye pangwa.
Waandishi walikuwa wasimamizi waliyo wajibika katika kuandika au kunakili nyaraka muhimu za serikali au za kidini kwa mkono. Jina lingine la mwandishi wa Kiyahudi ni "mtaalamu katika sheria ya Kiyahudi."
Mwenzi ni mtu anayekwenda na mtu mwingine au mwenye ushirika na mtu mwingine kwa mfano urafiki au ndoa.
Neno "mwezi" linataja kipindi cha kuishia karibia majuma manne. Idadi ya majuma katika kila mwezi yalitofautiana kulingana na matumizi ya kalenda iliyotumika kwamba ilikumia jua au mwezi.
Vicha vya miba na mbaruti ni majani matawi yaliyo chongoka au maua. Haya majani haya zalishi matunda au chochote kinacho tumika.
Neno "mwili" kwa kawaida linamaanisha mwili wa binadamu au mnyama. Nene hili hutumika pia kitamathari kurejerea kitu au jumla ya kundi lenye wajumbe.
Katika Biblia, msemo "mwili" una maana ya tishu laini ya mwili wa mwanadamu au mnyama.
Biblia pia hutumia msemo "mwili" kitamathali kumaanisha wanadamu wote au viumbe wote.
Katika Agano Jipya, msemo "mwili" unatumika kumaanisha asili ya dhambi ya wanadamu. Hii hutumika mara kwa mara kinyume na asili yao ya kiroho.
Msemo, "mwili na damu yake" ina maana ya mtu ambaye anahusiana kibiolojia na mtu mwingine, kama vile mzazi, ndugu, mtoto au mjukuu.
Msemo "mwili na damu" pia unaweza kumaanisha mababu au vizazi vya mtu.
Msemo "mwili mmoja" una maana ya muungano wa kimwili wa mwanamume na mwanamke katika ndoa.
Mapendekezo ya Tafsiri
Katika muktadha wa mwili wa mnyama, "mwili" unaweza kutafsiriwa kama "mwili" au "ngozi" au "nyama".
Inapotumika kumaanisha viumbe wote hai, msemo huu unaweza kutafsiriwa kama "viumbe hai" au "kila kitu chenye uhai".
Inapomaanisha kwa jumla watu wote, msemo huu unaweza kutafsiriwa kama "watu" au "binadamu" au "kila mtu anayeishi".
Msemo "mwili na damu" unaweza kutafsiriwa kama "jamaa" au "familia" au "ndugu wa karibu" au "ukoo wa familia". Kunaweza kuwa na muktadha ambapo inaweza kutafsiriwa kama "mababu" au "vizazi".
Baadhi ya lugha zinaweza kuwa na msemo ambao unafanana na "mwili na damu".
Msemo "kuwa mwili mmoja" unaweza kutafsiriwa kama "kuungana kimapenzi" au "kuwa kama mwili mmoja" au "kuwa kama mtu mmoja kimwili na roho". Tafsiri ya msemo huu unaweza kuangaliwa kuhakikisha inakubalika katika lugha na utamaduni wako.
Haya maneno "mwizi" na "wezi" yanaeleza kwa jumla watu wanao iba pesa au mali kwa wengine. Neno "jambazi" mara nyingi la eleza mwizi anaye dhuru kimwili au kutishia watu anao waibia.
Mzigo ni kitu kizito. Kwa uhalisia inamaanisha uzito wa kitu ambacho mnyama wa kazi angeweza kubeba. Neno "mzigo" pia linamaana kadhaa za kimafumbo:
Nabii wa uongo ni mtu ambaye hudai kimakosa ya kwamba ujumbe wake unatoka kwa Mungu.
Tabiri za manabii wa uongo mara kwa mara hazitimiliki. Yaani, haziji kuwa kweli.
Manabii wa uongo hufundisha ujumbe ambao kwa juu juu au kwa ukamili hupingana na kile ambacho Biblia husema.
Msemo huu unaweza kutafsiriwa kama "mtu ambaye hudai kwa uongo ya kuwa ni msemaji wa Mungu" au "mtu ambaye hudai kimakosa kuzungumza maneno ya Mungu".
Agano Jipya hufundisha ya kwamba kipindi cha mwisho kutakuwa na manabii wengi wa uongo ambao watajaribu kudanganya watu kufikiri ya kwamba wanatoka kwa Mungu.
Nafsi ni sehemu ya ndani, isiyo onekana ya mtu. Ya husu sehemu isiyo ya kimwili ya mtu.
Msemo wa "najisi" na "kunajisiwa" ina maana ya kuchafuliwa au uchafu. Kitu kinaweza kunajisiwa kihalisia, kimaadili au kwa kaida za dini.
Mungu aliwaonya Waisraeli wasijinajisi kwa kula au kugusa vitu ambavyo vimewekwa wakfu kuwa "chafu" au "kiovu".
Baadhi ya vitu kama maiti na magonjwa ya kuambukiza vilitamkwa na Mungu kuwa vichafu na vinaweza kunajisi mtu iwapo atavigusa.
Mungu aliwaamuru Waisraeli kuacha uasherati. Hivi vingewatia unajisi na kuwafanya kutokubalika kwa Mungu.
Pia kulikuwa na aina kadhaa ya hatua za kimwili ambazo zilimnajisi mtu kwa muda mfupi hadi atakapokuwa safi kwa kaida za dini tena.
Katika Agano Jipya, Yesu alifundisha ya kwamba mawazo ya dhambi na matendo ndiyo haswa yanayomnajisi mtu.
Mapendekezo ya Tafsiri
Msemo wa "najisi" unaweza kutafsiriwa kama "kusababisha kuwa chafu" au "kusababisha kuwa muovu" au "kusababisha kutokubalika kwa kaida za dini".
"Kunajisiwa" kunaweza kutafsiriwa kama "kuwa mchafu" au "kusababisha kutokubalika kimaadili"
Ndoto ni kitu ambacho watu huna au kupitia akilini mwao wanapokuwa wamelala.
Ndoto mara kwa mara huonekana kama zinatokea kihalisia, lakini haziko hivyo.
Mara nyingine Mungu husababisha watu kuota juu ya kitu ili waweze kujifunza kutoka na hicho kitu. Pia anaweza kuzungumza moja kwa moja na watu ndani ya ndoto zao.
Katika Biblia, Mungu alitoa ndoto maalumu kwa baadhi ya watu kuwapa ujumbe, mara nyingi kuhusu jambo ambalo lingetoke hapo baadaye.
Ndoto ni tofauti na maono. Ndoto hutokea wakati mtu amelala, lakini maono mara kwa mara hutokea wakati mtu yupo macho.
Neno "ndugu" kwa kawaida linamaanisha ndugu wa kiume ambaye wanaunganishwa angalau na mzazi mmoja.
Ngao ni chombo kinacho shikiliwa na mwanajeshi katika pambano kuweza kujilinda hasiumizwe na silaha za maadui.
Neno "nia" la husu sehemu ya mtu inayo fikiri na kufanya maamuzi.
Msemo "njaa" una maana ya upungufu mkubwa sana wa chakula katika nchi au eneo lote, mara nyingi kutokana na kutokuwa na mvua ya kutosha.
Mazao ya chakula yanawvza kushindwa kutokana na sababu za asili kama vile ukosefu wa mvua, magonjwa ya mazao, au wadudu.
Upungufu wa chakula pia unaweza kusababishwa na watu, kama vile adui kuangamiza mazao.
Katika Biblia, Mungu mara nyingi huleta njaa kama njia ya kuadhibu mataifa wanapotenda dhambi dhidi yake.
Katika Amosi 8:11 msemo "njaa" unatumika kitamathali kumaanisha kipindi ambapo Mungu aliadhibu watu wake kwa kutozungumza nao. Hii naweza kutafsiriwa kwa neno moja kwa ajili ya "njaa" kwa lugha yako, au kwa msemo kama wa "upungufu mkubwa".
Njiwa na ninga ni aina mbili ya ndege wadogo wa kijivu na kahawia ambao wanafanana. Njiwa mara nyingi hufikiriwa kuwa na rangi iliyo nyepesi, karibu na nyeupe.
Baadhi ya lugha zina majina mawili tofauti kwa ajili yao, wakati wengine wanatumia jina moja kwa wote wawili.
Njiwa na ninga walitumiwa katika sadaka kwa Mungu, hasa kwa watu ambao hawakuweza kununua wanyama wakubwa.
Njiwa mara nyingine huashiria usafi, sio na hatia, au amani.
Kama njiwa au ninga hawajulikani katika lugha ambayo tafsiri inafanywa, msemo huu unaweza kutafsiriwa kama "ndege mdogo, wa kijivu na kahawia anayeitwa njiwa".
Kama njiwa na ninga wote wanawekwa katika mstari mmoja, ni vyema kutumia maneno mawili tofauti kwa ndege hawa, ikiwezekana.
Kuna matumizi kadhaa ya kimafumbo ya neno "nuru" katika Biblia. Mara nyingi inatumika kama sitiari ya haki, utakatifu, na ukweli.
Yesu alisema, "Mimi ni nuru ya ulimwengu" kumaanisha kuwa analeta ujumbe wa kweli wa Mungu duniani na kuwaokoa watu kutoka kwenye giza la dhambi zao. Wakristo wanaamriwa "kutembea nuruni," ambayo inamaanisha wanatakiwa kuishi jinsi Mungu anavyotaka waishi na kuacha kutenda maovu. Mtume Paulo alisema kuwa "Mungu ni nuru," na hakuna giza ndani yake. Nuru na giza ni tofauti kabisa. Giza ni ukosefu wa nuru. Yesu alisema kuwa yeye "ni nuru ya ulimwengu" na kwamba wafuasi wake wanapaswa kung'aa kama nuru duniani, kwa kuishi kwa naamna inayoonesha ukubwa wa Mungu. "Kutembea nuruni" inaonesha kuishi njia inayompendeza Mungu, kufanya yaliyo mema na sawa. Kutembea gizani inaonesha kuishi kwa kuasi dhidi ya Mungu, kufanya mambo maovu.
Neno "nyoka" la husu
Neno "nzige" linamaanisha aina kubwa ya panzi anayepaa ambaye wakati mwingine hupaa katika makundi makubwa ambayo huleta madhara makubwa, wakila mboga zote njiani.
Nzige na panzi wengine ni wakubwa, wenye mabawa yaliyo wima na miguu ya nyuma mirefu inayowapa uwezo wa kuruka mbali. Katika Agano la Kale, makundi ya nzige yanazungumziwa kimafumbo kama alama au picha ya uharibifu mkubwa utakaokuja kama matokeo ya kutokutii kwa Israeli. Mungu alituma nzige kama moja ya mapigo kumi dhidi ya Wamisri. Agano Jipya linasema kuwa nzige walikuwa chanzo kikubwa cha chakula cha Yohana mbatizaji alipokuwa akiishi jangwani.
Neno "okoa" la husu kumzuia mtu kutopitia kitu kibaya au cha hatari. Kuwa "salama" ya maanisha kulindwa na hatari au majanga.
usemi "omboleza" na "maombolezo" yanamaanisha hisia kali ya kulia, majonzi au huzuni.
Wakati mwingine hii ni pamoja na kujuta kwa kina kwa ajili ya dhambi, au huruma kwa watu waliopitia maafa. Maombolezo yanaweza kujumuisha kulia, kutoa machozi au kulia kwa sauti.
"kupanda" ina maana kuweka mbegu kwenye ardhi ilikuweza kuotesha mimea. "Mpandaji" ni mtu anaye mpanda au kupanda mbegu.
Punda ni mnyama wa kazi mwenye miguu minne, anayefanana na farasi, lakini mdogo kidogo na mwenye masikio marefu zaidi.
Nyumbu ni uzao tasa atokanaye na punda dume na farasi jike.
Nyumbu ni wanyama wenye nguvu sana na kwa hiyo ni wanyama wa kazi wenye thamani sana.
Punda na nyumbu wote wanatumika kubeba mizigo na watu wanaposafiri.
Katika kipindi cha Biblia, wafalme huendesha punda katika wakati wa amani, kuliko farasi, ambaye alitumika katika kipindi cha vita.
Yesu aliendesha kuingia Yerusalemu juu ya punda mdogo wiki moja kabla hajasulubiwa kule.
Neno "rehema" lina husu kusaidia mtu waliyo na shida, hususani wanapo kuwa chini au hali ngumu.
Maneno "rithi" na "urithi" zinamaanisha kupokea kitu cha dhamani kutoka kwa mzazi au mtu mwingine kwa sababu ya uhusiano maalumu na huyo mtu. "Mrithi" ni mtu ambaye anapokea urithi.
Urithi wa halisia ambao unapokelewa unaweza kuwa fedha, ardhi, au aina zingine za mali. Urithi wa kiroho ni vyote ambavyo Mungu huwapa watu wanaomuamini Yesu, zikiwemo baraka za maisha ya sasa pamoja na maisha ya milele pamoja naye. Biblia pia inawaiita watu wa Mungu urithi wake, kinachomaanisha kuwa ni wake, ni mali yake ya dhamani. Mungu alimuahidi Abrahamu na uzao wake kuwa watarithi nchi ya Kanaani, kwamba itakuwa yao milele. Kuna maana ya kitamathali na kiroho ya jinsi watu walio wa Mungu wanasemwa "kurithi nchi." Hii inamaanisha kuwa watafanikiwa na kubarikiwa na Mungu kwa mambo ya kimwili na kiroho. Katika Agano Jipya, Mungu anaahidi kuwa wale wanaomuamini Yesu "watarithi wokovu" na "kurithi uzima wa milele." Pia inaelezwa kama, "kurithi ufalme wa Mungu." Huu ni urithi wa milele unaodumu milele. Kuna maana zingine za kitamathali za haya maneno: Biblia inasema kuwa watu wenye hekima "watarithi utukufu" na watakatifu "watarithi vitu vizuri." "Kurithi ahadi" inamaanisha kupokea vitu vizuri ambavyo Mungu ameahidi kuwapa watu wake. Msemo huu pia unatumika kwa njia ya uhasi kumaanisha watu wapumbavu au wasiotii ambao "wanarithi upepo" au "kurithi upumbavu." Hii inamaanisha wanapokea matokeo ya matendo yao ya dhambi, ikiwemo adhabu na maisha yasiyo na maana.
Neno "roho" la eleza sehemu isiyo ya kimwili ya watu isiyo onekana. Mtu anapo kufa, roho yake inaacha mwili wake. "Roho" inaweza eleza tabia au hali ya kihisia ya mtu.
Neno "saa" linatumika mara kwa mara katika Biblia kuonesha muda wa siku jambo fulani lilipotendeka. Pia linatumia tamathari kumaanisha "wakati" au "kitambo"
Kuwa "safi" inamaana kutokuwa na mapungufu au kutochanganya kitu ndani ya kitu ambacho hakitakiwi kuchanganywa. Kukisafisha kitu ni kitendo cha kukisafisha na kuondoa chochote kinachoweza kuchafua.
Kumsamehe mtu ina maana ya kutokaa na kinyongo dhidi ya mtu ambaye alifanya jambo la kuumiza. "Kusamehe" ni tendo la kumsamehe mtu.
Kumsamehe mtu mara nyingi humaanisha kutomuadhibu mtu huyo kwa jambo ambalo amekosa.
Msemo huu unaweza kutumika kitamathali kumaanisha, "katisha" kama msemo "kusamehe deni".
Watu wanapokiri dhambi zao, Mungu huwasamehe kutokana na sadaka ya kifo cha Yesu msalabani.
Yesu aliwafundisha wanafunzi wake kusamehe wengine kama jinsi alivyowasamehe wao.
Mapendekezo ya Tafsiri
Kulingana na muktadha, "samehe" inaweza kutafsiriwa kama "omba radhi" au "katisha" au "achilia" au "kutoshikilia dhidi ya"
Neno "shaba" linamaanisha aina ya madini yatengenezwayo kwa kuyeyusha kwa pamoja metali, shaba nyekundu na bati. Ina rangi nyeusi inayoelekea njano, nyekundu kiasi.
Shahidi ni mtu ambaye amepata uzoefu binafsi wa kitu kilichotokea. Maranyingi shahidi ni mtu anayetoa ushahidi wa jambo analijua kuwa ni kweli. Shahidi pia aneweza kuwa mtu aliyekuwepo pale na kuona kilichotokea.
Misemo ya "shahidi wa uongo" na "shahidi aliyepotoka" ina maana ya mtu anayesema vitu vya uongo juu ya mtu au tukio, mara kwa mara katika mahala rasmi kama mahakamani.
"Ushuhuda wa uongo" au "taarifa ya uongo" ni uongo halisia ambao unaambiwa.
"kutoa ushahidi wa uongo" ina maana ya kudanganya au kutoa taarifa ya uongo kuhusu jambo.
Biblia hutoa habari kadhaa ambapo mashahidi wa uongo waliajiriwa kudanganya kuhusu mtu ili kumfanya mtu huyo kuadhibiwa au kuuwawa.
Mapendekezo ya Tafsiri
"Kuwa shahidi wa uongo" au "kutoa ushahidi wa uongo" unaweza kutafsiriwa kama "kushuhudia uongo" au "kutoa taarifa ya uongo juu ya mtu" au "kuzungumza uongo dhidi ya mtu" au "uongo".
Pale ambapo "shahidi wa uongo" ina maana ya mtu, inaweza kutafsiriwa kama "mtu anayedanganya" au "mtu anayeshuhudia uongo" au "mtu anayesema mambo ambayo siyo ya kweli".
Msemo "shawishi" una maana ya kumsihi mtu kwa nguvu na kumbembeleza mtu kufanya kilicho sahihi. Aini hii ya kusihi inaitwa "kushawishi".
Kusudi la kushawishi ni kusihi watu wengine kuepukana na dhambi na kufuata mapenzi ya Mungu.
Agano Jipya hufundisha Wakristo kujishawishi baina yao kwa upendo, sio kwa ukali au ghafula.
Mapendekezo ya Tafsiri
Kulingana na muktadha, "kushawishi" pia inaweza kutafsiriwa kama "kubembeleza kwa nguvu" au "kusihi" au "kushauri".
Hakikisha tafsiri ya msemo huu hainyoeshi ya kuwa anayeshawishi ana hasira. Msemo unatakiwa kuonyesha nguvu na uzito, lakini usionyeshe kauli ya ukali.
Katika muktadha nyingi, msemo "shawishi" unatakiwa kutafsiriwa tofauti na "kutia moyo" ambayo ina maana ya kutia msukumo, aminisha, au kufariji mtu.
Mara kwa mara msemo huu pia unatafsiriwa tofauti na "onya" ambayo ina maana ya kuonya au kusahisha mtu kwa tabia yake mbaya.
Misemo hii yote inamaanisha amri na maelekezo ambayo Mungu alimpa Musa kwa ajili ya Waisraeli kutii. Misemo "sheria" na "sheria ya Mungu" zinatumika pia kwa ujumla kumaanisha kila kitu Mungu anachotaka watu wake kutii.
Kulingana na mazingira, "sheria" inaweza kumaanisha: Amri kumi ambazo Mungu aliandika katika jiwe kwa ajili ya Waisraeli. sheria zote alizopewa Musa vitabu vitano vya kwanza vya Agano la Kale. Agano lote la Kale (pia inajulikana kama "maandiko" katika Agano Jipya). maelekezo yote ya Mungu na mapenzi yake. Usemi "sheria na manabii" inatumika katika Agano Jipya kumaanisha maandiko ya Kihebrania (au "Agano la Kale").
"Sheria" ni amri ambayo kawaida huandikwa chini na kushurutishwa na mtu aliye madarakani. "Kanuni" ni uongozo kwa ajili ya kufanya maamuzi na tabia.
Zote "sheria" na "kanuni" zinaweza kumaanisha amri au imani inayoongoza tabia ya mtu. Maana hii ya "sheria" ni tofauti kwa maana ya kutoka "sheria ya Musa" ambapo inamaanisha amri na maelekezo ambayo Mungu aliwapa Waisraeli. Wakati sheria ya ujumla inapotajwa,"sheria" inaweza kutafsiriwa kama "kanuni" au "amri ya jumla."
Sifa ni kitendo cha kujulikana na kuwa na sifa.
Neno "siku" kwa kawaida lamaanisha kipindi cha masaa 24 kuanzia kuzama kwa jua. Linatumika pia kitamathari.
Usemi "siku ya hukumu" inamaanisha siku ya usoni ambapo Mungu atamhukumu kila mtu.
Mungu amemfanya Mwanaye, Yesu Kristo, kuhukumu watu wote. Katika siku ya hukumu, Kristo atawahukumu watu kulingana na asili yake ya haki.
Kwa ujumla, sikukuu ni sherehe iliyofanyika na jamii ya watu.
Neno kwa ajili ya "sikukuu" katika Agano la Kale lina maana ya "muda ulioteuliwa".
Sikukuu zinazosherehekewa na Waisraeli zilikuwa nyakati maalumu zilizoteuliwa au nyakati ambazo Mungu aliwaamuru wao kuzifuata.
Katika baadhi ya tafasiri za Kiingereza, neno "sikukuu" linatumika badala ya karamu kwa sababu sherehe zilijumuisha mlo mkubwa wa pamoja.
Kulikuwa na karamu kadhaa ambazo Waisraeli walisherehekea kila mwaka: Pasaka Sikukuu ya Mkate Usiotiwa Chachu Mavuno ya Kwanza Sikukuu ya Wiki (Pentakuki) Sikukuu ya Tarumbeta Sikukuu ya Kulipia Kosa Sikukuu ya Vibanda Kusudi la sikukuu hizi ilikuwa kumshukuru Mungu na kukumbuka mambo ya ajabu aliyofanya kuwaokoa, kuwalinda na kuwapa watu wake.
Sinagogi ni jengo la watu wa Kiyahudi wanapo kutania pamoja kumuabudu Mungu.
Usemi "sio na hatia" unamaanisha kutokuwa na hatia la uhalifu au makosa mengine. Inaweza pia kumaanisha kwa ujumla watu ambayo hawahusiki na matendo maovu.
Mtu anayetuhumiwa kwa kufanya kitu kibaya hana hatia kama hataambatanishwa na hilo kosa. Wakati mwingine usemi "sio na hatia" unatumika kumaanisha watu ambao hawajafanya kosa kustahili ubaya wanaoupata, kama jeshi la adui kushambulia "watu wasio na hatia."
Katika Biblia, neno "siri" la husu kitu kisicho julikana au kigumu kuelewa ambacho Mungu sasa anaelezea.
"Stahili" linaelezea mtu au kitu kinachofaa kupewa heshima. "Kustahilisha" inamaana ya kuwa na thamani au muhimu. "isiyo na maana" inamaanisha isiyo na thamani.
Neno "taa" kawaida inamaanisha kitu kinachotoa mwanga. Taa zilizotumika nyakati za Biblia kawaida zilikuwa taa za mafuta. Aina ya taa iliyotumika katika Biblia ni chombo na sehemu ya kuwekea mafuta, yanayotoa mwanga inapowashwa.
Kawaida taa za mafuta zilitengenezwa kwa chombo cha kawaida cha udongo kilichojaa mafuta ya mzeituni, na utambi ukiwekwa kwenye mafuta ili uwake. Kwa baadhi ya taa, chombo lilikuwa na umbo la yai, na sehemu moja ikiwa imefinywa karibu kuushikilia utambi. Taa ya mafuta iliweza kubebwa au kuwekwa katika kinara ili mwanga wake ujaze chumba au nyumba. Katika maandiko, taa zinatumika kwa njia kadhaa kimithali kama ishara ya mwanaga na uhai.
Neno "tafuta" la maanisha kutafuta kitu au mtu. Inaweza kuwa na maana ya "jaribu kwa bidii" au "tia juhudi" kufanya kitu.
Tai ni ndege mbua mkubwa sana, mwenye nguvu ambaye hula wanyama wadogo kama vile samaki, panya, nyoka na kuku.
Biblia hulinganisha kasi na nguvu ya jeshi kwa jinsi tai hupaa chini kukamata nyama yake kwa kasi na ghafla.
Isaya anasema ya kwamba wale wanaomtumaini Bwana watapaa juu kama tai afanyavyo. Hii ni lugha ya tamathali inayotumika kuelezea uhuru na nguvu ambao unakuja kutokana na kumuamini na kumtii Mungu.
Katika kitabu cha Danieli, urefu wa nywele za Mfalme Nebukadreza zililinganishwa na urefu wa manyoya ya tai, ambayo yanaweza kuwa zaidi ya sentimita 50.
Msemo "takatifu" una maana ya kitu chochote kinachomhusu Mungu.
Baadhi ya njia ambazo msemo huu unatumika ni, "mamlaka takatifu", "hukumu takatifu", "asili takatifu", "nguvu takatifu", na "utukufu mtakatifu".
Katika sehemu moja ndani ya Biblia, msemo "takatifu" unatumika kuelezea jambo juu ya uungu wa uongo.
Mapendekezo ya Tafsiri
Njia za kutafsiri msemo wa "takatifu" zinaweza kujumuisha "ya Mungu" au "kutoka kwa Mungu" au "fungamana na Mungu" au "huonyesha ni ya Mungu".
Kwa mfano, "mamlaka takatifu" inaweza kutafsiriwa kama "mamlaka ya Mungu" au "mamlaka ambayo yanatoka kwa Mungu".
Msemo wa "utukutufu takatifu" unaweza kutafsiriwa kama "utukufu wa Mungu" au "utukufu ambao Mungu ame" au "utukufu unatoka kwa Mungu".
Baadhi ya tafsiri zinapendelea kutumia neno tofauti wanapofafanua jambo ambalo linafungamana na mungu wa uongo.
Maneno 'takatifu' na 'utakatifu' hurejelea tabia ya Mungu ambayo imetengwa na kutofautishwa na kila kitu ambacho ni chenye dhambi na kisicho kamili. Mungu pekee ndiye mtakatifu kweli. Hufawafanya watu na vitu kuwa vitakatifu. Mtu aliye mtakatifu ni mali ya Mungu na ametengwa maalumu kwa kusudi la kumtumika Mungu na kumpa utukufu Yeye. Na kitu ambacho Mungu amekitangaza kuwa ni kitakatifu ni kile ambacho Mungu amekitenga kwa ajili ya utukufu wake na matumizi yake, kwa mfano madhabahu ambayo makusudi yake ni kumtolea Mungu sadaka. Kwa kuwa Mungu ni mtakatifu, hakuna mtu awezaye kumkaribia Mungu isipokuwa awe ameruhusiwa na Yeye kufanya hivyo, hii ni kwasababu wao ni watu tu, wenye dhambi na wasiokamili. katika Agano la Kale, Mungu alitenga makuhani kama watakatifu kwa huduma maalumu kwake. Walitakiwa kutakaswa kwa sherehe maalumu ili waweze kumkaribia Mungu. Mungu pia aliweza kutenga sehemu na vitu maalumu kuwa vitakatifu vilivyo mali yake au kupitia kwa vitu hivyo aweze kujifunua mwenyewe, vitu hivi ni kama hekalu.
Mapendekezo ya tafsiri Njia za kutafsiri neno 'takatifu' zinaweza kuwa ' kutengwa kwa ajili ya Mungu,' au "kuwa mali ya Mungu" au "hali ya kutokuwa na dhambi" au "kuwa safi." kufanya kitu/kuwa kuwa mtakatifu ina maana ya "kutakasa'' au ''kutenga''
Neno "takatifu" la elezea kitu kinacho husu kumuabudu Mungu au wapagani wanao abudu miungu ya uongo.
Msemo "tambua" una maana ya kuweza kuelewa jambo, haswa kuweza kujua kama jambo ni sahihi au baya.
Msemo wa "tambuzi" una maana ya kuelewa na kuamua kwa hekima kuhusu jambo fulani.
Ina maana kuwa na hekima na maamuzi mazuri.
Mapendekezo ya Tafsiri
Kulingana na muktadha, "tambua" inaweza pia kutafsiriwa kama "kuelewa" au "kujua tofauti kati ya" au "kutofautisha mema na mabaya" au "kuhukumu sahihi kuhusu" au "kuelewa mema kwa mabaya".
"Tambuzi" inaweza kutafsiriwa kama, "uelewa" au "uwezo wa kuchambua mema na mabaya"
Msemo wa "tamka" au "tamko" una maana ya kutoa kauli maalumu kwa umma, mara nyingi kusisitiza jambo.
"Tamko" halisisitizi umuhimu tu wa kile kinachotamkwa, lakini inavuta nadhari kwa yule anayetoa tamko hilo.
Kwa mfano, katika Agano la Kale, ujumbe kutoka kwa Mungu mara nyingi hutanguliwa na "tamko la Yahwe" au "hivi ndivyo Yahwe asemavyo". Msemo huu unasisitiza ya kwamba ni Yahwe mwenyewe anayesema hivi. Ukweli ya kwamba ujumbe unatoka kwa Yahwe unaonyesha jinsi ujumbe ulivyo na umuhimu.
Mapendekezo ya Tafsiri
Kulingana na muktadha, "tamka" inaweza pia kutafsiriwa kama "tangaza" au "eneza wazi" au "sema kwa nguvu" au "tamka kwa kishindo".
Msemo "tamko" unaweza kutafsiriwa kama, "kauli" au "tangazo".
Msemo, "hili ni tamko la Yahwe" linaweza kutafsiriwa kama, "hivi ndivyo Yahwe anavyotamka" au "hivi ndivyo Yahwe anavyosema".
Neno "tarumbeta" la eleza chombo cha kutoa mziki au kuita watu pamoka kwa mkutano au kikao.
Msemo "tawanya" na "mtawanyiko" ina maana ya kutawanya watu au vitu katika pande nyingi tofauti.
Katika Agano la Kale, Mungu anazungumza kuhusu "kutawanya" watu, kusababisha wao wajitenge na kuishi katika maeneo tofauti kati yao. Alifanya hivi kuwaadhibu kwa dhambi yao. Huenda kutawanyika ingeweza kuwasaidia kutubu na kuanza kumwabudu Mungu tena.
Msemo "mtawanyiko" unatumika katika Agano Jipya kumaanisha Wakristo ambao walitakiwa kuacha nyumba zao na kuhamia katika mahali tofauti nyingi kutoroka mateso.
Msemo "tawanyiko" unaweza kutafsiriwa kama "waumini katika maeneo mengi tofauti" au "watu waliohama kuishi katika mataifa tofauti".
Msemo "tawanya" unaweza kutafsiriwa kama "kutuma mbali katika maeneo mengi tofauti" au "kusambaza ng'ambo" au "kusababisha kuhamisha mbali kuishi katika nchi tofauti"
Msemo wa "kuteketezwa" au "uharibifu" ina maana ya kufanya mali ya mtu au ardhi kuharibika au kuangamizwa. Pia mara kwa mara hujumuisha kuangamiza au kukamata watu waishio katika ardhi hiyo.
Hii ina maana ya maangamizi kamili na makali sana.
Kwa mfano, mji wa Sodoma uliteketezwa na Mungu kama adhabu kwa dhambi za watu walioishi pale.
Msemo "uharibifu" unaweza kujumuisha kusababisha majonzi ya hisia yatokanayo na hiyo adhabu au uharibifu.
Mapendekezo ya Tafsiri
Msemo "teketeza" unaweza kutafsiriwa kama "kuangamiza kabisa" au "kuharibu kabisa".
Kulingana na muktadha, "uharibifu" inaweza kutafsiriwa kama "maangamizi kamili" au "uharibifu kamili" au "majonzi ya juu sana" au "balaa".
Maneno "teseka" na "kuteseka" yanaeleza kupitia kitu kisicho pendeza, kama ugonjwa, maumivu, au magumu.
Neno "tetemeka" lina maana ya kutikisika kwa hofu au msongamano wa mawazo.
Neno "theluji" ya husu chembe nyeupe za maji yaliyo ganda yanayo anguka kutoka mawinguni sehemu ambazo hali ya hewa ni ya baridi.
Thibitisha au uthibitisho ni kuwa na hakika kuwa jambo fulani ni la kweli au kuaminika.
Neno "tii" lina maana ya kufanya unachopaswa au kuamriwa. Neno "mtiifu" la eleza tabia ya mtu anaye tii. Wakati mwengine amri ni kuhusu kutofanya kitu, "usiibe"
Msemo "timiza" una maana ya kukamilisha au fanikisha jambo ambalo lilitarajiwa.
Pale ambapo unabii unatimizwa, ina maana ya kwamba Mungu alisababisha itokee kile kilichotabiriwa katika unabii.
Kama mtu anatimiza ahadi au kiapo, ina maana ya kwamba anafanya kile alichoahidi kufanya.
Kutimiza jukumu ina maana kufanya kazi ambayo ulipangiwa au unapaswa kufanya.
Mapendekezo ya Tafsiri
Kulingana na muktadha, "timiza" unaweza kutafsiriwa kama "fanikisha" au "kamilisha" au "kusababisha kutokea" au "kutii" au "kutenda".
Msemo "imetimizwa" inaweza kutafsiriwa kama "imekuwa kweli" au "imetokea".
Njia za kutafsiri "timiza" kama vile "timiza huduma yako" inaweza kujumuisha, "maliza" au "fanya" au "mazoezi" au "tumikia watu wengine kama vile Mungu amekuita kufanya"
Mara kwa mara, "towashi" ina maana ya mwanamume ambaye amehanithishwa. Msemo baadaye ukawa msemo wa jumla kumaanisha afisa yeyote wa serikali, hata wale ambao hawana ulemavu huu.
Yesu alisema ya kwamba baadhi ya towashi walizaliwa vile, yawezekana kwa sababu ya uharibifu ya viuongo vya siri au kwa sababu ya kutokuwa kutekeleza jukumu la kuingiliana. Wengine huchagua kuishi kama towashi kwa maisha ya mseja.
Katika nyakati za kale, matowashi mara nyingi walikuwa watumishi wa wafalme ambao waliwekwa kama walinzi katika maeneo ya wanawake.
Baadhi ya matowashi walikuwa maafisa muhimu wa serikali, kama vile towashi wa Ethiopia ambaye alikutana na mtume Filipo katika jangwa.
Kutukuza ni kusifu kwa juu sana na kumheshimu mtu. Inaweza kumaanisha kumweka mtu katika nafasi ya juu.
Katika Biblia, msemo "tukuza" unatumika sana kwa ajili ya kumtukuza Mungu.
Mtu anapojitukuza mwenyewe, ina maana anawaza juu yake mwenyewe kwa hali ya kujiinua au namna ya kiburi.
Mapendekezo ya Tafsiri
Njia za kutafsiri "tukuza" zinaweza kujumuisha "kusifu kwa juu" au "kuheshimu sana" au "sifu sana" au "kuzungumza kwa juu sana"
Katika baadhi ya muktadha, inaweza kutafsiriwa kwa neno au msemo ambao una maana ya "kuweka nafasi ya juu zaidi" au "kutoa heshima zaidi" au "kuzungumza kuhusu kwa kiburi".
"Usijitukuze mwenyewe" inaweza kutafsiriwa kama "Usijiwazie kuwa juu sana" au "Usijidai juu yako mwenyewe".
"Wale wanaojiinua wenyewe" inaweza kutafsiriwa kama "Wale ambao hufikiri kwa kiburi kuhusu wao wenyewe" au "Wale wanaojidai juu yao wenyewe"
Msemo "tukuza" ina maana ya kuonyesha au kunena jinsi gani kitu au mtu ni mkubwa au muhimu. Ina maana ya "kutoa utukufu".
Watu wanaweza kumtukuza Mungu kwa kunena juu ya mambo mazuri aliyoyafanya.
Wanaweza kumtukuza Mungu kwa kuishi kwa njia ambayo inampa heshima na kuonyesha jinsi alivyo mkuu na wa ajabu.
Biblia inaposema ya kwamba Mungu hujitukuza mwenyewe, ina maana anajifunua kwa watu ukubwa wake wa ajabu, mara kwa mara kupitia miujiza.
Mungu Baba atamtukuza Mungu Mwana kwa kudhihirisha kwa watu ukamilifu wa Mwana, ufaharu na ukuu.
Kila mtu anayemwamini Kristo atatukuzwa na yeye. Wanapofufuliwa katika uzima, watabadilishwa kuakisi utukufu wake na kuonyesha neema yake kwa uumbaji wote.
Mapendekezo ya Tafsiri
Msemo huu unaweza kutafsiriwa kama "kutoa utukufu kwa" au "kuleta utukufu kwa" au "kusababisha kuonekana kubwa".
Msemo "mtukuza Mungu" unaweza kutafsiriwa kama "kumsifu Mungu" au "kuzungumza juu ya ukuu wa Mungu" au "kuonyesha jinsi Mungu alivyo mkuu" au "kumheshimu Mungu"
"Kutuma" ni kusababisha mtu au kitu kwenda sehemu. "Kutuma nje" mtu ni kumwambia huyu mtu kwenda na kufanya japo au shughuli.
Msemo "tunda" lina maana ya sehemu ya mmea ambao inaweza kuliwa. Kitu ambacho "kinazaa" kina matunda mengi. Misemo hii pia hutumika kitamathali katika Biblia.
Biblia mara kwa mara hutumia "tunda" kumaanisha matendo na mawazo ya mtu. Kama vile tunda juu ya mti linavyoonyesha ni aina gani ya mti, vile vile maneno na matendo ya mtu hudhihirisha silika yake ikoje.
Mtu anaweza kuzaa matunda ya kiroho mazuri au mabaya, lakini msemo "kuzaa" mara kwa mara una maana chanya ya kuzaa matunda mema.
Msemo "kuzaa" pia hutumika kitamathali kumaanisha "mafanikio". Hii mara kwa mara humaanisha kuwa na watoto na uzao mwingi, pamoja na kuwa na chakula kingi na utajiri mwingine.
Kwa ujumla, msemo "tunda la" una maana ya kitu chochote ambacho hutoka kwa au ambacho huzalishwa na kitu kingine. Kwa mfano, "tunda la hekima" lina maana ya mambo mazuri ambayo hutokana na kuwa na hekima.
Msemo "tunda la roho" una maana kijumla ya kila kitu ambacho nchi huzaa kwa ajili ya watu kula. Hii inajumlisha sio matunda pekee kama mizabibu au tende, lakini pia mboga, karanga na nafaka.
Msemo wa tamathali "tunda la Roho" una maana ya sifa nzuri ambazo Roho Mtakatifu hutoa katika maisha ya watu ambao humtii yeye.
Msemo "tunda la tumbo" una maana ya "kile ambacho tumbo huzaa" yaani, watotot.
"Ua" ni eneo ambalo liko wazi juu na limezungukwa na ukuta. Neno "mahakama" linamaanisha sehemu ambayo hakimu huamua mambo ya sheria na jinai.
Ufalme ni kundi la watu linalotawalwana mfalme. Linamaanisha pia dola au sehemu za kisiasa ambalo mfalme au kiongozi mwingine ana madaraka na mamlaka.
Ufalme unaweza kuwa na ukubwa wowote kijiografia. Mfalme anaweza kutawala taifa au nchi au mji mmoja tu. Neno "ufalme" linaweza pia kumaanisha utawala wa kiroho au madaraka, kama usemi "ufalme wa Mungu." Mungu ni mtawala wa viumbe vyote, lakini usemi "ufalme wa Mungu" kwa mahsusi linamaanisha utawala juu ya watu waliomwamini Yesu na walionyenyekea kwa utawala wake. Biblia pia inazungumzia kuhusu Shetani kuwa na "ufalme" anao tawala kwa muda juu ya vitu vingi duniani. Ufalme wake ni uovu na unajulikana kama wa "giza."
Usemi wa "ufalme wa Mungu" na "ufalme wa mbinguni" zote zinamaanisha utawala wa Mungu na madaraka yake juu ya watu wake na viumbe vyote.
Wayahudi mara nyingi hutumia neno "mbingu" kumaanisha Mungu, ili kuepuka kutaja jina lake moja kwa moja. Katika kitabu cha Agano Jipya alichoandika Mathayo, aliuita ufalme wa Mungu kama "ufalme wa mbinguni," inawezekana kwa sababu alikuwa akiwaandikia zaidi Wayahudi. Ufalme wa Mungu unamaanisha Mungu kuwatawala watu kiroho pamoja na kuwatawala katika dunia ya kimwili. Manabii wa Agano la Kale walisema kuwa Mungu atamtuma Masihi kutawala kwa haki. Yesu, mwana wa Mungu, ndiye Masihi atakaye tawala juu ya watu wa Mungu milele.
Ujasiri ni kitendo cha kukabiliana au kufanya jambo gumu au la hatari.
Neno "ukoma" linatumika katika Biblia kumaanisha aina kadhaaza magonjwa ya ngozi. "Mkoma" ni mtu mwenye ukoma. Neno "ukoma" pia linaweza kutumika kuelezea mtu au sehemu ya mwili iliyoadhirika na ukoma.
Aina flani za ukoma zinasababisha ngozi kupoteza rangi na mabaka meupe, kama Miriamu na Naamani walivyokuwa na ukoma. Katika nyakati za sasa, ukoma mara nyingi husababisha mikono, miguu, na sehemu zingine za mwili kuharibika. Kulingana na maelekezo ambayo Mungu aliwapa Waisraeli, mtu akiwa na ukoma, alionekana "mchafu" na ilimbidi kukaa mbali na watu wengine ili asiwaambukize na ugonjwa. Mkoma kawaida angasema "mchafu" ili wengine waonywe wasije karibu yake. Yesu aliponya wakoma wengi, pamoja na aina zingine za magonjwa.
Maneno haya yote yanatumika kumaanisha sanamu ambazo zimetengenezwa kwa ajili ya kuabudu miungu ya uongo. Katika mazingira ya kuabudu sanamu, neno "sanamu" ni njia fupi ya kusema "sanamu ya kuchonga."
"Sanamu ya kuchonga" au "umbo la kuchonga" ni kitu cha mbao kilichofanywa kuonekana kama mnyama, mtu, au kitu. "Umbo la chuma" ni kitu au sanamu iliyoundwa kwa kuyeyusha chuma na kuimwaga katika umbo tupu ambalo lina umbo la kitu, mnyama, au mtu. Vitu hivi vya mbao na chuma vilitumika katika kuabudu miungu ya uongo. Neno "umbo" wakati wa kuzungumzia sanamu inamaanisha kati ya sanamu ya mbao au ya chuma.
Neno "kilichopotoka" linatumika kumuelezea mtu au tendo fulani ambalo linapotosha kimaadili. Neno "ukaidi" linamaana ya tabia ya kikaidi". Kupotosha kitu inamaana ya kugeuza jambo toka kwenye usahihi wake au uzuri wake.
Neno "uovu" ni neno ambalo liko karibu kwa maana na neno "dhambi," lakini inaweza kumaanisha zaidi matendo ya ufahamu mabaya au uovu mkubwa.
Neno "uovu" ina maana halisi ya kupindisha au kupotosha (sheria). Inamaanisha udhalimu mkubwa. Uovu unaweza kuelezwa kama matendo ya kudhuru ya makusudi dhidi ya watu wengine. Maana zingine za uovu ni pamoja na "ukaidi" na "kunyima," ambayo yote ni maneno yanayoeleza hali za dhambi mbaya.
Upanga ni silaha ya chuma nyembamba inayo tumika kukata au kuchoma. Ina mshikio na nch ndefu.
Kumpenda mtu mwingine ni kumjali huyo mtu na kufanya vitu vitakavyo msaidia. Kuna maana tofauti za "upendo" ambazo lugha zingine zinawezakueleza kwa kutumia maneno tofauti:
Yesu alionesha aina hii ya upendo kwa kujitolea maisha yake kama sadak ili kutuokoa kutoka kwenye dhambi na mauti. Aliwafundisha pia wafuasi wake kuwapenda wengine kwa kujitolea. Watu wanapowapenda wengine na aina hii ya upendo, inahusisha matendo yanayoonesha kuwa mtu anafikiria yale yatakomsaidia mtu mwingine kufanikiwa. Aina hii ya upendo inahusisha zaidi kusamehe wengine. Katika ULB, neno "upendo" linamaanisha aina hiiya upendo wa kujitoa, isipokuwa noti ya tafsiri iashirie maana tofauti.
Neno hili linamaanisha upendo wa asili wa binadamu kati ya marafiki na ndugu. Inawezekana kutumika katika mazingira kama, "Wanapenda kukaa kwenye viti muhimu katika sherehe." Hii inamaanisha "wanatamani sana" kufanya hivyo.
Neno "upole" la elezea mtu aliye mtaratibu, mnyenyekevu, na aliye tayari kuteseka dhuluma. Upole ni uwezo wa kuwa mtaratibu ata kama ukali au nguvu inaonekana ni sahihi.
Ushauri inamaana ya kumsaidia mtu kuamua kwa busara juu ya jambo fulani. Mshauri mwenye busara ni mtu anayetoa ushauri ambao utamsaidia mtu kuamua kwa usahihi.
Maneno, "ushuhuda" na "shuhudia" yanaeleza kutamka tamko kuhusu kitu ambacho mtu anajua kuwa ni kweli.
Neno "ushuru" la husu zawadi kutoka kwa mtawala mmoja kwenda kwa mwingine, kwa kusudi la ulinzi na mausiano mema kati ya mataifa yao.
Ushuru ni pesa au bidha watu wanazo lipa kwa serikali iliyo na mamlaka juu yao.
Neno "uso" lina maana ya sehemu ya mbele ya kichwa cha mtu. Msemo huu pia una maana kadhaa za tamathali.
Msemo wa "uso wako" mara kwa mara ni njia ya tamathali ya kusema "wewe". Vivyo hivyo, msemo "uso wangu" mara kwa mara una maana ya "Mimi".
Katika hali ya kimwili, "kumkabili" mtu au kitu ina maana ya kutazama upande wa huyo mtu au kitu.
"Kukabiliana" ina maana ya "kutazamana"
Kuwa "uso kwa uso" ina maana ya kwamba watu wawili wanatazamana katika umbali wa karibu.
Yesu "alipoweka uso wake kuelekea Yerusalemu" ina maana ya kwamba aliamua kwa dhati kwenda.
"Kuweka uso dhidi ya" watu au mji ina maana kuamua kwa nguvu: kutoimarisha tena, au kumkataa mtu au mji huo.
Msemo "uso wa nchi" una maana ya sehemu ya juu ya dunia na mara kwa mara ni kumbukumbu ya jumla ya dunia nzima. Kwa mfano, "njaa inayofunika uso wa dunia" ina maana ya njaa inayosambaa ambayo hugusa watu wengi wanaoishi juu ya nchi.
Msemo wa tamathali, "usifiche uso wako kwa watu wako" una maana "usiwakatae watu wako" au "usiwaache watu wako" au "usiache kuwatunza watu wako".
Mapendekezo ya Tafsiri
Ikiwezekana, ni bora kubaki na msemo au kutumia msemo katika lugha hii ambayo ina maana ya kufanana.
Msemo "kukabili" unaweza kutafsiriwa kama "kugeuka upande wa" au "kutazama moja kwa moja" au "kuangalia uso wa".
Msemo "uso kwa uso" unaweza kutafsiriwa kama "karibu kabisa" au "mbele ya" au "katika uwepo wa".
Kulingana na muktadha, msemo "mbele ya uso wake" unaweza kutafsiriwa kama "kabla yake" au "mbele yake" au "katika uwepo wake".
Msemo "weka uso wake kuelekea" unaweza kutafsiriwa kama "kuanza kusafiri kuelekea" au "aliamua akilini mwake kuondoka".
Msemo "kuficha uso wake kutoka kwa" unaweza kutafsiriwa kama "kugeuka kutoka kwa" au "kuacha kusaidia au kulinda" au "kukataa".
"Kuweka uso wake dhidi ya" mji au watu inaweza kutafsiri kama "kutazama kwa hasira na kushutumu" au "kukataa kukubali" au "kuamua kukataa" au "kulaumu na kukataa" au "kutoa kuhukumu".
Msemo "tamka mbele ya uso wao" inaweza kutafsiriwa kama "sema kwao moja kwa moja".
Msemo " katika uso wa nchi" inaweza kutafsiriwa kama "katika nchi yote" au "juu ya dunia nzima" au "kuishi katika dunia".
Kwa ujumla, msemo "utukufu" una maana ya heshima, fahari, na ukuu wa hali ya juu sana. Kitu chochote ambacho kina utukufu kinasemekana kuwa na "fahari".
Mara nyingi, "utukufu" ina maana ya kitu chenye thamani kubwa na umuhimu. Katika muktadha zingine inawasilisha ufahari, mwanga, au hukumu.
Kwa mfano, msemo "utukufu wa wafugaji" una maana ya malisho yaliyostawi sana ambapo kondoo wao walikuwa na nyasi nyingi za kula.
Utukufu haswa hutumika kumfafanua Mungu, ambay ana ufahari zaidi ya yeyote au chochote katika ulimwengu. Kila kitu katika tabia yake huonyesha utukufu na ufahari wake.
Msemo "kutukuzwa na" una maana ya kujidai juu ya au kujivunia na kitu.
Neno "utukufu" la eleza uzuri wa ajabu na umaridadi ambao una ambatana na utajiri na muonekano wa kuvutia.
Neno "uvumba" linamaanisha mchanganyiko wa vikolezo vyenye manukato mazuri vinavyochomwa kutoa moshi wenye harufu nzuri.
Mungu aliwaambia Waisraeli kuchoma uvumba kama sadaka kwake. Huu uvumba ulitakiwa kutengenezwa kwa kuchanganya kiwango sawa cha vikolezo maalumu vitano kama Mungu alivyoagiza. Huu ulikuwa uvumba mtakatifu, kwa hiyo hawakutakiwa kuutumia kwa kitu kingine chochote. "Madhabahu ya kufukuzia uvumba" ilikuwa madhabahu maalumu ya kuchomea uvumba. Uvumba ulitolewa angalau mara nne kwa siku, kwa kila saa ya maombi. Ilitolewa pia kila wakati sadaka ya kuteketeza ilipotolewa. Kuchomwa kwa uvumba kunaashiria maombi na kuabudu vinaponyanyuka juu kwa Mungu kutoka kwa watu wake. Njia zingine za kutafsiri "uvumba" zinaweza kuwa, "vikolezo vya manukato mazuri" au "mimea yenye harufu nzuri."
Neno "uwezo" la husu kuwa na nguvu nyingi.
Neno "uwezo" la husu hali ya kuwa na nguvu kimwili, kihisia, au kiroho.
"Uzao" ni mtu ambaye ni ndugu wa damu moja kwa moja wa mtu mwingine nyuma kabisa katika historia.
Kwa mfano, Abrahamu alikuwa uzao wa Nuhu. Uzao wa mtu ni watoto wake, wajukuu, na watukuu, na kuendelea. Vizazi vya Yakobo vilikuwa makabila kumi na mawili ya Israeli.
msemo "kutokana na" ni njia nyingine ya kusema "uzao wa" kama vile "Abrahamu alitokana na Nuhu". Hii inaweza kutafsiriwa kama "kutokana na uzao wa"
Msemo "vumilia" una maana ya kudumu muda mrefu au kustahamili jambo gumu kwa uvumilivu.
Pia ina maana ya kusimama imara wakati wa mitihani kuwepo, bila kukata tamaa.
Msemo "uvumilivu" unaweza kumaanisha "subira", "ustahamilivu katika majaribu" au "kustahamili pale unapoteswa".
Faraja kwa Wakristo "kuvumilia mpaka mwisho" ni kuwaambia wamtii Yesu, hata kama hili litasababisha wao kuteseka.
"Kuvumilia mateso" pia inaweza kumaanisha "kupitia mateso".
Mapendekezo ya Tafsiri
Njia za kutafsiri msemo "vumilia" zinaweza kujumuisha "stahamili" au "kuendelea kuamini" au "kuendelea kufanya kile Mungu anachotaka ufanye" au "simama imara".
Katika baadhi ya muktadha, "kuvumilia" kunaweza kutafsiriwa kama, "kupitia jaribu" au "kupitia".
Kwa maana ya kudumu muda mrefu, msemo "vumilia" unaweza kutafsiriwa kama "kudumu" au "kuendelea". Msemo, "hatavumilia" unaweza kutafsiriwa kama, "hatadumu" au "hataendele kuishi".
Njia za kutafsiri "uvumilivu" unaweza kujumuisha "ustahamilivu" au "kuendelea kuamini" au "kubaki mwaminifu".
Jina, "wana wa Mungu" ni msemo wa mfano wenye maana kadhaa.
Neno "watakatifu" lina maana ya halisi ya "waliyo wasafi" na kueleza waamini wa Yesu.
"Mtoza ushuru" alikuwa mfanya kazi wa serikali ambaye kazi yake ilikuwa kupokea pesa watu waliyo paswa kulipa serikali ushuru.
Wavuvi ni wanamume ambao hukamata samaki kutoka majini kama njia ya kupata pesa. Katika Agano Jipya, wavuvi walitumia mitego mikubwa kukamata samaki. Msemo "wavuvi" ni jina lingine la mvuvi.
Petro na mitume wengine walifanya kazi kabla ya kuitwa na Yesu.
Kwa kuwa nchi ya Israeli ilikuwa karibu na maji, Biblia ina kumbukumbu nyingi ya samaki na wavuvi.
Msemo huu unaweza kutafsiriwa na msemo kama "wanamume wanaokamata samaki" au "wanamume wanaopata pesa kwa kukamata samaki"
Kuweka wakfu ni kuweka kando kitu kwa ajili ya kusudi maalumu au shughuli.
Daudi aliweka wakfu dhahabu na fedha zake kwa Bwana.
Mara kwa mara, neno "kujitolea" lina maana ya tukio rasmi au sherehe ya kuweka kando kitu kwa ajili ya kusudi maalumu.
Kuweka wakfu kwa madhabahu ilijumuisha kutoa sadaka kwa Mungu.
Nehemia aliwaongoza Waisraeli katika kuweka wakfu kwa kuta za Yerusalemu zilizotengenezwa kwa ahadi mpya ya kumtumikia Yahwe pekee kwa vyombo vya muziki na kuimba.
Msemo wa "kuweka wakfu" unaweza kutafsiriwa kama "kutenga kusudi maalumu" au "kabidhi kitu kutumika kwa kazi maalumu" au "kabidhi mtu kutenda tendo maalumu".
Neno "uzuri" una maana nyingi kutegemea na muktadha. Lugha nyingi hutumia maneno tofauti kutafsiri maana hizi tofauti.
Kwa ujumla, kitu ni kizuri kama kinalingana na tabia ya Mungu, kusudi na mapenzi.
Kitu ambacho ni "kizuri" kinaweza kufurahisha, bora, msaada, kinachofaa, chenye manufaa, au sahihi kimaadili.
Ardhi ambayo ni "nzuri" inaweza kuitwa "yenye rutuba" au "yenye kuzaa".
Zao "zuri" linaweza kuwa zao "la wingi".
Mtu anaweza kuwa "mzuri" katika kile afanyacho kama ana ujuzi katika kazi yao, yaani "mkulima mzuri".
Katika Biblia, maana ya jumla ya "nzuri" mara nyingi hutofautishwa na "uovu".
Msemo "wema" mara nyingi humaanisha kuwa mzuri kimaadili kwa kutoa mambo mazuri na yenye manufaa. Inaweza kumaanisha utimilifu wake wa kimaadili.
Msemo "woga" au "hofu" ina maana ya hisia zisizo nzuri mtu huwa nazo ambapo kuna tishio la kudhuriwa kwake au kwa wengine.
Msemo "hofu" unaweza kumaanisha heshima kubwa na hofu mtu huwa nayo kwa mamlaka.
Msemo "hofu ya Yahwe" na misemo ya kufanana "hofu ya Mungu" an "hofu ya Bwana" ina maana ya kumheshimu sana Mungu na konyesha heshima kwa kumtii yeye. Hofu hii inahamasishwa kwa kujua ya kwamba Mungu ni mtakatifu na anachukia dhambi.
Biblia inafundisha ya kwamba mtu anayemwogopa Yahwe atakuwa na hekima.
Mapendekezo ya Tafsiri
Kulingana na muktadha, "kuwa na hofu" kunaweza kutafsiriwa kama "kuogopa" au "kuheshimu sana" au "kuhofu" au " kuwa na hofu ya"
Msemo "woga" inaweza kutafsiriwa kama "kuogopa".
Sentensi, "Hofu ya Mungu ilianguka juu yao wote" inaweza kutafsiriwa kama, "Ghafla wote wakapatwa na hofu kuu na heshima kwa Mungu" au "Mara ghafla wote wakahisi kushangazwa sana na kumhofu Mungu sana" au "Wakati huo huo, wote wakapatwa na hofu ya Mungu"
Istilahi ' hofu' hurejelea hisia kali za woga or kitisho. Mtu aliye na hofu huwa ameogopa. woga ni hali kali na kubwa zaidi ya hofu, zaidi ya hofu ya kawaida. Mara kwa mara mtu anapokuwa ametishwa huwa ameshitushwa na ameshangazwa sana.
Neno "woga" uelezea hisia ya hofu kuu. "Kuogopesha" mtu ina maana ya kusababisha huyo mtu kujisikia wasi wasi sana.
Msemo "zawadi" una maana ya kitu chochote ambacho hupewa au kutolvwa kwa mtu. Zawadi inatolewa bila matarajio ya kurudishiwa kitu chochote.
Pesa, chakula, mavazi, au vitu vingine zitolewazo kwa watu maskini zinaitwa "zawadi".
Katika Biblia, sadaka itolewayo kwa Mungu pia hujulikana kama zawadi.
Zawadi ya wokovu ni kitu ambacho Mungu anatupatia kupitia imani kwa Yesu.
Katika Agano Jipya, msemo "zawadi" pia hutumika kumaanisha uwezo maalumu wa kiroho ambao Mungu hutoa kwa Wakristo wote kutumikia watu wengine.
Mapendekezo ya Tafsiri
Msemo wa jumla wa "zawadi" unaweza kutafsiriwa na neno au msemo ambao una maana ya "kitu ambacho kinatolewa".
Katika muktadha wa mtu kuwa na zawadi au uwezo maalumu ambao unatoka kwa Mungu, msemo "zawadi kutoka kwa Roho" unaweza kutafsiriwa kama "uwezo wa kiroho" au "uwezo maalumu kutoka kwa Roho Mtakatifu" au "kipaji maalumu cha kiroho ambacho Mungu ametoa"
Msemo "zinaa" una maana ya tendo la ngono ambalo hufanyika nje ya mahusiano ya ndoa ya mwanamume na mwanamke. Hii ni kinyume na mpango wa Mungu.
Msemo huu unaweza kumaanisha tendo lolote la kingono ambalo ni kinyume na mapenzi ya Mungu, ikiwemo matendo ya usenge na ponografia.
Aina moja ya zinaa ni uzinzi, ambayo ni tendo la ngono haswa kati ya mtu aliyeoa na mtu ambaye sio mke au mume wake.
Aina nyingine ya zinaa ni "ukahaba" ambayo uhusisha kulipwa kufanya ngono na mtu.
Msemo huu pia hutumika kitamathali kumaanisha ukosefu wa uaminifu wa Israeli kwa Mungu walipoabudu miungu ya uongo.
Mapendekezo ya Tafsiri
Msemo "zinaa" unaweza kutafsiriwa kama "uzinzi" ikiwa maana sahihi ya msemo inaeleweka.
Njia zingine za kutafsiri msemo huu zinaweza kujumuisha "matendo mabaya ya ngono" au "ngono nje ya ndoa".
Msemo huu unaweza kutafsiriwa katika njia nyingine kutoka kwa neno "uzinzi".
Tafsiri ya matumizi ya tamathali ya msemo huu unatakiwa kukaa na maana halisi ikiwezekana kwa kuwa kuna ulinganisho wa kufanana katika Biblia kati ya kutokuwa mwaminifu kwa Mungu na kutokuwa mwaminifu katika mahusiano ya kimapenzi.